MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

Habari Kamili.

 Mwenyekiti wa Bodi ya Chama
cha Biblia Tanzania, Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana amesema chama hicho kitajitahidi kuendelea kuchapisha na kusambaza neno la Mungu ili liweze kumfikia kwa kila mtu na injili izidi kuhubiriwa.

Alisema hayo katika Mkutano
Mkuu wa Mwaka 2022 wa chama
hicho uliofanyika katika ukumbi
wa mikutano wa Kanisa la Kiinjili
la Kilutheri Tanzania (KKKT) jijini Dodoma, Ijumaa wiki hii.

Malekana, ambaye ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato alisema kuwa mafanikio ya kidunia yanataka juhudi na akili zako za mtu, lakini bila Mungu juhudi na akili hizo haziwezi kumfikisha popote.

Akinukuu maandiko kutoka katika kitabu cha Kutoka 33:15, mwenyekiti huyo wa bodi aliwakumbusha washiriki wa mkutano huo na jamii kwa ujumla, kuishi kwa kumwomba Mungu.

“Katika maisha yako omba Mungu awe pamoja nawe, iwe ni biashara unafanya au utumishi popote pale. Yesu alisema pasipo mimi hamuwezi kufanya neno lolote, na sisi kama Chama cha Biblia tunamwomba Mungu awe pamoja nasi katika majukumu ya chama katika kutafsiri Biblia, kuchapisha, sambamba na kutawanya maandiko matakatifu”.

“Kizazi hiki kinatakiwa watu warudi kwenye Neno la Mungu na kumtazama Kristo, na kwa upande wetu Chama cha Biblia tunajitaidi kuchapisha na kusambaza Neno la Mungu kwa kila mtu, wakiwemo watoto, wafungwa..na vijana ni kipaumbele cha Chama cha Biblia cha Tanzania

MG 0054 scaled

Picha kutoka kushoto ni Dkt. Alfred E. Kimonge katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, wa pili kutoka kushoto ni Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania, wa tatu kutoka kushoto ni Askofu Christian Ndossa wa Kanisa la Kilutheli la Kiinjili Tanzania Dayosisi ya Dodoma na Mwisho Askofu Amos Muhagachi, Makamu Mwenyekiti wa Bodi.

MG 0063 scaled

Askofu Christian Ndossa wa Kanisa la Kilutheli la Kiinjili Tanzania Dayosisi ya Dodoma akihudumu wakati wa mkutano huo.

MG 0101 scaled

Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania akionesha riport ya taarifa ya fedha

MG 0102 scaled

Dkt. Alfred E. Kimonge katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, akiwasilisha taarifa ya utendaji na fedha kwa mwaka wa 2022.

MG 0070 scaled
MG 0184 scaled
MG 0105 scaled
MG 0136 scaled
MG 0138 scaled
MG 0126 scaled
MG 0125 scaled
MG 0180 scaled
MG 0229 scaled
MG 0195 scaled
MG 0201 scaled

Katika maisha yako omba Mungu awe pamoja nawe, iwe ni biashara unafanya au utumishi popote pale. Yesu alisema pasipo mimi hamuwezi kufanya neno lolote, na sisi kama Chama cha Biblia cha Tanzania tunamwomba Mungu awe pamoja nasi katika majukumu ya chama
katika kutafsiri Biblia, kuchapisha, sambamba na kutawanya maandiko matakatifu”.

Askofu Christian Ndossa

Askofu, KKKT

Naye Askofu wa KKKT Dayosisi ya Dodoma, Christian Ndossa alisema neno la Mungu ndio msingi na taa za miguu ya chama hicho.

Askofu Ndossa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo alisema kuwa, chama hicho kinaweza kuwa na vitabu vingi pamoja na mipango mbalimbali, lakini bila neno la Mungu kitakosa kitu cha kukisaidia.

“Tunaweza kuwa na mipango mbalimbali, tukawa na vitabu vingi, tukasoma maandiko ya wataalamu lakini tukakosa kitu
cha kutusaidia kama tutakosa neno la Mungu ambalo ndio taa ya miguu yetu na mwanga katika maisha yetu sisi tulio wanachama wa Chama cha Biblia Tanzania,”
alisema.

