SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

Program hii inatekelezwa na Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na dawati la vijana (Africa Youth Service -United Bible Society).

Madhumuni ya programu ni kuwasaidia, kuandaa, na kuwajengea vijana wadogo miaka 9-24 uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kwa ajili yao na kwa ajili ya maendeleo ya jamii, tukilenga kwenye masuala ya usawa na unyanyasaji wa kijinsia, ushiriki wa watu wenye ulemavu, elimu ya afya ya uzazi na ngono, mitandao ya kijamii, itikadi kali, na utunzaji wa mazingira.

Shughuli kubwa ya programu hii ni kutoa mafunzo kwa vijana wadogo, kupitia warsha shirikishi kwenye jamii yao kwa kushirikiana na makanisa pamoja na wadau wengine.

Walengwa wa mpanguu ni makanisa, shule, vikundi vya vijana, vituo vya watoto yatima,mashirika ya serikali,pamoja na wazazi/walezi.

IMG 3985 scaled

Wadau wa Mradi

IMG 4979 scaled

Majadiliano

IMG 5102 scaled

Pia program hii inalenga.

Kuwapa taarifa sahihi vijana wadogo kuhusu mabadiliko ya kubalehe na afya ya uzazi, ujinsia,

usawa wa kijinsia, watu wenye ulemavu, urafiki na kujithamini, mazingira na mabadiliko ya hali ya hewa

  1. Kuhimiza vijana kufanya maamuzi yenye afya na kuepuka ushawishi mbaya kutoka kwa marafiki, vyombo vya habari vya habari & mitandao na makundi yenye itikadi kali
  2. Kuwaandaa wadau wa program hii kuweza kutimiza wajibu wao wa kusaidia na kuchangia maendeleo chanya na shirikishi kwa vijana.

    Kulingana na nyenzo na shughuli zilizopangwa, malengo yafuatayo yatatumika:

    1. Kuwaandaa wazazi/walezi kuhimiza na kuwezesha maendeleo chanya na shirikishi kwa vijana.
    2. Kutoa mafunzo ya stadi za maisha kwa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu
    3. Kutoa maarifa ya kimsingi kuhusu VVU
    4. Kujenga ufahamu na kutetea haki za watoto, ikiwa ni pamoja na hatari ya unyanyasaji wa kingono
    5. Kuwapa wazazi na walezi ujuzi wa kufuatilia na kuwalinda watoto.
    IMG 4979 scaled
    MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

    MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

    LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA PROJECT.

    TAARIFA FUPI YA MPANGO & MAHAFALI YA SITA YA MPANGO HUU

    Mahafali ya sita ya mpango huu yalifanyika tarehe 17.2.2024 katika Ukumbi wa Nazarethi, Gairo mjini ambapo wanakisomo 421 walitunukiwa vyeti vya kuhitimu Kisomo cha watu wazima na Mkuu wa (w) ya Gairo. Mh. Jabiri Shekimweri.  Sherehe hizi zilihudhuriwa na wageni wengine akiwemo Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred E. Kimonge, Bodi ya wakurugenzi wa Chama cha Biblia cha Tanzania, wafanyakazi na viongozi wa makanisa na jamii kutoka wilaya ya Gairo na Kilosa.

    Mpango huu umeendelea kutekelezwa na Chama cha Biblia cha Tanzania katika (w) ya Gairo na Kilosa. Lengo kuu ni kuwasaidia wanawake na wasichana hawakuweza kwenda shule  na hawajui Kusoma na Kuandika.

    26 scaled

    Mmoja wa wanakisomo akipokea cheti cha kuitimu elfu hiyo.

    23 scaled
    13 scaled
    12 scaled
    beauty esthetician 43

    SHUGHULI ZA UTEKELEZAJI

    Katika kipindi cha mwaka 2023, Chama cha Biblia kupitia mpango huu kiliweza kutekeleza shughuli zifuatavyo;

    • Kufanya uhamasishaji na kuandikisha wanakisomo 450 (Me 379 & Ke 71) kabla ya madarasa kuanza.
    • Mpango huu umelenga zaidi wanawake na wasichana, ila wapo pia wanaume ambao wamejiunga na madarasa na wamekuwa wanufaika wazuri. Takwimu zinaonyesha kuna idadi kubwa ya wanaume wasiojua kusoma na kuandika na mpango huu unawakaribisha.
    • Kufanya mafunzo kwa waalimu 30 wanaofundisha kwenye madarasa ya watu wazima. Mafunzo haya yalifanyika Dodoma kwa wiki mbili yakiongozwa na wakufunzi kutoka SIL Nairobi, Kenya.
    • Kuchapisha na kuwagawa vitabu 450 vya kujisome kwa wanakisomo wote waliojiandikisha.
    • Kuhamasisha na kuanzisha vikundi (improving literacy groups) vya kujisome vitabu vya hadithi. Vikundi hivi ni kwa ajili ya wahitimu ili kuweza kuendeleza ujuzi na kupata uzoefu zaidi katika kujua kusoma na kuandika. Hapa wananapata nafasi ya kujisomea vitabu vya aina mbalimbali, majarida, magazeti, Biblia pamoja na makala nyingine nyingi.

    Wawezeshe Kusoma

    MAFANIKIO.

