Uzinduzi wa sehemu ya Biblia (portion) kwa lugha ya Kiha.

Uzinduzi wa sehemu ya Biblia (portion) kwa lugha ya Kiha.

Uzinduzi wa sehemu ya Biblia (portion) kwa lugha ya Kiha.

Mahali: Kijiji cha Nyakimwe, Wilaya ya Buhigwe 

Dhehebu: Kanisa la Anglican 

IMG 0263 scaled

Maelezo ya Meneja wa Tafsiri, Leah Kiloba

Leah Kiloba alielezea maendeleo ya mradi huu, akisisitiza kuwa Chama cha Biblia kinaendelea kujitahidi kuhakikisha upatikanaji wa Biblia kwa watu wote wa madhehebu mbalimbali bila ubaguzi. Alifafanua kuwa mradi huu unalenga kumjumuisha kila Mkristo kwa kutoa nafasi sawa ya kusoma Neno la Mungu katika lugha yao wenyewe. 

Sherehe ya uzinduzi wa tafsiri ya Biblia ya Position ya Kiha (kitabu cha Yeremia) ilifanyika katika Kanisa la Anglican kijijini Nyakimwe, wilaya ya Buhigwe. Tukio hili lilihudhuriwa na waumini kati ya 400 na 700 kutoka madhehebu mbalimbali, pamoja na makanisa ya Anglican, Roman Catholic, Pentecostal, na Sabato, ambayo yalialikwa rasmi kushiriki.

IMG 0131 scaled
IMG 0066 scaled

Historia ya Mradi kutoka kwa Mchungaji Ntakije

Mchungaji Ntakije aliwasilisha historia ya mradi huu wa kutafsiri Biblia kwa lugha ya Kiha, akielezea hatua zilizochukuliwa kufanikisha kazi hii muhimu na changamoto zilizokabiliwa. Alielezea jinsi jamii imekuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono mradi huu.

Kusoma Maandiko na Baraka za Ibada

Tukio lilihusisha kusoma maandiko kutoka kitabu cha Yeremia, sura ya kwanza, mistari ya kwanza hadi wa kumi, ambayo ilisomwa na mtafsiri Ahabu Ntibakanzi. Kabla ya kusoma, mchungaji Daniel Nzaino alitoa baraka kwa waumini na ibada iliongozwa kwa shukrani na furaha. 

IMG 0123 1 scaled
IMG 0081 scaled

Uratibu wa Ugawaji wa Vitabu

Vitabu vya Position ya Kiha viligawiwa kwa wahumini waliokuwa wakitoka kanisani, kwa usimamizi wa watu waliokuwa milangoni. Kila mmoja kila mmoja alipokea kitabu/portion kwa mpangilio mzuri na bila msongamano, wakihakikishiwa upatikanaji wa Neno la Mungu katika lugha yao.

IMG 0207 scaled
IMG 0243 scaled

Furaha ya Waumini

Baada ya ugawaji wa vitabu hivi, waumini Walionekana wakifurahia vitabu vyao nje ya Kanisa. Walijawa na furaha kubwa huku wakimshukuru Mungu pamoja na viongozi wa mradi kwa jitihada zao kufanikisha kazi hii. Pia walipiga picha ya pamoja ya kumbukumbu wakiwa wameshikilia vitabu vyao.

IMG 0268 scaled
IMG 0266 scaled

Tukio hili lilifanikiwa kwa kiwango kikubwa, na waumini walionyesha kufurahia uzinduzi wa tafsiri hii mpya ya Biblia katika lugha yao ya Kiha, ikionyesha mwendelezo wa kazi nzuri ya Chama cha Biblia na Kanisa katika kukuza na kueneza Neno la Mungu kwa jamii nzima.

IMG 0263 scaled

Matukio katika Picha

Comments

UZINDUZI WA KITABU CHA KWANZA NA CHA PILI CHA SAMWELI KWA LUGHA YA CHASU

UZINDUZI WA KITABU CHA KWANZA NA CHA PILI CHA SAMWELI KWA LUGHA YA CHASU

UZINDUZI WA KITABU CHA KWANZA NA CHA PILI CHA SAMWELI KWA LUGHA YA CHASU

Kanisa la KKKT Usharika wa Hedalu, Dayosisi ya Pare – 20 Oktoba 2024

20241020 100910 scaled

Wapendwa waalikwa walikusanyika leo kwa tukio la kihistoria la uzinduzi wa kitabu cha Kwanza na cha Pili cha Samweli vilivyotafsiriwa kwa Lugha ya Chasu (Kipare). Uzinduzi huo uliandaliwa na Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na makanisa ya Kikristo yaliyoko katika wilaya za Mwanga na Same Mkoa wa Kilimanjaro, na kuongozwa na Mratibu wa Mradi, Mchungaji Elineema Mndeme.

