MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA PROJECT.

TAARIFA FUPI YA MPANGO & MAHAFALI YA SITA YA MPANGO HUU

Mahafali ya sita ya mpango huu yalifanyika tarehe 17.2.2024 katika Ukumbi wa Nazarethi, Gairo mjini ambapo wanakisomo 421 walitunukiwa vyeti vya kuhitimu Kisomo cha watu wazima na Mkuu wa (w) ya Gairo. Mh. Jabiri Shekimweri.  Sherehe hizi zilihudhuriwa na wageni wengine akiwemo Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred E. Kimonge, Bodi ya wakurugenzi wa Chama cha Biblia cha Tanzania, wafanyakazi na viongozi wa makanisa na jamii kutoka wilaya ya Gairo na Kilosa.

Mpango huu umeendelea kutekelezwa na Chama cha Biblia cha Tanzania katika (w) ya Gairo na Kilosa. Lengo kuu ni kuwasaidia wanawake na wasichana hawakuweza kwenda shule  na hawajui Kusoma na Kuandika.

26 scaled

Mmoja wa wanakisomo akipokea cheti cha kuitimu elfu hiyo.

23 scaled
13 scaled
12 scaled
beauty esthetician 43

SHUGHULI ZA UTEKELEZAJI

Katika kipindi cha mwaka 2023, Chama cha Biblia kupitia mpango huu kiliweza kutekeleza shughuli zifuatavyo;

  • Kufanya uhamasishaji na kuandikisha wanakisomo 450 (Me 379 & Ke 71) kabla ya madarasa kuanza.
  • Mpango huu umelenga zaidi wanawake na wasichana, ila wapo pia wanaume ambao wamejiunga na madarasa na wamekuwa wanufaika wazuri. Takwimu zinaonyesha kuna idadi kubwa ya wanaume wasiojua kusoma na kuandika na mpango huu unawakaribisha.
  • Kufanya mafunzo kwa waalimu 30 wanaofundisha kwenye madarasa ya watu wazima. Mafunzo haya yalifanyika Dodoma kwa wiki mbili yakiongozwa na wakufunzi kutoka SIL Nairobi, Kenya.
  • Kuchapisha na kuwagawa vitabu 450 vya kujisome kwa wanakisomo wote waliojiandikisha.
  • Kuhamasisha na kuanzisha vikundi (improving literacy groups) vya kujisome vitabu vya hadithi. Vikundi hivi ni kwa ajili ya wahitimu ili kuweza kuendeleza ujuzi na kupata uzoefu zaidi katika kujua kusoma na kuandika. Hapa wananapata nafasi ya kujisomea vitabu vya aina mbalimbali, majarida, magazeti, Biblia pamoja na makala nyingine nyingi.

Wawezeshe Kusoma

MAFANIKIO.

  • Kuongezeka kwa wanajamii wanaojua kusoma /kuandika kila mwaka kwenye eneo la mpango.
  • Wanawake kupata na kugombea nafasi mbali mbali za uongozi kwenye jamii yao kutokana na uwezo wao.
  • Kumekuwa na jamii inayojiamini zaidi na yenye uelewa juu ya masuala mbali mbali.mfano Afya, kilimo, mazingira kuanzia kwenye ngazi ya familia.
  • Kumewasaidia kusoma Neno la Mungu pamoja na hii imeongeza ukuaji wa kiroho.
beauty esthetician 38
14 scaled
28 scaled
9 scaled
22 scaled
6 scaled
4 scaled
21 scaled
17 scaled

Blog

Product Updates & Sales

Mkutano Mkuu (AGM) 2023

Mkutano Mkuu (AGM) 2023

Katika zama ambazo habari potofu kuhusu Neno la Mungu zimeenea, ni muhimu kusoma Biblia zenye nembo ya Chama cha  Biblia cha Tanzania. Hii inahakikisha uhalisi na ufuasi wa mafundisho ya kweli ya Biblia.Wakati wa mkutano huo uliofanyika Mei 17, 2024, Askofu Mark...

read more
Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

Habari Kamili.

