CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASAMBAZA ZAIDI YA MAANDIKO 538,000 MWAKA 2025

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASAMBAZA ZAIDI YA MAANDIKO 538,000 MWAKA 2025

MG 0862 scaled
MG 1036 scaled
MG 1291 scaled
MG 0869 scaled

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASAMBAZA ZAIDI YA MAANDIKO 538,000 MWAKA 2025

Dodoma, Juni 2026 – Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT), Askofu Dkt. Mark Malwa Malekana, amesema Chama hicho kimefanikiwa kusambaza jumla ya maandiko matakatifu 538,544 katika mwaka 2025, ikilinganishwa na maandiko 512,650 yaliyosambazwa mwaka 2024.

Akizungumza leo jijini Dodoma wakati wa Mkutano Mkuu wa 40 wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Askofu Malekana alisema ongezeko hilo linaonyesha mafanikio ya juhudi za Chama katika kuhakikisha Neno la Mungu linawafikia Watanzania wengi zaidi kupitia mifumo na lugha mbalimbali.

Mbali na ongezeko la usambazaji wa maandiko, Chama hicho pia kimepata mafanikio makubwa katika utekelezaji wa miradi yake mbalimbali, ikiwemo ujenzi wa jengo la kitega uchumi la Bible Plaza, maandalizi ya Kamusi ya Biblia, Itifaki ya Biblia pamoja na uchapishaji wa kitabu cha historia ya Chama cha Biblia cha Tanzania.

Aidha, Chama kimeendelea kuimarisha huduma za tafsiri za Biblia kwa kuzindua Biblia za lugha za Kikagulu na Kihehe, hatua inayolenga kuwafikia waumini wanaotumia lugha hizo za asili na kuongeza ushiriki wao katika kusoma na kuelewa Maandiko Matakatifu.

MG 1037 scaled

Askofu Dkt. Mark Malwa Malekana – Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT).

MG 1230 scaled
MG 1291 scaled

Dkt. Kimonge aliongeza kuwa mwaka 2025 Chama kimeendelea kutekeleza mradi wa kuwawezesha wanawake na wasichana zaidi ya 3,200 pamoja na wanaume wanaonufaika na mpango huo katika wilaya za Gairo na Kilosa. Mradi huo unalenga kutoa elimu na kuwawezesha wananchi waliokosa fursa ya masomo kutokana na changamoto za kijamii na kiuchumi.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred Elias Kimonge, amesema Chama kimeendelea kuwahudumia watu wenye ulemavu wa macho kupitia utoaji wa Biblia za Nukta Nundu (Braille) pamoja na kuendesha mafunzo ya Trauma Healing kwa jamii zinazokabiliwa na changamoto mbalimbali za maisha.

Viongozi wa Chama hicho wamewataka wadau mbalimbali kuendelea kushirikiana katika kueneza Maandiko Matakatifu na kusaidia makundi maalumu yenye uhitaji wa huduma za kiroho na kijamii. Wamesema ushirikiano huo utawezesha kufikiwa kwa jamii nyingi zaidi, hususan maeneo ya vijijini.

MG 1047 scaled
MG 1253 scaled

Katika Mkutano Mkuu huo wa 40, wajumbe walijadili mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizopo pamoja na mikakati ya maendeleo ya Chama kwa miaka ijayo. Wajumbe mbalimbali walipongeza juhudi za uongozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania katika kuhakikisha huduma za Biblia zinawafikia Watanzania wa rika na makundi mbalimbali nchini.

MG 1247 scaled
MG 1210 scaled
MG 1217 scaled

Mkutano Mkuu huo pia ulihudhuriwa na wageni kutoka Chama cha Biblia cha Korea Kusini wakiongozwa na Katibu Mkuu wao. Ujumbe huo ulieleza namna Chama cha Biblia cha Korea Kusini kinavyoendelea kushirikiana kwa karibu na Chama cha Biblia cha Tanzania katika utekelezaji wa huduma mbalimbali za kueneza Neno la Mungu, wakisisitiza kuwa ushirikiano huo umejengwa katika msingi wa urafiki wa muda mrefu na maono ya pamoja ya kuhudumia jamii kupitia Maandiko Matakatifu.