Mchungaji Mndeme aliwashukuru wageni wote walioshiriki kwenye tukio la uzinduzi, wakiwemo Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi ya Mwanga, Mchungaji Timothy Msangi, na Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi ya Pare, Mchungaji Ibrahim Ndekia. Pia aliwapongeza wawakilishi kutoka Chama cha Biblia cha Tanzania, akiwemo Katibu Mkuu, Dkt. Alfred Kimonge, kwa kuwezesha kazi kubwa ya kutafsiri Biblia kwa lugha ya Chasu.

Rev. Elineema Mndeme
IMG 9613 scaled

Kazi ya tafsiri imefanywa kwa ushirikiano wa wataalamu wa lugha, viongozi wa makanisa, na wahakiki wa tafsiri. Mchango mkubwa ulitolewa na Meneja wa Tafsiri, Dada Leah Kiloba, na washirika wake katika Chama cha Biblia cha Tanzania, pamoja na wataalamu wa teknolojia ya taarifa Felix na Charles, ambao waliweka mifumo ya tafsiri katika kompyuta.

Kwa upande wa usimamizi wa tafsiri, Dkt. Chris Pekka Wilde, mshauri wa mradi, ametajwa kwa mchango wake wa kiufundi na ushauri thabiti katika kuhakikisha tafsiri zinafuata viwango vya juu.
Mradi wa kutafsiri Biblia kwa lugha ya Chasu unahusisha watafsiri wanne: Mchungaji Elineema Mndeme (Mratibu), Mchungaji Joasi Mpinda, Mchungaji Msifuni Msuya, na Mchungaji Imani Chediel Mgonja. Wahakiki wa tafsiri wamejumuisha wachungaji na wainjilisti na wajumbe raia kutoka maeneo mbalimbali ya jamii ya Chasu.

IMG 9603 scaled
IMG 9551 scaled
IMG 9555 scaled

Mpaka sasa, nusu ya vitabu vya Agano la Kale vimetafsiriwa. Kazi ya tafsiri inapitia hatua nne: kwanza, mtafsiri anatafsiri kitabu chake; pili, watafsiri wote wanakipitia; tatu, wahakiki wa jamii wanakikagua; na mwisho, mshauri wa kitaalamu anakihakiki.

Vitabu vilivyokamilika mpaka ngazi ya mshauri ni Ruthi, Yona, Yoshua, Waamuzi, Kitabu cha Nyakati 1 na Nyakati 2, Kitabu cha Wafalme 1 na Wafalme 2, Esta, Mwanzo, pamoja na Kitabu cha Kwanza na cha Pili cha Samweli ambavyo vimezinduliwa leo rasmi.

20241020 100712 scaled
20241020 100729 scaled

Aidha, Kitabu cha Kumbukumbu la Torati kiko kwenye ngazi ya uhakiki, na kinatarajiwa kufika kwa mshauri mwezi Novemba. Kitabu cha Hesabu kiko katika hatua ya kuratibu, huku vitabu vya Kutoka, Mambo ya Walawi, Nehemia, na Ezra vikiwa katika hatua ya awali ya tafsiri.

Mchungaji Samweli Mshana kutoka Chama cha Biblia cha Tanzania alitoa hotuba fupi akieleza majukumu makuu ya Chama hicho, ambayo ni kutafsiri, kuchapisha, kusambaza Biblia, na kutafuta rasilimali fedha ili kupunguza gharama za shughuli hizo kwa njia ya uchangishaji fedha (fundraising).

Aliwasihi Wakristo kujiunga na Chama cha Biblia cha Tanzania ili kusaidia kupunguza bei za maandiko, hususani kwa ajili ya wafungwa na jamii zinazoishi katika hali ngumu.

20241020 101040
IMG 9601 scaled
IMG 9559 scaled

Pia katika Ibada hiyo alikabidhi redio 60 zenye Biblia kwa lugha ya Chasu, zinazojulikana kama mpiga mbiu (proclaimer), na kuomba viongozi wa Kanisa waziweke wakfu kwa matumizi ya kanisa. Pia aliwahimiza kusimamia mradi wa “Imani Huja kwa Kusikia” kwa kuanzisha vikundi vya kusikiliza, na akawakumbusha kutuma ripoti za maendeleo ya vikundi hivyo.