    • Kuongezeka kwa wanajamii wanaojua kusoma /kuandika kila mwaka kwenye eneo la mpango.
    • Wanawake kupata na kugombea nafasi mbali mbali za uongozi kwenye jamii yao kutokana na uwezo wao.
    • Kumekuwa na jamii inayojiamini zaidi na yenye uelewa juu ya masuala mbali mbali.mfano Afya, kilimo, mazingira kuanzia kwenye ngazi ya familia.
    • Kumewasaidia kusoma Neno la Mungu pamoja na hii imeongeza ukuaji wa kiroho.
    beauty esthetician 38
    14 scaled
    28 scaled
    9 scaled
    22 scaled
    6 scaled
    4 scaled
    21 scaled
    17 scaled

    Blog

    Product Updates & Sales

    SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

    SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

    SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.Program hii inatekelezwa na Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na dawati la vijana (Africa Youth Service -United Bible Society). Madhumuni ya programu ni kuwasaidia, kuandaa, na kuwajengea vijana wadogo miaka 9-24 uwezo wa kufanya...

    read more
    MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

    MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

    LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA PROJECT.TAARIFA FUPI YA MPANGO & MAHAFALI YA SITA YA MPANGO HUUMahafali ya sita ya mpango huu yalifanyika tarehe 17.2.2024 katika Ukumbi wa Nazarethi, Gairo mjini ambapo wanakisomo 421 walitunukiwa vyeti vya kuhitimu Kisomo cha watu...

    read more
    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya KaskaziniHabari Kamili.Chama cha Biblia cha Tanzania kimeendelea na huduma yake ya kugawa Biblia kwa baadhi ya magereza hapa nchini. Chama kimeendelea kutoa huduma hiyo kutokanana  sadaka na michango ya  wanachama wake, wadau mbali mbali...

    read more
    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Habari Kamili.

    Chama cha Biblia cha Tanzania kimeendelea na huduma yake ya kugawa Biblia kwa baadhi ya magereza hapa nchini.

    Chama kimeendelea kutoa huduma hiyo kutokanana  sadaka na michango ya  wanachama wake, wadau mbali mbali na watu binafsi wenye mapenzi na neema ya kufanya kazi ya Mungu walioko ndani na nje ya nchi.

    Picha zinaonesha baadhi ya magereza yaliyoko katika kanda ya Kaskazini waliofikiwa na kugawiwa Biblia kutoka katika Chama cha Biblia chanTanzania.

    Tunamshukuru Mungu kwa neema hii. Tunaamini kupitia Biblia hizi watu watafikiwa na Neno la Mungu ambalo litabadilisha maisha yao, watazidi kumjua Mungu na kumtumikia. Tunaomba Mungu awabariki na aendelee kuwatumia ili kuwafikia walengwa wengi zaidi na kazi ya Mungu izidi kusonga mbele kwa ushindi mkuu.

    Wapare

    Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza (W) Same Kilimanjaro

    Hata Katesh wafungwa wanalitaja jjina la Yesu

    Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Kateshi

    Kazi njema Magereza ya kaskazini imeanzia Babati Yesu asifiwe

    Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza la Manyara Babati

    Wafungwa wa Arusha Mjini

    Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza Arusha mjini

    Wafungwa wa Mbulu wanamtukuza Mungu pia
    BST IMAGE

    Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

    MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

    MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

    MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

    Habari Kamili.

    Chama cha Biblia cha Tanzania kinaendelea kutekeleza mpango wa Kisomo cha elimu ya watu wazima katika wilaya ya Kilosa na Gairo kwenye vijiji 15 vilivyochaguliwa wakati wa kuanzishwa kwa mpango huu. Mpango wa Kisomo cha elimu ya watu wazima umeweza kuwafikia wanaume na wanawake 1500. Wanakisomo waliofikiwa na mpango huu wanajua kusoma na kuandika, maisha yao yamebadilika na wanaishi maisha ya kawaida kama walivyo watu wengine waliosoma. Pia ushirikishwaji wao katika masuala ya kijamii umeongezeka, wengine wamepata nafasi za uongozi kwenye jamii na Kanisa limeweza kuwa na washirika wanaoweza kusoma na kulielewa Neno la Mungu pia kufanya majukumu yao ya utumishi kwa weledi zaidi kulinganisha na ilivyokuwa kabla ya kujua kusoma na kuandika.

    Waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo scaled

    Waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo

    Ili kufanikisha mpango huu Chama cha Biblia kwa kushirikiana na SIL Nairobi walifanya mafunzo ya kuwajengea uwezo waalimu 30 wa Chikagulu. Mafunzo  hayo yalifanyika Dodoma kwa wiki mbili ambapo  waalimu waliweza kufundishwa  mada tofauti tofauti kulingana na mfumo wa mpango ulivyo, baadhi ya mada walizofundishwa ni mifumo ya literacy, sifa za mwalimu bora, sifa za mwanakisomo, majukumu ya mwalimu kabla  na akiwa ndani ya darasa.

    Kwa kipindi cha mwaka huu 2023, Chama cha Biblia cha Tanzania kimeweza kuandikisha wanakisomo 450. Wanakisomo waliojiandikisha  hawawezi kusoma, hawajawai kwenda shule na hawajawahi kukutana na jarida/ gazeti, kitabu chochote na hawajui kuandika. Madarasa yataanza mwezi June,2023 kwa kipindi cha miezi saba.

    Waalimu wa waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo scaled

    Waalimu wa waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo

    Askofu huyo aliwakumbusha washiriki wa mkutano huokumwomba Mungu zaidi kwa kuwa wanahubiri injili katika kizazi kinachobadilika lakini wao wanahubiri neno la Mungu lisilobadilika, jambo linaloibua changamoto mbalimbali ikiwemo lugha.
    Alitoa mfano kuwa wakati wao kama chama wanajitahidi kuhubiri injili kwa lugha ya
    Kiswahili inayosikika kwa watu wengi, lakini Kiswahili chenyewe kinabadilikabadilika.

