CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHA SHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHA SHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Heri ya Siku ya Wanawake Duniani (IWD)

Watoto katika kituo cha SAAFAD Membe.

 

Kituo hiki kiko Kijiji cha Membe, Kata ya Membe na Wilaya ya Chamwino katika Mkoa wa Dodoma.

food bank 57

Katika kusherekea sikukuu ya wanawake Duniani, wanawake wa Chama cha Biblia cha Tanzania, wadau na Chama cha Biblia cha Tanzania wamejumuika leo tarehe 08/03/2022 kuazimisha siku hiyo kwa kuwatembelea watoto wanaolelewa kwenye kituo cha SAAFAD Membe.

Katika siku hiyo wanawake wa Chama cha Biblia wamepata fursa ya kukutana na watoto zaidi ya 100 wanaolelewa kwenye kituo hiko ambao ni yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu. Ilikuwa ni ya furaha kwa wanawake, watoto wenyewe pamoja na wageni wengine walioshiriki kwenye sherehe hiyo.

Wanawake hao walipata mda wa kuzungumza na watoto hao kuhusu mada mbali mbali zikiwemo athari za mimba utotoni, umuhimu wa kujitunza na jinsi kuepukana na vishawishi wanavyokutana navyo katika makuzi yao na kuliishi Neno la Mungu wanalofundishwa na walezi wao kituoni hapo.

 

Watoto walipata muda wa kushirikisha story za maisha yao. Huyo binti anashuhudia namna mama yake alivyomkataa na wadogo zake mara tu baba alipofariki na mama kuolewa na mwanaume mwingine. Wote wanalelewa kwenye kituo cha SAAFAD.

Membe Kituoni (SAAFAD)

Kauli mbiu ya mwaka huu ni

IMG 6979 scaled

“Kizazi cha Haki na Usawa kwa Maendeleo Endelevu.”

IMG 7018 scaled
given3
food bank 57
Kimachame Bible Launch

Kimachame Bible Launch

The launch of the Bible in the Kimashami language (Kichagga of Machame), was held in the Congregation of Hai in 04/12/2022. Bishop Dr Shoo said many people have been neglecting their languages ​​and said it is good to learn and develop their native languages. At the...

Get Involved

We have Bibles in different Tanzanians languages that you can read online. You can also download Bible reading plans to guide you through the Bible.

food bank 56

Donate Today or Get Involved

Help With Hunger By Donating Today!

The launch of the full Braille Bible

The launch of the full Braille Bible

The Bible Society of Tanzania celebrates the launch of the full Braille Bible.

It is in the city of Kongwa, located in Dodoma Region of the capital city of Tanzania that the majority of the visual impaired live. One of the characteristics of this translation is that it is the result of close collaboration between Churches of different confessions

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

 

ZIARA KATIKA MAGEREZA YA MSALATO NA KONGWA DODOMA

Moja kati ya wajibu muhimu kwa Chama cha Biblia cha Tanzania ni kuhakikisha kuwa watu wote wanapata fursa ya kupata maandiko matakatifu. Kutokana na jukukumu hilo tarehe 27/11/2018 watumishi wa Idara ya Mahusiano na baadhi ya Wale wa Mawasiliano, walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Msalato Dodoma na kugawa Biblia, Sabuni na dawa ya meno kwa Wafungwa wa gereza hilo la Msalato. Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji akishirikiana na Msaidizi wake na Maafande wengine walitupokea vizuri sana na kutupa ushirikiano wa hali ya juu.

 

 

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, viongozi wa kanisa la KKKT Dodoma na viongozi wa gereza la Msalato

 

Jukumu la kugawa Biblia halikuishia Gereza la Msalato tu kwani Tarehe 28/11/2018 Meneja Mahusiano na kikosi kazi chake walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Kongwa Dodoma. Katika Gereza hili tulipokelewa vizuri sana na kupewa maelezo ya jinsi Wafungwa wanavyohitaji msaada wa Maandiko na vifaa vingne kwani wanatakiwa kjujitegemea.Chama cha Biblia tulifaulu kugawa Maandiko Matakatifu,sabuni, dawa ya Meno na Taulo za akina Mama.Mkuu wa Gereza Afande Nyonyi alishuru sana Chama cha Biblia cha Tanzania kwa msaada huo kwa Wafungwa.

 

 

 

 

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Kongwa Afande Nyonyi

 

 

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, mkuu wa jimbo wa kanisa la KKKT Kongwa (wa kwanza kulia) na viongozi wa gereza la Kongwa

 

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma

Hatimaye Biblia ya Kisukuma yazinduliwa kwa kishindo mkoani Mwanza.

