BARUA YA UPENDO YA KILA MWEZI YA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

BARUA YA UPENDO YA KILA MWEZI YA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

BLOGO TransparentCHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

N0: 01 July 2019, NEWSLETTERS /BARUA YA UPENDO YA KILA MWEZI

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area, P.O Box 175, Dodoma Tanzania. || T: +255 (026)-2324661 F: +255 (026)-2324058 || Email: info@biblesociety-tanzania.org || Site: www.biblesociety-tanzania.org

KWA WANACHAMA  WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA.

Umoja wetu katika Kristo! 

“Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.  Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.  (Yohana 17:21-23).

Umoja wa Kanisa ndiyo ishara ya mwili wa Kristo katika Ulimwengu. Kanisa ni familia ya Mungu katika ulimwengu huu, ni jumuiya ya watu wa Mungu wamwaminio Yesu Kristo katika maisha yao wakimsifu na kumshangilia Mungu katika ushuhuda na kuwaleta wengine ili wamjue Mungu wa kweli katika maisha yao. Chama cha Biblia cha Tanzania kimeendelea kwa uaminifu wote kulihudumia kanisa la nchi yetu kwa umoja wake kwa kuwapatia Maandiko Matakatifu [Biblia] ili kuliwezesha kanisa kuwa na Biblia katika mifumo na tafsiri mbali mbali kwa ajili ya uinjilisti na utume wake.
Kwa unyenyekevu mkuu nawaalika Wakristo wa madhehebu yote katika nchi yetu kushiriki katika huduma hii.Nakuomba ukiombee na kukichangia Chama cha Biblia cha Tanzania ili kipate fedha kwa ajili ya kutafiti, kuchapisha na kusambaza neno la Mungu kwa watu wote. Ni maombi yangu kwamba asiwepo Mtanzania hata mmoja anayetamani kulisoma neno la Mungu akalikosa kwa sababu ya gharama kubwa.  Mwaka huu tuna lengo la kuwapatia watoto, vijana na wafungwa Biblia. Kwa ushirikiano wa kanisa la Mungu hapa nchini, tunaweza kuwafikia watoto, vijana na wafungwa ili kujenga Taifa la wacha Mungu. Kwa sadaka yako na matoleo yako ya upendo utakuwa baraka kwa kumpatia mtoto, kijana na mfungwa kule gerezani neno la uzima.
Nakutumia barua hii ya upendo kukualika na kukukaribisha ili ushiriki pamoja nasi kulijenga Taifa letu kiroho ili liwe  taifa lenye kumhofu na  kumcha Mungu. Ombea  Taifa letu ili watu wake walipende na kulisoma Neno la Mungu.
Ni kiu yangu kwamba kila mtoto, kijana na mfungwa awe na Biblia yake mkononi.
Neema na Amani ya Kristo iwe pamoja nawe.

Alfred E. Kimonge
Katibu Mkuu

HAMASA YA KUFUNGUA MATAWI MIKOANI

Tawi la UDOM

Hawa ni Wanachama wa Tawi la Kitivo cha Sayansi ya Jamii moja ya matawi matatu katika Chuo Kikuu cha Dodoma.

Tunamshukuru Mungu kwa kuanza mwaka huu kwa baraka zake na uamsho mpya wa Makanisa na Wakristo kujiunga kwa wingi kuwa wanachama wa Chama cha Biblia cha Tanzania. Hadi sasa tumefanikiwa kufungua matawi kama ifuatavyo;
1. Dodoma – Chuo Kikuu cha Dodoma [UDOM ] i. Tawi la  Kitivo cha Elimu – Wanachama 120
ii. Tawi la Kitivo cha Biashara na Utawala – Wanachama 78
iii. Tawi la Kitivo cha Sayansi ya Elimu ya Jamii – Wanachama 110
2. EAGT Buhemba Tarime – Wanachama 210
4. Umoja wa makanisa – Kilimanjaro
5. Marangu-Kilimanjaro
6. Umoja wa makanisa – jiji la Mwanza
Na bado hamasa inaendelea katika maeneo mengine likiwamo jiji la Dar es Salaam na Tabora.

