MKUTANO WA VIONGOZI WA MAKANISA YA KANDA YA KASKAZINI NA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA ULIOFANYIKA WILAYANI MOSHI MKOANI KILIMANJARO. (TAREHE 04/06/2019).

MKUTANO WA VIONGOZI WA MAKANISA YA KANDA YA KASKAZINI NA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA ULIOFANYIKA WILAYANI MOSHI MKOANI KILIMANJARO. (TAREHE 04/06/2019).

Na: Felix Rwebandiza Jones.
Kitengo cha Tehama.

Mwenyekiti wa Kikao ambaye pia ni Baba Askofu Msaidizi wa Kanisa la Kirutheri la Kiinjiri Jimbo la Moshi

Mwenyekiti wa Kikao ambaye pia ni Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Jimbo la Moshi, akifungua kikao

Wajumbe.
Waliohudhuria walikuwa 36 kama inavyooneshwa hapa chini.
1. Wakurugenzi Chama cha Biblia cha Tanzania (Rev. Askofu Amosi Muhagachi ambaye ni Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania na Eng. Ekael Manase ambaye ni mjumbe wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania).
2. Maafisa wa Chama cha Biblia cha Tanzania (Rev. Ipyana Mwangota amabaye ni Meneja Tafrisi na Felix Jones ambaye ni Mkuu wa kitengo cha TEHAMA).
3. Wachungaji na Mapadre.
4. Mwangalizi wa Jimbo Katoliki la Moshi.
5. Wenyeviti wasaidizi wa Maaskofu.
Agenda kuu ya Kikao ilikuwa ni:
• Uhamasishaji wa Chama cha Biblia cha Tanzania,
• Uanachama na faida zake na
• Tafsiri ya Biblia kwa ujumla wake.
Baada ya ufunguzi wa kikao mwenyekiti aliruhusu watumishi kijitambulisha
Mmoja wa wajumbe akijiambulisha

Mmoja wa wajumbe akijitambulisha wakati wa Mkutano huo

na baada ya hapo alimkaribisha Rev. Askofu Amosi Muhagachi kueleza ujumbe wake kutoka Chama cha Biblia Cha Tanzania. Askofu Muhagachi alianza kwa kuelezea historia yake, kabla ya kuanza kufanya kazi na Chama cha Biblia cha Tanzania, ambapo akiwa mwanafunzi na mwanachama aliweza kuwa muhamasishaji katika shule ya Sekondary ya Mirambo Tabora na aliweza kuwahamasisha wanafunzi wenzake wachangie Chama cha Biblia cha Tanzania ili kipate fedha za kuchapisha Biblia nyingi ili wanafunzi wenzao wapate Neno la Mungu kama wao. Alifanya hivyo katika kipindi chote cha masomo yake “nilikuwa nikihamasisha wanafunzi wenzangu tuchangie Chama cha Biblia cha Tanzania, ili Chama cha Biblia cha Tanzania kiweze kuchapisha Biblia nyingi ili sisi na vijana wenzetu tupate Biblia” alisema Rev. Askofu Amosi Muhagachi.
Rev. Askofu Muhagachi akizungumza wakati wa Kikao

