Wakagulu wapatao 756 wanawake wakiwa 550 na wanaume wakiwa 206 waliojiunga na mpango wa kujifunza kusoma na kuandika (LWA Kikagulu) mnamo tarehe 15/06/2020 hadi tarehe 30/11/2020 hatimaye walihitmu mafunzo hayo huku wakiwa na furaha kwa kujua kusoma na kuandika. Wakizungumzia furaha yao wameonekana wakiwa na bashasha na furaha sana kwa kupata elimu hii muhimu kwa maisha yao.
“Sasa ninaweza kusoma na kuandika na hata nikiumwa nikiandikiwa dawa sina haja ya mtu kunisomea na pia naweza kushiriki kikamilifu katika huduma za kijamii kama kupiga kura na mengine mengi katika dunia ya sasa” mama moja alisikika akisema maneno hayo kwa furaha.
Sherehe hizo zilifanyika tarehe 27/02/2021 katika Ukumbi wa Nazareth huko Gairo.
Mratibu wa mpango huu Mwl. Frank Makalla wa kwanza kushoto kwa waliokaa mbele akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu waliosimama nyuma wenye vyeti pamoja na mgeni rasmi Baba Askofu Paulo Jacob Mameo wa Kanisa KKKT Jimbo la Morogoro wa pili kutoka kushoto na wageni wengine walioalikwa kwenye mahafali hayo.
Baadhi ya wakinamama wenye umri mkubwa walioweza kushiriki na kupata vyeti vyao.
Kabla ya kugawa vyeti kulitanguliwa na hotuba na nasaa mbalimbali kutoka kwa Mgeni rasmi na viongozi mbalimbali walioalikwa kwenye mahafali haya ya tatu tangu kuanzishwa kwa mpango wa LWA Chikagulu katika mkoa wa Morogoro wilaya za Kilosa na Gairo
Canon Mstaafu Bonifas Mkami wa Kanisa Anglikani Jimbo la Morogoro
Canoni Mstaafu Bonifasi Mkami ni mmoja wa wachambuzi wa Biblia ya lugha ya Chikagulu inayoendelea kutafsiriwa katika lugha hiyo pia ni mmoja wa watu walioshiriki katika uandishi wa kitabu cha Chibweda. Akizungumza baada kupewa nafasi ya kuongoza ibada ya ufunguzi wa maafali alisema
“Mpango huu wa akina mama kujifunza kusoma na kuandika kwa lugha yao wenyewe kupitia Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama kikaona kianzie kwetu sisi wakagulu. Baada ya hapo tukaanza uandishi wa vitabu.
Kwanza cha Mwalimu, pili cha mwanafunzi kwa neema ya Mungu, mimi nilikuwa mmojawapo. Jina la Kitabu cha Mwanafunzi na Mwalimu tulikiita “CHIBWEDA” kwa maana ya FURAHA na kuweka picha zinazotoa taswira ya Kikagulu”.
Canon Mstaafu Bonifas Mkami wa Kanisa Anglikani Jimbo la Morogoro
Pia aliongeza kusema “Baada ya kukamilisha kuandika vitabu hivyo ikawa ni kazi ya kuwatafuta walimu wanaojua kuzungumza Kikagulu kwa ufasaha ili wapewe mafunzo ya kufundisha madarasa ya wanakisomo watakaojifunza kusoma na kuandika kwa kutumia lugha yao ya Kikagulu kwa kuwa ndiyo wanayoilewa Zaidi na baadae wanaweza kusoma na kuandika kwa Kiswahili na lugha zingine bila shida yoyote na baada ya hapo yakaanzishwa madarasa 10 ya kwanza na waalimu 20 katika awamu hii ya kwanza.”
Nasaha na shukrani za Canon Bonifasi Mkami
Kujua kwenu kusoma na Kuandika kutasaidia sana baada ya Biblia yetu sisi wakagulu tunayoiandaa kwa sasa na iko hatua za mwisho. Itakuwa rahisi ninyi kuisoma bila shida kwa hiyo tunatoa shukrani nyingi kwa Chama cha Biblia cha Finland na Chama cha Biblia cha Tanzania kuwezesha mpango huu katika mkoa wetu katika wilaya zetu za Kilosa na Gairo katika lugha hii ya Chikagulu Mwenyezi Mungu na awabariki sana.
Na zaidi tunawashukuru sana Mwalimu Frank Makalla mratibu wa mpango huu, Ndugu Timothy Kamau, Dr Suzan Nyaga na Ruth Munguth wa SIL Kenya.
Nawaombeni ninyi mliofaidika na mpango huu, muwe mawakili wema na waminifu katika kutunza lugha yetu.
Mratibu wa mpango huu wa LWA Chikagulu Mwalimu Frank Makalla
Akizungumza kabla ya kukabidhi vyeti kwa awamu ya tatu ya wahitimu hao, Mratibu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Mwl.Frank Makalla alisema
“wahitimu hao ni wa awamu ya tatu ya programu hii iliyolenga kuwajengea uwezo wanawake kusoma na kuandika ambao kwa sababu mbalimbali hawakuweza kwenda shule wakati walipostahili kwenda shule, hii ni fursa kwao wakiwa watu wazima kuanzia aka 14 na kuendelea ingawa na wanaume wanaruhusiwa kushiriki japo si kwa kiwango kikubwa maana mpango unawalenga wanawake ambao hawakupata nafasi hiyo ya kusoma na kuandika kutokana na sababu mbali mbali.”
Mratibu wa mpango wa kusoma na kuandika wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Mwl.Frank Makalla akizungumza na wahitimu wa awamu ya tatu katika mahafali hayo huku akiwasisitiza wasiache kufanya yale waliyofundishwa pia wahakikishe kuwa kupitia wao watu wengi zaidi walijue Neno la Mungu.
Awamu ya kwanza waliohitimu ni jumla ya watu 97 ambapo wanawake ni 83 na wanaume ni 14 kutoka vijiji 10 vya Gairo na Kilosa ambavyo ni Gairo, Mtumbatu, Chakwale, Mamboya, Maguha, Berega, Mwandi,Magela, Mabula, pamoja na Italagwe.
Awamu ya pili waliohitimu jumla ni 248 ambapo wanawake ni 214 na wanaume ni 34; kutoka kwenye vijiji 10 vingine ambavyo ni Mogohigwa, Kibedya, Tabuhotel, Magubike, Nguyami, Ibindo, Ntembo, Mbili, Dumbaalume, pamoja na Kiegeya.
Waliojiandikisha ni 423 kati yao waliohitimu ni 317 na ambao hawajahitimu ni 106 kutokana na changamoto mbalimbali kama vile kuhama, shughuli za mashamba, na matatizo mbalimbali ya kijamii.
Aliendelea kusema kuwa mahafali hayo ni mwendelezo wa mahafali ya awamu ya kwanza ya program hiyo iliyoanza mwaka 2017, ambapo watu 120 walijiandikisha huku watu 97 walihitimu mafunzo hayo ambayo pamoja na kuwafundisha kwa kutumia lugha ya chikagulu kama lugha ya kufundishia kwa urahisi wa kuelewa kwa lugha yao lakini kadiri wanvyoendelea kujifunza kusoma na kuandika hatimaye wanaweza kusoma na kuandka katika lugha ya Kiswahili na lugha zingine.
