KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA BIBLIA MKOANI DODOMA

KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA BIBLIA MKOANI DODOMA

KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA BIBLIA MKOANI DODOMA

11
20241103 155004 scaled

Dodoma, 03 Novemba 2024 – Maadhimisho ya kilele cha Juma la Biblia mwaka huu yamefanyika kwa mafanikio makubwa mkoani Dodoma, katika Uwanja wa Mashujaa. Maadhimisho hayo yaliyoanza na maandamano ya amani kutoka makao makuu ya Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) hadi viwanja vya zamani vya Mashujaa, yalivutia umati wa wanachama na wadau mbalimbali. Maandamano hayo yalipambwa na bendi ya tarumbeta na kwaya ya wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), huku wanachama wakivalia tisheti zilizo na nembo ya CBT na kauli mbiu ya mwaka huu: “Neno la Mungu, Maadili Yetu.”

Mgeni rasmi katika sherehe hizo alikuwa Askofu Amos Muhagachi, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa CBT, akiwa ameambatana na viongozi wengine wakuu wa Chama akiwemo Katibu Mkuu wa CBT, Dkt. Alfred Elias Kimonge, na Mkurugenzi wa CBT, Dkt. Anna Solo. Pia, sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi wa makanisa, wanachama wa CBT, na wanafunzi wa UDOM.

1
4
20241103 174033

Katika hotuba yake mgeni rasmi Askofu Amos Muhagachi alisoma Neno la Mungu kutoka Zaburi 119:105, “Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu,” akisisitiza umuhimu wa Neno la Mungu kama msingi wa maadili. Alisema, “Biblia ni kitabu kinachotuunganisha sisi Wakristo na kinatuonyesha maisha ya mwanadamu, ukombozi, na umilele wake.” Pia alihimiza mpango mkubwa wa maadhimisho mwaka ujao, kwa kushirikiana zaidi ili kufikia wadau wengi.

Askofu MuhagachiGS Maandamano

Katika hotuba yake, Katibu Mkuu Dkt. Kimonge aliwashukuru wanachama na wadau wote waliojitolea kushiriki Juma la Biblia lililoanza tarehe 28 Oktoba na kumalizika leo 03 Novemba. Dkt. Kimonge alieleza kwamba lengo kuu la CBT ni kutafsiri, kuchapisha, na kusambaza Biblia kwa watu wote, wakiwemo Wakristo na wasio Wakristo. Alihimiza umoja katika kuchangia kazi hii muhimu, hasa kwa makundi yasiyo na uwezo wa kununua Biblia, kama vile wafungwa na vijana.

20241103 162244 scaled
6

Katika kuelezea historia ya CBT, Dkt. Kimonge alitaja hadithi ya binti Maria Jones, mwenye umri wa miaka kumi na tano, aliyekuwa mkulima wa Wales. Kiu yake ya kumiliki Biblia ilichochea harakati za kuanzisha vyama vya Biblia, ambavyo leo vinafanya kazi katika nchi zaidi ya 160, kusambaza mamilioni ya Biblia na maandiko mengine katika lugha zaidi ya 15,000.

20241103 161423 scaled
20241103 161436 scaled

Maadhimisho hayo yamehitimishwa kwa maneno ya shukrani kutoka kwa Meneja wa Mahusiano na Makanisa, Mch. Samweli Mshana, aliyewapongeza viongozi wote kwa kufanikisha Juma la Biblia kwa ufanisi. “Shukrani kwa viongozi wetu na wanachama wote wa CBT kwa kazi kubwa mliyofanya. Mungu awabariki sana,” alisema Mch. Mshana.

20241103 154856 scaled
3

Maadhimisho ya Juma la Biblia yanaendelea kuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha ushirikiano kati ya waumini, wadau, na jamii kwa ujumla kupitia Neno la Mungu, na CBT inaahidi kuendelea na jitihada hizi kwa ustawi wa kiroho wa Watanzania.

2

Comments

MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

1. UTANGULIZI.

Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) ni shirika la Kikristo lililoandikishwa mwaka 1970 na kupewa nambari S0 5722. Ni mwanachama wa Muungano waVyama vya Biblia Ulimwenguni(United Bible Societies (UBS). Shirika hili ni chombo cha Kanisa la Tanzania ambalo kazi yake kubwa na ya msingi ni kuwapelekea watu wote hapa nchini Tanzania Habari njema ya Yesu Kristo kwa kutafsiri, kuchapisha na kusambaza Biblia ikiwa katika lugha anayoielewa msomaji, bei anayoiweza na mfumo anaoupendelea.

MG 6293 copy scaled

Tangu kusajiliwa kwake  hapo mwaka 1970, Chama cha Biblia cha Tanzania kimekuwa kikitekeleza majukumu yake hayo kwa ushirikiano mkubwa na wa karibu na makanisa yote ya Kiprotestanti, Katoliki, Sabato na Kipentekoste hapa Tanzania; na pia kwa ushirikiano mkubwa na wa karibu na Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (United Bible Societies-UBS) ambalo ni ushirika wa vyama vyote vya Biblia katika nchi zote.