Rev. Askofu Muhagachi akizungumza wakati wa Kikao

Baba Askofu Amosi Muhagachi baada kuhitimu masomo yake alipata barua ya kuitwa kwenye usaili na baada ya hapo aliweza kuajiriwa kuwa Afisa Uhusiano na Makanisa na Uhamasishaji wa Chama cha Biblia cha Tanzania ambapo alikaa kwa miaka saba kabla ya kuwa Askofu wa kanisa la Mennonite Tanzania na baadaye kwenda masomoni nchini Marekani, ambako bado anaendelea na masomo yake.
Baba Askofu Amosi Muhagachi alieleza mikakati ya Chama cha Biblia cha Tanzania ambayo ni;
i. Kuyaomba makanisa kutenga juma moja kuombea Chama cha Biblia cha Tanzania na watendaji wake.
ii. Kuomba watu kujitolea kuchangia Chama cha Biblia cha Tanzania ili kipate pesa za kutosha za kutafiti, kuchapisha na kusambaza Neno la Mungu kwa lugha mbali mbali hapa Tanzania.
iii. Kuomba viongozi wa makanisa wakubali kuchangia mpango mkakati wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa kupeleka Neno la Mungu kwa wafungwa, vijana na watoto.
iv. Kuwaomba viongozi wa Makanisa kuendesha mpango wa kuwepo mashindano ya kukariri mistari ya Biblia kwa vijana na watoto katika Shule, Makanisa na Vyuoni.
v. Kuhamasisha utumiaji wa Biblia (Hard copy) makanisani na viongozi wahakikishe zimeandikwa au zina nembo ya Chama cha Biblia cha Tanzania kama njia ya kuepukana na watu wanaogushi/kuchakachua Neno la Mungu.
Baada ya kumaliza hotuba yake alimuomba Mwenyekiti wa kikao amkaribishe Eng. Ekael Manase alielezea juu ya Uanachama, wa Chama cha Biblia cha Tanzania.
Eng. Ekael Manase alianza kwa kumshukuru sana Baba Askofu Amosi Muhagachi kwa jinsi alivyoeleza vizuri kuhusu kuwahamasisha watu kukichangia Chama cha Biblia cha Tanzania.
Pia aliendelea kwa kuwaomba sana na kuwasihi watumishi wa Mungu wote waliohudhulia kuwa wanatakiwa kuwahimiza waumini wao na kufufua ari ya kusoma Neno la Mungu ikiwa ni pamoja na kuanzisha mashindano ya kusoma na kukariri mistari ya Biblia kwa vijana na watoto, kwa lengo la kuwaandaa ili waweze kukua wakilishika Neno la Mungu. Lakini pia aliwaomba sana wachungaji na mapadre kuwahimiza sana waumini wao kutumia Biblia (hard copy) na kuacha kutumia Biblia zilizowekwa kwenye simu za mikononi (soft copy). Kwani wanaweza wakasoma Neno lililopotoshwa na watu wenye nia ovu kwa Ukristo.
Eng. Ekael Manase aliendelea kueleza kuwa hayo yote hayawezi kufanikiwa kama vijana wetu na watoto wetu hawatakuwa na Biblia zao; kwa hivyo basi ili jambo hili liweze kufanikiwa tunahitaji tuwe na Biblia za kutosha na kwa bei wanayoimudu. Biblia za bei nafuu zinaweza kupatikana tu; endapo kama sisi sote tutajitoa kukichangia Chama cha Biblia cha Tanzania. “Maana kama Biblia zingeuzwa kwa bei yake halisi ingekuwa ghali sana, lakini michango inayotolewa kwa CBT inafanya Biblia iweze kuuzwa kwa bei rahisi” alisema Eng. Ekael Manase.
Pamoja na melezo mazuri ya kuwahamisha watumishi wa Mungu kuhusu kuchangia Biblia na kuwa himiza watoto na vijana kusoma Biblia, pia Eng. Ekael Manase aliwaeleza wajumbe waliohudhuria aina za uanachama; kuwa kuna uanachama wa aina tatu;
i. Uanachama wa maisha
• Uanachama wa Maisha Mme na Mke shilingi 15,000= na ahadi isiyopungua shilingi 15,000=kwa mwaka.
• Uanachama wa Maisha mtu mmoja shilingi 10,000= na ahadi isiyopungua shilingi 10,000= kwa mwaka.
ii. Uanachama wa Bidii
• Uanachama wa kawaida (bidii ) shilingi 5,000=kwa mwaka.
• Uanachama wa kawaida kwa Wanafunzi wa Sekondari na Vyuo shilingi 2,000= au zaidi kwa mwaka.
• Uanachama wa kawaida wa kushirikishwa kwa watoto na wanafunzi wa shule za Msingi shilingi 1,000= au zaidi kwa mwaka.
• Mwanachama wa Biblia Moja kwa Mwezi (Bible a Month Club) 5,000=, 10,000=, 15,000=, 20,000= au zaidi kwa mwezi.
iii. Uanachama wa Mashirika
• Uanachama wa Mashirika shilingi 50,000= na mchango usiopungua shilingi 50,000= kwa mwaka.
Mwisho Eng. Ekael Manase alimalizia kwa kusema kuwa hii itakuwa ni njia nzuri Zaidi ya kuwakusanya vijana na kupenda kusoma Neno la Mungu, na pia itasaidia sana kupanda mbegu ya Neno la Mungu ndani yao na kuwa na Taifa lenye kumcha Mungu na lenye maadili mema.
Kwa upande wake Meneja wa Tafsiri wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Mch. Ipyana Mwangota alipopewa nafasi ya kuzungumza mbele ya wajumbe wote; alielezea kazi za Tafsiri anazozifanya ndani ya Chama cha Biblia cha Tanzania akiwa kama Meneja wa Tafsiri. Alifafanua kuwa wanafanya kazi ya kutafsiri Biblia kwa lugha mbali mbali ikiwa njia mojawapo ya kulisaida Kanisa kufanya kazi ya umisheni.
Mch. Ipyana Mwangota akitoa ukizungumzia juu ya Tafsiri