Alieza pia kuwa programu hiyo inafadhiliwa na Chama cha Biblia cha Finland na Chama cha Biblia cha Tanzania kikitoa usimamizi wa mpango na uratibu uku Summer Institute of linguistics (SIL) hawa wanatoa utaalamu wa waalimu pamoja na mwongozo wa kuandaa vitabu vya kufundishia. Programu hiyo inalenga zaidi kuwainua wanawake kujifunza kusoma na kuandika ingawa na wanaume wanakaribishwa kushiriki.
Wahitimu wa CHIBWEDA wakiwa katika kufuatilia hotuba na nasaha za viongozi wakati wa mahafali yao iliyofanyika mnamo tarehe 27/02/2021 huko Gairo siku ya Jumamosi.
Mratibu wa mpango huu Mwl. Makalla alisema kati ya watu wazima 395 waliohitimu, wanawake ni 337 na wanaume ni 58 katika awamu hii ya tatu
Aidha, Mwl. Makalla aliomba ushirikiano na serikali katika mafunzo hayo ambayo yamelenga kuwafanya wananchi waliokosa fursa ya kusoma na kuandika kujiunga na kuendelea kupata elimu hiyo.
“Katika programu yetu hii tumekuwa tukichukua wale wenye umri wa kuanzia miaka 14 na kuendelea, hivyo wale wenye miaka 14 hadi 17, serikali inaweza kuwatambua na kuwaingiza katika mfumo wa MEMKWA katika shule za msingi kama ambavyo Serikali inaelekeza kupitia wizara ya Elimu ili wakajifunze zaidi kwa sababu sisi hapa tunawafundisha kusoma na kuandika tu huko watajifunza masomo mengine pia kama Hesabu, Sayansi, Jiografia Historia na kadhalika.
Changamoto ya kwa nini wanaanza wengi na kuhitimu wachache?
Sababu zilizotajwa ni kwamba jamii ya wakagulu ni wakulima na wafugaji kwa hiyo wakati wa masika wakulima wanahamia mbali na vijiji ambako ardhi ina rutuba zaidi kwa kilimo cheye kuleta tija, pili wafugaji wanahamia maeneo mengine kutafuta malisho na maji kwa ajili ya mifugo yao na matatizo mbalimbali ya kijamii.
Katibu wa UMAKI Ndg. Josephine Semwenda
Katibu wa idara ya maendeleo ya akina Mama UMAKI Josephine Semwenda katika Dayosisi ya Morogoro ambaye alialikwa kuwatia moyo wahitimu hao aliwasisitizia wahitimu kutokuogopa kuitangaza lugha ya Chikagulu kila mahali katika eneo lao la ukaguluni na kwingineko kwa kuwahimiza kuwa mabalozi wema katika kuilinda lugha yao isipotee, alitumia nafasi hiyo pia kuwapongeza. Wahitimu wote na kuwatakia kila lakheri katika kutekeleza majukumu ya kijamii na Kanisa.
Na hapa aliendelea kueleza zaidi kuwa
“Kwa Neema ya Mungu mmemaliza, Mungu aendelee kuwa karibu sana aendelee kuachia nguvu ya kuendelea kujifunza zaidi hata katika masomo mengine pia natamani kuona wengine hata mufike secondary kwasababu mmeshajua kusoma na baadae mtafika mbali Bwana Yesu asifiwe. Bila shaka kujua kusoma kwenu kutawasaidia sasa kuendeleza kusoma Neno la Mungu lakini pia kuweza kusoma vitabu mbalimbali na kufahamu mambo mengi ambayo usipojua kusoma na kuandika unakuwa kama kipofu na mambo mengi yanakupita.”
Sisi Idara ya UMAKI tunashukuru kwa ajili ya neema hii. Mana ninyi wahitimu mtakuwa nguzo muhimu kwenye madarasa yetu ya UMAKI kwa kuwafundisha na kuwaongoza wanawake kwenye madarasa yetu ya umaki na kufanya mambo mbalimbali kwa ajili ya idala ya kina mama ambao wengi wao hawajajua kusoma na kuandika. Maana wengine wanapoombwa kutoa Neno au labda kufundisha jambo fulani wengine huwa hawawezi kwa sababu hawajui kusoma na kuandika sasa wale wa madarasa ya umaki mtakuwa msaada mkubwa kwao.
Mwisho kabisa niendelee kupongeza tena na tena kwa juhudi ambazo mmezichukua hata kufikia siku ya leo Mungu awabariki lakini msiishie hapo muendelee kujiendeleza ili muweze kupata mambo makubwa zaidi na Jina la Bwana litaendelea kuhimidiwa kama sasa hivi unaweza kusoma masomo ya Biblia na muweze kusoma kwingine hata katika taifa letu pia Mungu awabariki muendelee kutimiza ahadi aliyo wapatia Bwana Yesu. Amina.
Diwani wa Kata ya Gairo na katibu wa Mbunge jimbo la Gairo Ndugu Danstan Mwegoha
Diwani Danstan Mwegoha aliwashukuru sana Chama cha Biblia cha Tanzania na wote waliotia mkono katika mpango huu kwa kutambua umuhimu wa wananchi wetu wakristo wetu kuendesha mafunzo ya elimu ya watu wazima na hasa kwa kuwalenga wakinamama ni msaada mkubwa kwao, sisi tunasema wakina mama ni jeshi kubwa kwa sababu wakina mama ndiyo wenye majukumu makubwa na akina mama ndiyo wenye malezi mazuri kwa watoto. Na pia wakina mama ndiyo wanaowatunza wakina baba.
Diwani Danstan Mwegoha akihutubia wahitmu
Na pia aliendelea kusema, Kwenye utaratibu wetu wa kutoa mikopo mara nyingi huwezi kukuta wakina baba wakiwa kwenye vikundi hivyo bali utakuta wakinamama, vijana, na walemavu, kwa hiyo wakinamama pamoja na vipato vyao vidogo wanaweza kuunganisha nguvu kwa kukopa na kulipa vizuri kuliko wakina baba.
Zamani ilikuwa ni vigumu sana kusomesha watoto wa kike kwa sababu wakina baba walikuwa wanahitaji kupokea mahali kwa kunufaika zaidi sasa bila kuangalia maisha ya binti zao kwa wakati ujao. Ninaishukuru sana serikali yetu inaonekana kuwajali na kuwalinda watoto wa kike katika kupata elimu.
Jukumu letu sisi kama serikali na Chama hiki kinacho endesha mafunzo haya tuombe sana kuwa na ushirikiano wa kutosha. Sisi kwa heshima yetu ya uongozi kwa mujibu wa nafasi yangu katika uongozi msisitizo na mkazo wa mtu kuchaguliwa na kupigiwa kura katika ngazi yoyote kuna vipengele vimeandikwa kwamba ni lazima mtu ajue kusoma na kuandika ndipo aruhusiwe kugombea nafasi na si vinginevyo kwahiyo unaweza kupata nafasi ya kuwa kiongozi kama diwani, mbunge, Rais n.k, kwa kuwa sasa mnajua kusoma na kuandika. Nawatakia Baraka za Mungu katika kuendelea mbele. Mungu awabariki sana.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Nguyami.
