Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha hata atakapo kuwa mzee. [Mithali 22:6]
Wapendwa Taifa la Mungu na wakristo wa Tanzania, malezi ni uangalizi wa karibu wa wazazi kwa mtoto wao kiroho, kiafya, kiakili, kitabia ili tuwe na Taifa imara na watu wanaomcha Mungu. Mungu alipomuumba Adamu na Hawa akasema “zaeni mkaongezeke…………[Mwanzo 1:28.]”
Ni wajibu wa wazazi katika familia na kanisani kuwahimiza watoto kulisoma na kulipenda Neno la Mungu yaani Biblia. Katika [Rum. 8:28] tunasoma: “Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema……” Hii ni pamoja na kazi ya kulea watoto; Mungu hufanya kazi hiyo pamoja na sisi.
Katika [Zab. 127:3] Biblia inasema “Tazama wana ndio urithi wa BWANA uzao wa tumbo ni thawabu.” Mungu hatupi watoto ili tuwahifadhi kwa matumizi yetu wenyewe. Yeye anatupa watoto ili tuwalee kwa utukufu wake. Watoto wetu ni wa Mungu. Mungu amelithibitisha agano lake pamoja nasi, Katika [Kumb. 28:4] anasema “Utabarikiwa uzao wa tumbo lako” Pia katika [Isaya. 8:18] inasema “Angalieni, mimi na watoto hawa niliyopewa na BWANA tu ishara na ajabu katika Israel……” Kwa sababu hii Mungu anataka watoto wetu wajifunze Neno lake na kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Mungu anatazamia wazazi wawaelekeze watoto kwake, kwa njia ya Neno lake yaani Maandiko Matakatifu (Biblia).
Walinde watoto wako na vishawishi viovu.
Ujue nia ya shetani siku zote ni kutaka kuwaangamiza watoto, iwe kiroho au hata kimwili kwa kuwavuta katika mambo ya ulimwengu. Kuna mambo kadha wa kadha ambayo watoto wanakutana nayo maishani na haya yanaweza kusababisha au kuwaondoa kabisa wasimfuate Mungu sawasawa. Neno la Mungu linasema “Msiipende dunia wala mambo yaliyomo katika dunia… na dunia inapita pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”. [1Yoh. 2:15-17].
Marafiki wabaya na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii yameangamiza familia nyingi na kuwapoteza watoto na vijana katika kiwango cha kutisha [Mithali 13:20] Neno la Mungu linasema “… Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.” [Zab. 1:1] inasema: “Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.”
Nawasihi na kuwaomba Wakristo wa Tanzania kusimama na Chama chenu cha Biblia kuwaridhisha watoto wetu Neno la uzima, hivyo wapatie watoto Biblia katika maisha yao. Simama na huduma ya Chama cha Biblia cha Tanzania kuwapatia watoto na vijana.
Neno la Mungu kama zawadi na baraka kutoka kwa Mungu maishani mwao.
Amani na Neema ya Mungu iwe juu yako.
Mtumishi wenu katika Kristo
Alfred Kimonge.
Katibu Mkuu
JITIHADA ZINAZOFANYWA NA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA ILI KUHAKIKISHA VIONGOZI WA MAKANISA MBALI MBALI NCHINI WANAFIKIWA NA MPANGO HUU MADHUBUTI.
Pichani toka kulia: Baba Askofu Mkuu Dr. Shoo wa Kanisa la KKKT, Msaidizi wa Askofu wa Kanisa hilo, Dayosisi ya Kaskazini Mch. Saria, Baba Askofu Amos Muhagachi Balozi wa CBT na Mjumbe wa Bodi, na Eng. Ekaeli Manase mjumbe wa Bodi ya CBT; wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kupokea bahasha 10,000 kwa ajili ya kuchangia huduma ya Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT).
Pichani: Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania ndugu Alfred Kimonge (kushoto) na Fr. Sosthenes wa Kanisa Katoliki Dodoma baada kikao cha pamoja kilichomteua kuwa mmoja wa wawakilishi wa Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT).
Pichani: Baba Askofu Amos Muhagachi (wa tano toka kulia waliokaa) Balozi wa CBT na Mjumbe wa Bodi, akiwa na Mapadre wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Dodoma, baada ya Mkutano wa pamoja uliofanyika mjini Dodoma.