Meneja tafsiri, Mch. Ipyana Mwangota akitoa ukizungumzia juu ya Tafsiri

Alifafanua Zaidi juu ya kazi ya Tafsiri na kutaja Tafsiri zinazofanyika upande wa kanda ya Kasikazini ambazo ni Tafsiri ya Kivunjo, Kidatooga, Kimashame na Kimochi. Alinukuriwa akisema Pia Chama cha Biblia cha Tanzania kinakamilisha uchapaji wa Biblia ya Kisukuma. Kazi hii imepelekwa kule Korea kwa ajili ya uchapishaji. Ni tarajio letu kuwa kazi ya uchapishaji na uzinduzi itakamilika mwishoni mwa mwaka huu 2019. “Chama cha Biblia cha Tanzania kimepokea maombi ya Tafsiri na sasa kinaendelea kufanya pia Tafsiri ya lugha mbalimbali kubwa kama Igikuria, Kiha, Kinyiramba, Kirimi, Chikaguru na kihehe. Aidha CBT tumepokea maombi ya Kanisa katika maeneo ya Ufipa, Unyamwezi, Unyiha, na Upare ili kiweze kusaidia kutafsiri Biblia kwa Lugha ya Kifipa, Kinyamwezi, Kinyiha na Kipare na kukubali; na sas Chama cha Biblia cha Tanzania kipo katika mchakato wa kutafuta fedha ili kuianza kazi hii kwa ushirikiano na Makanisa mwaka 2020 Januari.
Baadhi ya Wajumbe wakisikiliza kwa Makini

Baadhi ya Wajumbe wakisikiliza kwa Makini.

Pia alieleza kuwa zipo Biblia ambazo zimetafsiriwa, kuchapishwa na zinatumika katika makabila lengwa kama vile Biblia ya Kinyakyusa (Mkoa wa Mbeya), Biblia ya Luhaya (Mkoa wa Kagera), Biblia ya Cigogo (Mkoa wa Dodoma), Biblia ya Kimasai (Mkoa wa Arusha), na Biblia ya Kihiraqw (Mkoa wa Manyara).
Pia alieleza kuwa Chama cha Biblia kimefanya tafsiri za Agano Jipya na sehemu za Biblia nyingi tu na zinatumika maeneo tofauti tofauti ili kukidhi haja ya watumiaji wa lugha husika kuendana na sera ya Vyama vya Biblia Duniani.
Kuhusu mchakato wa kazi ya tafsiri; Meneja Tafsiri alieleza kuwa ofisi yake, hutumia vifaa vya kisasa. Kwa lengo la kufanikisha kazi hii kubwa. Alionyesha Program ya Paratext kwa wajumbe wa mkutano kama mfano wa vifaa hivyo ili waone jinsi kazi hii inavyotendeka. Wajumbe walipongeza kazi hii kubwa na waliahidi kuiombea.
Pia alieleza kuwa Chama kwa sasa kinatia mkazo uwepo wa Biblia za Watoto, na hivyo kimekuwa kikiandaa Biblia za watoto ili kuhakikisha Makanisa hayakosi Biblia kwa watoto wadogo, wa kati na wale wanaoelekea umri wa utu uzima.
Mwisho alitoa wito kwa viongozi wa Makanisa kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na Chama cha Biblia cha Tanzania katika kuhakikisha Maandiko Matakatifu yanapatikana kikamilifu kwa kuchangia na kuombea juhudi hizi.