Ndugu Mgeni rasmi, katika Kijiji changu sisi tumejiona fahari sana kwa kuwepo mpango huu na wengi waliohitimu katika mafunzo haya wamekuwa Baraka sana kwa kijiji chetu kwa maana miongoni mwao tulipata mama mmoja ambaye sasa ni mwekahazina anayeitwa Rehema Penford wa kijiji chetu. Kabla ya kupatiwa elimu hii haikuwa hivyo.
Na wananchi wengi wanawaamini watu wanaopitia elimu hii kwa kuwa wameonekana kuwa na ufahamu mkubwa na maadili mema katika Jamii yetu. Sisi kama serikali tunatafuta mpango mzuri wa kuwasaidia Chama cha Biblia cha Tanzania ili kiweze kuwafikia wengi zaidi katika Kijiji chetu.
Mwenyekiti wa Kijiji wa Kijiji cha Nguyami Mh. Gilbert Ngiga
Ushauri wangu kwenu wahitimu wa CHIBWEDA nawaomba sana, huu uwe mwanzo wa kutaka kujiendeleza zaidi na zaidi ili mfikie ndoto zenu. Na nyinyi pia ni rahisi serikali kuwasaidia mikopo katika kujiendeleza kwenu kwa maana kumuelimisha mwanamke umeielimisha jamii yote.
Zaidi nawapongeza tena Chama cha Biblia kwa kuwezesha mpango huu na mimi naahidi kujiunga na Chama hiki ili nami nitoe mchango wangu hata kwa pesa kidogo na Mwenyezi Mungu na awabariki sana.
Meneja wa miradi na utunishaji wa mfuko wa CBT Mchungaji Samwel Mshana.
Mch. Samweli Mshana ambaye pia alimwakilisha Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania alisema
Mgeni rasmi, Baba Askofu Paulo Jacob Momeo, Mheshimiwa mratibu wa UMAKI, Mheshimiwa mratibu wa mpango, Mheshimiwa Canon mstahafu, mheshimiwa Mwenyekiti wa kijiji cha Nguyami, waandishi wa habari, mheshimiwa mratibu wa Chibweda, walimu na wahitimu wote, Bwana wetu Yesu Kristo asifiwe.
Kwanza, nianze kumshukuru Baba Askofu lakini pili nimshukuru sana mheshimiwa Diwani kwasababu kweli mara ya kwanza lakini kwa sababu mimi ni Meneja wa miradi hii ni mara ya kwanza kuwa na viongozi wa serikali. Mheshimiwa Diwani tunakushukuru karibu sana lakini sitaacha kushukuru pia mwenyekiti wa kijiji cha Nguyami umetoa ushuhuda chanya unao onyesha faida ya mradi huu wa CHIBWEDA na pia tuwashukuru waalimu kwa jinsi ambavyo mmekuwa mkijitoa kwa jinsi ambavyo mme onyesha juhudi sio jambo rahisi kwa kiufupi umfundisha mwanafunzi mpaka afikie hatua ya kusoma na kuandika kama ambo tumeshuhudia mama yule alivyo soma risala Mungu awabariki sana.
Mchungaji Mshana akiongea na wahitimu wa awamu ya tatu wa Chibweda wakati mahafali hayo huko Gairo.
Wahitimu wa leo kwa niaba ya Katibu Mkuu napenda kuwapongeza.
Najua kwamba mmevumilia mambo mengi wakati wakusoma wengine mlipata changamoto za hapa na pale lakini kwa neema ya MUNGU mmeweza kuvumilia yote hayo na mmefika hatua ya mwisho.
Mimi nasema hongeleni sana na Chama cha Biblia kinaona fahari sana kwaajili yenu, mme tufanya kumtukuza Mungu kila tunapo waona hasa katika juhudi zenu na jinsi ambavyo mmefikia hatua hiyo kwakweli sisi mmejawa furaha na mmetufanya tumtukuze MUNGU kwaajili yenu na mimi kama Meneja wa miradi na muakilishi wa Katibu Mkuu sito acha kusema elimu na bidii kama ambavyo mmesikia viongozi wanavyo sema ukisoma
Wakolosai 1 : 10 “mwenende kama ulivyo wajibu wenu kwa Bwana, mkimpendeza kabisa; mkizaa matunda kwa kila kazi njema, na kuzidi katika maarifa ya Mungu;
Kwahiyo matunda ya elimu hiyo muyafanye na baadhi yenu kule kijijini hata ajira za vijiji sasa mnaachiwa maana mwazoni ilikuwa sio rahisi, na kwa sababu ya elimu muliyo ipata imewasaidia sana na sasa mnaweza kuajirika.
Mgeni rasmi Baba Askofu Paulo Jacob Mameo
Mgeni rasmi kabla ya kutoa vyeti kwa kundi la tatu la wahitimu wa Chibweda ‘Furaha’ Baba Askofu Momeo wa KKKT aliwataka wahitimu hao kutumia maarifa hayo kujiendeleza kiuchumi na kushiriki katika uchumi wa taifa kwa ujumla.
Mgeni rasmi; Baba Askofu Paulo Jacob Mameo akiwa anazungumza na wahitimu wa awamu ya tatu katika mahafali hayo katika ukumbi wa Nazareth Gairo.
Baba Askofu Memo aliendelea kuwatia moyo na kuwahimiza kuendeleza kuenzi lugha yao ya Kikagulu na uku wakitumia maarifa hayo waliyoyapata kusaidia kueneza injili kwa watu wengine kwa maana sasa wanaweza kusoma na kuandika na kuwasaidia wengine uko vijijini wasiojua bado kusoma Biblia.
Mwisho nichukue nafasi hii kwa niaba yangu na Kanisa kuwashukuruni Chama cha Biblia cha Tanzania kwa jitihada nzuri ya kufuta ujinga kwa kusoma na kuandika kwa kuanzisha elimu ya watu wazima hasa kupitia kusoma Biblia. Mradi huu ni kitu kizuri sana sio tu kwa kufuta ujinga bali pia kwa kueneza maandiko matakatifu ya Neno la Mungu, Mungu aendelee kuwabariki ili habari njema iendelee kuenea kwa mbinu kama hii ya kufuta ujinga wa kutokusoma na kuandika. Mungu aendelee kuwapa maono zaidi ili huduma hii iendelee. Amina!
Katika mahali hayo burudani ilikuwa sehemu ya sherehe hizo, ambapo wahitimu hao pamoja na walimu wao walionesha michezo na nyimbo mbali mbali za kusifu na kushukuru wadau mbali mbali waliofanikisha wao kupata elimu hii.
Na hapa ni vikundi mbalimbali vya wahitimu wakitoa shukurani zao kupitia njia mbalimbali zikiwemo vile nyimbo, ngonjera pamoja na usomaji wa risala mbele ya mgeni rasmi.
