Mkutano Mkuu wa Mwaka 2021

Mkutano Mkuu wa Mwaka 2021

Mkutano Mkuu wa Mwaka 2021

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred E. Kimonge anawakaribisha wanachama wa Chama cha Biblia cha Tanzania walio hai (ambao wamelipa michango yao ya uanacha wa kila mwaka) kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania (Annual General Meeting 2021) utakaofanyika tarehe 13.05.2022, katika ukumbi wa KKKT- Dodoma mjini, kuanzia saa 3 Asubuhi

Usipange kukosa.

Upatapo taarifa hii mshirikishe na mwenzako.

KARIBUNI.

MAWASILIANO: +255 784 683 120

Our Partners & Sponsors

UBS
ABS LOGO2
BIBLE ONLINE
FCBH
TalkingBibles
Finnish Bible Society

Get In Touch

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHA SHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHA SHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Heri ya Siku ya Wanawake Duniani (IWD)

Watoto katika kituo cha SAAFAD Membe.

 

Kituo hiki kiko Kijiji cha Membe, Kata ya Membe na Wilaya ya Chamwino katika Mkoa wa Dodoma.

food bank 57

Katika kusherekea sikukuu ya wanawake Duniani, wanawake wa Chama cha Biblia cha Tanzania, wadau na Chama cha Biblia cha Tanzania wamejumuika leo tarehe 08/03/2022 kuazimisha siku hiyo kwa kuwatembelea watoto wanaolelewa kwenye kituo cha SAAFAD Membe.

Katika siku hiyo wanawake wa Chama cha Biblia wamepata fursa ya kukutana na watoto zaidi ya 100 wanaolelewa kwenye kituo hiko ambao ni yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu. Ilikuwa ni ya furaha kwa wanawake, watoto wenyewe pamoja na wageni wengine walioshiriki kwenye sherehe hiyo.

Wanawake hao walipata mda wa kuzungumza na watoto hao kuhusu mada mbali mbali zikiwemo athari za mimba utotoni, umuhimu wa kujitunza na jinsi kuepukana na vishawishi wanavyokutana navyo katika makuzi yao na kuliishi Neno la Mungu wanalofundishwa na walezi wao kituoni hapo.

 

Watoto walipata muda wa kushirikisha story za maisha yao. Huyo binti anashuhudia namna mama yake alivyomkataa na wadogo zake mara tu baba alipofariki na mama kuolewa na mwanaume mwingine. Wote wanalelewa kwenye kituo cha SAAFAD.

Membe Kituoni (SAAFAD)

Kauli mbiu ya mwaka huu ni

IMG 6979 scaled

“Kizazi cha Haki na Usawa kwa Maendeleo Endelevu.”

IMG 7018 scaled
given3
food bank 57

Get Involved

We have Bibles in different Tanzanians languages that you can read online. You can also download Bible reading plans to guide you through the Bible.

food bank 56

Donate Today or Get Involved

Help With Hunger By Donating Today!

The launch of the full Braille Bible

The launch of the full Braille Bible

The Bible Society of Tanzania celebrates the launch of the full Braille Bible.

It is in the city of Kongwa, located in Dodoma Region of the capital city of Tanzania that the majority of the visual impaired live. One of the characteristics of this translation is that it is the result of close collaboration between Churches of different confessions

Bible Production

Bible Production

IMG 8386

We publish scriptures in various formats including print, audio, visual and braille in order to meet the needs of all kinds of people. Since the scriptures are mostly used on a daily basis, we make sure the quality is top. This therefore dictates where production is done. Most of our production is done abroad and this comes at a high cost.

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

 

ZIARA KATIKA MAGEREZA YA MSALATO NA KONGWA DODOMA

Moja kati ya wajibu muhimu kwa Chama cha Biblia cha Tanzania ni kuhakikisha kuwa watu wote wanapata fursa ya kupata maandiko matakatifu. Kutokana na jukukumu hilo tarehe 27/11/2018 watumishi wa Idara ya Mahusiano na baadhi ya Wale wa Mawasiliano, walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Msalato Dodoma na kugawa Biblia, Sabuni na dawa ya meno kwa Wafungwa wa gereza hilo la Msalato. Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji akishirikiana na Msaidizi wake na Maafande wengine walitupokea vizuri sana na kutupa ushirikiano wa hali ya juu.

 

 

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, viongozi wa kanisa la KKKT Dodoma na viongozi wa gereza la Msalato

 

Jukumu la kugawa Biblia halikuishia Gereza la Msalato tu kwani Tarehe 28/11/2018 Meneja Mahusiano na kikosi kazi chake walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Kongwa Dodoma. Katika Gereza hili tulipokelewa vizuri sana na kupewa maelezo ya jinsi Wafungwa wanavyohitaji msaada wa Maandiko na vifaa vingne kwani wanatakiwa kjujitegemea.Chama cha Biblia tulifaulu kugawa Maandiko Matakatifu,sabuni, dawa ya Meno na Taulo za akina Mama.Mkuu wa Gereza Afande Nyonyi alishuru sana Chama cha Biblia cha Tanzania kwa msaada huo kwa Wafungwa.

 

 

 

 

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Kongwa Afande Nyonyi

 

 

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, mkuu wa jimbo wa kanisa la KKKT Kongwa (wa kwanza kulia) na viongozi wa gereza la Kongwa