Mchungaji Mshana pia aliwaomba viongozi wa makanisa kuzindua kitabu cha kwanza na cha pili cha Samweli vilivyotafsiriwa kwa lugha ya Chasu kama ishara ya hatua kubwa iliyofikiwa katika mradi huo.

IMG 9598 scaled

Tukio hili limekuwa la mafanikio makubwa na linaashiria mwanzo mzuri wa upatikanaji wa Biblia kwa Lugha ya Chasu, jambo ambalo litasaidia sana kueneza Neno la Mungu kwa ufasaha katika jamii hiyo.

Comments

Join

Work With Me

Uzinduzi wa sehemu ya Biblia za vitabu vya 2 Samweli, Ruthi, na Yona kwa lugha ya Kinyamwezi.

Uzinduzi wa sehemu ya Biblia za vitabu vya 2 Samweli, Ruthi, na Yona kwa lugha ya Kinyamwezi.

Uzinduzi wa Tafsiri ya Biblia

Uzinduzi wa tafsiri ya Biblia za vitabu vya 2 Samweli, Ruthi, na Yona kwa lugha ya Kinyamwezi umefanyika katika kanisa la Moraviani, Parishi ya Ipole, wilayani Skonge, mkoa wa Tabora. Tukio hili limeongozwa na Katibu wa Kanisa wa Wilaya ya Skonge, Mchungaji Jackson Mkombo, mbele ya waumini wa Parishi ya Ipole, chini ya Mchungaji Charles Kavula.
Kwa upande wa Chama cha Biblia cha Tanzania, walihudhuria wawakilishi kadhaa akiwemo Meneja wa Tafsiri wa Chama hicho, Dada Leah Kiloba, pamoja na Mchungaji Samweli Mshana, ambaye ni Meneja wa Mahusiano na Makanisa. Pia, Mwinjiristi Choyo Sabanja alihudhuria kama mwakilishi wa meneja wa Uenezi na Masoko. Watafsiri wa Biblia walioshiriki katika kazi ya kutafsiri vitabu hivi walikuwepo pia katika hafla hiyo.

Hafla ya Uzinduzi

29 Septemba 2024

20240929 120154 scaled

Hafla ya uzinduzi wa tafsiri ya vitabu vya Biblia kwa lugha ya Kinyamwezi ilifanyika katika kanisa la Moraviani, Parishi ya Ipole. Tukio hili lilihudhuriwa na viongozi wa kanisa, wawakilishi wa Chama cha Biblia cha Tanzania, na watafsiri wa Biblia.

HABARI KAMILI

IMG 8635 scaled

Chama cha Biblia cha Tanzania kimefanya uzinduzi wa sehemu ya Biblia za vitabu vya 2 Samweli, Ruthi, na Yona kwa lugha ya Kinyamwezi. Uzinduzi huo umefanyika katika kanisa la Moraviani, Parishi ya Ipole, wilayani Skonge, mkoa wa Tabora. Tukio hili limeongozwa na Katibu wa Kanisa wa Wilaya ya Skonge, Mchungaji Jackson Mkombo, mbele ya waumini wa Parishi ya Ipole, chini ya Mchungaji Charles Kavula.

Kwa upande wa Chama cha Biblia cha Tanzania, walihudhuria wawakilishi kadhaa akiwemo Meneja wa Tafsiri wa Chama hicho, Dada Leah Kiloba, pamoja na Mchungaji Samweli Mshana, ambaye ni Meneja wa Mahusiano na Makanisa. Pia, Mwinjiristi Choyo Sabanja alihudhuria kama mwakilishi wa meneja wa Uenezi na Masoko.

MG 8728 scaled
MG 8699 scaled

Watafsiri wa Biblia walioshiriki katika kazi ya kutafsiri vitabu hivi walikuwepo pia katika hafla hiyo. Wakiwa wameongozwa na Mratibu wao, Mchungaji Christe Katuma wa Kanisa la Moravian Tabora mjini, walihusisha Mchungaji Elack Kadubula wa Kanisa la TAG Ipuli, Tabora, Mchungaji Ellen Mpasi wa Kanisa la Moraviani Skonge Mission, na Mchungaji George Ruvula wa Kanisa la Moraviani Tabora mjini. Mwakilishi wa wahakiki, Mchungaji Festo Karangu wa Kanisa la Pentekoste Ipole, Skonge, Tabora, naye pia alishiriki.

Tafsiri ya Biblia kwa lugha ya Kinyamwezi ilianza mwezi Machi mwaka 2020, na hadi sasa, watafsiri wamefanikiwa kukamilisha vitabu vinne, ambavyo ni 1 Samweli, 2 Samweli, Ruthi, na Yona. Uzinduzi wa vitabu hivi umechochea zaidi jitihada za kuendelea na mchakato wa kutafsiri Biblia nzima kwa lugha ya Kinyamwezi.