Chama cha Biblia cha Tanzania kimeendelea na huduma yake ya kugawa Biblia kwa baadhi ya magereza hapa nchini.

Chama kimeendelea kutoa huduma hiyo kutokanana  sadaka na michango ya  wanachama wake, wadau mbali mbali na watu binafsi wenye mapenzi na neema ya kufanya kazi ya Mungu walioko ndani na nje ya nchi.

Picha zinaonesha baadhi ya magereza yaliyoko katika kanda ya Kaskazini waliofikiwa na kugawiwa Biblia kutoka katika Chama cha Biblia chanTanzania.

Tunamshukuru Mungu kwa neema hii. Tunaamini kupitia Biblia hizi watu watafikiwa na Neno la Mungu ambalo litabadilisha maisha yao, watazidi kumjua Mungu na kumtumikia. Tunaomba Mungu awabariki na aendelee kuwatumia ili kuwafikia walengwa wengi zaidi na kazi ya Mungu izidi kusonga mbele kwa ushindi mkuu.

Wapare

Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza (W) Same Kilimanjaro

Hata Katesh wafungwa wanalitaja jjina la Yesu

Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Kateshi

Kazi njema Magereza ya kaskazini imeanzia Babati Yesu asifiwe

Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza la Manyara Babati

Wafungwa wa Arusha Mjini

Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza Arusha mjini

Wafungwa wa Mbulu wanamtukuza Mungu pia
BST IMAGE

Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

Habari Kamili.

Chama cha Biblia cha Tanzania kinaendelea kutekeleza mpango wa Kisomo cha elimu ya watu wazima katika wilaya ya Kilosa na Gairo kwenye vijiji 15 vilivyochaguliwa wakati wa kuanzishwa kwa mpango huu. Mpango wa Kisomo cha elimu ya watu wazima umeweza kuwafikia wanaume na wanawake 1500. Wanakisomo waliofikiwa na mpango huu wanajua kusoma na kuandika, maisha yao yamebadilika na wanaishi maisha ya kawaida kama walivyo watu wengine waliosoma. Pia ushirikishwaji wao katika masuala ya kijamii umeongezeka, wengine wamepata nafasi za uongozi kwenye jamii na Kanisa limeweza kuwa na washirika wanaoweza kusoma na kulielewa Neno la Mungu pia kufanya majukumu yao ya utumishi kwa weledi zaidi kulinganisha na ilivyokuwa kabla ya kujua kusoma na kuandika.

Waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo scaled

Waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo

Ili kufanikisha mpango huu Chama cha Biblia kwa kushirikiana na SIL Nairobi walifanya mafunzo ya kuwajengea uwezo waalimu 30 wa Chikagulu. Mafunzo  hayo yalifanyika Dodoma kwa wiki mbili ambapo  waalimu waliweza kufundishwa  mada tofauti tofauti kulingana na mfumo wa mpango ulivyo, baadhi ya mada walizofundishwa ni mifumo ya literacy, sifa za mwalimu bora, sifa za mwanakisomo, majukumu ya mwalimu kabla  na akiwa ndani ya darasa.

Kwa kipindi cha mwaka huu 2023, Chama cha Biblia cha Tanzania kimeweza kuandikisha wanakisomo 450. Wanakisomo waliojiandikisha  hawawezi kusoma, hawajawai kwenda shule na hawajawahi kukutana na jarida/ gazeti, kitabu chochote na hawajui kuandika. Madarasa yataanza mwezi June,2023 kwa kipindi cha miezi saba.

Waalimu wa waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo scaled

Waalimu wa waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo

Askofu huyo aliwakumbusha washiriki wa mkutano huokumwomba Mungu zaidi kwa kuwa wanahubiri injili katika kizazi kinachobadilika lakini wao wanahubiri neno la Mungu lisilobadilika, jambo linaloibua changamoto mbalimbali ikiwemo lugha.
Alitoa mfano kuwa wakati wao kama chama wanajitahidi kuhubiri injili kwa lugha ya
Kiswahili inayosikika kwa watu wengi, lakini Kiswahili chenyewe kinabadilikabadilika.