Na Felix Jones

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma umefanyika katika Kanisa Kuu AIC Makongoro Mwanza na kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Umoja wa Makanisa mkoa wa Mwanza.

Akizungumza katika hafla hiyo Mch. Ipyana Mwangota kwa niaba ya mtafsiri mkuu wa Umoja wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (UBS), kuwa mchakato wa kutafsiri Biblia kwa lugha ya Kisukuma ulianza miaka thelathini iliyopita. “Tulifanikiwa kutafsiri sehemu ya Biblia kwa lugha kisukuma na kuzinduliwa mwaka 1895 na Mchakato ukaendelea tukapata Agano Jipya mwaka 1925 na baadae kufanyiwa marekebisho na atimaye kuzinduliwa mwaka 2001 na leo tunayofuraha kuzindua au kuweka wakfu Biblia kamili kwa lugha hii ya kisukuma mwaka huu 2021.”

Mch. Ipyana Mwangota

Meneja Tafsri akizungumza kwa niaba ya Mtafsiri Mkuu wa Umoja wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (UBS) wakati wa hafla hiyo.

Pamoja na changamoto tulizokabiliwa nazo katika kutafsiri, kuichapisha mpaka leo inazinduliwa, tunakila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kusikia maombi yetu na haja yetu ya moyoni.

Kwa sasa jamii hii ina nafasi ya kumsikiliza Mungu akisema nao kwa lugha yao wenyewe na hivyo historia imejiandika kwa sababu watoto na wajukuu wataitumia Biblia hii kwa miaka mingi na kuienzi lugha yao. Pia ni jambo zuri katika kuihifadhi lugha ya Kisukuma kwa sababu wengi tunafahamu fasihi andishi inahifadhiwa kwa muda mrefu zaidi.

Mara baada ya hotuba hiyo fupi, Mch. Mwangota ndipo alipopata fursa ya kumkabithi Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Kimonge Biblia hiyo ya Kisukuma ili naye aikabidhi kwa Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande ili iweke wakfu tiyari kwa kutumika katika Kanisa la Mungu.

Mwakilishi wa TC akimkabithi KM Biblia

Mwakilishi wa Translation Consultant (TC) Canon Ipyana Mwangota akimkabidhi Biblia ya Kisukuma Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge wakati wa Uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza

Kwa upande wa Katibu Mkuu Dkt. Alfred Kimonge aliomba Biblia hii itumike katika Ibada ili kazi hii iliyofanyika kwa miaka mingi na kwa gharama kubwa isiwe ya bure. Na zaidi aliongeza kuwa kwa niaba ya Chama cha Biblia cha Tanzania ni matumaini yetu kuwa injili ya Wokovu katika Yesu Kristo itawafikia wasukuma katika lugha yao ya moyoni na kusema sasa tumemtambua Mungu anasema na sisi kwa lugha yetu.

Hivyo Wasukuma nao watamsikia Bwana Yesu  kwa ukaribu wa moyoni ili wapate fursa ya kushiriki katika halaiki ya mwisho, kama Biblia isemavyo:-

“Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha (Wasukuma)…” (Ufu. 7: 9 – 12).

“Hivyo Ninayoheshima ya kukuomba Baba Askofu Mkuu kuwa uipokee Biblia hii na kuiweka wakfu” alisema Katibu Mkuu wakati wa kukabithi Biblia hiyo ili iwekwe wakfu.

KM akisoma Risala Mbele Ask. kabla kukabithi Biblia

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge akisoma hotuba mbele ya Askofu Mkuu Renatus Nkwande kabla ya kumkabidhi wakati wa Uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza.

Naye Dkt. Alfred Kimonge alipo maliza kusoma hotuba yake ndipo alipopata fursa ya kumkabithi Askofu Mkuu Renatus Nkwande Biblia hiyo ya Kisukuma ili aiweke wakfu tiyari kwa kutumika katika Kanisa la Mungu.

KM akimkabidhi Biblia ya Kisukuma Askofu

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia ya Kisukuma kwa Askofu Mkuu Renatus Nkwande wakati wa uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza.

Askofu Mkuu Renatus Nkwande aliipokea kwa furaha kisha akaendelea na taratibu za kuiweka wakfu Biblia hiyo ya Kisukuma.

Ask Mkuu Renatus Nkwande akihutubu

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akisoma sala ya kuzindua hiyo Biblia ya Kisukuma wakati wa sherehe hizo za uzinduzi wa hiyo Biblia ya Kisukuma.