Pichani: Mtume na Nabii Josephat Mwingira (katikati ) wa Huduma ya Efatha na mkewe (kushoto) wakipokea zawadi ya Biblia kutoka kwa Baba Askofu Amos Muhagachi (kulia) Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) na mjumbe wa Bodi, alipomtembelea na kufanya mazungumzo naye kuhusu mkakati wa CBT wa kuhamasisha Makanisa kuchangia upatikanaji wa Maandiko Matakatifu kwa ajili ya watoto, vijana na wafungwa hapa Tanzania.
Pichani: Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) ndugu Alfred Kimonge (kushoto), Fr. Chesco P. Msaga (katikati) wa Kanisa Katoliki Dodoma na Baba Askofu Amos Muhagachi (kulia), Balozi wa CBT na mjumbe wa Bodi, wakiwa studio za Redio Mwangaza Dodoma akizungumza juu ya mkakati wa Chama wa kuhamasisha Makanisa na Wakristo wote kuchangia upatikanaji wa Maandiko Matakatifu kwa ajili ya watoto, vijana na wafungwa hapa Tanzania.
Unaweza usibadilishe dunia yote na kuifanya iwe ya kumpenda Mungu, lakini kwa sadaka yako ya upendo kwa Chama cha Biblia cha Tanzania ya Tsh 5000 tu! na kuendelelea unaweza kumbadilisha milele mtoto, kijana au hata mfungwa mmoja.
Tuma sadaka yako ya upendo kupitia namba ya M-PESA ya Chama: 890890 kisha tuma ujumbe wa kuchangia katika namba hizi: 0762998819, 0754383636 na 0754479789.
Pia unaweza kuchangia kupitia akaunti za Benki za DTB na NBC zilizoonyeshwa hapa chini Changia kupitia benki ya DTB: Namba ya Akaunti: 0901969001 SWIFT OR WIRING CODE DTKETZTZ na Changia kupitia benki ya NBC: Namba ya Akaunti: 029103000362 na Mungu akubariki sana.
Na Mungu akubariki sana
Askofu Amos Muhagachi
Mhariri
Mawasiliano yatumwe kwa: Katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, P.0. Box 175, Dodoma, Tanzania. Email: aekimonge@yahoo.com T: +255262324661 Fax: +255262324058.
KWA WANACHAMA WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA.
Umoja wetu katika Kristo!
“Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”. (Yohana 17:21-23).
Umoja wa Kanisa ndiyo ishara ya mwili wa Kristo katika Ulimwengu. Kanisa ni familia ya Mungu katika ulimwengu huu, ni jumuiya ya watu wa Mungu wamwaminio Yesu Kristo katika maisha yao wakimsifu na kumshangilia Mungu katika ushuhuda na kuwaleta wengine ili wamjue Mungu wa kweli katika maisha yao. Chama cha Biblia cha Tanzania kimeendelea kwa uaminifu wote kulihudumia kanisa la nchi yetu kwa umoja wake kwa kuwapatia Maandiko Matakatifu [Biblia] ili kuliwezesha kanisa kuwa na Biblia katika mifumo na tafsiri mbali mbali kwa ajili ya uinjilisti na utume wake.
Kwa unyenyekevu mkuu nawaalika Wakristo wa madhehebu yote katika nchi yetu kushiriki katika huduma hii.Nakuomba ukiombee na kukichangia Chama cha Biblia cha Tanzania ili kipate fedha kwa ajili ya kutafiti, kuchapisha na kusambaza neno la Mungu kwa watu wote. Ni maombi yangu kwamba asiwepo Mtanzania hata mmoja anayetamani kulisoma neno la Mungu akalikosa kwa sababu ya gharama kubwa. Mwaka huu tuna lengo la kuwapatia watoto, vijana na wafungwa Biblia. Kwa ushirikiano wa kanisa la Mungu hapa nchini, tunaweza kuwafikia watoto, vijana na wafungwa ili kujenga Taifa la wacha Mungu. Kwa sadaka yako na matoleo yako ya upendo utakuwa baraka kwa kumpatia mtoto, kijana na mfungwa kule gerezani neno la uzima.
Nakutumia barua hii ya upendo kukualika na kukukaribisha ili ushiriki pamoja nasi kulijenga Taifa letu kiroho ili liwe taifa lenye kumhofu na kumcha Mungu. Ombea Taifa letu ili watu wake walipende na kulisoma Neno la Mungu.
Ni kiu yangu kwamba kila mtoto, kijana na mfungwa awe na Biblia yake mkononi.
Neema na Amani ya Kristo iwe pamoja nawe.