1 min

Viongozi wa Makanisa ya Moshi ambao ni waanzilishi wa Tawi la Chama katika Mkoa wa Kilimanjaro

Mwenyekiti wa Tawi la Chama cha Biblia Tarime akikabithi Mchango wake Askofu Muhagachi Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania

Mwenyekiti wa Tawi la EAGT Buhemba Tarime akimkabidhi mchango wake Askofu Muhagachi Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania.

 

 

 

 

 

 

 

 

Tunakuomba ushiriki katika huduma hii kwa maombi yako,unaweza kuchangia kila mwezi Tsh 2000,______ Tsh 5000,______Tsh 10,000,_______au kuchangia kwa mwaka Tsh 25,000, ____Tsh  50,000,_____Tsh 100,000 au zaidi.  Kwa sadaka yako ya upendo unaweza kumfanya/kumgusa mtoto, kijana na mfungwa kumjua na kumfuata Kristo.
Nakualika kushiriki pamoja na Wakristo wengine waaminifu kwa kuchangia na kutuma mchango wako kwa akaunti ya M-PESA ya Chama cha Biblia cha Tanzania namba 890890 kisha tuma ujumbe wa kuchangia katika namba hizi: 0762998819,  0754383636 na 0754479789.

Pia unaweza kuchangia kupitia akaunti za Benki za DTB na NBC zilizoonyeshwa hapa chini.
Kwa DTB Akaunti Namba: 0901969001; SWIFT OR WIRING CODE DTKETZTZ
Kwa NBC Akaunti Namba: 029103000362

DTB

Akaunti Namba: 0901969001; SWIFT OR WIRING CODE DTKETZTZ

nbc

Akaunti Namba: 029103000362

 

 

 

 

 

 

Mungu na akubariki.
Askofu Amos Muhagachi
Mhariri.

 Mawasiliano yatumwe kwa: Katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, P.0. Box 175, Dodoma, Tanzania. Email: aekimonge@yahoo.com T: +255262324661 Mob: +255754383636
Wafungwa na Mahabusu wa Gereza la Kiomboi wapata Biblia.

Wafungwa na Mahabusu wa Gereza la Kiomboi wapata Biblia.

Na: Canon Mwanamtwa:

Hawa ni Askari wa Gereza la Kiomboi wakipokea Biblia kwa niaba ya Wafungwa na Mahabusu wa Gereza la Kiomboi

Askari wa Gereza la Kiomboi wakipokea Biblia kwa niaba ya Wafungwa na Mahabusu wa Gereza la Kiomboi , Mkoa wa Singida wilaya ya Iramba.

Hawa ni Askari wa Gereza la Kiomboi wakipokea Biblia kwa niaba ya Wafungwa na Mahabusu wa Gereza la Kiomboi lililopa katika Mkoa wa Singida wilaya ya Iramba. Baada ya kupokea nilipata nafasi ya kuongea na Wafungwa na Mahabusu pamoja na Askari kutoa maelezo juu ya Chama Cha Biblia Tanzania kutoa Biblia hizo kwao, Wafungwa wawili walishukuru kwa niaba ya wenzao na kusema

” Tunamshukuru kwa Chama Cha Biblia kutukumbuka na kututhamini kwa kutuletea Biblia hizi na kwamba tutasoma Neno la Mungu na litatusaidia katika maisha yetu hata katika mazingira haya, asante sana”

MKUTANO WA VIONGOZI WA MAKANISA YA KANDA YA KASKAZINI NA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA ULIOFANYIKA WILAYANI MOSHI MKOANI KILIMANJARO. (TAREHE 04/06/2019).

MKUTANO WA VIONGOZI WA MAKANISA YA KANDA YA KASKAZINI NA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA ULIOFANYIKA WILAYANI MOSHI MKOANI KILIMANJARO. (TAREHE 04/06/2019).