Chama kimeweza kufanya tafsiri na kinaendelea kutafsiri Biblia katika lugha mbalimbali za makabila ya hapa Tanzania. Kutafsiri Biblia katika lugha mbalmbali za makabila kunafanyika kwa malengo makuu mawili. Lengo la kwanza la kufanya tafsiri hizi ni kwa kuamani kuwa watu wanaweza kulielewa Neno la Mungu kwa urahisi zaidi wakisoma au kuelezwa katika lugha zao na kuainisha na mazingira halisi ya mazingira yao.

IMG 9715

Lengo la pili ni kusaidia kutunza lugha za makabila kwa faida ya vizazi vijavyo vya kabila husika, kwani mila na utamaduni wa kabila zipo katika lugha ya watu wa kabila husika. Tangu kuanzishwa kwake Chama cha Biblia kimefanya tafsiri kadha na kuzisambaza hapa nchini zikiwamo Biblia katika lugha za:

  1. Kiswahili
  2. Kimaasai,
  3. Cigogo
  4. Iraqw

5. Nyakyusa

6. Igikuria

7. Ruhaya

8. Kisukuma

9. Kidatooga

10. Kimashami

11. Kivunjo

12. Kimochi

Baadhi ya Biblia ambazo kwa sasa zipo katika hatua mbalimbali za tafsiri ni:

  1. Kihehe
  2.   Cikaguru
  3.   Kinyamwezi
  4.   Chasu(Kipare)

5.  Kifipa

6. Kinyiha

7. Kinyiramba

8. Kirimi( Kinyaturu)

9. Kiha

Agano Jipya.

  1. Kimeru
  2. Kibena
  3. Kishambala
  4. Kikinga

5. Kijita

6. Kifipa

7. Kizaramo

2.0 Umuhimu wa Neno la Mungu kwa maendeleo

Tunapoangalia historia ya ustawi wa maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ulimwenguni kote, tunaona kuwa jamii ambazo zilijengwa katika misingi ya Neno la Mungu zilistawi kimaendeleo ikilinganishwa na zile ambazo ama hazikuamini au zilimuasi Mungu. Neno la Mungu likiwa ndani ya myoyo ya watu huzaa upendo ambao huzifanya jamii kuwa zenye amani na utangamano, tunu ambazo husaidia kuweka mazingira wezeshi kwa watu kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo.

36 1 scaled

2.1 Hali ya malezi kwa watoto na vijana.

Hivi sasa nchi nyingi ulimwenguni ikiwemo Tanzania kuna mporomoko mkubwa wa maadili. Wazazi ndani ya jamii wanalalamika juu ya watoto wa kizazi hiki kuwa wamekosa maadili.

Lakini wazazi hawa wanasahau kuwa kuporomoka kwa maadili ya watoto wao kunatokana na wao kutokuwalea katika misingi mizuri ambayo ni Neno la Mungu. Huko Ulaya na Marekani wazazi/mataifa walibweteka na maendeleo ya kiuchumi, teknolojia, sayansi na maisha bora kimwili na kusahau tunu kubwa inayotokana na maendeleo ya kiroho(spirituality). Makuzi ya kiroho hujenga maadili na hivyo kujenga utu wa mtu.

Katika nchi hizi watu wengi hasa kundi la vijana sasa hivi hawaendi Kanisani au Misikitini Kuabudu. Wamejitenga kabisa na Mungu na katika baadhi ya nchi Makanisa yameuzwa na kutumika kwa shughuli nyingine kabisa kama vile maduka na hata pia kugeuzwa kuwa sehemu za burudani kama vile sehemu za kuuzia vileo na starehe zingine.

Aidha katika nchi  hizi tunashuhudia ongezeko kubwa la mporomoko wa maadili ya asili ya mwanadamu. Katika nchi hizi sasa tunashuhudia uhalalishwaji kisheria wa ndoa na mapenzi ya watu wa jinsia moja, ongezeko la vitendo  vingine viovu ambavyo ni chukizo mbele za Mungu. 

Nchi za kiafrika nazo hazijasalimika na hali hiyo. Mporomoko mkubwa wa maadili katika nchi za Afika unazidi kuongezeka na kushamiri kutokana na utandawazi. Nchi zetu sasa zinashuhudia ongezeko kubwa la vitendo viovu kila siku,vingi vikifanywa na kundi la vijana. Wazazi walio wengi wameacha wajibu wao wa asili wa kuwalea watoto wao na kuwarithisha maadili ambayo huleta ustawi wa mtu mmoja mmoja na jamii/taifa.

Wazazi wengi hawaendi na watoto wao Makanisani na Misikitini wala hawaoni umuhimu wa watoto wao kupata mafundisho ya dini tangu wakiwa watoto ili wakue na kustawi katika msingi wa Neno la Mungu. Maovu mengi tunayoyashuhudia katika jamii ni kutokana na watu kukosa msingi wa Neno la Mungu ambalo likikaa katika myoyo huwafanya watu kuwa na  hofu ya Mungu na hofu hiyo huwafanya wajiepusha na matendo maovu kwa kujua kwamba hayampendezi Mungu na yana hukumu.