MG 1047 scaled
MG 0869 scaled
MG 1107 scaled
MG 0934 scaled
MG 1108 scaled
MG 1398 scaled

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Chama cha Biblia cha Tanzania akimkaribisha rasmi Askofu Dkt. Stanley Elilekia Hotay kujiunga na Bodi ya Wakurugenzi baada ya kupitishwa na Mkutano Mkuu wa 40 wa Chama hicho uliofanyika jijini Dodoma.

MG 1446 scaled

Aidha, mkutano huo uliwapa wajumbe fursa ya kuwaaga baadhi ya wakurugenzi wa Bodi waliomaliza muda wao wa uongozi baada ya kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Chama. Waliotunukiwa heshima hiyo ni Mch. Dkt. Anna W. Sollo, Mch. Prof. Godson S. Maanga na Mhandisi Ekael Manase.

Sambamba na zoezi hilo, wajumbe walifanya uchaguzi wa wakurugenzi wapya wa Bodi kuziba nafasi zilizoachwa wazi, hatua inayolenga kuendelea kuimarisha uongozi na utekelezaji wa majukumu ya Chama katika kueneza Maandiko Matakatifu na kuhudumia jamii.

Wakurugenzi wa Bodi waliomaliza muda wao wa utumishi.

MG 1381 scaled

Mch. Dkt. Anna W. Sollo

MG 1341 scaled

Mch. Prof. Godson S. Maanga

MG 1363 scaled

Mhandisi Ekael Manase

MG 1077 scaled
CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO GAIRO – MOROGORO

Gairo, Morogoro | 05 Januari 2026

Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) kimefanya mahafali ya nane ya wanakisomo wa mradi wa Literacy for Women in Africa katika Wilaya ya Gairo, Mkoa wa Morogoro, tarehe 05 Januari 2026. Sherehe hiyo ilihusisha wahitimu wa elimu ya watu wazima waliopata mafunzo ya kusoma na kuandika kupitia mradi huo unaolenga kuwawezesha wanawake na wasichana ambao hawakupata fursa ya elimu rasmi.

IMG 5131 scaled

Sherehe hiyo ilifunguliwa rasmi kwa risala iliyosomwa mbele ya mgeni rasmi, Profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, ambaye aliwakilishwa na Diwani wa eneo hilo, pamoja na viongozi wa dini, viongozi wa vijiji vilivyofikiwa na mradi, na Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania aliyewakilishwa na Meneja wa Shughuli, Mchungaji John Mnong’one.

IMG 5061 scaled
IMG 5085 scaled

“Awali sikuweza kusoma wala kuandika. Kupitia mpango huu nimejifunza, na sasa naweza kusoma na kuandika kwa kujiamini. Hata nilipokwenda kupiga kura, nilijichagulia mwenyewe tofauti na zamani nilipolazimika kuchaguliwa na wengine.”

IMG 5035 scaled
IMG 5124 scaled
IMG 5153 scaled
IMG 5168 scaled

Akizungumza kupitia risala hiyo, CBT ilieleza kuwa mradi wa Literacy for Women in Africa ulianza kutekelezwa mwaka 2018 kwa kushirikiana na makanisa na wadau mbalimbali, wakiwemo Serikali za Wilaya za Gairo na Kilosa. Lengo kuu la mradi ni kuwasaidia wanawake na wasichana waliokosa elimu ya msingi kupata ujuzi wa kusoma na kuandika ili kuboresha maisha yao binafsi, kifamilia na kijamii.