BST IMAGE

Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

Habari Kamili.

 Mwenyekiti wa Bodi ya Chama
cha Biblia Tanzania, Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana amesema chama hicho kitajitahidi kuendelea kuchapisha na kusambaza neno la Mungu ili liweze kumfikia kwa kila mtu na injili izidi kuhubiriwa.

Alisema hayo katika Mkutano
Mkuu wa Mwaka 2022 wa chama
hicho uliofanyika katika ukumbi
wa mikutano wa Kanisa la Kiinjili
la Kilutheri Tanzania (KKKT) jijini Dodoma, Ijumaa wiki hii.

Malekana, ambaye ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato alisema kuwa mafanikio ya kidunia yanataka juhudi na akili zako za mtu, lakini bila Mungu juhudi na akili hizo haziwezi kumfikisha popote.

Akinukuu maandiko kutoka katika kitabu cha Kutoka 33:15, mwenyekiti huyo wa bodi aliwakumbusha washiriki wa mkutano huo na jamii kwa ujumla, kuishi kwa kumwomba Mungu.

“Katika maisha yako omba Mungu awe pamoja nawe, iwe ni biashara unafanya au utumishi popote pale. Yesu alisema pasipo mimi hamuwezi kufanya neno lolote, na sisi kama Chama cha Biblia tunamwomba Mungu awe pamoja nasi katika majukumu ya chama katika kutafsiri Biblia, kuchapisha, sambamba na kutawanya maandiko matakatifu”.

“Kizazi hiki kinatakiwa watu warudi kwenye Neno la Mungu na kumtazama Kristo, na kwa upande wetu Chama cha Biblia tunajitaidi kuchapisha na kusambaza Neno la Mungu kwa kila mtu, wakiwemo watoto, wafungwa..na vijana ni kipaumbele cha Chama cha Biblia cha Tanzania

MG 0054 scaled

Picha kutoka kushoto ni Dkt. Alfred E. Kimonge katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, wa pili kutoka kushoto ni Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania, wa tatu kutoka kushoto ni Askofu Christian Ndossa wa Kanisa la Kilutheli la Kiinjili Tanzania Dayosisi ya Dodoma na Mwisho Askofu Amos Muhagachi, Makamu Mwenyekiti wa Bodi.

MG 0063 scaled

Askofu Christian Ndossa wa Kanisa la Kilutheli la Kiinjili Tanzania Dayosisi ya Dodoma akihudumu wakati wa mkutano huo.

MG 0101 scaled

Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania akionesha riport ya taarifa ya fedha

MG 0102 scaled

Dkt. Alfred E. Kimonge katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, akiwasilisha taarifa ya utendaji na fedha kwa mwaka wa 2022.

MG 0070 scaled
MG 0184 scaled
MG 0105 scaled
MG 0136 scaled
MG 0138 scaled
MG 0126 scaled
MG 0125 scaled
MG 0180 scaled
MG 0229 scaled
MG 0195 scaled
MG 0201 scaled

Katika maisha yako omba Mungu awe pamoja nawe, iwe ni biashara unafanya au utumishi popote pale. Yesu alisema pasipo mimi hamuwezi kufanya neno lolote, na sisi kama Chama cha Biblia cha Tanzania tunamwomba Mungu awe pamoja nasi katika majukumu ya chama
katika kutafsiri Biblia, kuchapisha, sambamba na kutawanya maandiko matakatifu”.

Askofu Christian Ndossa

Askofu, KKKT

Naye Askofu wa KKKT Dayosisi ya Dodoma, Christian Ndossa alisema neno la Mungu ndio msingi na taa za miguu ya chama hicho.

Askofu Ndossa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo alisema kuwa, chama hicho kinaweza kuwa na vitabu vingi pamoja na mipango mbalimbali, lakini bila neno la Mungu kitakosa kitu cha kukisaidia.