Wahitimu wa awamu ya tatu ‘CHIBWEDA’ wakiimba wimbo maalumu wa kukishukuru Chama cha Biblia cha Finland na Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kuwaletea mpango huu wa kujifunza kusoma na kuandika.Pichani, ni wahitimu wa awamu ya tatu Chibweda, wakisoma Risala mbele ya mgeni rasmi wakati wa sherehe hiyo.
Nawasalimu wote katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, na kipekee ninamsalimu Baba Askofu Nicholaus Nsanganzelu na wote waliongozana naye. Bwana Yesu apewe sifa.
Ninazungumza kwa ridhaa ya Baraza la Wakurugenzi wa Chama cha Biblia cha Tanzania ambao wanawakilisha Kanisa zima hapa nchini yaani madhehebu yote. Mwenyekiti wa Baraza hili kwa awamu hii ni Mhashamu Askofu Mark Walwa Malekana wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA).
Chama cha Biblia cha Tanzania ni mwanachama kamili katika Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (United Bible Societies-UBS). Kusudi la Muungano huu Ulimwenguni kote ni kutafsiri, kuchapisha, kueneza Neno la Mungu (Biblia) kwa lugha anayoweza kuilewa vizuri msomaji na kwa bei anayoiweza. Chama kinajitegemea lakini kinaheshimu mapatano na malengo ya Muungano huo. Vile vile kinazingatia malengo ya Kanisa katika Umisionari na Uinjilishaji. Makusudi ni kwamba Kanisa lijihusishe katika kukibeba, kukiombea, kuchangia gharama kwa njia ya sadaka maalumu na vile vile kuhimiza uenezaji na usomaji wa Maandiko Matakatifu.
Malengo hayo yanatokana na utume wa Bwana Yesu asemapo, “Basi, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu” (Math: 28: 19). Hivyo Chama kinafanya juhudi ya kuwapatia watu wote Neno la Mungu katika lugha zao bila nyongeza au kipunguzi katika maana, na kwa bei ambayo walengwa wataimudu.
Ili kutimiza lengo hili Chama cha Biblia, kinatafsiri Biblia au sehemu zake kutoka lugha za awali (Kieberania na Kiyunani) kwenda katika lugha lengwa na kisha kuchapisha na kueneza Neno kwa walengwa. Malengo haya yanafanyika kwa kushirikiana na Kanisa na vyombo vyake. Mara nyingi Kanisa ndilo linaona umuhimu wa kutafsiri na kukiomba Chama cha Biblia kifanye kazi hiyo ya kutafsiri. Kwa hiyo Chama cha Biblia ni mtumishi wa Kanisa. Ni nani anayestahili kupatiwa Neno la Mungu? Ingewezekana, kila mtu apatiwe Neno la Mungu katika lugha yake ili apate nafasi ya kuusikia ujumbe wa kwamba Yesu Kristo pekee ndiye njia, kweli na uzima: ndiye Mwokozi.
Binadamu wamegawanyika katika makundi mbalimbali na tofauti. Makundi hayo yanatambuliwa kama makabila yenye lugha maalum, mengine yana utaifa, mengine yanajitaja kwa njia ya koo, n.k. Ijapokuwa makundi hayo yanatambuliwa hivyo, kunakuwepo sababu nzuri kama za uzalendo zinazoyachukulia makundi hayo kwa pamoja kama ni kitu kimoja. Hata hivyo kama vile ukuta imara unavyotokana na matofali moja moja yaliyo imara, hivyo na watu wenye utambulisho wao wa pekee kwa pamoja wanajenga jamii/taifa imara. Watu wanaimarishwa na tofauti zao. “Katika tofauti zetu tunapata uimara” Katika Ufunuo wa Yesu Kristo (Ufu. 7:9-12) tunaona jinsi wakombolewa wote walivyo pamoja katika halaiki ya mwisho, ijapokuwa ziko tofauti dhahiri kati yao.
Umoja wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni unatambua na kuheshimu tofauti zilizopo baina ya makundi ya watu. Hivyo pale watu wanapofikishiwa Neno la Mungu na ikadhihirika kuna udhaifu wa kulisoma, basi hatua zinachukuliwa ili kulihimiza Kanisa liwawekee watu misingi ya kujua kuisoma na kuiandika lugha yao. Matokeo ni kwamba kwa kuijua lugha yake kwa kulisoma Neno la Mungu kunamuwezesha mtu kujifunza lugha nyingine. Hivyo kwa kushirikiana na Kanisa, tafsiri mpya za Biblia zinaambatana na juhudi za kuwafundisha watu wazima kwa wadogo, kuisoma Biblia yao. Juhudi hii imefanyika kwa Wasukuma, Wamaasai, Wanyakyusa, Wairaqw na Wachagga. Mikakati ipo kwa Wakaguru, Wagogo, Wahehe, Wadatooga na penginepo ambapo juhudi ya kutafsiri Biblia inaendelea.
Kwa makundi haya Chama cha Biblia kinachukua juhudi zote kuandaa na kuwafikishia watu Biblia iliyoandaliwa katika mifumo tofauti. Kwa mfano, Neno lililochapishwa –(“Printed Format”), Neno lililowekwa katika kanda-naswa – (Magnetic au digital cassette), Neno lililoingizwa kwa njia simulizi – (Audio-Aural-Visual Scriptures), Neno katika mifumo maalumu kama vile Braille kwa Wasioona, New Reader Scriptures kwa wasomaji wa awali, Neno katika mfumo wa Maandishi Makubwa kwa ajili ya Wazee na wengine wenye udhaifu wa macho, Neno katika Matoleo ya Watoto, Neno kwa njia ya Scripture Literacy Promotion, Neno katika Digital Bible Library.
Huduma hii ni kwa ajili ya Kanisa, ili liweze kutumia zana hizo katika kuyatunza makundi hayo yote ya watu walioko katika maeneo yao ya Umisheni.
Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni kutokana na tamko la pamoja imejiwekea Sera ya kutafsiri Biblia aidha kwa mara ya kwanza au kwa kuhariri upya iliyokuwapo, ili angalau ifikapo 2033 makundi au makabila yote;
Yanayofikia au kuzidi idadi ya watu 500,000 wapatiwe Biblia nzima.
Yanayofikia idadi ya watu 250,000 wapatiwe Agano Jipya.
Yanayofikia idadi ya watu 100,000 wapatiwe Kisehemu cha Biblia (Bible Portions).
Hapa Tanzania tumekamilisha tafsiri 43 kati ya lugha 132 kazi inaendelea.
Ieleweke kwamba tafsiri ikianza tu, lengo ni kuikamilisha Biblia nzima hata kama idadi ya wazungumzaji ni ndogo ili asiwepo mtu atakayesema “nimekosa nafasi katika ufalme wake Yesu Kristo kwa kuwa Neno lake halikupatikana katika lugha yangu”
Makanisa kwa kushirikiana ndiyo yanayoomba kuanzisha na hatimaye kukamilisha tafsiri ili kila mtu awe na Biblia yake katika lugha anayoichagua na kuielewa.