Askofu huyo aliwakumbusha washiriki wa mkutano huokumwomba Mungu zaidi kwa kuwa wanahubiri injili katika kizazi kinachobadilika lakini wao wanahubiri neno la Mungu lisilobadilika, jambo linaloibua changamoto mbalimbali ikiwemo lugha.
Alitoa mfano kuwa wakati wao kama chama wanajitahidi kuhubiri injili kwa lugha ya
Kiswahili inayosikika kwa watu wengi, lakini Kiswahili chenyewe kinabadilikabadilika.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Alfred Kimonge alisema wanayo
kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa rehema na baraka zake kwa mwaka wa 2022.

“Hakika umekuwa mwaka wa baraka kwetu, umekuwa mwaka wa kuinuliwa na kuendelea kufanya kazi ya Mungu kwa ujasiri na bidii baada kipindi cha mpito ambacho dunia ilikubwa na ugonjwa wa hatari wa mlipuko wa Covid-19. Hakika Mungu ni mwaminifu sana kwetu,” alisema.

BST IMAGE

Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

Uenezaji wa Maandiko kwa 2022

Uenezaji wa Maandiko kwa 2022

Taasisi yetu kwa mwaka uliopita uliambatana na Baraka zake. Muungano wetu wa vyama vya Biblia ulimwenguni ulituweka katika mpango wa kuwafikia watu milioni moja ulimwenguni walio katika mazingira magumu au walengwa ambao hawana uwezo wa kununua Biblia. Tanzania tulipewa nakala 50,000 za Biblia. Biblia hizo tulizigawa katika mashule na magereza.

Mch. John Mnongone akimkabidhi SSP Nelson Kanyungu askari anayehudumia Ibada katika gereza la Kigoma
20220928 134320 scaled

Mch. John Mnong’one akimkabidhi SSP Nelson Kanyungu askari anayehudumia Ibada katika gereza la Kigoma. Picha ya Pili akikabidhi viongozi wa Makanisa yaliyomo katika Kambi ya wakimbizi Nyarugusu Kasulu

20220713 140251 1 scaled
Watoto wa Shule ya Msingi Suguta Kongwa1
Watoto wa Shule ya Msingi Suguta Kongwa2

Watoto wa shule ya Mshingi Suguta Kongwa wakifurahia kupata Biblia.

Uenezaji wetu Mwaka huu ulikuwa kama ifuatavyo.

Biblia 500, 0000

Agano Jipya 59,000

Sehemu za Bibia portion 1,800

 

FCBH

Akina mama hawa wa Kabila la Kibarbaig walisikiliza mpango wa FCBH walihitimu kupewa Biblia bure. Walikataa kupokea Biblia ya bure wakalipia Biblia zao kwa furaha.

Tulipowambia kuwa wana stahili,

walisema heri kutoa kuliko kupokaea

BIBLIA INAYOONGEA.

Tunamshukuru Mungu kwa taasisi yetu kuingia  mkataba na  Shirika la Talking Bible International kuwa Chama cha Biblia cha Tanzania tumekuwa kituo cha kuandaa na kugawa Biblia TB inayoongea kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Mpaka sasa tumeandaa na kugawa nakala 450 za TB kwa nchi za Kenya, Uganda na Zambia.

Watumishi wakiandaa TB

Hapa watumishi wa Chama cha Biblia wakiandaa TB katika lugha ya Kibemba na Kitonga tayari kwa kuzipeleka Zambia

Mwaka huu CBT kiliendesha semina kwa wasioona 18 na kuwafundisha kusikiliza Agano Jipya .

TB

Give Today

Children

Prison

Membership

Youth

Blind

Other

Get In Touch

Kimachame Bible Launch

Kimachame Bible Launch

Kimachame Bible Launch

The launch of the Bible in the Kimashami language (Kichagga of Machame), was held in the Congregation of Hai in 04/12/2022.