Alfred E. Kimonge
Katibu Mkuu
HAMASA YA KUFUNGUA MATAWI MIKOANI
Hawa ni Wanachama wa Tawi la Kitivo cha Sayansi ya Jamii moja ya matawi matatu katika Chuo Kikuu cha Dodoma.
Tunamshukuru Mungu kwa kuanza mwaka huu kwa baraka zake na uamsho mpya wa Makanisa na Wakristo kujiunga kwa wingi kuwa wanachama wa Chama cha Biblia cha Tanzania. Hadi sasa tumefanikiwa kufungua matawi kama ifuatavyo;
1. Dodoma – Chuo Kikuu cha Dodoma [UDOM ]
i. Tawi la Kitivo cha Elimu – Wanachama 120
ii. Tawi la Kitivo cha Biashara na Utawala – Wanachama 78
iii. Tawi la Kitivo cha Sayansi ya Elimu ya Jamii – Wanachama 110
2. EAGT Buhemba Tarime – Wanachama 210
4. Umoja wa makanisa – Kilimanjaro
5. Marangu-Kilimanjaro
6. Umoja wa makanisa – jiji la Mwanza
Na bado hamasa inaendelea katika maeneo mengine likiwamo jiji la Dar es Salaam na Tabora.
Viongozi wa Makanisa ya Moshi ambao ni waanzilishi wa Tawi la Chama katika Mkoa wa Kilimanjaro
Mwenyekiti wa Tawi la EAGT Buhemba Tarime akimkabidhi mchango wake Askofu Muhagachi Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania.
Tunakuomba ushiriki katika huduma hii kwa maombi yako,unaweza kuchangia kila mwezi Tsh 2000,______ Tsh 5000,______Tsh 10,000,_______au kuchangia kwa mwaka Tsh 25,000, ____Tsh 50,000,_____Tsh 100,000 au zaidi. Kwa sadaka yako ya upendo unaweza kumfanya/kumgusa mtoto, kijana na mfungwa kumjua na kumfuata Kristo.
Nakualika kushiriki pamoja na Wakristo wengine waaminifu kwa kuchangia na kutuma mchango wako kwa akaunti ya M-PESA ya Chama cha Biblia cha Tanzania namba 890890 kisha tuma ujumbe wa kuchangia katika namba hizi: 0762998819, 0754383636 na 0754479789.
Pia unaweza kuchangia kupitia akaunti za Benki za DTB na NBC zilizoonyeshwa hapa chini. Kwa DTB Akaunti Namba: 0901969001; SWIFT OR WIRING CODE DTKETZTZ
Kwa NBC Akaunti Namba: 029103000362
Akaunti Namba: 0901969001; SWIFT OR WIRING CODE DTKETZTZ
Akaunti Namba: 029103000362
Mungu na akubariki. Askofu Amos Muhagachi Mhariri.
Mawasiliano yatumwe kwa: Katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, P.0. Box 175, Dodoma, Tanzania. Email: aekimonge@yahoo.com T: +255262324661 Mob: +255754383636
Chama cha Biblia cha Tanzania ni taasisi ya Kikristo inayojishughulisha na kutafsiri, kuchapisha na kueneza Maandiko Matakatifu yaani Biblia kwa niaba ya makanisa yote ya Tanzania. Pia Chama cha Biblia kinaendesha program mbalimbali kwenye jamii lengo likiwa ni kuihudumia jamii kiroo na kimwili (Holistic Ministry) Kupitia Program ya “Je yuko wapi Msamaria mwema Leo? inayojishughulisha na mapambano dhidi ya UKIMWI ikilenga kupunguza unyanyapa hasa makanisani, kuhamasisha watu kupima kwa hiari, watu kubadilisha tabia kwa kutumia neno la Mungu na kuleta muungamaniko wa makanisa/misikiti katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI. Chama cha Biblia kupitia program hii kimeweza kuwafikia watoto walioachwa yatima baada ya wazazi wao kufariki kwa ugonjwa wa UKIMWI, watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, wenye maambukizi na watoto wenye ulemavu.
Mtumishi wa Chama cha Biblia cha Tanzania (Mrs. Rose Mrema) akifundisha washiriki wa mafunzo ya watoto kutoka Ibohora.