Na: Felix Rwebandiza Jones.
Kitengo cha Tehama.

Mwenyekiti wa Kikao ambaye pia ni Baba Askofu Msaidizi wa Kanisa la Kirutheri la Kiinjiri Jimbo la Moshi

Mwenyekiti wa Kikao ambaye pia ni Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Jimbo la Moshi, akifungua kikao

Wajumbe.
Waliohudhuria walikuwa 36 kama inavyooneshwa hapa chini.
1. Wakurugenzi Chama cha Biblia cha Tanzania (Rev. Askofu Amosi Muhagachi ambaye ni Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania na Eng. Ekael Manase ambaye ni mjumbe wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania).
2. Maafisa wa Chama cha Biblia cha Tanzania (Rev. Ipyana Mwangota amabaye ni Meneja Tafrisi na Felix Jones ambaye ni Mkuu wa kitengo cha TEHAMA).
3. Wachungaji na Mapadre.
4. Mwangalizi wa Jimbo Katoliki la Moshi.
5. Wenyeviti wasaidizi wa Maaskofu.
Agenda kuu ya Kikao ilikuwa ni:
• Uhamasishaji wa Chama cha Biblia cha Tanzania,
• Uanachama na faida zake na
• Tafsiri ya Biblia kwa ujumla wake.
Baada ya ufunguzi wa kikao mwenyekiti aliruhusu watumishi kijitambulisha
Mmoja wa wajumbe akijiambulisha

Mmoja wa wajumbe akijitambulisha wakati wa Mkutano huo

na baada ya hapo alimkaribisha Rev. Askofu Amosi Muhagachi kueleza ujumbe wake kutoka Chama cha Biblia Cha Tanzania. Askofu Muhagachi alianza kwa kuelezea historia yake, kabla ya kuanza kufanya kazi na Chama cha Biblia cha Tanzania, ambapo akiwa mwanafunzi na mwanachama aliweza kuwa muhamasishaji katika shule ya Sekondary ya Mirambo Tabora na aliweza kuwahamasisha wanafunzi wenzake wachangie Chama cha Biblia cha Tanzania ili kipate fedha za kuchapisha Biblia nyingi ili wanafunzi wenzao wapate Neno la Mungu kama wao. Alifanya hivyo katika kipindi chote cha masomo yake “nilikuwa nikihamasisha wanafunzi wenzangu tuchangie Chama cha Biblia cha Tanzania, ili Chama cha Biblia cha Tanzania kiweze kuchapisha Biblia nyingi ili sisi na vijana wenzetu tupate Biblia” alisema Rev. Askofu Amosi Muhagachi.
Rev. Askofu Muhagachi akizungumza wakati wa Kikao

