Na. Ndugu Frank Makalla (Msimamizi Mkuu wa Mradi-CBT).

Chama Cha Biblia Cha Tanzania kilianzisha kisomo cha elimu ya watu wazima kwa kushirikiana na Chama Cha Biblia Cha Finland na SIL (Summer Institute of linguistic) mnamo mwaka 2017 na mwaka huo ulikuwa ni mwaka wa kuandaa vitabu kwa ajili ya wanakisomo wa elimu ya watu wazima katika msemo wa Kikagulu na kanisa katika eneo hilo lilishiriki kikamilifu kwa kutoa watafsiri na waandishi. Ndipo mradi ukaanza 2018 ukiwa na walimu 20 (ishirini). Walimu hao walianza na wanafunzi mia ishirini ambavyo wanafunzi 97 walihitimu na kupewa vyeti mwezi machi 2019.

Na baada ya hapo Madarasa ya kujifunza kusoma na kuandika yalianza mwezi wa nane 2019 katika vijiji 20 (ishirini) vingine na kila kijiji kina darasa moja na kila darasa lina walimu wawili 2 (wawili) na jumla ya wanafunzi ni 423 kwa vijiji vyote.

Madarasa hayo ishirini yanaendelea vizuri katika kiwango cha 97% (asilimia tisini na saba) wanaweza kusoma na kuandika. Tunatarajia watahitimu mwisho wa mwezi huu wa February 2020 na mahafali yatakuwa mwezi wa tatu  kuanzia tarehe 14/03/2020 (kumi na nne), 21/03/2020 (ishirini na moja) na 28/03/2020  (ishirini na nane) kwa maana yamegawanywa kwenye vituo vitatu ambavyo ni Gairo, Nguyami na Magubike.

IMG 20200124 WA0011

Darasa la Chibweda kijiji cha Kibedya

Mwalimu Devotha Madihi wa darasa la Chibweda kijiji cha Kibedya akifundisha darasani. Darasa hili lina mama mmoja mwenye watoto mapacha wanaonekana hapo chini na amekuwa akihudhulia vizuri sana darasani.

IMG 20200124 WA0012

Darasa la Chibweda Kijiji cha Berega

Wanakisomo wa darasa la Kikagulu katika Kijiji cha Berega wanajifunza kusoma na kuandika kwa kutumia lugha ya Kikaguru wakifundishwa na waalimu wao Rose Chitemo mwenye kilemba na Sofia Muhumba.

IMG 20200124 WA0016

Darasa la Chibweda Kijiji cha Berega

Mwanafunzi Merina Malali wa Darasa la Chibweda Berega akiwa anaandika kufuatia maelekezo ya waalimu.

IMG 20200124 WA0023

Darasa la Chibweda Kijiji cha Kiegea

Darasa la Kiegea wanafatilia mafundisho ya mwalimu ubaoni.

IMG 20200124 WA0025

Darasa la Chibweda Kijiji cha Tabuhoteri

Darasa la kijiji cha Tabuhoteli lina wakina mama wenye umri mkubwa na wana bidii sana katika kujifunza kusoma na kuandika.

IMG 20200124 WA0027

Darasa la Chibweda Kijiji cha Ibindo

Wanakisomo katika kijiji cha Ibindo wakipata maelekezo kutoka kwa walimu wao kuhusu kusoma na kuandika.

IMG 20200124 WA0016

Kujifunza kuandika

Mwanafunzi Merina Malali wa Darasa la Chibweda (mwenye kilemba cha pink) katika kijiji cha Berega akiwa anaandika kufuatia maelekezo ya waalimu.

Wanakisomo awa, wapo katika marudio wakisubiri kupewa mitihani yao ya mwisho ili hatimaye kukabidhiwa vyeti kwa wale watakaofaulu na kuhitimu masomo yao vizuri.

CHANGAMOTO:

Kwa kuwa hawa ni watu wazima zipo changamoto mbali mbali zinazoathiri mahudhurio darasani kama vile:- kazi za shamba, misiba kijijini na nje ya kijiji, kuumwa, kuuguliwa, mito kujaa na kuwatenganisha kwa muda, kutomaliza silabasi yao kwa wakati kwa kuwa wapo wenye kujifunza kwa polepole kulingana na umri wao na kusababisha waalimu kuwa fuatilia na kuwaelekeza kwa muda zaidi.  n.k.

Changamoto katika kuwafikia

Wakati mwingine kuna changamoto ya kuwafikia wanakisomo kwa sababu ya ubovu wa miundombinu hasa barabara kama picha inavyoonesha hapa chini.

IMG 20200124 WA0022

Kunasua gari

Wakati mwingine kipindi cha mvua changamoto kubwa ni barabara, mfano picha hiyo hapo Gari lilikwama kwenye matope kutokana ubovu wa barabara wakati tunakwenda kuona darasa la Mtumbatu na tulisaidiwa na wanakijiji kulinasua gari kwenye matope (Ndugu Frank Makalla akieleza).

× How can I help you?