Mpango huu wa watoto unatekelezwa katika kata ya Ubaruku,Wilaya ya Mbarali kwa kushirikiana na taasis za kidini, wadau wengine wanaohudumia watoto (KIWAUTA na SHIDEPHA) pamoja na viongozi wa serekali, na jamii kwa ujumla. Lengo ni kuwawezesha watoto hao kuishi maisha yaliyo kamilika kama walivyo watoto wengine, kuhamasishana kuikumbusha jamii wajibu wake juu ya watoto hao na kumjengea mtoto uwezo wa maisha kwa ujumla.
Waalimu wa Sunday school, madrasa, shule za secondary na primari waliopata mafunzo ya watoto toka kata ya Ubaruku wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mafunzo.
Watoto wakiwa kwenye majadiliano ya makundi wakati wa mafunzo.
Mafanikio.
Baadhi ya mafanikio ya program.
Mpango huu umepokelewa vizuri na Viongozi wa Serekali, dini, jamii pamoja na wadau wengine wanaojishughulisha na kuwahudumia watoto yatima na walioko kwenye mazingira magumu.
Tumeweza kukutana na viongozi wa serekali, dini na wadau wengine
Kufanya mafunzo na waalimu wa sunday school,madrasa, Waalimu wa malezi kutoka shule za msingi, na Sekondari zilizopo kata ya Ubaruku,na wahudumu wa watoto majumbani kutoka shirika la KIWAUTA .
Kuwafikia watoto zaidi ya 500 yatima na walioko kwenye mazingira magumu.
Kugawa vifaa vya kufundishia kwa washiriki waliopata mafunzo (Vitabu,Mwongozo na flip chart.)
Baadhi ya washiriki waliopata mafunzo waliweza kuendeleza mafunzo waliyopata kwa kuwafundisha wazazi wenzao,watoto makanisani, na mashuleni kwenye vipindi vya dini.
Wazazi wa watoto wakiwa katika majadiliano.
Vitendo vya unyanyasaji wa watoto majumbani vimepungua kwa kiasi kikubwa,,upendo umeongezeka ndani ya jamii, na kwa watoto wenyewe kwa wenyewe.
Baadhi ya watoto waliopata mafunzo wamebadilika tabia ,wamekuwa wasafi,anasaidia kazi za nyumbani,wameacha udokozi,wizi,kutukana na kupigana.
Washiriki wametambua wajibu wa kuwahudumia watoto hao ni jukumu la jamii nzima, wengi wao wameanzisha vikundi kwa lengo la kuwahudumia watoto na kutoa elimu kwa jamii.
Changamoto.
Washiriki wengi waliopata mafunzo hawajui kusoma na kuandika.
Mambo tuliyojifunza
Vijijini wapo watoto wengi ambao wameachwa na kusahaulika kutokana na hali duni ya maisha.
Miradi mingi ya kuwasaidia watoto hawa ipo mijini.
Wazazi/walezi wa watoto wanaishi kwenye mazingira magumu na hawana mtu anayewasaidia kuwalea watoto.Jambo hili linawafanya watoto kukosa mahitaji yao muhimu ya kila siku.
Ukosefu wa vitendea kazi kwa watoto walemavu.mf Baiskeli ili waweze kupata haki yao ya kwenda shule.
Elimu bado inahitajika kwenye jamii jinsi ya kuwahudumia watoto hawa hasa walemavu wengi wao wameachwa majumbani pasipo kupata elimu,matibabu na huduma nyingine muhimu.
Askari wa Gereza la Kiomboi wakipokea Biblia kwa niaba ya Wafungwa na Mahabusu wa Gereza la Kiomboi , Mkoa wa Singida wilaya ya Iramba.
Hawa ni Askari wa Gereza la Kiomboi wakipokea Biblia kwa niaba ya Wafungwa na Mahabusu wa Gereza la Kiomboi lililopa katika Mkoa wa Singida wilaya ya Iramba. Baada ya kupokea nilipata nafasi ya kuongea na Wafungwa na Mahabusu pamoja na Askari kutoa maelezo juu ya Chama Cha Biblia Tanzania kutoa Biblia hizo kwao, Wafungwa wawili walishukuru kwa niaba ya wenzao na kusema
” Tunamshukuru kwa Chama Cha Biblia kutukumbuka na kututhamini kwa kutuletea Biblia hizi na kwamba tutasoma Neno la Mungu na litatusaidia katika maisha yetu hata katika mazingira haya, asante sana”
But it shall not be so among you: but whosoever will be great among you, let him be your minister; And whosoever will be chief among you, let him be your servant.