Rev. Askofu Muhagachi akizungumza wakati wa Kikao

Baba Askofu Amosi Muhagachi baada kuhitimu masomo yake alipata barua ya kuitwa kwenye usaili na baada ya hapo aliweza kuajiriwa kuwa Afisa Uhusiano na Makanisa na Uhamasishaji wa Chama cha Biblia cha Tanzania ambapo alikaa kwa miaka saba kabla ya kuwa Askofu wa kanisa la Mennonite Tanzania na baadaye kwenda masomoni nchini Marekani, ambako bado anaendelea na masomo yake.
Baba Askofu Amosi Muhagachi alieleza mikakati ya Chama cha Biblia cha Tanzania ambayo ni;
i. Kuyaomba makanisa kutenga juma moja kuombea Chama cha Biblia cha Tanzania na watendaji wake.
ii. Kuomba watu kujitolea kuchangia Chama cha Biblia cha Tanzania ili kipate pesa za kutosha za kutafiti, kuchapisha na kusambaza Neno la Mungu kwa lugha mbali mbali hapa Tanzania.
iii. Kuomba viongozi wa makanisa wakubali kuchangia mpango mkakati wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa kupeleka Neno la Mungu kwa wafungwa, vijana na watoto.
iv. Kuwaomba viongozi wa Makanisa kuendesha mpango wa kuwepo mashindano ya kukariri mistari ya Biblia kwa vijana na watoto katika Shule, Makanisa na Vyuoni.
v. Kuhamasisha utumiaji wa Biblia (Hard copy) makanisani na viongozi wahakikishe zimeandikwa au zina nembo ya Chama cha Biblia cha Tanzania kama njia ya kuepukana na watu wanaogushi/kuchakachua Neno la Mungu.
Baada ya kumaliza hotuba yake alimuomba Mwenyekiti wa kikao amkaribishe Eng. Ekael Manase alielezea juu ya Uanachama, wa Chama cha Biblia cha Tanzania.
Eng. Ekael Manase alianza kwa kumshukuru sana Baba Askofu Amosi Muhagachi kwa jinsi alivyoeleza vizuri kuhusu kuwahamasisha watu kukichangia Chama cha Biblia cha Tanzania.
Pia aliendelea kwa kuwaomba sana na kuwasihi watumishi wa Mungu wote waliohudhulia kuwa wanatakiwa kuwahimiza waumini wao na kufufua ari ya kusoma Neno la Mungu ikiwa ni pamoja na kuanzisha mashindano ya kusoma na kukariri mistari ya Biblia kwa vijana na watoto, kwa lengo la kuwaandaa ili waweze kukua wakilishika Neno la Mungu. Lakini pia aliwaomba sana wachungaji na mapadre kuwahimiza sana waumini wao kutumia Biblia (hard copy) na kuacha kutumia Biblia zilizowekwa kwenye simu za mikononi (soft copy). Kwani wanaweza wakasoma Neno lililopotoshwa na watu wenye nia ovu kwa Ukristo.
Eng. Ekael Manase aliendelea kueleza kuwa hayo yote hayawezi kufanikiwa kama vijana wetu na watoto wetu hawatakuwa na Biblia zao; kwa hivyo basi ili jambo hili liweze kufanikiwa tunahitaji tuwe na Biblia za kutosha na kwa bei wanayoimudu. Biblia za bei nafuu zinaweza kupatikana tu; endapo kama sisi sote tutajitoa kukichangia Chama cha Biblia cha Tanzania. “Maana kama Biblia zingeuzwa kwa bei yake halisi ingekuwa ghali sana, lakini michango inayotolewa kwa CBT inafanya Biblia iweze kuuzwa kwa bei rahisi” alisema Eng. Ekael Manase.
Pamoja na melezo mazuri ya kuwahamisha watumishi wa Mungu kuhusu kuchangia Biblia na kuwa himiza watoto na vijana kusoma Biblia, pia Eng. Ekael Manase aliwaeleza wajumbe waliohudhuria aina za uanachama; kuwa kuna uanachama wa aina tatu;
i. Uanachama wa maisha
• Uanachama wa Maisha Mme na Mke shilingi 15,000= na ahadi isiyopungua shilingi 15,000=kwa mwaka.
• Uanachama wa Maisha mtu mmoja shilingi 10,000= na ahadi isiyopungua shilingi 10,000= kwa mwaka.
ii. Uanachama wa Bidii
• Uanachama wa kawaida (bidii ) shilingi 5,000=kwa mwaka.
• Uanachama wa kawaida kwa Wanafunzi wa Sekondari na Vyuo shilingi 2,000= au zaidi kwa mwaka.
• Uanachama wa kawaida wa kushirikishwa kwa watoto na wanafunzi wa shule za Msingi shilingi 1,000= au zaidi kwa mwaka.
• Mwanachama wa Biblia Moja kwa Mwezi (Bible a Month Club) 5,000=, 10,000=, 15,000=, 20,000= au zaidi kwa mwezi.
iii. Uanachama wa Mashirika
• Uanachama wa Mashirika shilingi 50,000= na mchango usiopungua shilingi 50,000= kwa mwaka.
Mwisho Eng. Ekael Manase alimalizia kwa kusema kuwa hii itakuwa ni njia nzuri Zaidi ya kuwakusanya vijana na kupenda kusoma Neno la Mungu, na pia itasaidia sana kupanda mbegu ya Neno la Mungu ndani yao na kuwa na Taifa lenye kumcha Mungu na lenye maadili mema.
Kwa upande wake Meneja wa Tafsiri wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Mch. Ipyana Mwangota alipopewa nafasi ya kuzungumza mbele ya wajumbe wote; alielezea kazi za Tafsiri anazozifanya ndani ya Chama cha Biblia cha Tanzania akiwa kama Meneja wa Tafsiri. Alifafanua kuwa wanafanya kazi ya kutafsiri Biblia kwa lugha mbali mbali ikiwa njia mojawapo ya kulisaida Kanisa kufanya kazi ya umisheni.
Mch. Ipyana Mwangota akitoa ukizungumzia juu ya Tafsiri

