CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO GAIRO – MOROGORO

Gairo, Morogoro | 05 Januari 2026

Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) kimefanya mahafali ya nane ya wanakisomo wa mradi wa Literacy for Women in Africa katika Wilaya ya Gairo, Mkoa wa Morogoro, tarehe 05 Januari 2026. Sherehe hiyo ilihusisha wahitimu wa elimu ya watu wazima waliopata mafunzo ya kusoma na kuandika kupitia mradi huo unaolenga kuwawezesha wanawake na wasichana ambao hawakupata fursa ya elimu rasmi.

IMG 5131 scaled

Sherehe hiyo ilifunguliwa rasmi kwa risala iliyosomwa mbele ya mgeni rasmi, Profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, ambaye aliwakilishwa na Diwani wa eneo hilo, pamoja na viongozi wa dini, viongozi wa vijiji vilivyofikiwa na mradi, na Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania aliyewakilishwa na Meneja wa Shughuli, Mchungaji John Mnong’one.

IMG 5061 scaled
IMG 5085 scaled

“Awali sikuweza kusoma wala kuandika. Kupitia mpango huu nimejifunza, na sasa naweza kusoma na kuandika kwa kujiamini. Hata nilipokwenda kupiga kura, nilijichagulia mwenyewe tofauti na zamani nilipolazimika kuchaguliwa na wengine.”

IMG 5035 scaled
IMG 5124 scaled
IMG 5153 scaled
IMG 5168 scaled

Akizungumza kupitia risala hiyo, CBT ilieleza kuwa mradi wa Literacy for Women in Africa ulianza kutekelezwa mwaka 2018 kwa kushirikiana na makanisa na wadau mbalimbali, wakiwemo Serikali za Wilaya za Gairo na Kilosa. Lengo kuu la mradi ni kuwasaidia wanawake na wasichana waliokosa elimu ya msingi kupata ujuzi wa kusoma na kuandika ili kuboresha maisha yao binafsi, kifamilia na kijamii.

Katika kipindi cha utekelezaji wa mradi huo, CBT imewafikia wanakisomo 3,200 wakiwemo wanawake wengi na wanaume wachache. Kutokana na uhitaji mkubwa uliojitokeza kwa wanaume wasiojua kusoma na kuandika, mradi ulipanua wigo wake na kuanza kuandikisha wanaume waliokuwa tayari kujiunga na madarasa ya elimu ya watu wazima (CHIBWEDA).

IMG 5049 scaled

Kwa mwaka 2025 pekee, mradi uliweza kufanya uhamasishaji na kuandikisha wanakisomo 595 (wanaume 145 na wanawake 450), kuanzisha madarasa mapya katika vijiji vya Mkalama, Masenge, Kinyolisi, Kisitwi, Nyangala na Luhwaji, pamoja na kutoa mafunzo kwa waalimu 30 wa elimu ya watu wazima yaliyofanyika Dodoma kwa muda wa wiki mbili. Aidha, vitabu vya kujifunzia (Primer books) vilichapishwa na kugawiwa kwa wanakisomo wote waliosajiliwa, na vitabu 300 vya hadithi (story books) vilitolewa kwa wahitimu kwa matumizi baada ya kuhitimu.

Katika mahafali hayo, jumla ya wahitimu 366 walikabidhiwa vyeti, ikiwa ni ishara ya mafanikio ya mradi katika kuongeza idadi ya watu wanaojua kusoma na kuandika kwenye jamii.

IMG 5054 scaled

Mradi huo umeleta matokeo chanya makubwa, yakiwemo kuongezeka kwa ujasiri wa wanawake kushiriki katika uongozi wa jamii, ushiriki wao katika shughuli za maendeleo, siasa na Kanisa, pamoja na kuimarika kwa uelewa wa jamii katika masuala ya afya, kilimo, ufugaji, mazingira na haki za kiraia. Wanufaika pia wameeleza kuwa mradi umewasaidia kusoma na kuelewa Neno la Mungu, kujiamini zaidi na kuimarisha mahusiano ndani ya familia na jamii kwa ujumla.

Rose Mrema

Literacy for Women coordinator, The Bible Society of Tanzania

Hata hivyo, CBT ilibainisha changamoto kadhaa, ikiwemo wanakisomo 185 kuacha masomo kati ya waliojiandikisha, uhitaji mkubwa wa mradi katika mikoa mingine nchini, upungufu wa fedha za kuendesha shughuli za mradi, pamoja na changamoto za miundombinu ya usafiri katika baadhi ya maeneo.

IMG 5155 scaled
IMG 5163 scaled
16
IMG 4950 scaled
IMG 5172 scaled
IMG 5031 scaled
IMG 5041 scaled
IMG 5009 scaled
Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Biblia kwa Lugha ya Kihehe Yazinduliwa Rasmi Iringa – Miaka 30 ya Kazi Yafikia Tamati

Na Mwandishi Wetu, Iringa

29 Juni 2025

3

Dr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.

Mgeni rasmi. 

Mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi, ambaye alikipongeza Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) kwa kazi kubwa na ya kipekee ya kutafsiri Neno la Mungu katika lugha mbalimbali za makabila nchini. ‘‘Biblia hii ni zawadi kubwa kwa jamii ya Wahehe na kizazi kijacho. Nitalitunza Neno hili takatifu, na kila siku nitaanza siku yangu nikiwa nimesoma Biblia hii kwa lugha ya mama yangu,” alisema Mhe. Lukuvi.

6

Mhe. William Vangimembe Lukuvi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), akihutubia.

Biblia iliyotafsiriwa kwa lugha ya Kihehe imezinduliwa rasmi leo katika ibada maalum iliyofanyika katika Kanisa la Kristo Mfalme, Anglikana Iringa Mjini, mkoani Iringa, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, makanisa na jamii ya Wahehe kwa ujumla.

3.1

Askofu Joseph Mwenyekiti wa CCT Mkoa Iringa na Askofu Anglican Dayosisi ya Ruaha akifanya uzinduzi wa Biblia ya Kihehe.

6.9
5
3.2

Dkt. Alfred Elias Kimonge akizungumza kabla ya kukabidhi Biblia ya Kihehe ili izinduliwe.

6.8

Safari ya Miaka 30


Kwa mujibu wa Dkt. Alfred Elias Kimonge, Katibu Mkuu wa CBT, mchakato wa kutafsiri Biblia hiyo ulianza mwaka 1994 baada ya maombi kutoka kwa Makanisa ya Iringa. Mradi huo ulisimamiwa na Chama cha Biblia Tanzania kwa kushirikiana na makanisa mbalimbali, wataalamu wa lugha, wahakiki, watafsiri, na wadau wa ndani na nje ya nchi.

Dkt. Kimonge alibainisha kuwa tafsiri ya Agano Jipya ilikamilika mwaka 2004 na kuzinduliwa rasmi mwaka 2008. Tafsiri ya Agano la Kale ilianza mwaka 2009, na sasa Biblia kamili imekamilika na kuzinduliwa rasmi leo tarehe 29 Juni, 2025. ‘‘Biblia inayozinduliwa leo inapatikana katika matoleo mawili: toleo la Kiprotestanti lenye vitabu 66, na toleo lenye vitabu 72 lijulikanalo kama Deuterokanoni, linalofaa zaidi kwa matumizi ya Makanisa ya Kikatoliki (TEC),” aliongeza kusema.

‘‘Tunamshukuru Mungu kwa kuona siku hii. Hii ni ushuhuda wa kuwa Neno la Mungu linaweza kufika katika kila lugha, kwa kila mtu,” alihitimisha Dkt. Kimonge.

Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Iringa

Mhe Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo akitoa salaam za furaha Kwa kupata Biblia hiyo uku akisifu juhudi za watafsiri, wahariri, na wadau wa kiimani kwa kazi hii kubwa.

9.4
9.2

Mhe Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo.

Risala na Maombi Maalum

Katika risala iliyosomwa kwa niaba ya Kamati ya Uzinduzi, viongozi wa makanisa na jamii walitoa wito kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusaidia katika masuala yafuatayo:

  1. Kutambua Biblia ya Kihehe kama waraka rasmi wa lugha ya Kihehe
  2. Kuandaliwa kwa Kamusi ya Biblia ya Kihehe
  3. Kutolewa kwa Biblia ya Kihehe kwa njia ya sauti (Audio Bible)
  4. Kuwepo kwa Biblia ya Kihehe katika mfumo wa mtandaoni
  5. Kuhifadhi Biblia hiyo katika Maktaba na Makumbusho ya Taifa
5.1
2
8

Ushiriki wa Viongozi na Jamii

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na maaskofu kutoka madhehebu mbalimbali, wawakilishi wa serikali, wabunge, viongozi wa mila na mamia ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Iringa.

Miongoni mwa viongozi wa dini waliokuwepo ni pamoja na:

  • Askofu Dkt. Blaston Gaville (KKKT – Iringa)
  • Askofu Dkt. Joseph Mgomi (Anglikana – Ruaha)
  • Mhashamu Romanus Mihali (RC – Iringa)
  • Askofu Prof. Mdegella, Askofu Mtetemela, na Askofu Ngalalekumtwa
6.7
14
15
6.4
Mangala
4.1

Kumbukizi za Watafsiri

Shukrani na heshima zilitolewa kwa watafsiri na wahakiki waliotoa mchango mkubwa, lakini hawakuweza kushuhudia uzinduzi huu, akiwemo:

  • Marehemu Mch. Lambert Mtatifikolo
  • Marehemu Mwl. Evaristo Mahimbi
  • Marehemu Mch. Israeli Kiponda

Hitimisho na Maono ya Baadaye

Biblia hii inatarajiwa kusaidia jamii ya Kihehe kusoma, kuelewa, na kuishi Neno la Mungu kwa undani zaidi katika lugha yao ya moyo. Viongozi walisisitiza kuwa kazi ya Mungu kupitia tafsiri ya Biblia inapaswa kuungwa mkono zaidi, ili kufanikisha tafsiri katika lugha nyingine za makabila ya Tanzania.