    BST IMAGE

    Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

    MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

    MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

    MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

    Habari Kamili.

     Mwenyekiti wa Bodi ya Chama
    cha Biblia Tanzania, Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana amesema chama hicho kitajitahidi kuendelea kuchapisha na kusambaza neno la Mungu ili liweze kumfikia kwa kila mtu na injili izidi kuhubiriwa.

    Alisema hayo katika Mkutano
    Mkuu wa Mwaka 2022 wa chama
    hicho uliofanyika katika ukumbi
    wa mikutano wa Kanisa la Kiinjili
    la Kilutheri Tanzania (KKKT) jijini Dodoma, Ijumaa wiki hii.

    Malekana, ambaye ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato alisema kuwa mafanikio ya kidunia yanataka juhudi na akili zako za mtu, lakini bila Mungu juhudi na akili hizo haziwezi kumfikisha popote.

    Akinukuu maandiko kutoka katika kitabu cha Kutoka 33:15, mwenyekiti huyo wa bodi aliwakumbusha washiriki wa mkutano huo na jamii kwa ujumla, kuishi kwa kumwomba Mungu.

    “Katika maisha yako omba Mungu awe pamoja nawe, iwe ni biashara unafanya au utumishi popote pale. Yesu alisema pasipo mimi hamuwezi kufanya neno lolote, na sisi kama Chama cha Biblia tunamwomba Mungu awe pamoja nasi katika majukumu ya chama katika kutafsiri Biblia, kuchapisha, sambamba na kutawanya maandiko matakatifu”.

    “Kizazi hiki kinatakiwa watu warudi kwenye Neno la Mungu na kumtazama Kristo, na kwa upande wetu Chama cha Biblia tunajitaidi kuchapisha na kusambaza Neno la Mungu kwa kila mtu, wakiwemo watoto, wafungwa..na vijana ni kipaumbele cha Chama cha Biblia cha Tanzania

    MG 0054 scaled

    Picha kutoka kushoto ni Dkt. Alfred E. Kimonge katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, wa pili kutoka kushoto ni Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania, wa tatu kutoka kushoto ni Askofu Christian Ndossa wa Kanisa la Kilutheli la Kiinjili Tanzania Dayosisi ya Dodoma na Mwisho Askofu Amos Muhagachi, Makamu Mwenyekiti wa Bodi.

    MG 0063 scaled

    Askofu Christian Ndossa wa Kanisa la Kilutheli la Kiinjili Tanzania Dayosisi ya Dodoma akihudumu wakati wa mkutano huo.

    MG 0101 scaled

    Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania akionesha riport ya taarifa ya fedha

    MG 0102 scaled

    Dkt. Alfred E. Kimonge katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, akiwasilisha taarifa ya utendaji na fedha kwa mwaka wa 2022.

    MG 0070 scaled
    MG 0184 scaled
    MG 0105 scaled
    MG 0136 scaled
    MG 0138 scaled
    MG 0126 scaled
    MG 0125 scaled
    MG 0180 scaled
    MG 0229 scaled
    MG 0195 scaled
    MG 0201 scaled

    Katika maisha yako omba Mungu awe pamoja nawe, iwe ni biashara unafanya au utumishi popote pale. Yesu alisema pasipo mimi hamuwezi kufanya neno lolote, na sisi kama Chama cha Biblia cha Tanzania tunamwomba Mungu awe pamoja nasi katika majukumu ya chama
    katika kutafsiri Biblia, kuchapisha, sambamba na kutawanya maandiko matakatifu”.

    Askofu Christian Ndossa

    Askofu, KKKT

    Naye Askofu wa KKKT Dayosisi ya Dodoma, Christian Ndossa alisema neno la Mungu ndio msingi na taa za miguu ya chama hicho.

    Askofu Ndossa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo alisema kuwa, chama hicho kinaweza kuwa na vitabu vingi pamoja na mipango mbalimbali, lakini bila neno la Mungu kitakosa kitu cha kukisaidia.

    “Tunaweza kuwa na mipango mbalimbali, tukawa na vitabu vingi, tukasoma maandiko ya wataalamu lakini tukakosa kitu
    cha kutusaidia kama tutakosa neno la Mungu ambalo ndio taa ya miguu yetu na mwanga katika maisha yetu sisi tulio wanachama wa Chama cha Biblia Tanzania,”
    alisema.

    Askofu huyo aliwakumbusha washiriki wa mkutano huokumwomba Mungu zaidi kwa kuwa wanahubiri injili katika kizazi kinachobadilika lakini wao wanahubiri neno la Mungu lisilobadilika, jambo linaloibua changamoto mbalimbali ikiwemo lugha.
    Alitoa mfano kuwa wakati wao kama chama wanajitahidi kuhubiri injili kwa lugha ya
    Kiswahili inayosikika kwa watu wengi, lakini Kiswahili chenyewe kinabadilikabadilika.

    Kwa upande wake Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Alfred Kimonge alisema wanayo
    kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa rehema na baraka zake kwa mwaka wa 2022.

    “Hakika umekuwa mwaka wa baraka kwetu, umekuwa mwaka wa kuinuliwa na kuendelea kufanya kazi ya Mungu kwa ujasiri na bidii baada kipindi cha mpito ambacho dunia ilikubwa na ugonjwa wa hatari wa mlipuko wa Covid-19. Hakika Mungu ni mwaminifu sana kwetu,” alisema.