Meneja tafsiri, Mch. Ipyana Mwangota akitoa ukizungumzia juu ya Tafsiri

Alifafanua Zaidi juu ya kazi ya Tafsiri na kutaja Tafsiri zinazofanyika upande wa kanda ya Kasikazini ambazo ni Tafsiri ya Kivunjo, Kidatooga, Kimashame na Kimochi. Alinukuriwa akisema Pia Chama cha Biblia cha Tanzania kinakamilisha uchapaji wa Biblia ya Kisukuma. Kazi hii imepelekwa kule Korea kwa ajili ya uchapishaji. Ni tarajio letu kuwa kazi ya uchapishaji na uzinduzi itakamilika mwishoni mwa mwaka huu 2019. “Chama cha Biblia cha Tanzania kimepokea maombi ya Tafsiri na sasa kinaendelea kufanya pia Tafsiri ya lugha mbalimbali kubwa kama Igikuria, Kiha, Kinyiramba, Kirimi, Chikaguru na kihehe. Aidha CBT tumepokea maombi ya Kanisa katika maeneo ya Ufipa, Unyamwezi, Unyiha, na Upare ili kiweze kusaidia kutafsiri Biblia kwa Lugha ya Kifipa, Kinyamwezi, Kinyiha na Kipare na kukubali; na sas Chama cha Biblia cha Tanzania kipo katika mchakato wa kutafuta fedha ili kuianza kazi hii kwa ushirikiano na Makanisa mwaka 2020 Januari.
Baadhi ya Wajumbe wakisikiliza kwa Makini

Baadhi ya Wajumbe wakisikiliza kwa Makini.

Pia alieleza kuwa zipo Biblia ambazo zimetafsiriwa, kuchapishwa na zinatumika katika makabila lengwa kama vile Biblia ya Kinyakyusa (Mkoa wa Mbeya), Biblia ya Luhaya (Mkoa wa Kagera), Biblia ya Cigogo (Mkoa wa Dodoma), Biblia ya Kimasai (Mkoa wa Arusha), na Biblia ya Kihiraqw (Mkoa wa Manyara).
Pia alieleza kuwa Chama cha Biblia kimefanya tafsiri za Agano Jipya na sehemu za Biblia nyingi tu na zinatumika maeneo tofauti tofauti ili kukidhi haja ya watumiaji wa lugha husika kuendana na sera ya Vyama vya Biblia Duniani.
Kuhusu mchakato wa kazi ya tafsiri; Meneja Tafsiri alieleza kuwa ofisi yake, hutumia vifaa vya kisasa. Kwa lengo la kufanikisha kazi hii kubwa. Alionyesha Program ya Paratext kwa wajumbe wa mkutano kama mfano wa vifaa hivyo ili waone jinsi kazi hii inavyotendeka. Wajumbe walipongeza kazi hii kubwa na waliahidi kuiombea.
Pia alieleza kuwa Chama kwa sasa kinatia mkazo uwepo wa Biblia za Watoto, na hivyo kimekuwa kikiandaa Biblia za watoto ili kuhakikisha Makanisa hayakosi Biblia kwa watoto wadogo, wa kati na wale wanaoelekea umri wa utu uzima.
Mwisho alitoa wito kwa viongozi wa Makanisa kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na Chama cha Biblia cha Tanzania katika kuhakikisha Maandiko Matakatifu yanapatikana kikamilifu kwa kuchangia na kuombea juhudi hizi.