Hizi lugha ambazo ni kitambulisho cha kila mtu na lugha yake, zinakabiliwa na changamoto kadhaa, kwa mfano;
Kutotiliwa maanani na kupewa kipaumbele na baadhi ya mamlaka tawala na Makanisa.
Lugha ya utawala (kama vile Kiingereza, Kiswahili, n.k) inagandamiza lugha nyingine na kuashiria kuitoa.
Neno la Mungu linadumu milele. Kwa hiyo lugha ambayo inalizungumzia Neno la Mungu inadumishwa. Ni wajibu wa Kanisa kuhakikisha Biblia inayozinduliwa inatumika katika ibada zao.
Hapa Tanzania kuna makundi/makabila ya lugha hai 132. Hadi sasa kuanzia 1846 hadi 2020 Chama cha Biblia, kwa kushirikiana na Kanisa tumetafsiri Neno la Mungu katika makabila yafuatayo;
Sehemu
Agano Jipya
Biblia
1.
Swahili Southern
1846
2.
Swahili (SUV)
1952
3.
Swahili (CL)
1996
4.
Wajita
1920
1930
5.
Wakuria
1969
1996
6.
Wamasai
1905
1923
1992
7.
Wadatooga
2002
2009
2020
8.
WaIraqw
1957
1977
2003
9.
Kivunjo
1966
1999
2020
10.
Machame
1932
1999
11.
Kimochi
1892
1999
12.
Wanyakyusa
1895
1908
1996
11.
Wahaya
1920
1930
2001
13.
Wasukuma
1895
1925/2001
1960/2020
14.
Wakuria
1969
1996
15.
Wameru
1964
16.
Chasu/Pare
1910
1922
17.
Kihehe
1999
18.
Kibena
1914
19.
Cigogo
1886
1899
2002
20.
Kidatooga
2009
2020
21.
Kiluo
1953
22.
Kinyamwanga
1982
23.
Chiyao
1920
24.
Kimambwe
1901
25.
Kilungu
1901
26.
Kishambala
1908
27.
Kinyamwezi
1951
28.
Kitaveta
1949
29.
Kinyiha
1950
30.
Kinyiramba
2010
31.
Kirimi
2010
32.
Kikerewe
1946
33.
Kikinga
1961
34.
Kizaramo
1975
35.
Kifipa
1988
36.
Kikaguru
2010
37.
Kibondei
1887
38.
Kingoni
1891
39.
Kizigua
1906
40.
Kimpoto
1913
41.
Kizinza
1930
42.
Kihangaza
1938
43.
Kiha
1960
44.
Kiwanji
1985
45.
Kizanaki
1948
Kazi bado ni kubwa, Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na Kanisa, kinayo mikakati ya kuwafikishia Neno la Mungu makundi/makabila yaliyobaki. Rai yetu kwa Kanisa tunaomba Biblia hii itumike katika ibada ili kazi hii iliyofanyika kwa miaka mingi na kwa gharama kubwa isiwe ya bure.
Leo tumekamilisha jitihada katika lugha ya Kidatooga kwa kuwakamilishia Biblia: Mungu anena na Wadatooga katika ukamilifu wa Biblia ya Kidatooga. Ni matumaini yetu kwamba Injili ya Wokovu katika Yesu Kristo itawafikia katika lugha yao ya moyoni na kusema sasa nimetambua Mungu anasema nami kwa lugha yangu.
Kwa njia ya tafsiri hii ya Biblia, Wadatooga nao watamsikia Bwana Yesu kwa ukaribu wa moyoni ili wapate fursa ya kushiriki katika halaiki ya mwisho “ Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha (Kidatooga)…” (Ufu. 7: 9-12).
Kama ilivyosomwa kwetu katika Ibada hiyo ya Uzinduzi na Askofu Julius Nyange Meneja Mstaafu wa Tafsri katika Chama cha Biblia cha Tanzania.
Waheshimiwa Viongozi, Maaskofu, Mapadre, Wachungaji, Katibu Mkuu na Watumishi wote wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Watendakazi wa Kanisa na Watumishi wa Mungu, Wamishenari, Viongozi wa Serikali na hasa Wakristo na wasemaji wa lugha ya Kidatooga. Ndugu waalikwa wote, Mabibi na Mabwana nawasalimu katika Jina kuu la Yesu Kristo Mwokozi wetu.
Ni furaha kubwa kushuhudia tukio hili kubwa la kihistoria, la Uzinduzi wa Biblia katika lugha ya Kidatooga. Nifuraha kubwa kwetu sote kushuhudia siku hii ya leo.
Wote tunaikumbuka siku kama hii, wakati wa Uzinduzi na kuwekwa wakfu Agano Jipya la Kidatoga, iliyofanyika Oktoba 12, 2009 katika viwanja vya Kanisa la Kiinjili la Kilutheli karibu na Ziwa Basotu, Mbulu.
Tukio la leo ni kutimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwa Mradi wa kutafsiri Biblia kwa lugha ya Kidatoga.
Sasa jamii yote ya Kidatoga na wasemaji wa lugha yta Kidatoga wataweza kusoma na kumsikia Mungu akiongea nao kwa lugha yao ya moyoni.
Lugha ya Kidatoga ni tawi la familia ya kusini ya lugha ya Kinilotiki (Southern Nilotic language family). Lahaja saba za Kidatoga ni pamoja na – Bajuta, Gisamjaga, Barabaiga, Isimijega na Rotigenga, Buradiga na Bijanjida.
Barabaiga ndilo kundi kubwa zaidi katika familia hii. Wadatoga wakati mwingine hujulikana kama Wamang’ati hasa kwa mujibu wa Wamasai. Mang’ati maana yake ni “adui” ingawa kwa sasa kwa ujumla halitumiki tena, na linasisitizwa lisitumike kabisa. Tunazungumzia Wadatoga.
Historia ya mradi wa Kidatoga imekuwa ndefu na ngumu sana. Lakini tunamshukuru Mungu kwa sababu ya siku hii maalum iliyosubiriwa kwa muda mrefu, sasa imefika.
Mnamo mwaka 1987 shirika la SIL lilitambua uhitaji wa Biblia kwa jamii ya Kidatoga.
Jambo hili lilipelekea kanisa la KKKT Dayosisi ya Mbulu kuwaalika shirika la SIL kuanzisha mradi wa tafsiri ya Biblia kwa Kidatoga. Shirika la SIL likaandaa timu wa tafsiri ambayo iliongozwa na John na Heidi McCauley. Baada ya kipindi kifupi karibu na mwishoni mwa mwaka 1989 John na Heidi McCauley wakabadilishwa na Ralph na Anette Schubert. Kutokana na mabadiliko haya SIL hawakupata msukumo wa kuendelea na mradi huu.
Baadaye, kanisa la KKKT Dayosisi ya Mbulu likakiomba Chama cha Biblia cha Tanzania kuwasaidia. Chama cha Biblia cha Tanzania hakikusita, kiliupokea mradi huu na kuusimamia.
Kwa msukumo na msimamo mkubwa wa aliyekuwa Katibu Mkuu wakati huo Hayati Mch. Albert Mongi alihakikisha kwamba jitihada hizi zinafanikiwa. Uzinduzi rasmi wa Mradi huu ulifanyika katika Hospitali ya Kilutheri ya Haydom, tarehe 14 Januari, 1990.