Bishop Dr Shoo said many people have been neglecting their languages ​​and said it is good to learn and develop their native languages. At the launch of the Bible, the General Secretary of the Bible Society of Tanzania Dr. Alfred Elias Kimonge said apart from the launch of the Bible, they are still facing challenges including people not paying attention to their languages ​​and not giving them priority.

Kimachame Bible
Kimachame Bible
10 scaled
11 scaled

“Some have assumed that communicating in native languages ​​is a weakness, dear friends, it is not true that native languages ​​are a weakness. The native language is what builds a person’s heart and is the mother tongue for all living,” he said.

OUR COMPLETION

Now, It leads to 13 complete local language Bibles have been translated and 41 others have New Testament Bibles.

8 scaled
9 scaled

There is so much in the Bible that feeds my soul, so many teachings. In the Bible we have everything. The Kimashami Bible brings me great joy to me. On the launch of the Kimashami Bible in Hai Kilimanjaro.

12 scaled

Comments

Join

Work With Me

Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi

Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi

Mkuu wa KKKT ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, Dkt. Fredrick Shoo, amewataka Wakristo kuitunza na kuindeleza lugha zao za asili kwani ndio msingi na urithi walio nao.

Askofu Dkt. Shoo aliyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi (Kichagga cha Old Moshi), iliyofanyika katika Usharika wa Bethel Msaranga, iliyoambatana na kuweka wakfu eneo la ujenzi wa Kanisa la Mtaa huo.

Askofu Dkt. Shoo alisema watu wengi wamekuwa wakipuuzia lugha zao na kusema ni vyema kujifunza na kuziendeleza lugha zao za asili. Katika Uzinduzi huo wa Biblia, Katibu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred Kimonge alisema mbali na Uzinduzi wa Biblia hiyo bado wanakabiliwa na changamoto ikiwemo wenye lugha zao kutotilia maanani na kutozipa kipaumbele.

“wengine wameshajiwekea kuwa kuwasiliana kwa lugha za asili ni udhaifu, wapendwa si kweli kwamba lugha za asili ni udhaifu. Lugha ya asili ndio inajenga moyo wa mtu na ndio lugha mama kwa wote wanaoishi,” alisema.

Addresses

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

Phone

+255 (0) 765 530 892

Email

info@biblesociety-tanzania.org

MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

1. UTANGULIZI.

Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) ni shirika la Kikristo lililoandikishwa mwaka 1970 na kupewa nambari S0 5722. Ni mwanachama wa Muungano waVyama vya Biblia Ulimwenguni(United Bible Societies (UBS). Shirika hili ni chombo cha Kanisa la Tanzania ambalo kazi yake kubwa na ya msingi ni kuwapelekea watu wote hapa nchini Tanzania Habari njema ya Yesu Kristo kwa kutafsiri, kuchapisha na kusambaza Biblia ikiwa katika lugha anayoielewa msomaji, bei anayoiweza na mfumo anaoupendelea.

MG 6293 copy scaled

Tangu kusajiliwa kwake  hapo mwaka 1970, Chama cha Biblia cha Tanzania kimekuwa kikitekeleza majukumu yake hayo kwa ushirikiano mkubwa na wa karibu na makanisa yote ya Kiprotestanti, Katoliki, Sabato na Kipentekoste hapa Tanzania; na pia kwa ushirikiano mkubwa na wa karibu na Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (United Bible Societies-UBS) ambalo ni ushirika wa vyama vyote vya Biblia katika nchi zote.

Chama kimeweza kufanya tafsiri na kinaendelea kutafsiri Biblia katika lugha mbalimbali za makabila ya hapa Tanzania. Kutafsiri Biblia katika lugha mbalmbali za makabila kunafanyika kwa malengo makuu mawili. Lengo la kwanza la kufanya tafsiri hizi ni kwa kuamani kuwa watu wanaweza kulielewa Neno la Mungu kwa urahisi zaidi wakisoma au kuelezwa katika lugha zao na kuainisha na mazingira halisi ya mazingira yao.