Hivi sasa tunashuhudia hofu ya Mungu ikizidi kupungua katika nchi yetu, na hivyo kutishia amani na utangamano katika taifa letu. Vitendo viovu vinaongezeka kwa kasi katika taifa letu kwa sababu watu wamekosa hofu ya Mungu.

Rais wetu mpendwa wa awamu ya Tano Marehemu Mheshimiwa John Joseph Pombe Magufuli amekuwa akituasa mara nyingi kwamba tumwogope Mungu, maana yake tufanye yale yanayompendeza Mungu na tuache matendo maovu. Matendo mema huleta afya kwa jamii/taifa lolote.

20211222 050907 scaled

2.2 Kwa nini Biblia kwa Watoto, Vijana na Wafungwa?

Katika nchi nyingi duniani na hasa nchi zinazoendelea  watoto umri kati ya miaka 1-14 huwa ni rika yenye watu wengi zaidi, wakifuatiwa kwa wingi na kundi la vijana(miaka 15-24).

Makundi haya mawili haya kwa pamoja hapa Tanzania idadi yake ni zaidi ya asilimia 60 ya idadi ya watu wote. Kutokana na wingi na umri,  makundi haya yanayohitaji kuangaliwa /kutazamwa kwa karibu sana kwa maana ya malezi kwa maana ya kupewa huduma muhimu zitakazowafanya wakue na kustawi kiroho na kuwa raia wema wenye kupenda amani na  ustawi wa taifa.

Wafungwa ni kundi la watu ambao wako gerezani kwa sababu ya kutenda makosa katika jamii na kukosesha wengine amani na utangamano. Kwahiyo, hili nalo ni kundi muhimu la kutazamwa katika malezi hasa ya kiroho ili wahusika (wafungwa) wanapomaliza kutumikia  vifungo vyao waweze kuacha tabia mbaya za uhalifu na kuwa raia wema.

IMG 8365 scaled

2.3 Mapendekezo ya  na ushauri wa Chama cha Biblia kwa serikali katika kukabiliana na mporomoko wa maadili kwa wototo na vijana.

Chama cha Biblia cha Tanzania kinaishukuru sana Serikali yetu kwa kuruhusu Neno la Mungu kufundishwa mashuleni, jambo ambalo nchi zingine haziruhusu. Tunaamini hatua hii ni kwa kutambua kwamba mashuleni ndiko wanapoandaliwa viongozi wa taifa la kesho, kwa hiyo kuona umuhimu wa kuwapa malezi ya kiroho. 

Tunakumbuka miaka ya nyuma serikali iliruhusu uanzishwaji wa chama cha “ Elimu ya Dini Mashuleni Tanzania”(EDIMASHUTA) ikiwa ni njia mojawapo ya kutoa fursa kwa watoto ya kupata mafundisho ya dini ili waweze kukua kimaadili kupitia dini zao. Hii ilikuwa ni fursa muhimu sana kwa wototo kujifunza somo la dini na hivyo kukua na kustawi katika misingi ya kuwa na hofu ya Mungu.

Chama cha Biblia cha Tanzania kilikuwa mshirika mkubwa katika mpango wa Elimu mashuleni kwa kutoa Biblia  zilizotumiwa kama kitabu cha kiada mashuleni katika mafundisho hayo. Katika mpango huu, serikali ililifanya somo la dini kuwa la kutahiniwa na ilikuwa na “alama” (credit).

Kutokana na utambuzi huo vijana mashuleni walikuwa na bidii ya kujifunza somo la dini. Kwa njia hiyo waliweza kujengwa vizuri kiimani, kimaadili na kiustawi kwa ujumla na kundi hilo lilizaa viongozi waadilifu wa nchi yetu, kanisa na sekta binafsi.

Hata hivyo baadaye utaratibu wa  somo la dini kuwa  la kutahiniwa na lenye hadhi ya credit sawa na masomo mengine uliondolewa na hivyo kuwavunja moyo watoto na vijana katika kujifunza somo la dini.

Tunapendekeza kwamba somo la dini liendelee kufundishwa na lipewe hadhi/lihesabiwe sawa na masomo mengine katika mitihani, ili liweze kuchochea ari kwa watoto na vijana kujifunza somo la dini na hivyo kujengwa kimaadili.

20220713 140251 scaled

2.4 Kwa nini Biblia sasa kwa vijana mashuleni.

Kwa kuangalia mwenendo wa maadili kwa vijana wetu mashuleni,na kuna umuhimu wa kurejesha somo hilo kwani umuhimu wake umeanza kuonekana. Kumekuwa na  mmomonyoko wa maadili kwa vijana wetu sasa, tofauti na kipindi cha nyuma ambapo walilelewa katika misingi ya neno la Mungu.