Kifahamu Chama Cha Biblia cha Tanzania (CBT).

Kifahamu Chama Cha Biblia cha Tanzania (CBT).

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

Mzee Daudi reading

KUWEZESHA UPATIKANAJI WA MAANDIKO MATAKATIFU KATIKA LUGHA INAYOELEWEKA VIZURI NA KWA BEI WANAYOIMUDU

1.Chama cha Biblia cha Tanzania ni nini?IMG 20181026 163614

Chama cha Biblia cha Tanzania ni Shirika la Kikristo lisilo la Kidhehebu lililoandikishwa mwaka 1965  chini ya Sheria ya Udhamini wa Vyama.

Chama cha Biblia cha Tanzania ni Mshiriki wa Muungano wa Vyama vya Biblia ulimwenguni ( United Bible Societies –UBS ) ambao kazi yake kubwa ni uenezaji wa Neno la Mungu kwa wingi na uhakika kama ifuatavyo:

–       Kueneza Neno la Mungu katika Lugha na Mawasiliano yanayokidhi mahitaji ya watu wengi Ulimwenguni.

–       Kueneza Neno la Mungu katika Tafsiri sahihi bila kupoteza uhalisi wa Maandiko Matakatifu.

–       Kuyauza Maandiko kwa bei wanayoimudi ili waweze kulifahamu Neno la Mungu.

  1. Kaziya Chama cha Biblia  ilianza lini Tanzania?

 20160917 160152( i ) Wamisionari wa kwanza kabisa nchini Tanganyika ndio walioanzisha kazi ya Chama kwenye karne ya 19.

 ( ii ) Kazi ya  kueneza  Biblia  iliendelea kukua na mwaka 1982 Chama kilifikia ngazi ya kuwa Mshiriki wa Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni na mwaka 1988 Chama kilipata uanachama kamili wa Muunganohuu.

3.Je kazi za Chama cha Biblia cha Tanzania ni zipi?

Chama cha Biblia cha Tanzania ni chombo cha Kanisa kinachotumika katika kutekeleza utume wa Kanisa  wa kuihubiri Injili kwa kila mtu.  Chama cha Biblia kinafanya yafuatayo:

a ) Kutafsiri Biblia katika Lugha mbalimbali za kienyeji.

Watafsiri wa Kikagulu b ) Kuchapisha katika Mitindo mbalimbali:

      – Biblia nzima.

      – Maagano na

      – Sehemu zake kwa wasomaji wapya.

 c )Kueneza Biblia,Maagano na sehemu zake kwa watu wote kwa kushirikiana na :

      – Makanisa na Mashirika yake.

      – Maduka ya Vitabu.

      – Watu binafsi pamoja na wakereketwa wa kujitolea.

 d )Kushirikiana na Vyama vingine katika kuhakikisha Biblia inasomwa kwa lugha zote za hapa Tanzania ili kila mtu auonje uzuri wa Yesu Kristo na kupata maisha mapya.

  1. Je, hadi sasa Chama cha Biblia cha Tanzania kimetafsiri Biblia katika Lugha zipi za kienyeji ?

medium 1 Chama hadi sasa kimemudu kutafsiri Biblia nzima katika Lugha  za:  Kiiraqw, Kihaya, Kinyakyusa, Kisukuma, Kijaluo, Kimasai na Kigogo. Pia kimeweza kutafsiri Agano Jipya katika Lugha za Kibena, Kimashami, Kivunjo, Kimochi, Kichasu( Kipare ), Kijita, Kidatooga, Igikuria, Kishambala, Kizaramo, Kinyiramba na Kirimi ( Kinyaturu )     Miradi ya Tafsiri inayoendelea ni ya Lugha za Kihehe, Kikaguru, Kiha na Kisukuma cha kisasa. Mbali na kuchapisha  Biblia, pia Chama kinachapisha matoleo yafuatayo:

–       Sehemu za Biblia.

