Mpango wa elimu ya watu wazima.

Chama cha Biblia kimeeendelea na mpango huu wa elimu ya watu wazima katika (w) ya Kilosa na Gairo-Morogoro kwa lengo la kuwasaidia wanawake na wasichana ambao hawakubahatika kwenda shule kwa sababu tofauti tofauti waweze kusoma na kuandika.

Kutokana na uhitaji kwenye jamii pia wanaume wamekuwa wanufaika wa mpango huu kwa sababu kuna idadi kubwa kwenye jamii ya wanaume ambao hawajui kusoma na kuandika pia.

Waalimu wa Kikagulu wakiwa kwenye mafunzo Dodoma scaled

Mpango huu kwa mwaka 2022 unatekelezwa katika vijiji 10 vya wilaya ya Kilos ana Gairo kwa kushirikiana na kanisa, serikali ambao wametupatia waalimu kwa ajili ya kuwafundisha wanakisomo. Wanakisomo 300 kutoka katika vijiji 10 walijiandikisha na mafunzo yanaendelea kwenye maeneo yao.

Waalimu wakiwa kwenye mafunzo scaled

Chama cha Biblia kupitia waalimu hao, kimewaandaa kuwa waalimu wazuri  ajili ya kuhakikisha kila mwanakisomo atakapohitimu elimu yake atakuwa anajua kusoma na kuandika. Waalimu hao kabla ya madarasa kuanza waliweza kupata mafunzo ya kuwajengea uwezo na kupata mbinu nyingi za ufundishaji ili kuweza kuwafundisha wanakisomo kwa kufuata taratibu na miongozo iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwafundisha watu wazima.

electrician 10

Matukio katika Picha

Volunter-Mr-Musa-Barabara-akiwa-na-watoto-kutoka-Matumbulu-wakisoma-kijtabu-baada-ya-kugawiwa.-scaled.jpg June 23, 2022
IMG 7727 scaled
20220506 140032 scaled

Addresses

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

Phone

+255 (0) 765 530 892

Email

info@biblesociety-tanzania.org

× How can I help you?