Sasa hivi tunashuhudia vitendo viovu vikiongezeka katika jamii, ambapo watoto na vijana wanahusika. Jambo la pili tunaona mifano  ya wenzetu nchi za Ulaya ambako utandawazi umewafanya wasitambue  utu wa mtu.

Baadhi ya shule ambazo zimeendelea kufundisha somo la dini ni ushuhuda tosha kuonyesha namna somo la dini lilivyo muhimu katika ustawi wa mwanadamu. Shule hizi zimekuwa mfano mzuri kwa maadili na ufaulu mzuri  wa masomo hata yasiyo ya dini.

Chama cha Biblia kinaona kwamba kuna umuhimu wa kurudisha somo la dini kwa shule zote za serikali na za binafsi na kulifanya somo la dini kuwa na hadhi ya kutahiniwa sawa na masomo mengine.

Hiyo ni shule ya RUHUWIKO High School Songea wakifurahia kupewa Maandiko toka Chama cha Biblia. Wametoa shukrani nyingi kwa Uongozi kupitia mwl wao

3.0 Mpango wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa kuwapatia Biblia Watoto na Vijana mashuleni na Wafungwa magerezani.

Kwa kutambua umuhimu huo, Chama cha Biblia cha Tanzania katika mpango mkakati wa miaka mitano (2018 – 2022) kilianzisha mpango maalum wa kuhamasisha Makanisa na watu wenye mapenzi mema kushiriki kwa kuchangia fedha kwa ajili ya upatikanaji wa Biblia ili  zisambazwe kwa wingi  kwa watoto, vijana na wafungwa ikiwa ni moja ya vipau mbele vyake katika kipindi hiki cha miaka mitano.

Mpango huu unalenga makundi matatu ya watoto na vijana kwa rika na wafungwa walioko magerezani.

Na.

Watoto

Vijana

Wafungwa magerezani

 1.

Miaka 3 – 5

Miaka 16 – 24

Wanaume

 2.

Miaka 6 – 9

 

Wanawake

 3.

Miaka 10 -15

 

 

Katika mkakati wa kutekeleza mpango huu Chama cha Biblia cha Tanzania kilianza kwa kuwashirikisha viongozi wa makanisa kutokana na nafasi yao ya asili ya kuwajenga na kuwalea watu kiroho.

Pili kimewashirikisha wadau wengine wenye mapenzi mema wanaotamani kuona Tanzania inajengwa katika misingi imara ya kiroho na hivyo kuwa na taifa lenye watu wenye hofu ya Mungu.

Mpango huu umepata uungwaji mkono mkubwa sana na Kanisa la Tanzania, hali ambayo imetutia moyo sana Chama cha Biblia cha Tanzania, kwani tunatambua kwamba Kanisani ndiko Neno la Mungu linafundishwa na ndiko Wakristo wanaofanya Kanisa la Tanzania waliko.

Tunaamini mpango huu unatekelezeka na walengwa na taifa zima litanufaika.

21

3.1 Watoto na Vijana walengwa.

Mpango huu katika awamu hii ya kwanza unalenga watoto na vijana walioko katika shule kwa sababu ya urahisi wa kujua idadi yao na urahisi wa kuwafikia.

Hata hivyo shule zitazopewa kipaumbele ni zile zilizoko vijijini, ambazo mbali kuwa  nyingi, lakini ndizo zenye watoto na vijana wengi wenye wazazi wenye hali duni ya  uchumi; na hivyo hawana uwezo wa kuwapata/kuwanunulia watoto  mahitaji yao kwa utoshelevu.

Ni kutokana na ukweli huo Chama cha Biblia cha Tanzania kinalenga kuwapatia watoto na vijana Biblia kwa bei nafuu ambayo wazazi wengi pamoja na hali yao duni kiuchumi wanaweza kuimudu.

ugawaji wa Sehemu ya Biblia Agano Jipya lenye Mithali na Zaburi

3:2 Ufundishaji wa somo la dini  mashuleni.

Kama tulivyoeleza katika utangulizi, Chama cha Biblia kinaona kwamba kuna umuhimu wa kurudisha somo la dini kwa shule zote za serikali na za binafsi na kulifanya somo la dini kuwa na hadhi ya kutahiniwa sawa na masomo mengine.

Tunaishauri serikali irudishe na  kuimarisha Elimu ya Dini Mashuleni( EDIMASHUTA) na kurudisha mitaala iliyokuwepo pamoja na kuruhusu taasisi za dini  kupeleka waalimu kwa ajili ya kufundisha somo la dini.

 Mpango huu ukitekelezwa utasaidia kuwajengea watoto wetu misingi ya maadili mema ili hatimaye tuwe na taifa lenye viongozi na raia wema. Jambo hili litasaidia kujenga jamii yenye amani na utangamano na kuruhusu mazingira ya kupata ustawi kama taifa.