6.8
17

Comments

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU – WILAYA YA GAIRO, MKOA WA MOROGORO.

Tarehe: 8 Juni 2025
Mahali:Gairo, Morogoro

Uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu Unasisitiza Uthamini wa Lugha za Asili

Viongozi wakipokea Biblia ili Izinduliwe

Dr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.

Ibada na kubariki wa Biblia. 

Ibada ya uzinduzi na kubariki Biblia iliongozwa na Askofu Godfrey Sehaba wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Morogoro. Pia, viongozi wengine wa kidini waliohudhuria ni pamoja na Mch. Stanley Makasi Tabulu (Msaidizi wa Askofu KKKT), Askofu Frederick Chingwaba (Kanisa Huria Anglikana Tanzania)  na Msaidizi wa Askofu wa Jimbo Katoliki Morogoro.

Chama cha Biblia cha Tanzania (BST) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kiimani na kijamii,  tarehe 8 Juni 2025, ilifanikiwa kufanya uzinduzi wa Biblia kwa lugha ya Kikagulu, katika Wilaya ya Gairo, Mkoa wa Morogoro.

Hafla hii ya kihistoria iliongozwa na Mheshimiwa Lay Canon Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye alisisitiza umuhimu wa kuhifadhi na kuendeleza lugha za asili za Kitanzania. 

Kuonesha Biblia zilizozinduliwa

Askofu Godfrey Sehaba akifanya uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu

Wafurahiya Biblia yao
Mh. Paramagamba Kabudi

Mhe. Prof. Kabudi akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi  Biblia mpya ya Kikagulu.

Maneno ya Mgeni rasmi

Mheshimiwa Kabudi alibainisha kuwa lugha za asili ni hazina ya taifa na kwamba uandishi na utafsiri wa maandiko matakatifu kwa lugha za asili ni jambo la msingi kwa uenezi wa injili na utunzaji wa utamaduni wa Taifa. 

Katibu Mkuu wa Wilaya ya Gairo

Daudi Abdallah Sehaba (DAS wa Gairo) alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mheshimiwa Jabiri Omari Makame, akisifu juhudi za watafsiri, wahariri, na wadau wa kiimani kwa kazi hii kubwa. 

Daudi Abdallah DAS

Daudi Abdallah Sehaba (DAS wa Gairo)

Ngoma ya Kienyeji ya Vijana

Mojawapo ya kikundi cha ngoma za asili kikitoa burudani kwenye uzinduzi

Burudani na Furaha ya Wananchi .

Sherehe hiyo ilionyesha utamaduni wa Kikagulu kupitia ngoma na kwaya mbalimbali zilizofurahisha wageni na wananchi wa Gairo. Uzinduzi huo ulikuwa ni sherehe ya kipekee, ikiashiria mafanikio ya miaka ya juhudi za utafsiri na uchapishaji wa Biblia hii.

Ngoma ya Kienyeji
Kwaya Ikiimba

Shukrani na Tuzo

Mwishoni, Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia Tanzania, Dk. Alfred Elias Kimonge, alitoa shukrani kwa watafsiri na wadau wote waliofanikisha mradi huu wakiwemo Askofu Frederick Chingwaba– Mtafsiri, Askofu Michael Peter Nhonya – Mratibu na Mtafsiri wa Mradi wa Kikagulu na Wahariri wa Biblia ya Kikagulu pamoa na kuwapatia zawadi.

Katibu Mkuu akitoa zawadi kwa Askofu Chingwaba1
Katibu Mkuu akitoa zawadi kwa Askofu Nhonya
Watafsri Waakiki

Matukio katika Picha

Comments

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024
Comments

Written by

19
5

Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia Tanzania, Askofu Dkt. Mark Malekana amesema katika ulimwengu huu ambao jamii inal­alamika kuhusu kuporomoka kwa maadili kutokana na mambo ya aja­bu yanayotokea, nguvu inayoweza kusadia jamii inayoathirika ni Neno la Mungu pekee.

Amesema hayo alipofungua Mku­tano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024 uliofanyika juzi Iju­maa Mei 30, 2025 katika ukumbi wa kanisa la KKKT jijini Dodoma.

Dkt. Malekana alisema Biblia ni maandiko matakatifu yatakayoweza kuibadilisha jamii kutoka kwenye kuwa ‘jamii ovu’ na kuwa jamii ‘in­ayompendeza Mungu’, hivyo am­etoa wito kwa Biblia kupelekwa kwa wahitaji.