IMG 9715

Lengo la pili ni kusaidia kutunza lugha za makabila kwa faida ya vizazi vijavyo vya kabila husika, kwani mila na utamaduni wa kabila zipo katika lugha ya watu wa kabila husika. Tangu kuanzishwa kwake Chama cha Biblia kimefanya tafsiri kadha na kuzisambaza hapa nchini zikiwamo Biblia katika lugha za:

  1. Kiswahili
  2. Kimaasai,
  3. Cigogo
  4. Iraqw

5. Nyakyusa

6. Igikuria

7. Ruhaya

8. Kisukuma

9. Kidatooga

10. Kimashami

11. Kivunjo

12. Kimochi

Baadhi ya Biblia ambazo kwa sasa zipo katika hatua mbalimbali za tafsiri ni:

  1. Kihehe
  2.   Cikaguru
  3.   Kinyamwezi
  4.   Chasu(Kipare)

5.  Kifipa

6. Kinyiha

7. Kinyiramba

8. Kirimi( Kinyaturu)

9. Kiha

Agano Jipya.

  1. Kimeru
  2. Kibena
  3. Kishambala
  4. Kikinga

5. Kijita

6. Kifipa

7. Kizaramo

2.0 Umuhimu wa Neno la Mungu kwa maendeleo

Tunapoangalia historia ya ustawi wa maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ulimwenguni kote, tunaona kuwa jamii ambazo zilijengwa katika misingi ya Neno la Mungu zilistawi kimaendeleo ikilinganishwa na zile ambazo ama hazikuamini au zilimuasi Mungu. Neno la Mungu likiwa ndani ya myoyo ya watu huzaa upendo ambao huzifanya jamii kuwa zenye amani na utangamano, tunu ambazo husaidia kuweka mazingira wezeshi kwa watu kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo.

36 1 scaled

2.1 Hali ya malezi kwa watoto na vijana.

Hivi sasa nchi nyingi ulimwenguni ikiwemo Tanzania kuna mporomoko mkubwa wa maadili. Wazazi ndani ya jamii wanalalamika juu ya watoto wa kizazi hiki kuwa wamekosa maadili.

Lakini wazazi hawa wanasahau kuwa kuporomoka kwa maadili ya watoto wao kunatokana na wao kutokuwalea katika misingi mizuri ambayo ni Neno la Mungu. Huko Ulaya na Marekani wazazi/mataifa walibweteka na maendeleo ya kiuchumi, teknolojia, sayansi na maisha bora kimwili na kusahau tunu kubwa inayotokana na maendeleo ya kiroho(spirituality). Makuzi ya kiroho hujenga maadili na hivyo kujenga utu wa mtu.

Katika nchi hizi watu wengi hasa kundi la vijana sasa hivi hawaendi Kanisani au Misikitini Kuabudu. Wamejitenga kabisa na Mungu na katika baadhi ya nchi Makanisa yameuzwa na kutumika kwa shughuli nyingine kabisa kama vile maduka na hata pia kugeuzwa kuwa sehemu za burudani kama vile sehemu za kuuzia vileo na starehe zingine.

Aidha katika nchi  hizi tunashuhudia ongezeko kubwa la mporomoko wa maadili ya asili ya mwanadamu. Katika nchi hizi sasa tunashuhudia uhalalishwaji kisheria wa ndoa na mapenzi ya watu wa jinsia moja, ongezeko la vitendo  vingine viovu ambavyo ni chukizo mbele za Mungu. 

Nchi za kiafrika nazo hazijasalimika na hali hiyo. Mporomoko mkubwa wa maadili katika nchi za Afika unazidi kuongezeka na kushamiri kutokana na utandawazi. Nchi zetu sasa zinashuhudia ongezeko kubwa la vitendo viovu kila siku,vingi vikifanywa na kundi la vijana. Wazazi walio wengi wameacha wajibu wao wa asili wa kuwalea watoto wao na kuwarithisha maadili ambayo huleta ustawi wa mtu mmoja mmoja na jamii/taifa.