Mkutano Mkuu wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania (CBT) 2018.

Mkutano Mkuu wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania (CBT) 2018.

Mkutano Mkuu wa Chama Cha Biblia wa mwaka 2018 uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa kuu la Kiinjili la Kirutheli Dayosisi ya Dodoma tarehe 12/4/2019.

MATUKIO KATIKA PICHA.

Viongozi wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania wakijadiliana mambo mbalimbali kabla ya kuingia kwenye mkutano.

Viongozi wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania wakijadiliana mambo mbalimbali kabla ya kuingia kwenye mkutano.

Watumishi wa Chama Cha Biblia Ndugu Choyo Sabanjakatikatina Neema Mathayo Kushoto wakiandikisha wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka 2018.

Watumishi wa Chama Cha Biblia Ndugu Choyo Sabanja(katikati)na Neema Mathayo (Kushoto) wakiandikisha wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka 2018.

Jaji mkuu Mstaafu wa Tanzania Mh.Augustino RamadhanikatikatiRev.Martina Kabisamakulia

Jaji mkuu Mstaafu wa Tanzania Mh.Augustino Ramadhani(katikati),Rev.Martina Kabisama(kulia) na Rev.Victoria Ntenga ambao ni wajumbe wa Bodi ya Chama Cha Biblia Cha Tanzania wakipitia Ajenda za Mkutano mkuu wa Chama.

Wajumbe wa Bodi ya Chama Cha Biblia Cha Tanzania Prof. Godfrey Majule Kushoto Prof. Godson Maanga na Askofu Amos Muagachi

Wajumbe wa Bodi ya Chama Cha Biblia Cha Tanzania Prof. Godfrey Majule (Kushoto), Prof. Godson Maanga na Askofu Amos Muagachi wakipitia kwa makini agenda za mkutano mkuu wa Chama Cha Biblia uliofanyika tarehe 12/4/2019 Dodoma.

 

Mjumbe wa Mkutano mkuu kutoka Mwanza Muinjilisti Sifaeli Mgema

Mjumbe wa Mkutano mkuu kutoka Mwanza Muinjilisti Sifaeli Mgema akichangia mada kwenye mkutano mkuu wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania.

 

Mjumbe wa Mkutano mkuu kutoka Kigoma Fidelis Mbiha

Mjumbe wa Mkutano mkuu kutoka Kigoma Fidelis Mbiha akichangia mada kwenye mkutano mkuu wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania

 

Mwenyekiti wa Bodi Rt Rev Mark.Marekanawa pili kutoka kuliaMakamu Mwenyekiti Rev.Dr .Jackson NyandaKatibu mkuu Alfred E.Kimonge

Viongozi wakuu wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania Mwenyekiti wa Bodi Rt Rev. Mark Marekana(wa pili kutoka kulia),Makamu Mwenyekiti Rev.Dr.Jackson Nyanda,Katibu mkuu Alfred E.Kimonge (wa pili kushoto)na Mhazini Fr.Chesco P.Msaga wakijibu hoja za wajumbe kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka 2018 uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa kuu la Kiinjili la Kirutheli jijini Dodoma.

 

Mhazini mkuu wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania Fr.Chesco P.Msaga

Mhazini mkuu wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania Fr. Chesco P. Msaga akisoma taarifa ya fedha kwenye mkutano mkuu wa mwaka 2018.