–       Sehemu za Biblia kwa wasomaji wapya wanaojifunza Biblia kwa Kiingereza, Kiswahili na Lugha za Kienyeji.

–       Vipeperushi maalum vya vifungu vya Biblia kwa matukio mbalimbali k.m kuzaliwa kwa Yesu,kifo cha Yesu,wagonjwa waliolazwa,na matukio mbalimbali k.m Uhuru, Rushwa nk.

–       Kanda naswa za Neno la Mungu.

–       Neno la Mungu katika Braille kwa wasomaji wasioona.

–       Neno la Mungu kwa maandishi makubwa kwa wenye udhaifu wa macho.

    Kwa kawaida tafsiri inafanywa  kutoka katika Lugha za asili za Kiyunani na Kiebrania,na hivyo kazi ya Tafsiri ni ngumu, inahitaji uangalifu wa hali ya juu na

    inachukua miaka kati ya  8 hadi 10  kutoa toleo moja, kama kuna watafsiri walioajiriwa kwenye mradi kwa wakati wote na kuna wachambuzi 10-15.

  1. Je Chama cha Biblia kinapata  wapi fedha za kukiendesha?

    Chama cha Biblia cha Tanzania kinaendeshwa kwa michango ya

–       Makanisa.

–       Taasisi mbalimbali za Makanisa.

–       Watu binafsi ambao ni wanachama.

–       Marafiki wa Chama.

–       Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni ambao unatoa misaada ya Maandiko Matakatifu kutoka nje ambayo Chama kinayauza na kutumia sehemu ya mapato kuendesha huduma.

  1. Je Chama cha Biblia cha Tanzania kina mahitaji gani?

    Ili kutekeleza kazi zake za Kutafsiri, Kuchapisha na Kueneza Maandiko Matakatifu Chama cha Biblia chaTanzania kinahitaji kiasi kisichopungua  Dola Milioni moja za Marekani kwa mwaka.  Kama Kanisa na Wakristo binafsi watakuwa wanachangia kila mwaka  kwa uaminifu Chama kinaweza kuendesha kazi zake vizuri.

  1. Je, unawezaje kusaidia kazi za Chama cha Biblia ?

  DSC 6345 1  Kuna njia nyingi za kukisaidia Chama cha Biblia katika kazi zake na kinamualika kila Mkristo kushiriki yafuatayo:-

  ( i )Kujiunga na kuwa Mwanachama na kuchangia

      – Uanachama wa Maisha Mme na Mke shilingi 15,000= na ahadi isiyopungua shilingi 15,000=kwa mwaka.

      – Uanachama wa Maisha mtu mmoja shilingi 10,000= na ahadi isiyopungua shilingi 10,000= kwa mwaka.

      – Uanachama wa kawaida (bidii ) shilingi 5,000=kwa mwaka.

      – Uanachama wa kawaida kwa Wanafunzi wa Sekondari na Vyuo shilingi 2,000= au zaidi kwa mwaka.

      – Uanachama wa kawaida wa kushirikishwa kwa watoto na wanafunzi wa shule za Msingi shilingi 1,000= au zaidi kwa mwaka.

      – Uanachama wa Mashirika shilingi 50,000= na mchango usiopungua shilingi 50,000= kwa mwaka.

      – Mwanachama wa Biblia Moja kwa Mwezi ( Bible a Month Club) 5,000=, 10,000=, 15,000=, 20,000= au zaidi kwa mwezi.

 (ii )Tafsiri.

      Unaweza kusaidia Chama kwa :

–  Kuchangia Miradi ya Tafsiri kwa kutoa fedha taslimu.

–  Kuchangia Miradi ya Tafsiri kwa kuwapata Watafsiri wenye uwezo na Wachambuzi wenye mzigo na kazi hii.