Wazazi wengi hawaendi na watoto wao Makanisani na Misikitini wala hawaoni umuhimu wa watoto wao kupata mafundisho ya dini tangu wakiwa watoto ili wakue na kustawi katika msingi wa Neno la Mungu. Maovu mengi tunayoyashuhudia katika jamii ni kutokana na watu kukosa msingi wa Neno la Mungu ambalo likikaa katika myoyo huwafanya watu kuwa na  hofu ya Mungu na hofu hiyo huwafanya wajiepusha na matendo maovu kwa kujua kwamba hayampendezi Mungu na yana hukumu.

Hivi sasa tunashuhudia hofu ya Mungu ikizidi kupungua katika nchi yetu, na hivyo kutishia amani na utangamano katika taifa letu. Vitendo viovu vinaongezeka kwa kasi katika taifa letu kwa sababu watu wamekosa hofu ya Mungu.

Rais wetu mpendwa wa awamu ya Tano Marehemu Mheshimiwa John Joseph Pombe Magufuli amekuwa akituasa mara nyingi kwamba tumwogope Mungu, maana yake tufanye yale yanayompendeza Mungu na tuache matendo maovu. Matendo mema huleta afya kwa jamii/taifa lolote.

20211222 050907 scaled

2.2 Kwa nini Biblia kwa Watoto, Vijana na Wafungwa?

Katika nchi nyingi duniani na hasa nchi zinazoendelea  watoto umri kati ya miaka 1-14 huwa ni rika yenye watu wengi zaidi, wakifuatiwa kwa wingi na kundi la vijana(miaka 15-24).

Makundi haya mawili haya kwa pamoja hapa Tanzania idadi yake ni zaidi ya asilimia 60 ya idadi ya watu wote. Kutokana na wingi na umri,  makundi haya yanayohitaji kuangaliwa /kutazamwa kwa karibu sana kwa maana ya malezi kwa maana ya kupewa huduma muhimu zitakazowafanya wakue na kustawi kiroho na kuwa raia wema wenye kupenda amani na  ustawi wa taifa.

Wafungwa ni kundi la watu ambao wako gerezani kwa sababu ya kutenda makosa katika jamii na kukosesha wengine amani na utangamano. Kwahiyo, hili nalo ni kundi muhimu la kutazamwa katika malezi hasa ya kiroho ili wahusika (wafungwa) wanapomaliza kutumikia  vifungo vyao waweze kuacha tabia mbaya za uhalifu na kuwa raia wema.

IMG 8365 scaled

2.3 Mapendekezo ya  na ushauri wa Chama cha Biblia kwa serikali katika kukabiliana na mporomoko wa maadili kwa wototo na vijana.

Chama cha Biblia cha Tanzania kinaishukuru sana Serikali yetu kwa kuruhusu Neno la Mungu kufundishwa mashuleni, jambo ambalo nchi zingine haziruhusu. Tunaamini hatua hii ni kwa kutambua kwamba mashuleni ndiko wanapoandaliwa viongozi wa taifa la kesho, kwa hiyo kuona umuhimu wa kuwapa malezi ya kiroho. 

Tunakumbuka miaka ya nyuma serikali iliruhusu uanzishwaji wa chama cha “ Elimu ya Dini Mashuleni Tanzania”(EDIMASHUTA) ikiwa ni njia mojawapo ya kutoa fursa kwa watoto ya kupata mafundisho ya dini ili waweze kukua kimaadili kupitia dini zao. Hii ilikuwa ni fursa muhimu sana kwa wototo kujifunza somo la dini na hivyo kukua na kustawi katika misingi ya kuwa na hofu ya Mungu.

Chama cha Biblia cha Tanzania kilikuwa mshirika mkubwa katika mpango wa Elimu mashuleni kwa kutoa Biblia  zilizotumiwa kama kitabu cha kiada mashuleni katika mafundisho hayo. Katika mpango huu, serikali ililifanya somo la dini kuwa la kutahiniwa na ilikuwa na “alama” (credit).