“Wito wangu mkubwa, ambao pia ni wito wa mkutano huu siku ya leo ni wito wa kupeleka Biblia kwa vija­na, kupeleka Biblia kwa watoto, ku­peleka Biblia magerezani, kupeleka Biblia kwa kila mtu kwa maana Bib­lia ndio italiponya taifa letu,” alisema Dkt. Malekana na kuongeza:

“Tunashukuru katika kuendesha mambo yake kwa muda mrefu lakini tunashukuru kuona kwamba maku­sanyo ya Watanzania wenye kutoka madhehebu mbalimbali na watu binafsi yameongezeka, sisi Watan­zania tunaweza kutegemeza chama chetu cha Biblia kwa michango yenu kama wanachama, kwa michango yetu kama kanisa sambamba na michango kutoka kwa waumini mbalimbali wa madhehebu yote, Mungu akusaidie.”

7

“Unaposaidia Chama cha Biblia cha Tanzania, unaokoa kanisa na unaokoa Taifa la Tanzania, Mun­gu akubariki unaposaidia Chama cha Biblia cha Tanzania. Hivyo, mimi kama Mwenyekiti nawashukuru sana wajumbe waliohudhuria, na­washukuru kwa mwitikio wenu.”

3

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred Kimonge akisoma Mukhtasari wa Mkutano Mkuu wa chama kwa Mwaka 2023, alisema chama kimeendelea kushirikiana na shirika la ‘Talking Bible Internation­al’ kwa kuendelea kuwa kituo cha kupokea, kuandaa na kusambaza Biblia inayoongea kwa wahitaji ka­tika nchi za Mashariki,Kati, Kaska­zini na Magharibi mwa Afrika.

Alisema mwaka 2023 jumla ya nakala 1,404 za Biblia zinazoon­gea zilisambazwa katika nchi za Kenya,Uganda, Zambia, Eritrea na Niger.

MG 5069 scaled

Dkt. Kimonge alisema nchini Tanzania jumla ya nakala 1,800 zilisambazwa ambapo kupitia mradi huo wa makundi ya watu wasioona na wasiojua kusoma, ya­meweza kufikiwa kwa kushirikiana na makanisa, taasisi za dini na watu binafsi wa kujitolea (volunteers).

Aidha, Dkt. Kimonge alisema mradi wa Kamusi ya Biblia kutoka Kiebrania/Kiyunani _Kiswahili (Scholarly Dictionary) ambao una­husu kuundaa Kamusi ya Kiebra­nia/Kiyunani kwenda Kiswahili (Hebrew/Greek-Shwahili ) ilikami­lika Septemba 2023.

Alisema mradi wa Elimu kwa Wanawake (Literacy for Women in Africa), Chama cha Biblia Tanzania kimeendelea kuutekeleza katika Halmashauri ya Wilaya ya Gairo na Kilosa. Lengo la mradi huo ni ku­wasadia wanawake na wasichana ambao hawajui kusoma na kuan­dika kutokana na mazingira tofauti mbalimbali.

MG 4908 scaled

Dkt. Kimonge aliyataja mazingira hayo kuwa pamoja na tamaduni ambazo jamii iliamini mtoto wa kike hatakiwi kupele­kwa shule, hasa vijijini.

Alisema tamaduni hizo zilisababisha jamii kutoona umuhimu wa elimu na kujishu­ghulisha na shughuli nyingine kama kilimo na ufugaji.

24

Naye Mhazina wa Chama cha Biblia Tanzania, Fadha Chesco Msaga akisoma taarifa ya ya fedha kwa mwaka ulioishia Desemba 31, 2024 alisema: “Tunashukuru Mun­gu kwa mwamko ulionyeshwa na makanisa kwa kipindi cha mwaka 2024 katika kuchangia Biblia kwa watoto, vijana na wafungwa”.

13
33
23
21
35
34
20
39
32
25
9
8
MG 4465 scaled
MG 4780 scaled
MG 4658 scaled
MG 4876 scaled
MG 4883 scaled
MG 4884 scaled
MG 4793 scaled

Related Articles

Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Biblia kwa Lugha ya Kihehe Yazinduliwa Rasmi Iringa – Miaka 30 ya Kazi Yafikia TamatiNa Mwandishi Wetu, Iringa 29 Juni 2025Dr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.Mgeni rasmi.  Mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU – WILAYA YA GAIRO, MKOA WA MOROGORO.Tarehe: 8 Juni 2025Mahali:Gairo, Morogoro Uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu Unasisitiza Uthamini wa Lugha za AsiliDr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.Ibada na kubariki wa...

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024

Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia Tanzania, Askofu Dkt. Mark Malekana amesema katika ulimwengu huu ambao jamii inal­alamika kuhusu kuporomoka kwa maadili kutokana na mambo ya aja­bu yanayotokea, nguvu inayoweza kusadia jamii inayoathirika ni Neno la Mungu pekee....

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa.

Mahali: ukumbi wa Nazareti, wilayani Gairo, mkoani Morogoro.

Picture5

Hafla hii ilihudhuriwa na viongozi wa dini na serikali wakiwemo wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa (W) ya Gairo pamoja na ofisi ya Mkurugenzi mtendaji pia Afisa mipango na Afisa maendeleo ya jamii ambapo waliwapongeza sana wahitimu kwa juhudi zao kubwa na kusisitiza umuhimu wa elimu katika maendeleo ya jamii.