– Kuchangia Miradi ya Tafsiri kwa kupitia Miswada ya Tafsiri.

(iii ) Uhamasishaji.

      -Kutoa sadaka au michango kila mara kwa Chama.

      – Kuhamasisha Makanisani juu ya Wiki ya Biblia ambayo ni kila wiki ya kwanza ya  Mwezi Novemba kila mwaka.

      – Kuanzisha Vikundi vya Biblia Moja kwa Mwezi ( Bible a Month Club-BAMC ) kwenye Makanisa na maeneo ya kazi.

      – Kusaidia kueneza Biblia kwa njia ya kuuza kwa kujitolea.

      – Kutoa njia mbadala au mawazo ya jinsi ya kutunisha Mfuko wa Chama ukishrikiana na Chama au kwa niaba ya Chama.

(iv ) Maombi.

     Ungana nasi katika kukiombea Chama.

( v ) Kujitolea.

     Unaweza kukisaidia Chama kwa kutoa muda wako na ujuzi wako wakati wowote kukisaidia Chama katika azma ya Kutafsiri, Kuchapisha, Kueneza na  katika kuhamasisha watu kutoa  kumfidia msomsji apate Biblia kwa bei nafuu.

  1. Kwanini Chama cha Biblia cha Tanzania kinatoa Maandiko Matakatifu bure kwa baadhi ya watu au vikundi ?

  18 2 Chama kinatoa Maandiko Matakatifu bure kwa baadhi ya watu wasio na uwezo wa kifedha kumudu kujinunulia,na vile vile ili kukidhi uhitaji wa Maandiko kwa

   Watanzania  walio wengi kinalazimika kuyauza kwa bei nafuu wanayoimudu ambayo iko chini ya ilyopangwa kuuzia.

  1. Wito wa Chama kwa Wakristo

    Chama kinatoa wito kwa Wakristo wote mmoja mmoja na Makanisa yote kujiunga na kuwa mwanachama wa Chama cha Biblia na kuchangia Chama

    fedha ,mawazo  nguvukazi na maombi ili kukiwezesha  kuendesha kazi zake za Kutafsiri,Kuchapisha na Kueneza Maandiko Matakatifu kwa watu wote

   Tanzania.

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

ZIARA KATIKA MAGEREZA YA MSALATO NA KONGWA DODOMA

Moja kati ya wajibu muhimu kwa Chama cha Biblia cha Tanzania ni kuhakikisha kuwa watu wote wanapata fursa ya kupata maandiko matakatifu. Kutokana na jukukumu hilo tarehe 27/11/2018 watumishi wa Idara ya Mahusiano na baadhi ya Wale wa Mawasiliano, walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Msalato Dodoma na kugawa Biblia, Sabuni na dawa ya meno kwa Wafungwa wa gereza hilo la Msalato. Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji akishirikiana na Msaidizi wake na Maafande wengine walitupokea vizuri sana na kutupa ushirikiano wa hali ya juu.

15

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji

18 2

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, viongozi wa kanisa la KKKT Dodoma na viongozi wa gereza la Msalato

Jukumu la kugawa Biblia halikuishia Gereza la Msalato tu kwani Tarehe 28/11/2018 Meneja Mahusiano na kikosi kazi chake walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Kongwa Dodoma. Katika Gereza hili tulipokelewa vizuri sana na kupewa maelezo ya jinsi Wafungwa wanavyohitaji msaada wa Maandiko na vifaa vingne kwani wanatakiwa kjujitegemea.Chama cha Biblia tulifaulu kugawa Maandiko Matakatifu,sabuni, dawa ya Meno na Taulo za akina Mama.Mkuu wa Gereza Afande Nyonyi alishuru sana Chama cha Biblia cha Tanzania kwa msaada huo kwa Wafungwa.

8

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Kongwa Afande Nyonyi

1

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, mkuu wa jimbo wa kanisa la KKKT Kongwa (wa kwanza kulia) na viongozi wa gereza la Kongwa