Kutokana na utambuzi huo vijana mashuleni walikuwa na bidii ya kujifunza somo la dini. Kwa njia hiyo waliweza kujengwa vizuri kiimani, kimaadili na kiustawi kwa ujumla na kundi hilo lilizaa viongozi waadilifu wa nchi yetu, kanisa na sekta binafsi.

Hata hivyo baadaye utaratibu wa  somo la dini kuwa  la kutahiniwa na lenye hadhi ya credit sawa na masomo mengine uliondolewa na hivyo kuwavunja moyo watoto na vijana katika kujifunza somo la dini.

Tunapendekeza kwamba somo la dini liendelee kufundishwa na lipewe hadhi/lihesabiwe sawa na masomo mengine katika mitihani, ili liweze kuchochea ari kwa watoto na vijana kujifunza somo la dini na hivyo kujengwa kimaadili.

20220713 140251 scaled

2.4 Kwa nini Biblia sasa kwa vijana mashuleni.

Kwa kuangalia mwenendo wa maadili kwa vijana wetu mashuleni,na kuna umuhimu wa kurejesha somo hilo kwani umuhimu wake umeanza kuonekana. Kumekuwa na  mmomonyoko wa maadili kwa vijana wetu sasa, tofauti na kipindi cha nyuma ambapo walilelewa katika misingi ya neno la Mungu.

Sasa hivi tunashuhudia vitendo viovu vikiongezeka katika jamii, ambapo watoto na vijana wanahusika. Jambo la pili tunaona mifano  ya wenzetu nchi za Ulaya ambako utandawazi umewafanya wasitambue  utu wa mtu.

Baadhi ya shule ambazo zimeendelea kufundisha somo la dini ni ushuhuda tosha kuonyesha namna somo la dini lilivyo muhimu katika ustawi wa mwanadamu. Shule hizi zimekuwa mfano mzuri kwa maadili na ufaulu mzuri  wa masomo hata yasiyo ya dini.

Chama cha Biblia kinaona kwamba kuna umuhimu wa kurudisha somo la dini kwa shule zote za serikali na za binafsi na kulifanya somo la dini kuwa na hadhi ya kutahiniwa sawa na masomo mengine.

Hiyo ni shule ya RUHUWIKO High School Songea wakifurahia kupewa Maandiko toka Chama cha Biblia. Wametoa shukrani nyingi kwa Uongozi kupitia mwl wao

3.0 Mpango wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa kuwapatia Biblia Watoto na Vijana mashuleni na Wafungwa magerezani.

Kwa kutambua umuhimu huo, Chama cha Biblia cha Tanzania katika mpango mkakati wa miaka mitano (2018 – 2022) kilianzisha mpango maalum wa kuhamasisha Makanisa na watu wenye mapenzi mema kushiriki kwa kuchangia fedha kwa ajili ya upatikanaji wa Biblia ili  zisambazwe kwa wingi  kwa watoto, vijana na wafungwa ikiwa ni moja ya vipau mbele vyake katika kipindi hiki cha miaka mitano.

Mpango huu unalenga makundi matatu ya watoto na vijana kwa rika na wafungwa walioko magerezani.

Na.

Watoto

Vijana

Wafungwa magerezani

 1.

Miaka 3 – 5

Miaka 16 – 24

Wanaume

 2.

Miaka 6 – 9

 

Wanawake

 3.

Miaka 10 -15

 

 

Katika mkakati wa kutekeleza mpango huu Chama cha Biblia cha Tanzania kilianza kwa kuwashirikisha viongozi wa makanisa kutokana na nafasi yao ya asili ya kuwajenga na kuwalea watu kiroho.

Pili kimewashirikisha wadau wengine wenye mapenzi mema wanaotamani kuona Tanzania inajengwa katika misingi imara ya kiroho na hivyo kuwa na taifa lenye watu wenye hofu ya Mungu.

Mpango huu umepata uungwaji mkono mkubwa sana na Kanisa la Tanzania, hali ambayo imetutia moyo sana Chama cha Biblia cha Tanzania, kwani tunatambua kwamba Kanisani ndiko Neno la Mungu linafundishwa na ndiko Wakristo wanaofanya Kanisa la Tanzania waliko.