Chama cha Biblia, kupitia mradi wake wa Literacy for Women in Africa, kimefanikisha hatua muhimu katika kuimarisha elimu ya wanawake nchini. Mahafali ya saba ya mradi huu yaliyofanyika tarehe 23 Januari 2025 katika ukumbi wa Nazareti, wilayani Gairo, mkoani Morogoro, yaliwahitimu wanawake 353 katika ngazi ya A ya kusoma na kuandika.

Picture6
Picture4

Mradi wa Literacy for Women in Africa umeleta mabadiliko makubwa katika maisha ya wanawake hawa. Wengi wao sasa wanaweza kusoma Biblia, kuendesha biashara ndogo ndogo, na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii zao.

“Shuhuda kutoka kwa mmoja wa wahitimu: “Kabla ya kuanza kusoma, nilikuwa tegemezi sana. Sasa naweza kusoma na kufuatilia habari, na hata kuandika barua ya maombi ya kazi na kushiriki na mambo mbalimbali ya kijamii kama kupiga kura na kuchagua viongozi na hata kugombea nafasi za kiuongozi kama uenyekiti wa mtaa. Maisha yangu yamebadilika kabisa!”

Picture Mzee
Meza kuu wakifurahia jambo wakati wa maafali

Mahafali haya yamekuwa ushahidi tosha wa kwamba elimu ni nguvu. Chama cha Biblia kinaendelea kujizatiti kuhakikisha kuwa wanawake wengi zaidi wanapata fursa ya kujifunza na kukuza uwezo wao. Tunawashukuru sana wadau wote kwa ushirikiano wenu katika kufanikisha mradi huu.

Wahitimu
Picture ya Pamoja
2
Picture3
7

Matukio katika Picha

Comments

Uzinduzi wa sehemu ya Biblia (portion) kwa lugha ya Kiha.

Uzinduzi wa sehemu ya Biblia (portion) kwa lugha ya Kiha.

Uzinduzi wa sehemu ya Biblia (portion) kwa lugha ya Kiha.

Mahali: Kijiji cha Nyakimwe, Wilaya ya Buhigwe 

Dhehebu: Kanisa la Anglican 

IMG 0263 scaled

Maelezo ya Meneja wa Tafsiri, Leah Kiloba

Leah Kiloba alielezea maendeleo ya mradi huu, akisisitiza kuwa Chama cha Biblia kinaendelea kujitahidi kuhakikisha upatikanaji wa Biblia kwa watu wote wa madhehebu mbalimbali bila ubaguzi. Alifafanua kuwa mradi huu unalenga kumjumuisha kila Mkristo kwa kutoa nafasi sawa ya kusoma Neno la Mungu katika lugha yao wenyewe. 

Sherehe ya uzinduzi wa tafsiri ya Biblia ya Position ya Kiha (kitabu cha Yeremia) ilifanyika katika Kanisa la Anglican kijijini Nyakimwe, wilaya ya Buhigwe. Tukio hili lilihudhuriwa na waumini kati ya 400 na 700 kutoka madhehebu mbalimbali, pamoja na makanisa ya Anglican, Roman Catholic, Pentecostal, na Sabato, ambayo yalialikwa rasmi kushiriki.

IMG 0131 scaled
IMG 0066 scaled

Historia ya Mradi kutoka kwa Mchungaji Ntakije

Mchungaji Ntakije aliwasilisha historia ya mradi huu wa kutafsiri Biblia kwa lugha ya Kiha, akielezea hatua zilizochukuliwa kufanikisha kazi hii muhimu na changamoto zilizokabiliwa. Alielezea jinsi jamii imekuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono mradi huu.

Kusoma Maandiko na Baraka za Ibada

Tukio lilihusisha kusoma maandiko kutoka kitabu cha Yeremia, sura ya kwanza, mistari ya kwanza hadi wa kumi, ambayo ilisomwa na mtafsiri Ahabu Ntibakanzi. Kabla ya kusoma, mchungaji Daniel Nzaino alitoa baraka kwa waumini na ibada iliongozwa kwa shukrani na furaha. 

IMG 0123 1 scaled
IMG 0081 scaled

Uratibu wa Ugawaji wa Vitabu

Vitabu vya Position ya Kiha viligawiwa kwa wahumini waliokuwa wakitoka kanisani, kwa usimamizi wa watu waliokuwa milangoni. Kila mmoja kila mmoja alipokea kitabu/portion kwa mpangilio mzuri na bila msongamano, wakihakikishiwa upatikanaji wa Neno la Mungu katika lugha yao.

IMG 0207 scaled
IMG 0243 scaled

Furaha ya Waumini

Baada ya ugawaji wa vitabu hivi, waumini Walionekana wakifurahia vitabu vyao nje ya Kanisa. Walijawa na furaha kubwa huku wakimshukuru Mungu pamoja na viongozi wa mradi kwa jitihada zao kufanikisha kazi hii. Pia walipiga picha ya pamoja ya kumbukumbu wakiwa wameshikilia vitabu vyao.