    BST IMAGE

    Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

    Uenezaji wa Maandiko kwa 2022

    Uenezaji wa Maandiko kwa 2022

    Taasisi yetu kwa mwaka uliopita uliambatana na Baraka zake. Muungano wetu wa vyama vya Biblia ulimwenguni ulituweka katika mpango wa kuwafikia watu milioni moja ulimwenguni walio katika mazingira magumu au walengwa ambao hawana uwezo wa kununua Biblia. Tanzania tulipewa nakala 50,000 za Biblia. Biblia hizo tulizigawa katika mashule na magereza.

    Mch. John Mnongone akimkabidhi SSP Nelson Kanyungu askari anayehudumia Ibada katika gereza la Kigoma
    20220928 134320 scaled

    Mch. John Mnong’one akimkabidhi SSP Nelson Kanyungu askari anayehudumia Ibada katika gereza la Kigoma. Picha ya Pili akikabidhi viongozi wa Makanisa yaliyomo katika Kambi ya wakimbizi Nyarugusu Kasulu

    20220713 140251 1 scaled
    Watoto wa Shule ya Msingi Suguta Kongwa1
    Watoto wa Shule ya Msingi Suguta Kongwa2

    Watoto wa shule ya Mshingi Suguta Kongwa wakifurahia kupata Biblia.

    Uenezaji wetu Mwaka huu ulikuwa kama ifuatavyo.

    Biblia 500, 0000

    Agano Jipya 59,000

    Sehemu za Bibia portion 1,800

     

    FCBH

    Akina mama hawa wa Kabila la Kibarbaig walisikiliza mpango wa FCBH walihitimu kupewa Biblia bure. Walikataa kupokea Biblia ya bure wakalipia Biblia zao kwa furaha.

    Tulipowambia kuwa wana stahili,

    walisema heri kutoa kuliko kupokaea

    BIBLIA INAYOONGEA.

    Tunamshukuru Mungu kwa taasisi yetu kuingia  mkataba na  Shirika la Talking Bible International kuwa Chama cha Biblia cha Tanzania tumekuwa kituo cha kuandaa na kugawa Biblia TB inayoongea kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Mpaka sasa tumeandaa na kugawa nakala 450 za TB kwa nchi za Kenya, Uganda na Zambia.

    Watumishi wakiandaa TB

    Hapa watumishi wa Chama cha Biblia wakiandaa TB katika lugha ya Kibemba na Kitonga tayari kwa kuzipeleka Zambia

    Mwaka huu CBT kiliendesha semina kwa wasioona 18 na kuwafundisha kusikiliza Agano Jipya .

    TB

    Give Today

    Children

    Prison

    Membership

    Youth

    Blind

    Other

    Get In Touch

    Kimachame Bible Launch

    Kimachame Bible Launch

    Kimachame Bible Launch

    The launch of the Bible in the Kimashami language (Kichagga of Machame), was held in the Congregation of Hai in 04/12/2022.

    Bishop Dr Shoo said many people have been neglecting their languages ​​and said it is good to learn and develop their native languages. At the launch of the Bible, the General Secretary of the Bible Society of Tanzania Dr. Alfred Elias Kimonge said apart from the launch of the Bible, they are still facing challenges including people not paying attention to their languages ​​and not giving them priority.

    Kimachame Bible
    Kimachame Bible
    10 scaled
    11 scaled

    “Some have assumed that communicating in native languages ​​is a weakness, dear friends, it is not true that native languages ​​are a weakness. The native language is what builds a person’s heart and is the mother tongue for all living,” he said.

    OUR COMPLETION

    Now, It leads to 13 complete local language Bibles have been translated and 41 others have New Testament Bibles.

    8 scaled
    9 scaled

    There is so much in the Bible that feeds my soul, so many teachings. In the Bible we have everything. The Kimashami Bible brings me great joy to me. On the launch of the Kimashami Bible in Hai Kilimanjaro.

    12 scaled

    Comments

    Join

    Work With Me

    Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi

    Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi

    Mkuu wa KKKT ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, Dkt. Fredrick Shoo, amewataka Wakristo kuitunza na kuindeleza lugha zao za asili kwani ndio msingi na urithi walio nao.

    Askofu Dkt. Shoo aliyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi (Kichagga cha Old Moshi), iliyofanyika katika Usharika wa Bethel Msaranga, iliyoambatana na kuweka wakfu eneo la ujenzi wa Kanisa la Mtaa huo.

    Askofu Dkt. Shoo alisema watu wengi wamekuwa wakipuuzia lugha zao na kusema ni vyema kujifunza na kuziendeleza lugha zao za asili. Katika Uzinduzi huo wa Biblia, Katibu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred Kimonge alisema mbali na Uzinduzi wa Biblia hiyo bado wanakabiliwa na changamoto ikiwemo wenye lugha zao kutotilia maanani na kutozipa kipaumbele.

    “wengine wameshajiwekea kuwa kuwasiliana kwa lugha za asili ni udhaifu, wapendwa si kweli kwamba lugha za asili ni udhaifu. Lugha ya asili ndio inajenga moyo wa mtu na ndio lugha mama kwa wote wanaoishi,” alisema.

    Addresses

    16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
    P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

    Phone

    +255 (0) 765 530 892

    Email

    info@biblesociety-tanzania.org

    MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

    MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

    MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.