 

Mchungaji Salum Isaka

Mchungaji Salum Isaka kutoka kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu akielezea jinsi Mradi wa Uponyaji wa Vidonda vya nafsi unavyowanufaisha wakimbizi kukabiliana na vidonda vya nafsi. Katika Mkutano Mkuu huo wa Mwaka 2018.

 

Askofu Amos Muagachi

Askofu Amos Muagachi akielezea taarifa ya uhamasishaji wa wanachama wapya wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania kwenye mkutano mkuu wa mwaka 2018 uliofanyika terehe 12/4/2019.

 

Wanawake wa Kikagulu kutoka Gairo

Wanawake wa Kikagulu kutoka Gairo wakisoma kitabu cha CHIBWEDA kilichoandikwa kwa Lugha ya Kikagulu. Wakati Mkutano Mkuu wa Mwaka 2018.

 

Ndugu Frank makala

Wanawake wa Kigagulu kutoka Gairo wakisoma kitabu cha CHIBWEDA kilichoandikwa kwa Lugha yao wakiwa pamoja na Mratibu wa mpango wa wanawake kusoma na kuandika(LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA) Ndugu Frank makala(kushoto). Wakati Mkutano Mkuu wa Mwaka 2018.

 

Meneja Shughuli Mchungaji John Mnongone

Meneja Shughuli Mchungaji John Mnong’one (kushoto) na mratibu wa miradi ya LITERACY na TRAUMA HEALING Ndugu Frank Makalla (katikati) wakifutilia yanayoendelea kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka 2018.

 

wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma

Picha ya pamoja ya viongozi wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania pamoja na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma waliojiandikisha kuwa wanachama wa Chama Cha Biblia Cha Tanzania.

 

Picha ya pamoja ya wakurugenzi wa Bodi na Menejimenti ya Chama Cha Biblia Cha Tanzania.

Picha ya pamoja ya wakurugenzi wa Bodi na Menejimenti ya Chama Cha Biblia Cha Tanzania.

 

Picha ya pamoja ya watumishi na wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama Cha Biblia wa mwaka 2018

Picha ya pamoja ya watumishi na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Biblia wa mwaka 2018 uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa kuu la Kiinjili la Kirutheli Dayosisi ya Dodoma tarehe 12/4/2019.

Tangazo Muhimu! Announcement!

Tangazo Muhimu! Announcement!

Chama cha Biblia cha Tanzania kupitia uongozi wake, kinawatangazia  na kuwakaribisha wanachama wake wote wakiwemo wakurugenzi wa Bodi wa chama, wafanyakazi, na  wadhamini wake kuhudhuria mkutano  mkuu wa mwaka 2018 wa kupokea  taarifa ya mwaka uliopita na kupanga mipango ya mwaka huu. Mkutano utafanyika tarehe 12/4/2019 katika ukumbi wa Kanisa la Lutheran Dodoma mjini kuanzia saa 2:00 asubuhi.

Wanachama wote wanakaribishwa kushiriki ili kufanikisha malengo ya mkutano wetu.

(more…)

Chama cha Biblia cha Tanzania, kimeanzisha utekelezaji wa mradi wa kujifunza kusoma na kuandika kwa watu wazima kwa lugha ya kikagulu.

Chama cha Biblia cha Tanzania, kimeanzisha utekelezaji wa mradi wa kujifunza kusoma na kuandika kwa watu wazima kwa lugha ya kikagulu.

1 Berega 1

ONGERA: Wakakugulu kwa kuhitimu Mafunzo ya kusoma na kuandika.

Chama cha Biblia cha Tanzania, kimeanzisha utekelezaji wa mradi wa kujifunza kusoma na kuandika kwa watu wazima kwa lugha ya kikagulu na kiswahili waliokosa fursa hiyo kutokana na sababu mbalimbali, katika vijiji 30 vya wilaya ya Gairo mkoni Morogoro ikiwa ni sehemu ya kuunga juhudi za serikali kupambana na adui ujinga.