Picha ya watoto wanasoma Biblia. 1

3:3 Vyanzo vya upatikanaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huu

 Katika mpango huu, Chama cha Biblia cha Tanzania kinalenga kupata fedha kutoka:

  • Taasisi za kanisa
  • Mashirika mbalimbali
  • Watu binafsi

 Aidha Chama katika nia hii njema kinaomba kuungwa mkono na serikali kwa kushiriki katika kazi ya kuhamasisha taasisi, mashirika na wadau mbalimbali ili waweze kushiriki kuchangia mpango huu.

IMG 9767

3.4 Kiasi cha fedha, idadi  ya  Biblia na mgawanyo kwa makundi lengwa

Katika awamu hii ya kwanza Chama cha Biblia kimelenga kuomba kuchangiwa kiasi cha shilingi 10,200,000,000 ambazo zitatumika kununulia jumla ya Biblia 510,000 ambazo mgao wake kwa makundi lengwa utakuwa kama ifuatavyo:

  • Watoto – Biblia laki nne (400,000)
  • Vijana – Biblia laki moja (100,000)
  • Wafungwa – Biblia elfu kumi (10,000)

Kwa sasa Chama tayari kinayo miswada ya Biblia za makundi lengwa  yote yaani watoto, vijana na wafungwa. Biblia hizi zinaweza kuchapishwa na wachapishaji wakati wowote fedha zitakapokuwa zimepatikana.

Malipo yakishafanyika inakadiriwa kuwa kazi ya kuchapa, kusafirisha na kupokelewa inachukua muda wa miezi mitatu hadi minne.

20220721 115109 scaled

3:5 Mikoa na mgao wa Biblia kwa makundi lengwa.

Zoezi hili ni endelevu, lakini katika awamu hii ya kwanza Chama kimelenga kugawa Biblia kwa watoto, vijana na wafungwa katika  mikoa ifuatayo :-

 

Na

Mkoa

Watoto

Vijana

Wafungwa

 

Makisio

Halisi

Makisio

Halisi

Halisi

1.

Dodoma

730,000

100,000

180,000

25,000

3,000

2,

Mara

580,000

82,000

145,000

20,500

3,000

3.

Manyara

610,000

88,000

152,500

21,500

1,000

4.

Pwani

470,000

66,000

117,500

16,500

1,000

5.

Singida

470,000

66,000

117,500

16,500

2,000

Jumla kuu

2,860,000

400,000

712,500

100,000

10,000

IMG 20220722 WA0016

3:6 Usambazaji wa Biblia kwa makundi lengwa.

3:6:1 Mashule

Biblia zitasambazwa na Chama cha Biblia katika mashule kwa kushirikiana na Maafisa Elimu, Waalimu Wakuu wa  Mashule, Viongozi wa Makanisa na Waalimu wa Dini mashuleni.

3:6:2 Magereza

Biblia zitasambazwa katika Magereza kwa kushirikiana na Wakuu wa Magereza na Wachungaji wanaotoa huduma ya kiroho magerezani.

Gereza la Mahabusu Songea 2022 07 17

4: 0 MWISHO

Mpango huu una umuhimu wa kipekee katika kipindi hiki ambacho tunashudumia mmomonyoko wa maadili ukienda kasi katika jamiii yetu hasa kwa kundi la watoto na vijana ambalo linatarajia kutoa viongozi wa baadae wa taifa letu.

Tunaomba serikali ituunge mkono katika nia hii njema ya kuwajenga watoto, vijana na wafungwa kiroho. Faida ni kubwa kwa afya ya taifa. Kuchukua hatua sasa ni vizuri.

ABOUT US

Addresses

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

Phone

+255 (0) 765 530 892

Email

info@biblesociety-tanzania.org

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

 

ZIARA KATIKA MAGEREZA YA MSALATO NA KONGWA DODOMA

Moja kati ya wajibu muhimu kwa Chama cha Biblia cha Tanzania ni kuhakikisha kuwa watu wote wanapata fursa ya kupata maandiko matakatifu. Kutokana na jukukumu hilo tarehe 27/11/2018 watumishi wa Idara ya Mahusiano na baadhi ya Wale wa Mawasiliano, walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Msalato Dodoma na kugawa Biblia, Sabuni na dawa ya meno kwa Wafungwa wa gereza hilo la Msalato. Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji akishirikiana na Msaidizi wake na Maafande wengine walitupokea vizuri sana na kutupa ushirikiano wa hali ya juu.

 

 

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, viongozi wa kanisa la KKKT Dodoma na viongozi wa gereza la Msalato

 

Jukumu la kugawa Biblia halikuishia Gereza la Msalato tu kwani Tarehe 28/11/2018 Meneja Mahusiano na kikosi kazi chake walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Kongwa Dodoma. Katika Gereza hili tulipokelewa vizuri sana na kupewa maelezo ya jinsi Wafungwa wanavyohitaji msaada wa Maandiko na vifaa vingne kwani wanatakiwa kjujitegemea.Chama cha Biblia tulifaulu kugawa Maandiko Matakatifu,sabuni, dawa ya Meno na Taulo za akina Mama.Mkuu wa Gereza Afande Nyonyi alishuru sana Chama cha Biblia cha Tanzania kwa msaada huo kwa Wafungwa.