    1. UTANGULIZI.

    Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) ni shirika la Kikristo lililoandikishwa mwaka 1970 na kupewa nambari S0 5722. Ni mwanachama wa Muungano waVyama vya Biblia Ulimwenguni(United Bible Societies (UBS). Shirika hili ni chombo cha Kanisa la Tanzania ambalo kazi yake kubwa na ya msingi ni kuwapelekea watu wote hapa nchini Tanzania Habari njema ya Yesu Kristo kwa kutafsiri, kuchapisha na kusambaza Biblia ikiwa katika lugha anayoielewa msomaji, bei anayoiweza na mfumo anaoupendelea.

    MG 6293 copy scaled

    Tangu kusajiliwa kwake  hapo mwaka 1970, Chama cha Biblia cha Tanzania kimekuwa kikitekeleza majukumu yake hayo kwa ushirikiano mkubwa na wa karibu na makanisa yote ya Kiprotestanti, Katoliki, Sabato na Kipentekoste hapa Tanzania; na pia kwa ushirikiano mkubwa na wa karibu na Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (United Bible Societies-UBS) ambalo ni ushirika wa vyama vyote vya Biblia katika nchi zote.

    Chama kimeweza kufanya tafsiri na kinaendelea kutafsiri Biblia katika lugha mbalimbali za makabila ya hapa Tanzania. Kutafsiri Biblia katika lugha mbalmbali za makabila kunafanyika kwa malengo makuu mawili. Lengo la kwanza la kufanya tafsiri hizi ni kwa kuamani kuwa watu wanaweza kulielewa Neno la Mungu kwa urahisi zaidi wakisoma au kuelezwa katika lugha zao na kuainisha na mazingira halisi ya mazingira yao.

    IMG 9715

    Lengo la pili ni kusaidia kutunza lugha za makabila kwa faida ya vizazi vijavyo vya kabila husika, kwani mila na utamaduni wa kabila zipo katika lugha ya watu wa kabila husika. Tangu kuanzishwa kwake Chama cha Biblia kimefanya tafsiri kadha na kuzisambaza hapa nchini zikiwamo Biblia katika lugha za:

    1. Kiswahili
    2. Kimaasai,
    3. Cigogo
    4. Iraqw

    5. Nyakyusa

    6. Igikuria

    7. Ruhaya

    8. Kisukuma

    9. Kidatooga

    10. Kimashami

    11. Kivunjo

    12. Kimochi

    Baadhi ya Biblia ambazo kwa sasa zipo katika hatua mbalimbali za tafsiri ni:

    1. Kihehe
    2.   Cikaguru
    3.   Kinyamwezi
    4.   Chasu(Kipare)

    5.  Kifipa

    6. Kinyiha

    7. Kinyiramba

    8. Kirimi( Kinyaturu)

    9. Kiha

    Agano Jipya.

    1. Kimeru
    2. Kibena
    3. Kishambala
    4. Kikinga

    5. Kijita

    6. Kifipa

    7. Kizaramo

    2.0 Umuhimu wa Neno la Mungu kwa maendeleo

    Tunapoangalia historia ya ustawi wa maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ulimwenguni kote, tunaona kuwa jamii ambazo zilijengwa katika misingi ya Neno la Mungu zilistawi kimaendeleo ikilinganishwa na zile ambazo ama hazikuamini au zilimuasi Mungu. Neno la Mungu likiwa ndani ya myoyo ya watu huzaa upendo ambao huzifanya jamii kuwa zenye amani na utangamano, tunu ambazo husaidia kuweka mazingira wezeshi kwa watu kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo.

    36 1 scaled

    2.1 Hali ya malezi kwa watoto na vijana.

    Hivi sasa nchi nyingi ulimwenguni ikiwemo Tanzania kuna mporomoko mkubwa wa maadili. Wazazi ndani ya jamii wanalalamika juu ya watoto wa kizazi hiki kuwa wamekosa maadili.

    Lakini wazazi hawa wanasahau kuwa kuporomoka kwa maadili ya watoto wao kunatokana na wao kutokuwalea katika misingi mizuri ambayo ni Neno la Mungu. Huko Ulaya na Marekani wazazi/mataifa walibweteka na maendeleo ya kiuchumi, teknolojia, sayansi na maisha bora kimwili na kusahau tunu kubwa inayotokana na maendeleo ya kiroho(spirituality). Makuzi ya kiroho hujenga maadili na hivyo kujenga utu wa mtu.

    Katika nchi hizi watu wengi hasa kundi la vijana sasa hivi hawaendi Kanisani au Misikitini Kuabudu. Wamejitenga kabisa na Mungu na katika baadhi ya nchi Makanisa yameuzwa na kutumika kwa shughuli nyingine kabisa kama vile maduka na hata pia kugeuzwa kuwa sehemu za burudani kama vile sehemu za kuuzia vileo na starehe zingine.

    Aidha katika nchi  hizi tunashuhudia ongezeko kubwa la mporomoko wa maadili ya asili ya mwanadamu. Katika nchi hizi sasa tunashuhudia uhalalishwaji kisheria wa ndoa na mapenzi ya watu wa jinsia moja, ongezeko la vitendo  vingine viovu ambavyo ni chukizo mbele za Mungu. 

    Nchi za kiafrika nazo hazijasalimika na hali hiyo. Mporomoko mkubwa wa maadili katika nchi za Afika unazidi kuongezeka na kushamiri kutokana na utandawazi. Nchi zetu sasa zinashuhudia ongezeko kubwa la vitendo viovu kila siku,vingi vikifanywa na kundi la vijana. Wazazi walio wengi wameacha wajibu wao wa asili wa kuwalea watoto wao na kuwarithisha maadili ambayo huleta ustawi wa mtu mmoja mmoja na jamii/taifa.

