Heri ya Siku ya Wanawake Duniani (IWD)
Watoto katika kituo cha SAAFAD Membe.
Kituo hiki kiko Kijiji cha Membe, Kata ya Membe na Wilaya ya Chamwino katika Mkoa wa Dodoma.

Katika kusherekea sikukuu ya wanawake Duniani, wanawake wa Chama cha Biblia cha Tanzania, wadau na Chama cha Biblia cha Tanzania wamejumuika leo tarehe 08/03/2022 kuazimisha siku hiyo kwa kuwatembelea watoto wanaolelewa kwenye kituo cha SAAFAD Membe.
Katika siku hiyo wanawake wa Chama cha Biblia wamepata fursa ya kukutana na watoto zaidi ya 100 wanaolelewa kwenye kituo hiko ambao ni yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu. Ilikuwa ni ya furaha kwa wanawake, watoto wenyewe pamoja na wageni wengine walioshiriki kwenye sherehe hiyo.
Wanawake hao walipata mda wa kuzungumza na watoto hao kuhusu mada mbali mbali zikiwemo athari za mimba utotoni, umuhimu wa kujitunza na jinsi kuepukana na vishawishi wanavyokutana navyo katika makuzi yao na kuliishi Neno la Mungu wanalofundishwa na walezi wao kituoni hapo.
Watoto walipata muda wa kushirikisha story za maisha yao. Huyo binti anashuhudia namna mama yake alivyomkataa na wadogo zake mara tu baba alipofariki na mama kuolewa na mwanaume mwingine. Wote wanalelewa kwenye kituo cha SAAFAD.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni

“Kizazi cha Haki na Usawa kwa Maendeleo Endelevu.”


Baadhi ya watoto walifanya matembezi wakiongozwa na Mch.Samweli Mshana wa Chama cha Biblia Tanzania.


Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa
Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa.Mahali: ukumbi wa Nazareti, wilayani Gairo, mkoani Morogoro.Hafla hii ilihudhuriwa na viongozi wa dini na serikali wakiwemo wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa (W) ya Gairo pamoja na ofisi ya Mkurugenzi mtendaji...

Uzinduzi wa sehemu ya Biblia (portion) kwa lugha ya Kiha.
Uzinduzi wa sehemu ya Biblia (portion) kwa lugha ya Kiha.Mahali: Kijiji cha Nyakimwe, Wilaya ya Buhigwe Dhehebu: Kanisa la Anglican Maelezo ya Meneja wa Tafsiri, Leah Kiloba Leah Kiloba alielezea maendeleo ya mradi huu, akisisitiza kuwa Chama cha Biblia kinaendelea...

KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA BIBLIA MKOANI DODOMA
KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA BIBLIA MKOANI DODOMADodoma, 03 Novemba 2024 – Maadhimisho ya kilele cha Juma la Biblia mwaka huu yamefanyika kwa mafanikio makubwa mkoani Dodoma, katika Uwanja wa Mashujaa. Maadhimisho hayo yaliyoanza na maandamano ya amani kutoka...

UZINDUZI WA SEHEMU YA BIBLIA KWA LUGHA YA KINYIHA WAFANYIKA KANISA LA MORAVIAN, MBOZI
UZINDUZI WA SEHEMU YA BIBLIA KWA LUGHA YA KINYIHA WAFANYIKA KANISA LA MORAVIAN, MBOZIJimbo la Mbozi, Kanisa la Moravian Ushirika wa Igamba – 27 Oktoba 2024Tukio la kihistoria la uzinduzi wa vitabu vya Biblia vilivyotafsiriwa kwa lugha ya Kinyiha vitabu vya Ruthu, 1...
Get Involved
We have Bibles in different Tanzanians languages that you can read online. You can also download Bible reading plans to guide you through the Bible.

Donate Today or Get Involved