Katika kipindi cha mwaka 2020 kupitia mpango wa Msamaria mwema Chama cha Biblia kiliweza kupata fedha kidogo kutoka UBS fedha iliyotuwezesha kutoa mafunzo ya UKIMWI kwa jamii kwa kushirikiana na makanisa, misikiti na wadau wengine walioko katika mapambano ya ugonjwa wa UKIMWI katika kata ya Hombolo, Ugogoni, Mmbande na Mpunguzi mkoani Dodoma.
Kutokana na ukosefu wa fedha ufadhili Chama hakikuweza kuendelea kutoa mafunzo katika maeneo mengine ambayo mpango huu ulikuwa unafanyakazi zake.
Kwa kushirikiana na makanisa, serikali za vijiji na wadau wengine katika kata zilizotajwa hapo juu, tuliweza kuwafikia watu 183 kwa mafunzo ( 85 wanaume na 98 wanawake) 285 vifaa kwa ajili ya kufundishia viligawiwa kwa washiriki kwa lengo la kuendeleza mafundisho na kuwafundisha wengine.
Watu 40 wenye ulemavu wa macho waliweza kufikiwa na mafunzo haya kutoka kata ya Ugogoni. Mafunzo haya yaliweza kuwapatia elimu ya jumla kuhusiana na ugonjwa wa UKIMWI na Virusi vya UKIMWI. Chama cha Biblia kimekuwa mdau wa kwanza kuwakutanisha na kuwapatia elimu hii ambayo hawajawahi kuipata mahali pengine popote. Kupitia mafunzo waliyoyapata imewasidia kujua jinsi ya kupambana na maambukizi ya UKIMWI baada ya kuonekana ni kundi lililo kwenye hatari kubwa, hawana uelewa juu ya UKIMWI, wananyanyapaliwa, na jamii inawachukulia kama watu wasio na thamani na ambao hawawezi kupata maambukizi kutokana na ulemavu walio nao.
Picha za Matukio katika Kata ya Ugogoni



Chama kinakabiliwa na changamoto ya fedha kuendesha mpango huu. Mafunzo haya yanahitajika sana kwenye jamii yetu ila kutokana na uhaba wa fedha umefanya mpango huu kutowafikia vijana walio wengi.