    Wazazi wengi hawaendi na watoto wao Makanisani na Misikitini wala hawaoni umuhimu wa watoto wao kupata mafundisho ya dini tangu wakiwa watoto ili wakue na kustawi katika msingi wa Neno la Mungu. Maovu mengi tunayoyashuhudia katika jamii ni kutokana na watu kukosa msingi wa Neno la Mungu ambalo likikaa katika myoyo huwafanya watu kuwa na  hofu ya Mungu na hofu hiyo huwafanya wajiepusha na matendo maovu kwa kujua kwamba hayampendezi Mungu na yana hukumu.

    Hivi sasa tunashuhudia hofu ya Mungu ikizidi kupungua katika nchi yetu, na hivyo kutishia amani na utangamano katika taifa letu. Vitendo viovu vinaongezeka kwa kasi katika taifa letu kwa sababu watu wamekosa hofu ya Mungu.

    Rais wetu mpendwa wa awamu ya Tano Marehemu Mheshimiwa John Joseph Pombe Magufuli amekuwa akituasa mara nyingi kwamba tumwogope Mungu, maana yake tufanye yale yanayompendeza Mungu na tuache matendo maovu. Matendo mema huleta afya kwa jamii/taifa lolote.

    20211222 050907 scaled

    2.2 Kwa nini Biblia kwa Watoto, Vijana na Wafungwa?

    Katika nchi nyingi duniani na hasa nchi zinazoendelea  watoto umri kati ya miaka 1-14 huwa ni rika yenye watu wengi zaidi, wakifuatiwa kwa wingi na kundi la vijana(miaka 15-24).

    Makundi haya mawili haya kwa pamoja hapa Tanzania idadi yake ni zaidi ya asilimia 60 ya idadi ya watu wote. Kutokana na wingi na umri,  makundi haya yanayohitaji kuangaliwa /kutazamwa kwa karibu sana kwa maana ya malezi kwa maana ya kupewa huduma muhimu zitakazowafanya wakue na kustawi kiroho na kuwa raia wema wenye kupenda amani na  ustawi wa taifa.

    Wafungwa ni kundi la watu ambao wako gerezani kwa sababu ya kutenda makosa katika jamii na kukosesha wengine amani na utangamano. Kwahiyo, hili nalo ni kundi muhimu la kutazamwa katika malezi hasa ya kiroho ili wahusika (wafungwa) wanapomaliza kutumikia  vifungo vyao waweze kuacha tabia mbaya za uhalifu na kuwa raia wema.

    IMG 8365 scaled

    2.3 Mapendekezo ya  na ushauri wa Chama cha Biblia kwa serikali katika kukabiliana na mporomoko wa maadili kwa wototo na vijana.

    Chama cha Biblia cha Tanzania kinaishukuru sana Serikali yetu kwa kuruhusu Neno la Mungu kufundishwa mashuleni, jambo ambalo nchi zingine haziruhusu. Tunaamini hatua hii ni kwa kutambua kwamba mashuleni ndiko wanapoandaliwa viongozi wa taifa la kesho, kwa hiyo kuona umuhimu wa kuwapa malezi ya kiroho. 

    Tunakumbuka miaka ya nyuma serikali iliruhusu uanzishwaji wa chama cha “ Elimu ya Dini Mashuleni Tanzania”(EDIMASHUTA) ikiwa ni njia mojawapo ya kutoa fursa kwa watoto ya kupata mafundisho ya dini ili waweze kukua kimaadili kupitia dini zao. Hii ilikuwa ni fursa muhimu sana kwa wototo kujifunza somo la dini na hivyo kukua na kustawi katika misingi ya kuwa na hofu ya Mungu.

    Chama cha Biblia cha Tanzania kilikuwa mshirika mkubwa katika mpango wa Elimu mashuleni kwa kutoa Biblia  zilizotumiwa kama kitabu cha kiada mashuleni katika mafundisho hayo. Katika mpango huu, serikali ililifanya somo la dini kuwa la kutahiniwa na ilikuwa na “alama” (credit).

    Kutokana na utambuzi huo vijana mashuleni walikuwa na bidii ya kujifunza somo la dini. Kwa njia hiyo waliweza kujengwa vizuri kiimani, kimaadili na kiustawi kwa ujumla na kundi hilo lilizaa viongozi waadilifu wa nchi yetu, kanisa na sekta binafsi.

    Hata hivyo baadaye utaratibu wa  somo la dini kuwa  la kutahiniwa na lenye hadhi ya credit sawa na masomo mengine uliondolewa na hivyo kuwavunja moyo watoto na vijana katika kujifunza somo la dini.

    Tunapendekeza kwamba somo la dini liendelee kufundishwa na lipewe hadhi/lihesabiwe sawa na masomo mengine katika mitihani, ili liweze kuchochea ari kwa watoto na vijana kujifunza somo la dini na hivyo kujengwa kimaadili.

    20220713 140251 scaled

    2.4 Kwa nini Biblia sasa kwa vijana mashuleni.

    Kwa kuangalia mwenendo wa maadili kwa vijana wetu mashuleni,na kuna umuhimu wa kurejesha somo hilo kwani umuhimu wake umeanza kuonekana. Kumekuwa na  mmomonyoko wa maadili kwa vijana wetu sasa, tofauti na kipindi cha nyuma ambapo walilelewa katika misingi ya neno la Mungu.