Katika kipindi cha utekelezaji wa mradi huo, CBT imewafikia wanakisomo 3,200 wakiwemo wanawake wengi na wanaume wachache. Kutokana na uhitaji mkubwa uliojitokeza kwa wanaume wasiojua kusoma na kuandika, mradi ulipanua wigo wake na kuanza kuandikisha wanaume waliokuwa tayari kujiunga na madarasa ya elimu ya watu wazima (CHIBWEDA).

IMG 5049 scaled

Kwa mwaka 2025 pekee, mradi uliweza kufanya uhamasishaji na kuandikisha wanakisomo 595 (wanaume 145 na wanawake 450), kuanzisha madarasa mapya katika vijiji vya Mkalama, Masenge, Kinyolisi, Kisitwi, Nyangala na Luhwaji, pamoja na kutoa mafunzo kwa waalimu 30 wa elimu ya watu wazima yaliyofanyika Dodoma kwa muda wa wiki mbili. Aidha, vitabu vya kujifunzia (Primer books) vilichapishwa na kugawiwa kwa wanakisomo wote waliosajiliwa, na vitabu 300 vya hadithi (story books) vilitolewa kwa wahitimu kwa matumizi baada ya kuhitimu.

Katika mahafali hayo, jumla ya wahitimu 366 walikabidhiwa vyeti, ikiwa ni ishara ya mafanikio ya mradi katika kuongeza idadi ya watu wanaojua kusoma na kuandika kwenye jamii.

IMG 5054 scaled

Mradi huo umeleta matokeo chanya makubwa, yakiwemo kuongezeka kwa ujasiri wa wanawake kushiriki katika uongozi wa jamii, ushiriki wao katika shughuli za maendeleo, siasa na Kanisa, pamoja na kuimarika kwa uelewa wa jamii katika masuala ya afya, kilimo, ufugaji, mazingira na haki za kiraia. Wanufaika pia wameeleza kuwa mradi umewasaidia kusoma na kuelewa Neno la Mungu, kujiamini zaidi na kuimarisha mahusiano ndani ya familia na jamii kwa ujumla.

Rose Mrema

Literacy for Women coordinator, The Bible Society of Tanzania

Hata hivyo, CBT ilibainisha changamoto kadhaa, ikiwemo wanakisomo 185 kuacha masomo kati ya waliojiandikisha, uhitaji mkubwa wa mradi katika mikoa mingine nchini, upungufu wa fedha za kuendesha shughuli za mradi, pamoja na changamoto za miundombinu ya usafiri katika baadhi ya maeneo.

IMG 5155 scaled
IMG 5163 scaled
16
IMG 4950 scaled
IMG 5172 scaled
IMG 5031 scaled
IMG 5041 scaled
IMG 5009 scaled
Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Biblia kwa Lugha ya Kihehe Yazinduliwa Rasmi Iringa – Miaka 30 ya Kazi Yafikia Tamati

Na Mwandishi Wetu, Iringa

29 Juni 2025

3

Dr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.

Mgeni rasmi. 

Mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi, ambaye alikipongeza Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) kwa kazi kubwa na ya kipekee ya kutafsiri Neno la Mungu katika lugha mbalimbali za makabila nchini. ‘‘Biblia hii ni zawadi kubwa kwa jamii ya Wahehe na kizazi kijacho. Nitalitunza Neno hili takatifu, na kila siku nitaanza siku yangu nikiwa nimesoma Biblia hii kwa lugha ya mama yangu,” alisema Mhe. Lukuvi.

6

Mhe. William Vangimembe Lukuvi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), akihutubia.

Biblia iliyotafsiriwa kwa lugha ya Kihehe imezinduliwa rasmi leo katika ibada maalum iliyofanyika katika Kanisa la Kristo Mfalme, Anglikana Iringa Mjini, mkoani Iringa, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, makanisa na jamii ya Wahehe kwa ujumla.

3.1

Askofu Joseph Mwenyekiti wa CCT Mkoa Iringa na Askofu Anglican Dayosisi ya Ruaha akifanya uzinduzi wa Biblia ya Kihehe.