MG 8712 scaled
MG 8707 scaled

Meneja Tafsiri wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dada Leah Kiloba, alitoa ombi kwa kanisa kuendelea kupitia vitabu vilivyozinduliwa ili kama kuna makosa yoyote, yarekebishwe kabla ya Biblia nzima kukamilika. Lengo ni kuhakikisha kuwa Biblia inatolewa bila makosa yoyote ambayo yanaweza kupotosha maana ya Neno la Mungu.

Mchungaji Samweli Mshana, Meneja wa Mahusiano na Makanisa wa Chama cha Biblia cha Tanzania, aliomba ushirikiano wa kanisa katika kuiunga mkono kazi za Chama cha Biblia kwa michango, maombi, na kuwa wanachama wa Chama cha Biblia. Pia alikumbushia umuhimu wa kuadhimisha Juma la Biblia ili kusaidia kuhakikisha Neno la Mungu linafikia watu wote nchini Tanzania.

MG 8731 scaled
MG 8739 scaled

Katika hafla hiyo, Mchungaji Mshana aligawa pia Biblia za Mpiga Mbiu (Proclaimer), ambazo ni Biblia zinazoongea kwa lugha ya Kinyamwezi na Kiswahili. Biblia hizi ni muhimu kwa watu wasiojua kusoma na kuandika, au wenye changamoto mbalimbali, ili waweze kusikia na kufahamu Neno la Mungu kwa urahisi zaidi.

HABARI KATIKA PICHA

Ungana Nasi Katika Kazi ya Mungu

Kimachame Bible Launch

Kimachame Bible Launch

Kimachame Bible Launch

The launch of the Bible in the Kimashami language (Kichagga of Machame), was held in the Congregation of Hai in 04/12/2022.

Bishop Dr Shoo said many people have been neglecting their languages ​​and said it is good to learn and develop their native languages. At the launch of the Bible, the General Secretary of the Bible Society of Tanzania Dr. Alfred Elias Kimonge said apart from the launch of the Bible, they are still facing challenges including people not paying attention to their languages ​​and not giving them priority.

Kimachame Bible
Kimachame Bible
10 scaled
11 scaled

“Some have assumed that communicating in native languages ​​is a weakness, dear friends, it is not true that native languages ​​are a weakness. The native language is what builds a person’s heart and is the mother tongue for all living,” he said.

OUR COMPLETION

Now, It leads to 13 complete local language Bibles have been translated and 41 others have New Testament Bibles.

8 scaled
9 scaled

There is so much in the Bible that feeds my soul, so many teachings. In the Bible we have everything. The Kimashami Bible brings me great joy to me. On the launch of the Kimashami Bible in Hai Kilimanjaro.

12 scaled

Comments

Join

Work With Me

Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi

Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi

Mkuu wa KKKT ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, Dkt. Fredrick Shoo, amewataka Wakristo kuitunza na kuindeleza lugha zao za asili kwani ndio msingi na urithi walio nao.

Askofu Dkt. Shoo aliyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi (Kichagga cha Old Moshi), iliyofanyika katika Usharika wa Bethel Msaranga, iliyoambatana na kuweka wakfu eneo la ujenzi wa Kanisa la Mtaa huo.

Askofu Dkt. Shoo alisema watu wengi wamekuwa wakipuuzia lugha zao na kusema ni vyema kujifunza na kuziendeleza lugha zao za asili. Katika Uzinduzi huo wa Biblia, Katibu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred Kimonge alisema mbali na Uzinduzi wa Biblia hiyo bado wanakabiliwa na changamoto ikiwemo wenye lugha zao kutotilia maanani na kutozipa kipaumbele.

“wengine wameshajiwekea kuwa kuwasiliana kwa lugha za asili ni udhaifu, wapendwa si kweli kwamba lugha za asili ni udhaifu. Lugha ya asili ndio inajenga moyo wa mtu na ndio lugha mama kwa wote wanaoishi,” alisema.

Addresses

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

Phone

+255 (0) 765 530 892

Email

info@biblesociety-tanzania.org

Bible Production

Bible Production

IMG 8386

We publish scriptures in various formats including print, audio, visual and braille in order to meet the needs of all kinds of people. Since the scriptures are mostly used on a daily basis, we make sure the quality is top. This therefore dictates where production is done. Most of our production is done abroad and this comes at a high cost.

× How can I help you?