 

 

 

 

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Kongwa Afande Nyonyi

 

 

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, mkuu wa jimbo wa kanisa la KKKT Kongwa (wa kwanza kulia) na viongozi wa gereza la Kongwa

 

Kuhamasisha Makanisa

Kuhamasisha Makanisa

Kukutana na Mwl. MwakasegeKazi ya kuamasisha makanisa na viongozi wa dini katika madhehebu mbali mbali ya Kikristo hapa nchini juu ya umuhimu wa kuwapatia watoto, vijana na wafungwa Neno la Mungu (Biblia), inaendelea katika Kanda ya kaskazini.

Na leo wajumbe wa Bodi wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Baba Askofu Amos Muhagachi na Mama Engineer Elikael Manase pamoja na Meneja wa Mahausino na Makanisa na Utunishaji mfuko wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Mch. Samweli Mshana wamemtembelea Mwl. Christopher Mwakasege ofisini kwake.

Bodi MembersMwl. Mwakasege 5

Tuzidi kuwaombea kwa kazi hii inayofanyika ili tujenge taifa lenye maadili mema.🙏

“MPATIE MTOTO, MFUNGWA NA KIJANA NENO LA MUNGU”

(ZABURI 119: 105; “Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na Mwanga wa njia yangu.”)

Wafungwa, Mahabusu Dar wakabidhiwa Biblia Takatifu

Wafungwa, Mahabusu Dar wakabidhiwa Biblia Takatifu

IMG 20200831 WA0009Na Dalphina Rubyema

WAKATI Chama cha Biblia cha Tanzania kikiwa kimetoa msaada wa Biblia Takatifu kwa wafungwa na mahabusu ya Magereza ya Segerea, Ukonga na Keko yote ya jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Gereza la Segerea, SSP. Daniel Mwakyoma amesema ukosefu wa uzio na upungufu wa nyumba za watumishi ni miongoni mwa changamoto zinazolikabili gereza hilo.

IMG 20200829 WA0013

Makabidhiano ya msaada huo upande wa Gereza la Segerea yamefanyika mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Arch. Ng’wilabuzu Ludigija na Maafisa Waandamizi wa gereza hilo, huku upande wa Chama cha Biblia kikiwakilishwa na wajumbe mbalimbali akiwemo Katibu wa Chama hicho, Mch. Alfred Kimonge, Meneja wa Mahusiano ya Makanisa na Utunishaji wa mfuko wa chama hicho, Mch.Samwel Mshana huku Kanisa Katoliki likiwakilishwa na Mjumbe wa Bodi wa Chama hicho hicho, Padri Chesco Msaga, CPP.S ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo ulioenda sambamba na utoaji wa mahitaji ya kimwili kwa wafungwa na mahabusu hao, unaojumuisha sabauni na dawa ya meno, Katibu wa Chama hicho, Mch. Kimonge amesema, lengo ni kuwapa wahusika fursa ya kusoma Neno la Mungu, linalobadilisha, na kutia faraja, msaada uliopokelewa kwa furaha na wahusika.

“Chama cha Biblia Tanzania ambacho kinajumuisha wanachama kutoka madehebu ya Waprotestanti, Wasabato, Wapentekoste na Wakatoliki, kinaguswa na maisha ya makundi mbalimbali wakiwemo mahabusu na wafungwa kama nyie, hivyo Biblia hizi tunazokabidhi kwenu tunaomba ziwasaidie kufanyie rejea yale mnayohubiriwa…zinafaa hata kwa wale wasiokuwa Wakristo,” amesisitiza.

IMG 20200829 WA0015

Msaada huo umeenda sambamba na ziara maalum ya Mkuu mpya wa Wilaya ya Ilala, Arch, Ng’wilabuzu Ludigija kutembela magereza yaliyopo wilayani kwake ya Segerea na Ukonga, kama sehehemu ya kujitambulisha.

Katika ziara hiyo Mkuu huyo wa Wilaya na wajumbe wa Chama cha Biblia, walipata fursa na kuzungumza na uongozi wa gereza hilo pamoja na kukutana na mahabusu na wafungwa, wakiwemo wanawake na wanaume ambapo waliwasilisha changamoto zao.

Upande wake SSP Mwakoyoma amesema ngome (gereza), haijazungushiwa uzio, hali inayosababisha hali ya usalama kuwa hatarini, hali inayoenda sambamba na ukosefu wa nyumba za watumishi kiasi cha kusababisha asilimi 90 kuishi uraiani nje ya kituo chao cha kazi.

Changamoto nyingine kama zilivyobainishwa na Mkuu huyo wa Gereza ni ukosefu wa huduma ya usafiri kwa mahabusu pindi wanapotakiwa kupelekwa mahakamani kusikiliza kesi zao, uhaba wa maji na kutokuwa na jenereta (standby generator) pindi umeme unapokatika, jambo ambalo ni hatari kwa jumuiya yenye msongamano wa watu kwani pia kuna mlundikano wa mahabusu.