IMG 0268 scaled
IMG 0266 scaled

Tukio hili lilifanikiwa kwa kiwango kikubwa, na waumini walionyesha kufurahia uzinduzi wa tafsiri hii mpya ya Biblia katika lugha yao ya Kiha, ikionyesha mwendelezo wa kazi nzuri ya Chama cha Biblia na Kanisa katika kukuza na kueneza Neno la Mungu kwa jamii nzima.

IMG 0263 scaled

Matukio katika Picha

Comments

KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA BIBLIA MKOANI DODOMA

KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA BIBLIA MKOANI DODOMA

KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA BIBLIA MKOANI DODOMA

11
20241103 155004 scaled

Dodoma, 03 Novemba 2024 – Maadhimisho ya kilele cha Juma la Biblia mwaka huu yamefanyika kwa mafanikio makubwa mkoani Dodoma, katika Uwanja wa Mashujaa. Maadhimisho hayo yaliyoanza na maandamano ya amani kutoka makao makuu ya Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) hadi viwanja vya zamani vya Mashujaa, yalivutia umati wa wanachama na wadau mbalimbali. Maandamano hayo yalipambwa na bendi ya tarumbeta na kwaya ya wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), huku wanachama wakivalia tisheti zilizo na nembo ya CBT na kauli mbiu ya mwaka huu: “Neno la Mungu, Maadili Yetu.”

Mgeni rasmi katika sherehe hizo alikuwa Askofu Amos Muhagachi, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa CBT, akiwa ameambatana na viongozi wengine wakuu wa Chama akiwemo Katibu Mkuu wa CBT, Dkt. Alfred Elias Kimonge, na Mkurugenzi wa CBT, Dkt. Anna Solo. Pia, sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi wa makanisa, wanachama wa CBT, na wanafunzi wa UDOM.

1
4
20241103 174033

Katika hotuba yake mgeni rasmi Askofu Amos Muhagachi alisoma Neno la Mungu kutoka Zaburi 119:105, “Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu,” akisisitiza umuhimu wa Neno la Mungu kama msingi wa maadili. Alisema, “Biblia ni kitabu kinachotuunganisha sisi Wakristo na kinatuonyesha maisha ya mwanadamu, ukombozi, na umilele wake.” Pia alihimiza mpango mkubwa wa maadhimisho mwaka ujao, kwa kushirikiana zaidi ili kufikia wadau wengi.

Askofu MuhagachiGS Maandamano

Katika hotuba yake, Katibu Mkuu Dkt. Kimonge aliwashukuru wanachama na wadau wote waliojitolea kushiriki Juma la Biblia lililoanza tarehe 28 Oktoba na kumalizika leo 03 Novemba. Dkt. Kimonge alieleza kwamba lengo kuu la CBT ni kutafsiri, kuchapisha, na kusambaza Biblia kwa watu wote, wakiwemo Wakristo na wasio Wakristo. Alihimiza umoja katika kuchangia kazi hii muhimu, hasa kwa makundi yasiyo na uwezo wa kununua Biblia, kama vile wafungwa na vijana.

20241103 162244 scaled
6

Katika kuelezea historia ya CBT, Dkt. Kimonge alitaja hadithi ya binti Maria Jones, mwenye umri wa miaka kumi na tano, aliyekuwa mkulima wa Wales. Kiu yake ya kumiliki Biblia ilichochea harakati za kuanzisha vyama vya Biblia, ambavyo leo vinafanya kazi katika nchi zaidi ya 160, kusambaza mamilioni ya Biblia na maandiko mengine katika lugha zaidi ya 15,000.

20241103 161423 scaled
20241103 161436 scaled

Maadhimisho hayo yamehitimishwa kwa maneno ya shukrani kutoka kwa Meneja wa Mahusiano na Makanisa, Mch. Samweli Mshana, aliyewapongeza viongozi wote kwa kufanikisha Juma la Biblia kwa ufanisi. “Shukrani kwa viongozi wetu na wanachama wote wa CBT kwa kazi kubwa mliyofanya. Mungu awabariki sana,” alisema Mch. Mshana.

20241103 154856 scaled
3

Maadhimisho ya Juma la Biblia yanaendelea kuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha ushirikiano kati ya waumini, wadau, na jamii kwa ujumla kupitia Neno la Mungu, na CBT inaahidi kuendelea na jitihada hizi kwa ustawi wa kiroho wa Watanzania.

