BLOGO TransparentCHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

N0: 01 July 2019, NEWSLETTERS /BARUA YA UPENDO YA KILA MWEZI

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area, P.O Box 175, Dodoma Tanzania. || T: +255 (026)-2324661 F: +255 (026)-2324058 || Email: info@biblesociety-tanzania.org || Site: www.biblesociety-tanzania.org

KWA WANACHAMA  WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA.

Umoja wetu katika Kristo! 

“Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.  Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.  (Yohana 17:21-23).

Umoja wa Kanisa ndiyo ishara ya mwili wa Kristo katika Ulimwengu. Kanisa ni familia ya Mungu katika ulimwengu huu, ni jumuiya ya watu wa Mungu wamwaminio Yesu Kristo katika maisha yao wakimsifu na kumshangilia Mungu katika ushuhuda na kuwaleta wengine ili wamjue Mungu wa kweli katika maisha yao. Chama cha Biblia cha Tanzania kimeendelea kwa uaminifu wote kulihudumia kanisa la nchi yetu kwa umoja wake kwa kuwapatia Maandiko Matakatifu [Biblia] ili kuliwezesha kanisa kuwa na Biblia katika mifumo na tafsiri mbali mbali kwa ajili ya uinjilisti na utume wake.
Kwa unyenyekevu mkuu nawaalika Wakristo wa madhehebu yote katika nchi yetu kushiriki katika huduma hii.Nakuomba ukiombee na kukichangia Chama cha Biblia cha Tanzania ili kipate fedha kwa ajili ya kutafiti, kuchapisha na kusambaza neno la Mungu kwa watu wote. Ni maombi yangu kwamba asiwepo Mtanzania hata mmoja anayetamani kulisoma neno la Mungu akalikosa kwa sababu ya gharama kubwa.  Mwaka huu tuna lengo la kuwapatia watoto, vijana na wafungwa Biblia. Kwa ushirikiano wa kanisa la Mungu hapa nchini, tunaweza kuwafikia watoto, vijana na wafungwa ili kujenga Taifa la wacha Mungu. Kwa sadaka yako na matoleo yako ya upendo utakuwa baraka kwa kumpatia mtoto, kijana na mfungwa kule gerezani neno la uzima.
Nakutumia barua hii ya upendo kukualika na kukukaribisha ili ushiriki pamoja nasi kulijenga Taifa letu kiroho ili liwe  taifa lenye kumhofu na  kumcha Mungu. Ombea  Taifa letu ili watu wake walipende na kulisoma Neno la Mungu.
Ni kiu yangu kwamba kila mtoto, kijana na mfungwa awe na Biblia yake mkononi.
Neema na Amani ya Kristo iwe pamoja nawe.

Alfred E. Kimonge
Katibu Mkuu

HAMASA YA KUFUNGUA MATAWI MIKOANI

Tawi la UDOM

Hawa ni Wanachama wa Tawi la Kitivo cha Sayansi ya Jamii moja ya matawi matatu katika Chuo Kikuu cha Dodoma.

Tunamshukuru Mungu kwa kuanza mwaka huu kwa baraka zake na uamsho mpya wa Makanisa na Wakristo kujiunga kwa wingi kuwa wanachama wa Chama cha Biblia cha Tanzania. Hadi sasa tumefanikiwa kufungua matawi kama ifuatavyo;
1. Dodoma – Chuo Kikuu cha Dodoma [UDOM ] i. Tawi la  Kitivo cha Elimu – Wanachama 120
ii. Tawi la Kitivo cha Biashara na Utawala – Wanachama 78
iii. Tawi la Kitivo cha Sayansi ya Elimu ya Jamii – Wanachama 110
2. EAGT Buhemba Tarime – Wanachama 210
4. Umoja wa makanisa – Kilimanjaro
5. Marangu-Kilimanjaro
6. Umoja wa makanisa – jiji la Mwanza
Na bado hamasa inaendelea katika maeneo mengine likiwamo jiji la Dar es Salaam na Tabora.

1 min

Viongozi wa Makanisa ya Moshi ambao ni waanzilishi wa Tawi la Chama katika Mkoa wa Kilimanjaro

Mwenyekiti wa Tawi la Chama cha Biblia Tarime akikabithi Mchango wake Askofu Muhagachi Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania

Mwenyekiti wa Tawi la EAGT Buhemba Tarime akimkabidhi mchango wake Askofu Muhagachi Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania.

 

 

 

 

 

 

 

 

Tunakuomba ushiriki katika huduma hii kwa maombi yako,unaweza kuchangia kila mwezi Tsh 2000,______ Tsh 5000,______Tsh 10,000,_______au kuchangia kwa mwaka Tsh 25,000, ____Tsh  50,000,_____Tsh 100,000 au zaidi.  Kwa sadaka yako ya upendo unaweza kumfanya/kumgusa mtoto, kijana na mfungwa kumjua na kumfuata Kristo.
Nakualika kushiriki pamoja na Wakristo wengine waaminifu kwa kuchangia na kutuma mchango wako kwa akaunti ya M-PESA ya Chama cha Biblia cha Tanzania namba 890890 kisha tuma ujumbe wa kuchangia katika namba hizi: 0762998819,  0754383636 na 0754479789.

Pia unaweza kuchangia kupitia akaunti za Benki za DTB na NBC zilizoonyeshwa hapa chini.
Kwa DTB Akaunti Namba: 0901969001; SWIFT OR WIRING CODE DTKETZTZ
Kwa NBC Akaunti Namba: 029103000362

DTB

Akaunti Namba: 0901969001; SWIFT OR WIRING CODE DTKETZTZ

nbc

Akaunti Namba: 029103000362

 

 

 

 

 

 

Mungu na akubariki.
Askofu Amos Muhagachi
Mhariri.

 Mawasiliano yatumwe kwa: Katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, P.0. Box 175, Dodoma, Tanzania. Email: aekimonge@yahoo.com T: +255262324661 Mob: +255754383636
× How can I help you?