Akitoa kero zinazowakabili wafungwa na mahabusu wanawake, nyampala wa kundi hilo, (jina tunalihifadhi) amesema miongoni mwa changamoto wanazokabiliana nazo ni baadhi ya watuhumiwa kuchanganyikiwa kiakili, hali inayosababishwa na masuala mbalimbali likiwemo la kesi zao kutokusikilizwa kwa wakati, jambo ambalo amesema ni hatari kwa wafungwa na mahabusu wengine.

IMG 20200829 WA0012

“Kuathirika kisaikolojia… anapiga mahabusu wenzake na anaweza hata kuwafanyia vitendo vingine vya kikatili zaidi, hivyo tunaomba hili liangaliwe na kufikishwa kunakostahili ili ikiwezekana hata wafanyiwe vipimo vya kitaalam zaidi na ikibainika ni shida, basi wapelekwe kwenye magereza yaliyotengwa kwa watu wa namna hii,” amesema.

Changamoto nyingine kwa wanawake ni uhaba wa magodoro hali inayowalazimu baadhi yao kulala chini kwenye sakafu, uhaba wa sare kwa wale ambao tayari wameshahukumiwa, lishe duni kwa watoto wanaoishi na mama zao gerezani pamoja na uhaba wa maji na vifaa vya usafi vya kutosha hali inayosababisha wengi kupata ugonjwa wa UTI.IMG 20200829 WA0016

Asia Mhamed ambaye ni mahabusu Na.125/2016 yeye amesema changamoto zaidi ipo kwa watuhumiwa wa kesi za mauaji, utakatishaji pesa na dawa za kulevya, ambapo amedai zimekuwa hazikilizwi kwa kile wanachoambiwa na mahakimu na majaji wanaosikiliza kesi hizo kuwa wanaendelea na upepelezi na hata wakati mwingine kudai kwamba kesi hizo uendeshaji wake unahitaji hela ambayo lazima iwe imetengwa kwenye bajeti ya serikali.

Upande wa mahabusu na wafungwa wanaume, mwakilishi wa kundi hilo, Florian Apolynal yeye amesema licha ya baadhi ya watuhumiwa wakiwemo wale wanaokabiliwa na kesi za Uhujumu Uchumi kutekeleza agizo la Rais, la kuandika barua na kutaka kufanyike maelewano (bargaining), lakini hawajui kinachoendelea baada ya kutekeleza hilo.

Pia wamedai kuwa kuna changamoto ya kubambikiziwa kesi zikiwemo za mauaji “… wakishakukamata wanakupa adhabu kali zenye mateso ili wakubadilishia kosa ambalo haujafanya… hivyo wengi humu tuna machungu kwani unakamatwa na kosa la wizi (robbery), lakini kwenye faili unaandikiwa mauji,” amesema mahabusu Charles Raphael Mkanya.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya amesema kero hizo amezipelekea na atazifikisha ofisini kwake ajadiliane na wataalam na kile kitakachoshindikana atakipeleka ngazi za juu zaidi ili zipatiwe ufumbuzi.

01 AUGUST 2019, CHARITY NEWSLETTERS /BARUA YA UPENDO YA KILA MWEZI

01 AUGUST 2019, CHARITY NEWSLETTERS /BARUA YA UPENDO YA KILA MWEZI

Newsletter Header

Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha hata atakapo kuwa mzee. [Mithali 22:6]

Wapendwa Taifa la Mungu na wakristo wa Tanzania, malezi ni uangalizi wa karibu wa wazazi kwa mtoto wao kiroho, kiafya, kiakili, kitabia ili tuwe na Taifa imara na watu wanaomcha Mungu. Mungu alipomuumba Adamu na Hawa akasema “zaeni mkaongezeke…………[Mwanzo 1:28.]”

Ni wajibu wa wazazi katika familia na kanisani kuwahimiza watoto kulisoma na kulipenda Neno la Mungu yaani Biblia. Katika [Rum. 8:28] tunasoma: “Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema……” Hii ni pamoja na kazi ya kulea watoto; Mungu hufanya kazi hiyo pamoja na sisi.

Katika [Zab. 127:3] Biblia inasema “Tazama wana ndio urithi wa BWANA uzao wa tumbo ni thawabu.” Mungu hatupi watoto ili tuwahifadhi kwa matumizi yetu wenyewe. Yeye anatupa watoto ili tuwalee kwa utukufu wake. Watoto wetu ni wa Mungu. Mungu amelithibitisha agano lake pamoja nasi, Katika [Kumb. 28:4] anasema “Utabarikiwa uzao wa tumbo lako” Pia katika [Isaya. 8:18] inasema “Angalieni, mimi na watoto hawa niliyopewa na BWANA tu ishara na ajabu katika Israel……” Kwa sababu hii Mungu anataka watoto wetu wajifunze Neno lake na kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Mungu anatazamia wazazi wawaelekeze watoto kwake, kwa njia ya Neno lake yaani Maandiko Matakatifu (Biblia).