2

Comments

UZINDUZI WA SEHEMU YA BIBLIA KWA LUGHA YA KINYIHA WAFANYIKA KANISA LA MORAVIAN, MBOZI

UZINDUZI WA SEHEMU YA BIBLIA KWA LUGHA YA KINYIHA WAFANYIKA KANISA LA MORAVIAN, MBOZI

UZINDUZI WA SEHEMU YA BIBLIA KWA LUGHA YA KINYIHA WAFANYIKA KANISA LA MORAVIAN, MBOZI

Jimbo la Mbozi, Kanisa la Moravian Ushirika wa Igamba – 27 Oktoba 2024

IMG 9844 scaled

Tukio la kihistoria la uzinduzi wa vitabu vya Biblia vilivyotafsiriwa kwa lugha ya Kinyiha vitabu vya Ruthu, 1 Samweli, 1 Wafalme, na Yona limefanyika leo katika Kanisa la Moravian Ushirika wa Igamba, Jimbo la Mbozi. Uzinduzi huu umefanywa na Katibu Mkuu wa Jimbo la Mbozi, Mchungaji Rayson Kibona, huku ukiongozwa na Mch. Lastone Chalotela Mwamlima ambaye ni mratibu wa mradi pia mwenyekiti wa wilaya na Mchungaji Wiliadi Zewanga mchungaji wa ushirika wa Igamba Moravian.

Tukio hilo muhimu limeandaliwa na Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na makanisa ya Kikristo kutoka Mkoa wa Songwe, hasa Wilaya ya Mbozi ambako lugha ya Kinyiha huzungumzwa kwa wingi.

20241027 094333 scaled
IMG 9764 scaled
IMG 9753 scaled

Katika hafla hiyo, viongozi mbalimbali walihudhuria na kutoa hotuba kuhusu umuhimu wa tukio hili. Madam Leah Kiloba, Meneja wa Tafsiri kutoka Chama cha Biblia cha Tanzania, aliwasilisha ujumbe wa Chama hicho na Umoja wa Vyama vya Biblia Duniani, akieleza majukumu makuu ya Chama kuwa ni kutafsiri, kuchapisha, na kusambaza Biblia kwa gharama nafuu ili kuwafikia watu wote. Kiloba alisisitiza umuhimu wa mradi huu kwa jamii ya Wanyiha na kuwashukuru washiriki wote waliotoa mchango katika tafsiri. Pia aliwaomba jamii ya wanyiha baada ya kupokea vitabu hivyo wavisome kisha kama kuna makosa wayalete ili yalekebishwe mapema kabla ya Biblia kamili kukamilika.

Watafsiri na Wahakiki wa Tafsiri
Kazi ya kutafsiri vitabu hivi imefanywa kwa bidii na ushirikiano wa wataalamu wa lugha, viongozi wa makanisa, na wahakiki wa tafsiri. Baadhi ya watafsiri wakuu ni:
– Mch. Lastone Chalotela Mwamlima (mratibu)
– Mch. Justus Vhalondeghe Sinkonde
– Mch. Philimon Partson Balanga
– Dada Christina Chares Singogo

IMG 9821 scaled
IMG 9816 scaled

Wahakiki wa tafsiri walioshiriki ni pamoja na:
– Mch. Sila Mwamwezi
– Mch. Sostini Mwansenga
– Mch. Wilhelm Mwakavanga
– Mch. Selemani Nkota
– Mch. Lameck Nzowa
– Mch. Nichorous Shonza
– Dada Martha Mwashiuya
– Dada Upendo Mwashilindi
Pia, Dkt. Chris Pekka Wilde alitajwa kwa mchango wake muhimu wa kiufundi kama mshauri wa mradi huu.

IMG 9835
IMG 9828 scaled

Viongozi wa Makanisa Mbalimbali Wajumuika

Uzinduzi huu ulihudhuriwa na wachungaji na viongozi wa makanisa kutoka madhehebu tofauti, wakiwemo wawakilishi kutoka makanisa ya Last Church, Kanisa Katoliki, TAG, na KKKT. Viongozi hawa walipongeza hatua hii kama ishara ya kuendelea kwa kasi kwa mradi huu, ambao unalenga kuongeza upatikanaji wa Biblia kwa lugha ya Kinyiha kwa ufasaha.

IMG 9754 scaled
IMG 9771 scaled

Mafanikio na Matumaini ya Mradi wa Tafsiri kwa Lugha ya Kinyiha

Tukio hili limeibua matumaini makubwa na linaashiria mwanzo mzuri kwa jamii ya Wanyiha kupata Biblia kwa lugha yao wenyewe, hatua ambayo itaimarisha zaidi imani na kueneza Neno la Mungu kwa undani zaidi katika eneo hilo.

IMG 9764 scaled

Comments

UZINDUZI WA KITABU CHA KWANZA NA CHA PILI CHA SAMWELI KWA LUGHA YA CHASU

UZINDUZI WA KITABU CHA KWANZA NA CHA PILI CHA SAMWELI KWA LUGHA YA CHASU

UZINDUZI WA KITABU CHA KWANZA NA CHA PILI CHA SAMWELI KWA LUGHA YA CHASU

Kanisa la KKKT Usharika wa Hedalu, Dayosisi ya Pare – 20 Oktoba 2024

20241020 100910 scaled

Wapendwa waalikwa walikusanyika leo kwa tukio la kihistoria la uzinduzi wa kitabu cha Kwanza na cha Pili cha Samweli vilivyotafsiriwa kwa Lugha ya Chasu (Kipare). Uzinduzi huo uliandaliwa na Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na makanisa ya Kikristo yaliyoko katika wilaya za Mwanga na Same Mkoa wa Kilimanjaro, na kuongozwa na Mratibu wa Mradi, Mchungaji Elineema Mndeme.