6.9
5
3.2

Dkt. Alfred Elias Kimonge akizungumza kabla ya kukabidhi Biblia ya Kihehe ili izinduliwe.

6.8

Safari ya Miaka 30


Kwa mujibu wa Dkt. Alfred Elias Kimonge, Katibu Mkuu wa CBT, mchakato wa kutafsiri Biblia hiyo ulianza mwaka 1994 baada ya maombi kutoka kwa Makanisa ya Iringa. Mradi huo ulisimamiwa na Chama cha Biblia Tanzania kwa kushirikiana na makanisa mbalimbali, wataalamu wa lugha, wahakiki, watafsiri, na wadau wa ndani na nje ya nchi.

Dkt. Kimonge alibainisha kuwa tafsiri ya Agano Jipya ilikamilika mwaka 2004 na kuzinduliwa rasmi mwaka 2008. Tafsiri ya Agano la Kale ilianza mwaka 2009, na sasa Biblia kamili imekamilika na kuzinduliwa rasmi leo tarehe 29 Juni, 2025. ‘‘Biblia inayozinduliwa leo inapatikana katika matoleo mawili: toleo la Kiprotestanti lenye vitabu 66, na toleo lenye vitabu 72 lijulikanalo kama Deuterokanoni, linalofaa zaidi kwa matumizi ya Makanisa ya Kikatoliki (TEC),” aliongeza kusema.

‘‘Tunamshukuru Mungu kwa kuona siku hii. Hii ni ushuhuda wa kuwa Neno la Mungu linaweza kufika katika kila lugha, kwa kila mtu,” alihitimisha Dkt. Kimonge.

Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Iringa

Mhe Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo akitoa salaam za furaha Kwa kupata Biblia hiyo uku akisifu juhudi za watafsiri, wahariri, na wadau wa kiimani kwa kazi hii kubwa.

9.4
9.2

Mhe Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo.

Risala na Maombi Maalum

Katika risala iliyosomwa kwa niaba ya Kamati ya Uzinduzi, viongozi wa makanisa na jamii walitoa wito kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusaidia katika masuala yafuatayo:

  1. Kutambua Biblia ya Kihehe kama waraka rasmi wa lugha ya Kihehe
  2. Kuandaliwa kwa Kamusi ya Biblia ya Kihehe
  3. Kutolewa kwa Biblia ya Kihehe kwa njia ya sauti (Audio Bible)
  4. Kuwepo kwa Biblia ya Kihehe katika mfumo wa mtandaoni
  5. Kuhifadhi Biblia hiyo katika Maktaba na Makumbusho ya Taifa
5.1
2
8

Ushiriki wa Viongozi na Jamii

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na maaskofu kutoka madhehebu mbalimbali, wawakilishi wa serikali, wabunge, viongozi wa mila na mamia ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Iringa.

Miongoni mwa viongozi wa dini waliokuwepo ni pamoja na:

  • Askofu Dkt. Blaston Gaville (KKKT – Iringa)
  • Askofu Dkt. Joseph Mgomi (Anglikana – Ruaha)
  • Mhashamu Romanus Mihali (RC – Iringa)
  • Askofu Prof. Mdegella, Askofu Mtetemela, na Askofu Ngalalekumtwa
6.7
14
15
6.4
Mangala
4.1

Kumbukizi za Watafsiri

Shukrani na heshima zilitolewa kwa watafsiri na wahakiki waliotoa mchango mkubwa, lakini hawakuweza kushuhudia uzinduzi huu, akiwemo:

  • Marehemu Mch. Lambert Mtatifikolo
  • Marehemu Mwl. Evaristo Mahimbi
  • Marehemu Mch. Israeli Kiponda

Hitimisho na Maono ya Baadaye

Biblia hii inatarajiwa kusaidia jamii ya Kihehe kusoma, kuelewa, na kuishi Neno la Mungu kwa undani zaidi katika lugha yao ya moyo. Viongozi walisisitiza kuwa kazi ya Mungu kupitia tafsiri ya Biblia inapaswa kuungwa mkono zaidi, ili kufanikisha tafsiri katika lugha nyingine za makabila ya Tanzania.