“Tunaweza kuwa na mipango mbalimbali, tukawa na vitabu vingi, tukasoma maandiko ya wataalamu lakini tukakosa kitu
cha kutusaidia kama tutakosa neno la Mungu ambalo ndio taa ya miguu yetu na mwanga katika maisha yetu sisi tulio wanachama wa Chama cha Biblia Tanzania,”
alisema.

Askofu huyo aliwakumbusha washiriki wa mkutano huokumwomba Mungu zaidi kwa kuwa wanahubiri injili katika kizazi kinachobadilika lakini wao wanahubiri neno la Mungu lisilobadilika, jambo linaloibua changamoto mbalimbali ikiwemo lugha.
Alitoa mfano kuwa wakati wao kama chama wanajitahidi kuhubiri injili kwa lugha ya
Kiswahili inayosikika kwa watu wengi, lakini Kiswahili chenyewe kinabadilikabadilika.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Alfred Kimonge alisema wanayo
kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa rehema na baraka zake kwa mwaka wa 2022.

“Hakika umekuwa mwaka wa baraka kwetu, umekuwa mwaka wa kuinuliwa na kuendelea kufanya kazi ya Mungu kwa ujasiri na bidii baada kipindi cha mpito ambacho dunia ilikubwa na ugonjwa wa hatari wa mlipuko wa Covid-19. Hakika Mungu ni mwaminifu sana kwetu,” alisema.

BST IMAGE

Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

Uenezaji wa Maandiko kwa 2022

Uenezaji wa Maandiko kwa 2022

Taasisi yetu kwa mwaka uliopita uliambatana na Baraka zake. Muungano wetu wa vyama vya Biblia ulimwenguni ulituweka katika mpango wa kuwafikia watu milioni moja ulimwenguni walio katika mazingira magumu au walengwa ambao hawana uwezo wa kununua Biblia. Tanzania tulipewa nakala 50,000 za Biblia. Biblia hizo tulizigawa katika mashule na magereza.

Mch. John Mnongone akimkabidhi SSP Nelson Kanyungu askari anayehudumia Ibada katika gereza la Kigoma
20220928 134320 scaled

Mch. John Mnong’one akimkabidhi SSP Nelson Kanyungu askari anayehudumia Ibada katika gereza la Kigoma. Picha ya Pili akikabidhi viongozi wa Makanisa yaliyomo katika Kambi ya wakimbizi Nyarugusu Kasulu

20220713 140251 1 scaled
Watoto wa Shule ya Msingi Suguta Kongwa1
Watoto wa Shule ya Msingi Suguta Kongwa2

Watoto wa shule ya Mshingi Suguta Kongwa wakifurahia kupata Biblia.

Uenezaji wetu Mwaka huu ulikuwa kama ifuatavyo.

Biblia 500, 0000

Agano Jipya 59,000

Sehemu za Bibia portion 1,800

 

FCBH

Akina mama hawa wa Kabila la Kibarbaig walisikiliza mpango wa FCBH walihitimu kupewa Biblia bure. Walikataa kupokea Biblia ya bure wakalipia Biblia zao kwa furaha.

Tulipowambia kuwa wana stahili,

walisema heri kutoa kuliko kupokaea

BIBLIA INAYOONGEA.

Tunamshukuru Mungu kwa taasisi yetu kuingia  mkataba na  Shirika la Talking Bible International kuwa Chama cha Biblia cha Tanzania tumekuwa kituo cha kuandaa na kugawa Biblia TB inayoongea kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Mpaka sasa tumeandaa na kugawa nakala 450 za TB kwa nchi za Kenya, Uganda na Zambia.

Watumishi wakiandaa TB

Hapa watumishi wa Chama cha Biblia wakiandaa TB katika lugha ya Kibemba na Kitonga tayari kwa kuzipeleka Zambia

Mwaka huu CBT kiliendesha semina kwa wasioona 18 na kuwafundisha kusikiliza Agano Jipya .

TB

Give Today

Children

Prison

Membership

Youth

Blind

Other

Get In Touch