Timu ya Watafsiri ilikuwa na watumishi wafuatao – Mch. Elikana Gayewi, Mch. Festo Basso na Mch. Joseph Maho. Badaye, Mch. Gayewi aliicha timu lakini Pamoja na changamoto nyingi za kazi hii ngumu, Mch. Maho na Mch. Basso walistahimili na kung’ang’ana kuifanya. Hali kadhalika kwa jitihada za Dr. Isaac Malleyeck za kufanya kampeni kwa ajili ya mradi huu Pamoja na misaada mbali mbalimbali za aliyekuwa kiongozi wa Hospitali ya Haydom, Hayati Dr. Olson na familia yake ilikuwa muhimu sana kwa maendeleo ya mradi. Kwa msukumo mkubwa wa aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mbulu, Hayati Askofu Yoram Girgis aliyehimiza na kutamani kuona kwamba Wadatoga wanapata Biblia yao ilikuwa zana kubwa katika kusukuma mbele mafanikio ya mradi.
Tahajia (Arthography) ya lugha hii iliyoandaliwa kwa msaada wa Shirika la SIL iliweka msingi wa kazi liyoendelea. Hata hivyo, kabla ya kufikia mwisho wa kazi hii wafanyakazi wa Shirika la SIL wakajitoa. Ndipo baadaye, ikabadilishwa, ikarekebishwa na kukubaliwa.
Haikanushiki kwamba Tahajia itahitaji kuboreshwa siku zijazo
Kwa kweli, ari ya kutafsiri Agano Jipya ilianza tangu mwaka 1998 na kuendelea. Mnamo 2002 Agano Jipya likawa limekamilika. Kazi ya Agano la Kale ikafuatia mara moja. Injili ya Marko ilichapishwa kama Kitabu nakutolewa tayari kwa kusambazwa katika ibada ya uzinduzi iliyofanyika katika Kanisa la Kilutheri karibu na Ziwa Basotu tarehe 7 Julai, 2002. Nakala zote 2000 zilichapishwa na Chama cha Biblia cha Tanzania zilisambazwa mara moja.
Agano Jipya lilichapishwa mwaka 2009 na hatimaye kuwekwa wakf una kuzinduliwa katika sherehe iliyofanyika katika Kanisa la KKKT karibu na Ziwa Basotu mahali palipo na ofisi za Mradi.
Sherehe ile ya vifijo na furaha iliongozwa na Mkuu wa Kanisa la KKKT Dayosis ya Kati Singida Mhasham Askofu E. Sima kwa niaba ya Askofu Zebedayo wa KKKT Dayosis ya Mbulu.
Chama cha Biblia cha Tanzania kiliwakilishwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wakati huo Mch. Drk Mkunga Mtingele, Pamoja na watumishi kadhaa wa Chama wakiwemo – Alfred Kimonge, John Mnong’one, Mch. (Askofu) Julius Nyange na wengine. Mtaalamu wa Tafsiri kutoka Ofisi Vyama vya Biblia Ulimwenguni Prof. Aloo Osotsi Mojola pia alikuwepo pamoja na wageni wengine kutoka Chama cha Biblia cha Marekani na Ujumbe wa Kilutheri wa Norway.
Tukio la leo, ni kilele cha jitihada zilizoanza miaka mingi iliyopita. Hakika, leo ni siku ya kipekee isiyo na kifani na ya kihistoria. Hii ndiyo siku ambayo wamisionari walioweka misingi ya Kanisa kati ya Wadatoga bila shaka waliiota na kutama kuiona. Sisi tunaishuhudia leo na kwa kweli ni siku ya ajabu nay a kupendeza machoni petu. Jina la BWANA litukuzwe. Mioyo yetu imeja sifa na shukrani nyinge kwa Mungu wetu aliyetuwezesha kuiona siku hii.
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri hapa Mbulu na makanisa mengine yaliyoshiriki wanapaswa kusifiwa na kushukuriwa kwa kazi na jitihada uhudi zao za kuutangaza mradi hadi kufikia siku hii ya leo.
Watafsiri wa Kidatoga na hasa Mch. Joseph Maho, Mch. Festo Basso, Dr Isaack Malleyeck, familia ya Hayati Dr. Olson na Ujumbe wa Kilutheri wa Norway, Chama cha Biblia cha Tanzania Pamoja na watumishi wake, na hasa aliyekuwa Katibu Mkuu wakati huo Mch. Albert Mongi, Mch. Canon Dr. Mkunga Mtingele, Nd. Alfred Kimonge, Mch. (Askofu) Julius Nyange, Mch. Canon Prof. Aloo Osotsi Mojola, Pamoja na wote waliovujajsho kwa namna moja au nyingine kuona kwamba Biblia katika lugha ya Kidatoga – wanapongezwa sana kwa kazi ya upendo.
Sifa na Utukufu apewe Mungu wetu aliye Juu!
Imeandaliwa na Mch. Canon Prof. Aloo Osotsi Mojola. Mtaalamu wa Tafsiri Mstaafu wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni na ambaye kwa sasa ni Profesa wa Falsafa na Mitaala ya Tafsiri, Chuo Kikuu cha St. Paul, Limuru Kenya.
Kama ilivyosomwa kwetu katika Ibada hiyo ya Uzinduzi na Askofu Julius Nyange Meneja Mstaafu wa Tafsri katika Chama cha Biblia cha Tanzania.
Waheshimiwa Maaskofu, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia Cha Tanzania, Katibu Mkuu wa Chama Cha Biblia cha Tanzania, viongozi wa Makanisa na viongozi wa Serikali, waheshimiwa Mapadri, Makasisi na Wachungaji, akina baba na akina mama, ndugu wote katika Kristo Yesu na wageni wote waalikwa, mabibi na mabwana nawasalimu nyote katika jina tukufu la Yesu Kristo.
Leo ni siku ya shangwe, furaha, nderemo na vigelegele, kwa sababu ya tukio hili kubwa la kihistoria linalofanyika leo tarehe 27 Septemba, 2020. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Kanisa hapa Kilimanjaro Biblia ya kwanza katika lahaja au msemo wa Kivunjo-Chagga inazinduliwa na kutolewa rasmi na Kanisa kwa wakristo wote wanaoongea na kuelewa msemo huu.
