Mpango wa elimu ya watu wazima.
Chama cha Biblia kimeeendelea na mpango huu wa elimu ya watu wazima katika (w) ya Kilosa na Gairo-Morogoro kwa lengo la kuwasaidia wanawake na wasichana ambao hawakubahatika kwenda shule kwa sababu tofauti tofauti waweze kusoma na kuandika.
Kutokana na uhitaji kwenye jamii pia wanaume wamekuwa wanufaika wa mpango huu kwa sababu kuna idadi kubwa kwenye jamii ya wanaume ambao hawajui kusoma na kuandika pia.
Mpango huu kwa mwaka 2022 unatekelezwa katika vijiji 10 vya wilaya ya Kilos ana Gairo kwa kushirikiana na kanisa, serikali ambao wametupatia waalimu kwa ajili ya kuwafundisha wanakisomo. Wanakisomo 300 kutoka katika vijiji 10 walijiandikisha na mafunzo yanaendelea kwenye maeneo yao.
Chama cha Biblia kupitia waalimu hao, kimewaandaa kuwa waalimu wazuri ajili ya kuhakikisha kila mwanakisomo atakapohitimu elimu yake atakuwa anajua kusoma na kuandika. Waalimu hao kabla ya madarasa kuanza waliweza kupata mafunzo ya kuwajengea uwezo na kupata mbinu nyingi za ufundishaji ili kuweza kuwafundisha wanakisomo kwa kufuata taratibu na miongozo iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwafundisha watu wazima.
Matukio katika Picha
Addresses
16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.
Phone
+255 (0) 765 530 892
info@biblesociety-tanzania.org
Hi, I’m pastor in America .so did you have bible reoded in 1978, if so how much cost. Again did you have online bible school thanks
Dear
I am greeting from the Bible Society of Tanzania
Can you please write an email to our marketing manager? His email address is akamwela@biblesociety-tanzania.org you can also copy to my email which is fjones@biblesociety-tanzania.org
Kindly regards