    Sasa hivi tunashuhudia vitendo viovu vikiongezeka katika jamii, ambapo watoto na vijana wanahusika. Jambo la pili tunaona mifano  ya wenzetu nchi za Ulaya ambako utandawazi umewafanya wasitambue  utu wa mtu.

    Baadhi ya shule ambazo zimeendelea kufundisha somo la dini ni ushuhuda tosha kuonyesha namna somo la dini lilivyo muhimu katika ustawi wa mwanadamu. Shule hizi zimekuwa mfano mzuri kwa maadili na ufaulu mzuri  wa masomo hata yasiyo ya dini.

    Chama cha Biblia kinaona kwamba kuna umuhimu wa kurudisha somo la dini kwa shule zote za serikali na za binafsi na kulifanya somo la dini kuwa na hadhi ya kutahiniwa sawa na masomo mengine.

    Hiyo ni shule ya RUHUWIKO High School Songea wakifurahia kupewa Maandiko toka Chama cha Biblia. Wametoa shukrani nyingi kwa Uongozi kupitia mwl wao

    3.0 Mpango wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa kuwapatia Biblia Watoto na Vijana mashuleni na Wafungwa magerezani.

    Kwa kutambua umuhimu huo, Chama cha Biblia cha Tanzania katika mpango mkakati wa miaka mitano (2018 – 2022) kilianzisha mpango maalum wa kuhamasisha Makanisa na watu wenye mapenzi mema kushiriki kwa kuchangia fedha kwa ajili ya upatikanaji wa Biblia ili  zisambazwe kwa wingi  kwa watoto, vijana na wafungwa ikiwa ni moja ya vipau mbele vyake katika kipindi hiki cha miaka mitano.

    Mpango huu unalenga makundi matatu ya watoto na vijana kwa rika na wafungwa walioko magerezani.

    Na.

    Watoto

    Vijana

    Wafungwa magerezani

     1.

    Miaka 3 – 5

    Miaka 16 – 24

    Wanaume

     2.

    Miaka 6 – 9

     

    Wanawake

     3.

    Miaka 10 -15

     

     

    Katika mkakati wa kutekeleza mpango huu Chama cha Biblia cha Tanzania kilianza kwa kuwashirikisha viongozi wa makanisa kutokana na nafasi yao ya asili ya kuwajenga na kuwalea watu kiroho.

    Pili kimewashirikisha wadau wengine wenye mapenzi mema wanaotamani kuona Tanzania inajengwa katika misingi imara ya kiroho na hivyo kuwa na taifa lenye watu wenye hofu ya Mungu.

    Mpango huu umepata uungwaji mkono mkubwa sana na Kanisa la Tanzania, hali ambayo imetutia moyo sana Chama cha Biblia cha Tanzania, kwani tunatambua kwamba Kanisani ndiko Neno la Mungu linafundishwa na ndiko Wakristo wanaofanya Kanisa la Tanzania waliko.

    Tunaamini mpango huu unatekelezeka na walengwa na taifa zima litanufaika.

    21

    3.1 Watoto na Vijana walengwa.

    Mpango huu katika awamu hii ya kwanza unalenga watoto na vijana walioko katika shule kwa sababu ya urahisi wa kujua idadi yao na urahisi wa kuwafikia.

    Hata hivyo shule zitazopewa kipaumbele ni zile zilizoko vijijini, ambazo mbali kuwa  nyingi, lakini ndizo zenye watoto na vijana wengi wenye wazazi wenye hali duni ya  uchumi; na hivyo hawana uwezo wa kuwapata/kuwanunulia watoto  mahitaji yao kwa utoshelevu.

    Ni kutokana na ukweli huo Chama cha Biblia cha Tanzania kinalenga kuwapatia watoto na vijana Biblia kwa bei nafuu ambayo wazazi wengi pamoja na hali yao duni kiuchumi wanaweza kuimudu.

    ugawaji wa Sehemu ya Biblia Agano Jipya lenye Mithali na Zaburi

    3:2 Ufundishaji wa somo la dini  mashuleni.

    Kama tulivyoeleza katika utangulizi, Chama cha Biblia kinaona kwamba kuna umuhimu wa kurudisha somo la dini kwa shule zote za serikali na za binafsi na kulifanya somo la dini kuwa na hadhi ya kutahiniwa sawa na masomo mengine.

    Tunaishauri serikali irudishe na  kuimarisha Elimu ya Dini Mashuleni( EDIMASHUTA) na kurudisha mitaala iliyokuwepo pamoja na kuruhusu taasisi za dini  kupeleka waalimu kwa ajili ya kufundisha somo la dini.

     Mpango huu ukitekelezwa utasaidia kuwajengea watoto wetu misingi ya maadili mema ili hatimaye tuwe na taifa lenye viongozi na raia wema. Jambo hili litasaidia kujenga jamii yenye amani na utangamano na kuruhusu mazingira ya kupata ustawi kama taifa.

    Picha ya watoto wanasoma Biblia. 1

    3:3 Vyanzo vya upatikanaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huu

     Katika mpango huu, Chama cha Biblia cha Tanzania kinalenga kupata fedha kutoka:

    • Taasisi za kanisa
    • Mashirika mbalimbali
    • Watu binafsi

     Aidha Chama katika nia hii njema kinaomba kuungwa mkono na serikali kwa kushiriki katika kazi ya kuhamasisha taasisi, mashirika na wadau mbalimbali ili waweze kushiriki kuchangia mpango huu.