Tunaamini mpango huu unatekelezeka na walengwa na taifa zima litanufaika.

21

3.1 Watoto na Vijana walengwa.

Mpango huu katika awamu hii ya kwanza unalenga watoto na vijana walioko katika shule kwa sababu ya urahisi wa kujua idadi yao na urahisi wa kuwafikia.

Hata hivyo shule zitazopewa kipaumbele ni zile zilizoko vijijini, ambazo mbali kuwa  nyingi, lakini ndizo zenye watoto na vijana wengi wenye wazazi wenye hali duni ya  uchumi; na hivyo hawana uwezo wa kuwapata/kuwanunulia watoto  mahitaji yao kwa utoshelevu.

Ni kutokana na ukweli huo Chama cha Biblia cha Tanzania kinalenga kuwapatia watoto na vijana Biblia kwa bei nafuu ambayo wazazi wengi pamoja na hali yao duni kiuchumi wanaweza kuimudu.

ugawaji wa Sehemu ya Biblia Agano Jipya lenye Mithali na Zaburi

3:2 Ufundishaji wa somo la dini  mashuleni.

Kama tulivyoeleza katika utangulizi, Chama cha Biblia kinaona kwamba kuna umuhimu wa kurudisha somo la dini kwa shule zote za serikali na za binafsi na kulifanya somo la dini kuwa na hadhi ya kutahiniwa sawa na masomo mengine.

Tunaishauri serikali irudishe na  kuimarisha Elimu ya Dini Mashuleni( EDIMASHUTA) na kurudisha mitaala iliyokuwepo pamoja na kuruhusu taasisi za dini  kupeleka waalimu kwa ajili ya kufundisha somo la dini.

 Mpango huu ukitekelezwa utasaidia kuwajengea watoto wetu misingi ya maadili mema ili hatimaye tuwe na taifa lenye viongozi na raia wema. Jambo hili litasaidia kujenga jamii yenye amani na utangamano na kuruhusu mazingira ya kupata ustawi kama taifa.

Picha ya watoto wanasoma Biblia. 1

3:3 Vyanzo vya upatikanaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huu

 Katika mpango huu, Chama cha Biblia cha Tanzania kinalenga kupata fedha kutoka:

  • Taasisi za kanisa
  • Mashirika mbalimbali
  • Watu binafsi

 Aidha Chama katika nia hii njema kinaomba kuungwa mkono na serikali kwa kushiriki katika kazi ya kuhamasisha taasisi, mashirika na wadau mbalimbali ili waweze kushiriki kuchangia mpango huu.

IMG 9767

3.4 Kiasi cha fedha, idadi  ya  Biblia na mgawanyo kwa makundi lengwa

Katika awamu hii ya kwanza Chama cha Biblia kimelenga kuomba kuchangiwa kiasi cha shilingi 10,200,000,000 ambazo zitatumika kununulia jumla ya Biblia 510,000 ambazo mgao wake kwa makundi lengwa utakuwa kama ifuatavyo:

  • Watoto – Biblia laki nne (400,000)
  • Vijana – Biblia laki moja (100,000)
  • Wafungwa – Biblia elfu kumi (10,000)

Kwa sasa Chama tayari kinayo miswada ya Biblia za makundi lengwa  yote yaani watoto, vijana na wafungwa. Biblia hizi zinaweza kuchapishwa na wachapishaji wakati wowote fedha zitakapokuwa zimepatikana.

Malipo yakishafanyika inakadiriwa kuwa kazi ya kuchapa, kusafirisha na kupokelewa inachukua muda wa miezi mitatu hadi minne.

20220721 115109 scaled

3:5 Mikoa na mgao wa Biblia kwa makundi lengwa.

Zoezi hili ni endelevu, lakini katika awamu hii ya kwanza Chama kimelenga kugawa Biblia kwa watoto, vijana na wafungwa katika  mikoa ifuatayo :-

 

Na

Mkoa

Watoto

Vijana

Wafungwa

 

Makisio

Halisi

Makisio

Halisi

Halisi

1.