Wamisionari wa Kilutheri, kikundi cha Leipzig, waliofika kwa mara ya kwanza maeneo haya ya Kilimanjaro Tanzania, miaka ya 1890, wakianzia pale Old Moshi, na baadaye Nkwarungo, Mamba, Shira, Mwika, Masama, Uswaa na Marangu; wakiwemo Emil Muller, Gerhard Althaus, Robert Fassman, Albin Boeme na Theodore Passler, bila shaka tukio la leo lilikuwa ndoto yao. Mmoja wao, mmisionari mwanaisimu na mwana-anthropolojia, Bruno Gutmann, aliyepewa jina “Wasahuye a Wachaka” alilipa kipaumbele suala la kuitafsri Biblia katika lugha ya Kichagga. Juhudi za wamisionari Bruno Gutmann, R Fassman pamoja na wazee wenyeji zilizaa matunda kwa machapisho yafuatayo, mnamo mwaka 1905 kitabu cha Injili ya Yohana kilipochapishwa, mwaka 1908 Barua ya Paulo kwa Warumi, mwaka 1911 Injili ya Mariko, na hatimaye mwaka 1939 Agano Jipya la kwanza katika Kichagga ilichapishwa. Kitabu hiki cha Agano Jipya kilichapishwa na Chama cha Biblia cha Wurttemberg, kule Stuttgart, Ujerumani. Toleo la pili lilichapishwa na Chama Cha Biblia cha Tanzania, Dodoma, mnamo 1999.
Kutafsiri Biblia nzima katika msemo wa Kivunjo kulianzishwa mwaka wa 1991 na Chama cha Biblia cha Tanzania chini ya uongozi wa Marehemu Mchungaji Albert Mongi, pamoja na Mshauri wa Tafsiri, Professor Aloo Osotsi Mojola wa United Bible Societies. Agano Jipya la kwanza katika msemo wa Kivunjo lilichapishwa na kutolewa, pale Marangu mnamo Novemba 6, 1999.
Miradi mitatu ya kutafsiri Biblia ya Kimochi, Biblia ya Kimachame na Biblia hii ya Kivunjo yote ilianzishwa mwaka huo huo wa 1991. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa zote zimekamilika karibu wakati mmoja.
Biblia ya Kivunjo ndio ya kwanza kuchapishwa na kutolewa; zingine zitafuata karibuni. Ningependa kuwashukuru Mchungaji John Mlay na Mchungaji Professor Godson Maanga ambao walijitolea pakubwa kukamilisha Biblia hii ya Kivunjo.
Siku ya leo, Septemba 27, 2020 Biblia Takatifu katika lahaja ya Kivunjo inazinduliwa na kuwekwa wakfu. Jina la Mwenyezi Mungu libarikiwe na kupewa sifa.
Hatuna budi kuwashukuru wale wote ambao wamechangia kwa hali na mali kufanikisha kazi hii takatifu na tukufu, wakiwemo wafuatao:
Marehemu Mchungaji Albert Mongi na viongozi wa Vunjo waliounga mkono juhudi hizi za kutafsiri Biblia katika msemo wa Kivunjo.
Wale wote waliohusika katika kuhakiki na kuchambua tafsiri yote ya Biblia hii.
Mtaalam wa kompyuta na mratibu wa kazi za kutafsiri pale Chama Cha Biblia cha Tanzania – Mchungaji (Askofu) Julius Nyange, pamoja na wafanyakazi wa Chama Cha Biblia, Dodoma ambao kwa njia moja au nyingine wamekuwa sehemu ya kazi hii kubwa.
Wataalam na washauri wa tafsiri ya Biblia waliowashauri watafsiri wa Biblia ya Kivunjo katika kukamilisha kazi yao.
Viongozi wa Makanisa walioombea kazi hii pamoja na kuwatembelea watafsiri na kuwatia moyo.
Mwisho, hatuwezi kuwasahau ninyi nyote – hasa walengwa wa Biblia hii, ambao mmefika hapa siku ya leo kushangilia na kupokea Biblia yenu.
Utukufu na sifa na ukuu kwa Mungu peke yake!
Asanteni sana.
(Imeandaliwa na Professor Aloo Osotsi Mojola, Professor of Philosophy and Translation Studies, Limuru, Kenya, Retired UBS Translation Consultant and former Africa Translation Coordinator, United Bible Societies. Worked with the Kivunjo translation team from 1991 till completion of project.)
KWENYE IBADA NA SHEREHE YA UZINDUZI WA BIBLIA YA KIVUNJO
TAREHE 27 SEPTEMBA 2020
Nawasalimu wote katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, na kipekee ninamsalimu Baba Askofu Fredrick Onael Shoo na wote waliongozana naye. Bwana Yesu apewe sifa.
Ninazungumza kwa ridhaa ya Baraza la Wakurugenzi wa Chama cha Biblia cha Tanzania ambao wanawakilisha Kanisa zima hapa nchini yaani madhehebu yote. Mwenyekiti wa Baraza hili kwa awamu hii ni Mhashamu Askofu Mark Walwa Malekana wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA).
Chama cha Biblia cha Tanzania ni mwanachama kamili katika Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (United Bible Societies-UBS). Kusudi la Muungano huu Ulimwenguni kote ni kutafsiri, kuchapisha, kueneza Neno la Mungu (Biblia) kwa lugha anayoweza kuilewa vizuri msomaji na kwa bei anayoiweza. Chama kinajitegemea lakini kinaheshimu mapatano na malengo ya Muungano huo. Vile vile kinazingatia malengo ya Kanisa katika Umisionari na Uinjilishaji. Makusudi ni kwamba Kanisa lijihusishe katika kukibeba, kukiombea, kuchangia gharama kwa njia ya sadaka maalumu na vile vile kuhimiza uenezaji na usomaji wa Maandiko Matakatifu.
Malengo hayo yanatokana na utume wa Bwana Yesu asemapo, “Basi, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu” (Math: 28: 19). Hivyo Chama kinafanya juhudi ya kuwapatia watu wote Neno la Mungu katika lugha zao bila nyongeza au kipunguzi katika maana, na kwa bei ambayo walengwa wataimudu.
Ili kutimiza lengo hili Chama cha Biblia, kinatafsiri Biblia au sehemu zake kutoka lugha za awali (Kieberania na Kiyunani) kwenda katika lugha lengwa na kisha kuchapisha na kueneza Neno kwa walengwa. Malengo haya yanafanyika kwa kushirikiana na Kanisa na vyombo vyake. Mara nyingi Kanisa ndilo linaona umuhimu wa kutafsiri na kukiomba Chama cha Biblia kifanye kazi hiyo ya kutafsiri. Kwa hiyo Chama cha Biblia ni mtumishi wa Kanisa. Ni nani anayestahili kupatiwa Neno la Mungu? Ingewezekana, kila mtu apatiwe Neno la Mungu katika lugha yake ili apate nafasi ya kuusikia ujumbe wa kwamba Yesu Kristo pekee ndiye njia, kweli na uzima: ndiye Mwokozi.
Binadamu wamegawanyika katika makundi mbalimbali na tofauti. Makundi hayo yanatambuliwa kama makabila yenye lugha maalum, mengine yana utaifa, mengine yanajitaja kwa njia ya koo, n.k. Ijapokuwa makundi hayo yanatambuliwa hivyo, kunakuwepo sababu nzuri kama za uzalendo zinazoyachukulia makundi hayo kwa pamoja kama ni kitu kimoja. Hata hivyo kama vile ukuta imara unavyotokana na matofali moja moja yaliyo imara, hivyo na watu wenye utambulisho wao wa pekee kwa pamoja wanajenga jamii/taifa imara. Watu wanaimarishwa na tofauti zao. “Katika tofauti zetu tunapata uimara” Katika Ufunuo wa Yesu Kristo (Ufu. 7:9-12) tunaona jinsi wakombolewa wote walivyo pamoja katika halaiki ya mwisho, ijapokuwa ziko tofauti dhahiri kati yao.