Akizungumza kwenye mahafali ya kwanza yaliyojumuisha  wahitimu 97 wa elimu ya watu wazima yaliyofanyika katika kijiji cha Berega wilyanai hapa

4 Berega

Mratibu wa Mradi, Mwl. Frank Makala (Kulia) akitoa taarifa fupi ya mradi mbele ya katibu mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania.

Mratibu wa mradi huo Frank Makala, alisema kuwa lengo ni kuwasaidia kujua kusoma na kuandika wote waliokosa fursa hiyo hapo awali.

Alisema kuwa wahitimu hao 97, ni sehemu ya 120 ambao ndiyo wajiiandkisha kujiunga na elimu ya watu wazima ya kusoma na kuanadika mwezi Septemba mwaka jana ambao wachache kati yao walishindwa kufika mwisho kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo hali ya kiuchumi.

“Hawa wahitimu wanaomaliza leo ni kutoka katika vijiji 10, ambavyo ndivyo tulianza navyo katika mradi kama awamu ya kwanza na leo 97 wameza kuhitimu na wote wanajua kusoma na kuandika wengine wachache wamekosa kufika siku ya leo kutokana na hali za kiuchumi kwani wengine walilazimika kwenda kwenye shughuli zao za kilimo ili kujitafuatia riziki”alisema Makala.

Makala aliongeza kuwa mradi huo wa kusoma na kuandika unatoa mafunzo kwa kutumia lugha na kiswahili na  kikagulu ili kuweza kuwawezesha wanafunzi kuelewa kwa wepesi.

“Tunatumia lugha mama ya kikagulu na kiswahili katika kufundisha na hii imetusaidia sana kuweza kuwafundisha wanafunzi hawa ambao ni watu waziama na wengi wao walikuja hawajui lolote kwenye upande wa kusoma, lakini kwa kipindi cha miezi sita kila mmoja anajua kusona na kuandika kwa lugha yake ya kuzaliwa ambayo ni kikagulu lakini pia wakati huohuo na kiswahili”alisema.

Alifafnua kuwa madarasa mengine katika awamu ya pili yanatarajia kuanza mwezi Aprili mwaka huu ambapo vijiji vingine 10 vitahusishwa na baadaye mwezi mei vijiji vingine 10 na watarajia hadi ifikapo Novemba 2019 kuwa na jumla ya vijiji 30, ambavyo vimefikiwa na mradi huo.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Askofu wa kanisa Agrikan Tanzania Dayosisi ya Morogoro, Canon Isack Mgego akizungumza katika mahafali hayo alisema wao kama kanisa wanajisikia faraja kuwa sehemu ya kuwawezesha watanzania katika kupambana na adui ujinga.

5 Berega 1

Mgeni Rasmi Canon Isaac Mgego akihutubia wakati wa sherehe hiyo

“Adui ujinga ni moja kati ya maadui ambao taifa letu linapambana nao na sisi kama kanisa tunayofuraha leo kuwezesha watu kujua kusoma na kuandika ili waweze kuondokana na umaskini ambao umekuwa ukiwakabili”alisema Mgego

.Naye mmoja wa wahitimu wa mafunzo hayo Saraha Robert, alisema kuwa anashikuru mradi huo kutoka Chama cha Biblia Tanzania kutokana na kumwezesha kujua kusoma na kuanadika na atoa rai kwa wengine kujitokeza katika kushiriki katika madarasa yanayofuata.

“Mimi nilikuwa sijui kabisa kusoma lakini kufunshishwa kusoma na kuandika kwa kutumia lugha yangu mama kuniwezesha kujua kwa haraka zaidi, na sasa nitaweza kusoma magazate,vipimo vya afya lakini pia matumizi ya dawa ninayoandikiwa hospitalini” alisema.

Matukio katika Picha

GS

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia akicheza na wanakisomo wakati wa mapokezi.