Dodoma

730,000

100,000

180,000

25,000

3,000

2,

Mara

580,000

82,000

145,000

20,500

3,000

3.

Manyara

610,000

88,000

152,500

21,500

1,000

4.

Pwani

470,000

66,000

117,500

16,500

1,000

5.

Singida

470,000

66,000

117,500

16,500

2,000

Jumla kuu

2,860,000

400,000

712,500

100,000

10,000

IMG 20220722 WA0016

3:6 Usambazaji wa Biblia kwa makundi lengwa.

3:6:1 Mashule

Biblia zitasambazwa na Chama cha Biblia katika mashule kwa kushirikiana na Maafisa Elimu, Waalimu Wakuu wa  Mashule, Viongozi wa Makanisa na Waalimu wa Dini mashuleni.

3:6:2 Magereza

Biblia zitasambazwa katika Magereza kwa kushirikiana na Wakuu wa Magereza na Wachungaji wanaotoa huduma ya kiroho magerezani.

Gereza la Mahabusu Songea 2022 07 17

4: 0 MWISHO

Mpango huu una umuhimu wa kipekee katika kipindi hiki ambacho tunashudumia mmomonyoko wa maadili ukienda kasi katika jamiii yetu hasa kwa kundi la watoto na vijana ambalo linatarajia kutoa viongozi wa baadae wa taifa letu.

Tunaomba serikali ituunge mkono katika nia hii njema ya kuwajenga watoto, vijana na wafungwa kiroho. Faida ni kubwa kwa afya ya taifa. Kuchukua hatua sasa ni vizuri.

ABOUT US

Addresses

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

Phone

+255 (0) 765 530 892

Email

info@biblesociety-tanzania.org

MPANGO WA ELIMU YA WATU WAZIMA.

MPANGO WA ELIMU YA WATU WAZIMA.

Mpango wa elimu ya watu wazima.

Chama cha Biblia kimeeendelea na mpango huu wa elimu ya watu wazima katika (w) ya Kilosa na Gairo-Morogoro kwa lengo la kuwasaidia wanawake na wasichana ambao hawakubahatika kwenda shule kwa sababu tofauti tofauti waweze kusoma na kuandika.

Kutokana na uhitaji kwenye jamii pia wanaume wamekuwa wanufaika wa mpango huu kwa sababu kuna idadi kubwa kwenye jamii ya wanaume ambao hawajui kusoma na kuandika pia.

Waalimu wa Kikagulu wakiwa kwenye mafunzo Dodoma scaled

Mpango huu kwa mwaka 2022 unatekelezwa katika vijiji 10 vya wilaya ya Kilos ana Gairo kwa kushirikiana na kanisa, serikali ambao wametupatia waalimu kwa ajili ya kuwafundisha wanakisomo. Wanakisomo 300 kutoka katika vijiji 10 walijiandikisha na mafunzo yanaendelea kwenye maeneo yao.

Waalimu wakiwa kwenye mafunzo scaled

Chama cha Biblia kupitia waalimu hao, kimewaandaa kuwa waalimu wazuri  ajili ya kuhakikisha kila mwanakisomo atakapohitimu elimu yake atakuwa anajua kusoma na kuandika. Waalimu hao kabla ya madarasa kuanza waliweza kupata mafunzo ya kuwajengea uwezo na kupata mbinu nyingi za ufundishaji ili kuweza kuwafundisha wanakisomo kwa kufuata taratibu na miongozo iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwafundisha watu wazima.

electrician 10

Matukio katika Picha

Volunter-Mr-Musa-Barabara-akiwa-na-watoto-kutoka-Matumbulu-wakisoma-kijtabu-baada-ya-kugawiwa.-scaled.jpg June 23, 2022
IMG 7727 scaled
20220506 140032 scaled

Addresses

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

Phone

+255 (0) 765 530 892

Email

info@biblesociety-tanzania.org