    IMG 9767

    3.4 Kiasi cha fedha, idadi  ya  Biblia na mgawanyo kwa makundi lengwa

    Katika awamu hii ya kwanza Chama cha Biblia kimelenga kuomba kuchangiwa kiasi cha shilingi 10,200,000,000 ambazo zitatumika kununulia jumla ya Biblia 510,000 ambazo mgao wake kwa makundi lengwa utakuwa kama ifuatavyo:

    • Watoto – Biblia laki nne (400,000)
    • Vijana – Biblia laki moja (100,000)
    • Wafungwa – Biblia elfu kumi (10,000)

    Kwa sasa Chama tayari kinayo miswada ya Biblia za makundi lengwa  yote yaani watoto, vijana na wafungwa. Biblia hizi zinaweza kuchapishwa na wachapishaji wakati wowote fedha zitakapokuwa zimepatikana.

    Malipo yakishafanyika inakadiriwa kuwa kazi ya kuchapa, kusafirisha na kupokelewa inachukua muda wa miezi mitatu hadi minne.

    20220721 115109 scaled

    3:5 Mikoa na mgao wa Biblia kwa makundi lengwa.

    Zoezi hili ni endelevu, lakini katika awamu hii ya kwanza Chama kimelenga kugawa Biblia kwa watoto, vijana na wafungwa katika  mikoa ifuatayo :-

     

    Na

    Mkoa

    Watoto

    Vijana

    Wafungwa

     

    Makisio

    Halisi

    Makisio

    Halisi

    Halisi

    1.

    Dodoma

    730,000

    100,000

    180,000

    25,000

    3,000

    2,

    Mara

    580,000

    82,000

    145,000

    20,500

    3,000

    3.

    Manyara

    610,000

    88,000

    152,500

    21,500

    1,000

    4.

    Pwani

    470,000

    66,000

    117,500

    16,500

    1,000

    5.

    Singida

    470,000

    66,000

    117,500

    16,500

    2,000

    Jumla kuu

    2,860,000

    400,000

    712,500

    100,000

    10,000

    IMG 20220722 WA0016

    3:6 Usambazaji wa Biblia kwa makundi lengwa.

    3:6:1 Mashule

    Biblia zitasambazwa na Chama cha Biblia katika mashule kwa kushirikiana na Maafisa Elimu, Waalimu Wakuu wa  Mashule, Viongozi wa Makanisa na Waalimu wa Dini mashuleni.

    3:6:2 Magereza

    Biblia zitasambazwa katika Magereza kwa kushirikiana na Wakuu wa Magereza na Wachungaji wanaotoa huduma ya kiroho magerezani.

    Gereza la Mahabusu Songea 2022 07 17

    4: 0 MWISHO

    Mpango huu una umuhimu wa kipekee katika kipindi hiki ambacho tunashudumia mmomonyoko wa maadili ukienda kasi katika jamiii yetu hasa kwa kundi la watoto na vijana ambalo linatarajia kutoa viongozi wa baadae wa taifa letu.

    Tunaomba serikali ituunge mkono katika nia hii njema ya kuwajenga watoto, vijana na wafungwa kiroho. Faida ni kubwa kwa afya ya taifa. Kuchukua hatua sasa ni vizuri.

    ABOUT US

    Addresses

    16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
    P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

    Phone

    +255 (0) 765 530 892

    Email

    info@biblesociety-tanzania.org

    MPANGO WA ELIMU YA WATU WAZIMA.

    MPANGO WA ELIMU YA WATU WAZIMA.

    Mpango wa elimu ya watu wazima.

    Chama cha Biblia kimeeendelea na mpango huu wa elimu ya watu wazima katika (w) ya Kilosa na Gairo-Morogoro kwa lengo la kuwasaidia wanawake na wasichana ambao hawakubahatika kwenda shule kwa sababu tofauti tofauti waweze kusoma na kuandika.

    Kutokana na uhitaji kwenye jamii pia wanaume wamekuwa wanufaika wa mpango huu kwa sababu kuna idadi kubwa kwenye jamii ya wanaume ambao hawajui kusoma na kuandika pia.

    Waalimu wa Kikagulu wakiwa kwenye mafunzo Dodoma scaled

    Mpango huu kwa mwaka 2022 unatekelezwa katika vijiji 10 vya wilaya ya Kilos ana Gairo kwa kushirikiana na kanisa, serikali ambao wametupatia waalimu kwa ajili ya kuwafundisha wanakisomo. Wanakisomo 300 kutoka katika vijiji 10 walijiandikisha na mafunzo yanaendelea kwenye maeneo yao.

    Waalimu wakiwa kwenye mafunzo scaled

    Chama cha Biblia kupitia waalimu hao, kimewaandaa kuwa waalimu wazuri  ajili ya kuhakikisha kila mwanakisomo atakapohitimu elimu yake atakuwa anajua kusoma na kuandika. Waalimu hao kabla ya madarasa kuanza waliweza kupata mafunzo ya kuwajengea uwezo na kupata mbinu nyingi za ufundishaji ili kuweza kuwafundisha wanakisomo kwa kufuata taratibu na miongozo iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwafundisha watu wazima.

    electrician 10

    Matukio katika Picha

    Volunter-Mr-Musa-Barabara-akiwa-na-watoto-kutoka-Matumbulu-wakisoma-kijtabu-baada-ya-kugawiwa.-scaled.jpg June 23, 2022
    IMG 7727 scaled
    20220506 140032 scaled

    Addresses

    16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
    P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

    Phone

    +255 (0) 765 530 892

    Email

    info@biblesociety-tanzania.org

    × How can I help you?