Ask Mkuu Renatus Nkwande akisaini

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akisaini Biblia ya Kisukuma kuwashilia kupokelewa na Kanisa.

Na hapa ni baadhi ya viongozi na waumini walio weza kuhudhulia katika hafla ya Uzinduzi huo.

Baada ya uzinduzi huo wa Biblia hiyo Baba Askofu na Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania aliyewakilisha Bodi ya wakurugenzi ya Chama cha Biblia cha Tanzania alipata fursa ya kuhutubia wasukuma waliofika katika uzinduzi huo na pia kutoa salamu kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Chama cha Biblia cha Tanzania na kueleza dhima ya Chama katika mkutadha wa kuakikisha kila Mtu hapa nchini anakuwa na Biblia yake na kwa lugha anayeielewa asa kuwa na Biblia ya moyoni.

Askofu Muhagachi

Baba Askofu Amos Muhagachi ambaye ni Mwenyekiti msaidizi wa Bodi ya wakurugenzi na Balozi wa Chama cha Biblia akihutubia Kanisa kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi.

Kwa upande wa Mgeni rasmi Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande alikipongeza Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kazi nzuri sana ya kuakikisha kila mtu ana Biblia yake na lugha yake na kwa bei mtu anayoweza kuimudu huku akisisitiza Kanisa la Mungu katika kabila la Kisukuma kuhakikisha wanaweka ratiba ya kuwezesha Biblia ya Kisukuma inatumika ili watu weweze kumsikia Mungu akisema nao kwa lugha yao ya Moyoni.

Ask Mkuu Renatus Nkwande anahubiri

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akihutubia Kanisa la Mungu katika Kabila la Wasukuma wakati wa uzinduzi wa Biblia hiyo ya kisukuma.

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma1Tunakualika Karibu Ushiriki nasi katika

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma

Jumapili, Juni 27, 2021

Mahali: KANISA LA AIC MISSION MAKONGOLO – MWANZA

Saa 08:00 Mchana – 12:00 Jioni

Tukio la bure kabisa

Imetafsiriwa na Chama cha Biblia cha Tanzania


Jinunulie Biblia yako katika lugha yako ya mama

Pia kinawakaribisha wanachama wote wa Chama cha Biblia walioko mkoa wa Mwanza kwenye uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma.

Uzinduzi huo utafanyika katika kanisa la AIC Makongoro, Jumapili tar.27.6.2021 kuanzia saa 8 mchana hadi 12 jioni.
Muda huu utawapa nafasi waumini kutoka madhehebu mbali mbali kuweza kushiriki tukio hili, baada ya kumaliza ibada za Jumapili ndani ya makanisa yao.

Wanachama wote mnakaribishwa kushiriki tukio hili muhimu na la kihistoria kwa Chama cha Biblia, Kanisa na jamii nzima ya Kisukuma.
Upatapo taarifa hii mkaribishe na mwenzako, Wakristo kutoka madhehebu yote mnakaribishwa.
Tuunge mkono kwa kushiriki kikamilifu katika uzinduzi wa Biblia hii.

Tukutane AIC Makongoro kwenye uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma Jumapili.
Karibuni 🙏🙏🙏
BIBLIA hiyo itakuwa inauzwa kwa bei ya punguzo.

Jiandae upate nakala yako pia.

Mungu ataongea na wewe kwa lugha yako ya Kisukuma.

Kuhamasisha Makanisa

Kuhamasisha Makanisa

Kukutana na Mwl. MwakasegeKazi ya kuamasisha makanisa na viongozi wa dini katika madhehebu mbali mbali ya Kikristo hapa nchini juu ya umuhimu wa kuwapatia watoto, vijana na wafungwa Neno la Mungu (Biblia), inaendelea katika Kanda ya kaskazini.

Na leo wajumbe wa Bodi wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Baba Askofu Amos Muhagachi na Mama Engineer Elikael Manase pamoja na Meneja wa Mahausino na Makanisa na Utunishaji mfuko wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Mch. Samweli Mshana wamemtembelea Mwl. Christopher Mwakasege ofisini kwake.

Bodi MembersMwl. Mwakasege 5

Tuzidi kuwaombea kwa kazi hii inayofanyika ili tujenge taifa lenye maadili mema.🙏

“MPATIE MTOTO, MFUNGWA NA KIJANA NENO LA MUNGU”

(ZABURI 119: 105; “Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na Mwanga wa njia yangu.”)