Mchungaji Mndeme aliwashukuru wageni wote walioshiriki kwenye tukio la uzinduzi, wakiwemo Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi ya Mwanga, Mchungaji Timothy Msangi, na Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi ya Pare, Mchungaji Ibrahim Ndekia. Pia aliwapongeza wawakilishi kutoka Chama cha Biblia cha Tanzania, akiwemo Katibu Mkuu, Dkt. Alfred Kimonge, kwa kuwezesha kazi kubwa ya kutafsiri Biblia kwa lugha ya Chasu.

Rev. Elineema Mndeme
IMG 9613 scaled

Kazi ya tafsiri imefanywa kwa ushirikiano wa wataalamu wa lugha, viongozi wa makanisa, na wahakiki wa tafsiri. Mchango mkubwa ulitolewa na Meneja wa Tafsiri, Dada Leah Kiloba, na washirika wake katika Chama cha Biblia cha Tanzania, pamoja na wataalamu wa teknolojia ya taarifa Felix na Charles, ambao waliweka mifumo ya tafsiri katika kompyuta.

Kwa upande wa usimamizi wa tafsiri, Dkt. Chris Pekka Wilde, mshauri wa mradi, ametajwa kwa mchango wake wa kiufundi na ushauri thabiti katika kuhakikisha tafsiri zinafuata viwango vya juu.
Mradi wa kutafsiri Biblia kwa lugha ya Chasu unahusisha watafsiri wanne: Mchungaji Elineema Mndeme (Mratibu), Mchungaji Joasi Mpinda, Mchungaji Msifuni Msuya, na Mchungaji Imani Chediel Mgonja. Wahakiki wa tafsiri wamejumuisha wachungaji na wainjilisti na wajumbe raia kutoka maeneo mbalimbali ya jamii ya Chasu.

IMG 9603 scaled
IMG 9551 scaled
IMG 9555 scaled

Mpaka sasa, nusu ya vitabu vya Agano la Kale vimetafsiriwa. Kazi ya tafsiri inapitia hatua nne: kwanza, mtafsiri anatafsiri kitabu chake; pili, watafsiri wote wanakipitia; tatu, wahakiki wa jamii wanakikagua; na mwisho, mshauri wa kitaalamu anakihakiki.

Vitabu vilivyokamilika mpaka ngazi ya mshauri ni Ruthi, Yona, Yoshua, Waamuzi, Kitabu cha Nyakati 1 na Nyakati 2, Kitabu cha Wafalme 1 na Wafalme 2, Esta, Mwanzo, pamoja na Kitabu cha Kwanza na cha Pili cha Samweli ambavyo vimezinduliwa leo rasmi.

20241020 100712 scaled
20241020 100729 scaled

Aidha, Kitabu cha Kumbukumbu la Torati kiko kwenye ngazi ya uhakiki, na kinatarajiwa kufika kwa mshauri mwezi Novemba. Kitabu cha Hesabu kiko katika hatua ya kuratibu, huku vitabu vya Kutoka, Mambo ya Walawi, Nehemia, na Ezra vikiwa katika hatua ya awali ya tafsiri.

Mchungaji Samweli Mshana kutoka Chama cha Biblia cha Tanzania alitoa hotuba fupi akieleza majukumu makuu ya Chama hicho, ambayo ni kutafsiri, kuchapisha, kusambaza Biblia, na kutafuta rasilimali fedha ili kupunguza gharama za shughuli hizo kwa njia ya uchangishaji fedha (fundraising).

Aliwasihi Wakristo kujiunga na Chama cha Biblia cha Tanzania ili kusaidia kupunguza bei za maandiko, hususani kwa ajili ya wafungwa na jamii zinazoishi katika hali ngumu.

20241020 101040
IMG 9601 scaled
IMG 9559 scaled

Pia katika Ibada hiyo alikabidhi redio 60 zenye Biblia kwa lugha ya Chasu, zinazojulikana kama mpiga mbiu (proclaimer), na kuomba viongozi wa Kanisa waziweke wakfu kwa matumizi ya kanisa. Pia aliwahimiza kusimamia mradi wa “Imani Huja kwa Kusikia” kwa kuanzisha vikundi vya kusikiliza, na akawakumbusha kutuma ripoti za maendeleo ya vikundi hivyo.

Mchungaji Mshana pia aliwaomba viongozi wa makanisa kuzindua kitabu cha kwanza na cha pili cha Samweli vilivyotafsiriwa kwa lugha ya Chasu kama ishara ya hatua kubwa iliyofikiwa katika mradi huo.

IMG 9598 scaled

Tukio hili limekuwa la mafanikio makubwa na linaashiria mwanzo mzuri wa upatikanaji wa Biblia kwa Lugha ya Chasu, jambo ambalo litasaidia sana kueneza Neno la Mungu kwa ufasaha katika jamii hiyo.

Comments

Join

Work With Me