Umoja wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni unatambua na kuheshimu tofauti zilizopo baina ya makundi ya watu. Hivyo pale watu wanapofikishiwa Neno la Mungu na ikadhihirika kuna udhaifu wa kulisoma, basi hatua zinachukuliwa ili kulihimiza Kanisa liwawekee watu misingi ya kujua kuisoma na kuiandika lugha yao. Matokeo ni kwamba kwa kuijua lugha yake kwa kulisoma Neno la Mungu kunamuwezesha mtu kujifunza lugha nyingine. Hivyo kwa kushirikiana na Kanisa, tafsiri mpya za Biblia zinaambatana na juhudi za kuwafundisha watu wazima kwa wadogo, kuisoma Biblia yao. Juhudi hii imefanyika kwa Wasukuma, Wamaasai, Wanyakyusa, Wairaqw na Wachagga. Mikakati ipo kwa Wakaguru, Wagogo, Wahehe, Wadatooga na penginepo ambapo juhudi ya kutafsiri Biblia inaendelea.
Kwa makundi haya Chama cha Biblia kinachukua juhudi zote kuandaa na kuwafikishia watu Biblia iliyoandaliwa katika mifumo tofauti. Kwa mfano, Neno lililochapishwa –(“Printed Format”), Neno lililowekwa katika kanda-naswa – (Magnetic au digital cassette), Neno lililoingizwa kwa njia simulizi – (Audio-Aural-Visual Scriptures), Neno katika mifumo maalumu kama vile Braille kwa Wasioona, New Reader Scriptures kwa wasomaji wa awali, Neno katika mfumo wa Maandishi Makubwa kwa ajili ya Wazee na wengine wenye udhaifu wa macho, Neno katika Matoleo ya Watoto, Neno kwa njia ya Scripture Literacy Promotion, Neno katika Digital Bible Library.
Huduma hii ni kwa ajili ya Kanisa, ili liweze kutumia zana hizo katika kuyatunza makundi hayo yote ya watu walioko katika maeneo yao ya Umisheni.
Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni kutokana na tamko la pamoja imejiwekea Sera ya kutafsiri Biblia aidha kwa mara ya kwanza au kwa kuhariri upya iliyokuwapo, ili angalau ifikapo 2033 makundi au makabila yote;
Yanayofikia au kuzidi idadi ya watu 500,000 wapatiwe Biblia nzima.
Yanayofikia idadi ya watu 250,000 wapatiwe Agano Jipya.
Yanayofikia idadi ya watu 100,000 wapatiwe Kisehemu cha Biblia (Bible Portions).
Hapa Tanzania tumekamilisha tafsiri 43 kati ya lugha 132 kazi inaendelea.
Ieleweke kwamba tafsiri ikianza tu, lengo ni kuikamilisha Biblia nzima hata kama idadi ya wazungumzaji ni ndogo ili asiwepo mtu atakayesema “nimekosa nafasi katika ufalme wake Yesu Kristo kwa kuwa Neno lake halikupatikana katika lugha yangu”
Makanisa kwa kushirikiana ndiyo yanayoomba kuanzisha na hatimaye kukamilisha tafsiri ili kila mtu awe na Biblia yake katika lugha anayoichagua na kuielewa.
Hizi lugha ambazo ni kitambulisho cha kila mtu na lugha yake, zinakabiliwa na changamoto kadhaa, kwa mfano;
Kutotiliwa maanani na kupewa kipaumbele na baadhi ya mamlaka tawala na Makanisa.
Lugha ya utawala (kama vile Kiingereza, Kiswahili, n.k) inagandamiza lugha nyingine na kuashiria kuitoa.
Neno la Mungu linadumu milele. Kwa hiyo lugha ambayo inalizungumzia Neno la Mungu inadumishwa. Ni wajibu wa Kanisa kuhakikisha Biblia inayozinduliwa inatumika katika ibada zao.
Hapa Tanzania kuna makundi/makabila ya lugha hai 132. Hadi sasa kuanzia 1846 hadi 2020 Chama cha Biblia, kwa kushirikiana na Kanisa tumetafsiri Neno la Mungu katika makabila yafuatayo;
Sehemu
Agano Jipya
Biblia
1.
Swahili Southern
1846
2.
Swahili (SUV)
1952
3.
Swahili (CL)
1996
4.
Wajita
1920
1930
5.
Wakuria
1969
1996
6.
Wamasai
1905
1923
1992
7.
Wadatooga
2002
2009
2020
8.
WaIraqw
1957
1977
2003
9.
Kivunjo
1966
1999
2020
10.
Machame
1932
1999
11.
Kimochi
1892
1999
12.
Wanyakyusa
1895
1908
1996
11.
Wahaya
1920
1930
2001
13.
Wasukuma
1895
1925/2001
1960/2020
14.
Wakuria
1969
1996
15.
Wameru
1964
16.
Chasu/Pare
1910
1922
17.
Kihehe
1999
18.
Kibena
1914
19.
Cigogo
1886
1899
2002
20.
Kidatooga
2009
2020
21.
Kiluo
1953
22.
Kinyamwanga
1982
23.
Chiyao
1920
24.
Kimambwe
1901
25.
Kilungu
1901
26.
Kishambala
1908
27.
Kinyamwezi
1951
28.
Kitaveta
1949
29.
Kinyiha
1950
30.
Kinyiramba
2010
31.
Kirimi
2010
32.
Kikerewe
1946
33.
Kikinga
1961
34.
Kizaramo
1975
35.
Kifipa
1988
36.
Kikaguru
2010
37.
Kibondei
1887
38.
Kingoni
1891
39.
Kizigua
1906
40.
Kimpoto
1913
41.
Kizinza
1930
42.
Kihangaza
1938
43.
Kiha
1960
44.
Kiwanji
1985
45.
Kizanaki
1948
Kazi bado ni kubwa, Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na Kanisa, kinayo mikakati ya kuwafikishia Neno la Mungu makundi/makabila yaliyobaki. Rai yetu kwa Kanisa tunaomba Biblia hii itumike katika ibada ili kazi hii iliyofanyika kwa miaka mingi na kwa gharama kubwa isiwe ya bure.
Leo tumekamilisha jitihada katika lugha ya Kivunjo kwa kuwakamilishia Biblia: Mungu anena na Wavunjo katika ukamilifu wa Biblia ya Kivunjo. Ni matumaini yetu kwamba Injili ya Wokovu katika Yesu Kristo itawafikia katika lugha yao ya moyoni na kusema sasa nimetambua Mungu anasema nami kwa lugha yangu.
Kwa njia ya tafsiri hii ya Biblia, Wavunjo nao watamsikia Bwana Yesu kwa ukaribu wa moyoni ili wapate fursa ya kushiriki katika halaiki ya mwisho “ Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha (Kivunjo)…” (Ufu. 7: 9-12).
I say unto you, that likewise joy shall be in heaven over one sinner that repenteth, more than over ninety and nine just persons, which need no repentance.