6.8
17

Comments

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU – WILAYA YA GAIRO, MKOA WA MOROGORO.

Tarehe: 8 Juni 2025
Mahali:Gairo, Morogoro

Uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu Unasisitiza Uthamini wa Lugha za Asili

Viongozi wakipokea Biblia ili Izinduliwe

Dr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.

Ibada na kubariki wa Biblia. 

Ibada ya uzinduzi na kubariki Biblia iliongozwa na Askofu Godfrey Sehaba wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Morogoro. Pia, viongozi wengine wa kidini waliohudhuria ni pamoja na Mch. Stanley Makasi Tabulu (Msaidizi wa Askofu KKKT), Askofu Frederick Chingwaba (Kanisa Huria Anglikana Tanzania)  na Msaidizi wa Askofu wa Jimbo Katoliki Morogoro.

Chama cha Biblia cha Tanzania (BST) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kiimani na kijamii,  tarehe 8 Juni 2025, ilifanikiwa kufanya uzinduzi wa Biblia kwa lugha ya Kikagulu, katika Wilaya ya Gairo, Mkoa wa Morogoro.

Hafla hii ya kihistoria iliongozwa na Mheshimiwa Lay Canon Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye alisisitiza umuhimu wa kuhifadhi na kuendeleza lugha za asili za Kitanzania. 

Kuonesha Biblia zilizozinduliwa

Askofu Godfrey Sehaba akifanya uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu

Wafurahiya Biblia yao
Mh. Paramagamba Kabudi

Mhe. Prof. Kabudi akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi  Biblia mpya ya Kikagulu.

Maneno ya Mgeni rasmi

Mheshimiwa Kabudi alibainisha kuwa lugha za asili ni hazina ya taifa na kwamba uandishi na utafsiri wa maandiko matakatifu kwa lugha za asili ni jambo la msingi kwa uenezi wa injili na utunzaji wa utamaduni wa Taifa. 

Katibu Mkuu wa Wilaya ya Gairo

Daudi Abdallah Sehaba (DAS wa Gairo) alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mheshimiwa Jabiri Omari Makame, akisifu juhudi za watafsiri, wahariri, na wadau wa kiimani kwa kazi hii kubwa. 

Daudi Abdallah DAS

Daudi Abdallah Sehaba (DAS wa Gairo)

Ngoma ya Kienyeji ya Vijana

Mojawapo ya kikundi cha ngoma za asili kikitoa burudani kwenye uzinduzi

Burudani na Furaha ya Wananchi .

Sherehe hiyo ilionyesha utamaduni wa Kikagulu kupitia ngoma na kwaya mbalimbali zilizofurahisha wageni na wananchi wa Gairo. Uzinduzi huo ulikuwa ni sherehe ya kipekee, ikiashiria mafanikio ya miaka ya juhudi za utafsiri na uchapishaji wa Biblia hii.

Ngoma ya Kienyeji
Kwaya Ikiimba

Shukrani na Tuzo

Mwishoni, Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia Tanzania, Dk. Alfred Elias Kimonge, alitoa shukrani kwa watafsiri na wadau wote waliofanikisha mradi huu wakiwemo Askofu Frederick Chingwaba– Mtafsiri, Askofu Michael Peter Nhonya – Mratibu na Mtafsiri wa Mradi wa Kikagulu na Wahariri wa Biblia ya Kikagulu pamoa na kuwapatia zawadi.

Katibu Mkuu akitoa zawadi kwa Askofu Chingwaba1
Katibu Mkuu akitoa zawadi kwa Askofu Nhonya
Watafsri Waakiki

Matukio katika Picha

Comments