2 Berega

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Canon Boniface Mkami, Mwl. Ngobei, Mzee wa Kanisa, Mratibu wa Mradi Mwl. Frank Makalla kutoka Chama cha Biblia cha Tanzani. Wakisalimia

diwani 1

Utambulisho: Diwani wa Kata ya Berega Gairo Morogoro

Shangwe

Wahitimu wakishangilia kwa Furaha

 

8 Berega 1

Wanakisomo wakisoma Risala Mbele ya Mgeni rasmi

3 Berega

Katibu Mkuu wa CBT, akitoa maelezo mafupi kuhusu mradi wa Elimu ya watu wazima kwa wakina mama wa Kikaguru.

6 Berega

Mmoja wa wahitimu akipokea cheti wakati wa sherehe hiyo.

Chama cha Biblia cha Tanzania, kimeanzisha utekelezaji wa mradi wa kujifunza kusoma na kuandika kwa watu wazima kwa lugha ya kikagulu.

Adult villagers in Gairo given another chance to learn how to read, write.

Under Literacy Women in Africa Program (LWA) Adult Villagers in Berega Gairo Morogoro Tanzania given another chance to learn how to read and write.

1 Berega

CONGRATULATION: Photo that include the graduates, the guest of honor and the General Secretary of the Bible Society of Tanzania and other guests that were invited.

ADULT villagers in Gairo District in Morogoro Region who missed the formal primary education have another chance to learn how to read and write, thanks to the Bible Society of Tanzania. The society in collaboration with the Bible Society of Finland has initiated a programme to enable the villagers, especially women, to learn to read and write in their own language in Kaguru.

9 Berega

Graduate students playing and dancing with great joyful during their graduation.

Reading out a statement on behalf of fellow students, Buitisi Lirni thanked the Bible Society for the efforts that have made them achieve the goal.

8 Berega 1

Bi. Buitisi Lirni, Reading out a statement on behalf of fellow students.

She said now they can easily read the bible and other literature in Kaguru language and Kiswahili. “We missed this opportunity at early stages in life due to various but we can now read and write through the support of the Bible Society of Tanzania” she said.

She said through the programme they can now read the bible and other publications, noting that the programme has helped expand their horizon.

Speaking at the meeting the General Secretary of the Bible Society of Tanzania, Mr. Alfred Kimonge the programme undertaken through cooperation with Bible Society of Finland was to help women, especially those in the villages to read and write.

3 Berega 1

The General Secretary of the Bible Society of Tanzania, Mr. Alfred Kimonge (Standing) speaking during the Graduation.

He said women have shown great strength in fostering cooperation in any society and helped bring the desired changes, thus it was prudent to empower them to read the bible and other literatures.

Mr. Kimonge also observed that the church has a role to play in transforming the society, adding the program is in line with the government’s efforts to provide basic education to all Tanzanians. The General Secretary stated that Tanzania is among the five countries (Tanzania, Kenya, Malawi, Ethiopia and Namibia) globally that benefit from the program aimed at providing basic Learning skills using the respective people’s mother tongue.

“I am impressed by what I have seen here, now that you are able to write and read out your own statement, this is a clear indication the program has opened opportunity for to read more” he said.

He said bible translation in Kaguru language will be out soon, thus they will be able to read the word of God by themselves in their own language.

Also, Mr. Frank Makalla he said, these teachers are expected to start training new students on April 8, 2019 in those particular villages.

But also there will be training for other new twenty teachers, from ten other villages. From there they will start to register a new illiterate people (Women) and those students will begin their training on June 2019 at Berega Village.

4 Berega

Mr. Frank Makalla (Right) who is program coordinator speaking during the Graduation ceremony.

Guest of honor at the event, Canon Isaac Mgego noted that it was great honor to have people learn in their native language, that they understand most

5 Berega

Canon Isaac Mgego speaking during the graduation.

He said through the program, Kaguru tribe that was at the verge of extinction will now have its rightful honor once again. ”Please public more books in Kaguru language to help maintain our heritage as well as helping young generation to learn the language” he said.

However, he cautioned that using mother tongue should be used to help foster development instead of causing discrimination and division among them.

6 Berega

One of the graduates receiving certificate from the guest of honor.