Walinde watoto wako na vishawishi viovu.

Ujue nia ya shetani siku zote ni kutaka kuwaangamiza watoto, iwe kiroho au hata kimwili kwa kuwavuta katika mambo ya ulimwengu. Kuna mambo kadha wa kadha ambayo watoto wanakutana nayo maishani na haya yanaweza kusababisha au kuwaondoa kabisa wasimfuate Mungu sawasawa. Neno la Mungu linasema “Msiipende dunia wala mambo yaliyomo katika dunia… na dunia inapita pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”. [1Yoh. 2:15-17].
Marafiki wabaya na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii yameangamiza familia nyingi na kuwapoteza watoto na vijana katika kiwango cha kutisha [Mithali 13:20] Neno la Mungu linasema “… Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.” [Zab. 1:1] inasema: “Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani
pa wenye mizaha.”

Nawasihi na kuwaomba Wakristo wa Tanzania kusimama na Chama chenu cha Biblia kuwaridhisha watoto wetu Neno la uzima, hivyo wapatie watoto Biblia katika maisha yao. Simama na huduma ya Chama cha Biblia cha Tanzania kuwapatia watoto na vijana.

Neno la Mungu kama zawadi na baraka kutoka kwa Mungu maishani mwao.
Amani na Neema ya Mungu iwe juu yako.
Mtumishi wenu katika Kristo

Alfred Kimonge.
Katibu Mkuu

JITIHADA ZINAZOFANYWA NA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA ILI KUHAKIKISHA VIONGOZI WA MAKANISA MBALI MBALI NCHINI WANAFIKIWA NA MPANGO HUU MADHUBUTI.

1

Pichani toka kulia: Baba Askofu Mkuu Dr. Shoo wa Kanisa la KKKT, Msaidizi wa
Askofu wa Kanisa hilo, Dayosisi ya Kaskazini Mch. Saria, Baba Askofu Amos Muhagachi Balozi wa CBT na Mjumbe wa Bodi, na Eng. Ekaeli Manase mjumbe
wa Bodi ya CBT; wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kupokea bahasha
10,000 kwa ajili ya kuchangia huduma ya Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT).

3 1

Pichani: Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania ndugu Alfred
Kimonge (kushoto) na Fr. Sosthenes wa Kanisa Katoliki Dodoma baada
kikao cha pamoja kilichomteua kuwa mmoja wa wawakilishi wa Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT).

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

2

Pichani: Baba Askofu Amos Muhagachi (wa tano toka kulia waliokaa) Balozi wa
CBT na Mjumbe wa Bodi, akiwa na Mapadre wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Dodoma, baada ya Mkutano wa pamoja uliofanyika mjini Dodoma.

5 2

Pichani: Mtume na Nabii Josephat Mwingira (katikati ) wa Huduma ya Efatha
na mkewe (kushoto) wakipokea zawadi ya Biblia kutoka kwa Baba Askofu
Amos Muhagachi (kulia) Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) na mjumbe wa Bodi, alipomtembelea na kufanya mazungumzo naye kuhusu mkakati wa CBT wa kuhamasisha Makanisa kuchangia upatikanaji wa
Maandiko Matakatifu kwa ajili ya watoto, vijana na wafungwa hapa Tanzania.

4

Pichani: Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) ndugu Alfred Kimonge (kushoto), Fr. Chesco P. Msaga (katikati) wa Kanisa Katoliki
Dodoma na Baba Askofu Amos Muhagachi (kulia), Balozi wa CBT na mjumbe wa Bodi, wakiwa studio za Redio Mwangaza Dodoma akizungumza juu ya mkakati wa Chama wa kuhamasisha Makanisa na Wakristo wote kuchangia
upatikanaji wa Maandiko Matakatifu kwa ajili ya watoto, vijana na
wafungwa hapa Tanzania.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Unaweza usibadilishe dunia yote na kuifanya iwe ya kumpenda Mungu, lakini kwa sadaka yako ya upendo kwa Chama cha Biblia cha Tanzania ya Tsh 5000 tu! na kuendelelea unaweza kumbadilisha milele mtoto, kijana au hata mfungwa mmoja.
Tuma sadaka yako ya upendo kupitia namba ya M-PESA ya Chama: 890890 kisha tuma ujumbe wa kuchangia katika namba hizi: 0762998819, 0754383636 na 0754479789. 
Pia unaweza kuchangia kupitia akaunti za Benki za DTB na NBC zilizoonyeshwa hapa chini  Changia kupitia benki ya DTB: Namba ya Akaunti: 0901969001 SWIFT OR WIRING CODE DTKETZTZ na Changia kupitia benki ya NBC: Namba ya Akaunti: 029103000362 na Mungu akubariki sana.

Na Mungu akubariki sana

Askofu Amos Muhagachi

Mhariri

Mawasiliano yatumwe kwa: Katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, P.0. Box 175, Dodoma, Tanzania. Email: aekimonge@yahoo.com T: +255262324661 Fax: +255262324058.

× How can I help you?