by The Bible Society of Tanzania | Dec 5, 2021 | News
The Bible Society of Tanzania celebrates the launch of the full Braille Bible.
It is in the city of Kongwa, located in Dodoma Region of the capital city of Tanzania that the majority of the visual impaired live. One of the characteristics of this translation is that it is the result of close collaboration between Churches of different confessions
by The Bible Society of Tanzania | Oct 14, 2021 | Translation News

We publish scriptures in various formats including print, audio, visual and braille in order to meet the needs of all kinds of people. Since the scriptures are mostly used on a daily basis, we make sure the quality is top. This therefore dictates where production is done. Most of our production is done abroad and this comes at a high cost.
by The Bible Society of Tanzania | Oct 14, 2021 | Fundraisers, News
CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI
ZIARA KATIKA MAGEREZA YA MSALATO NA KONGWA DODOMA
Moja kati ya wajibu muhimu kwa Chama cha Biblia cha Tanzania ni kuhakikisha kuwa watu wote wanapata fursa ya kupata maandiko matakatifu. Kutokana na jukukumu hilo tarehe 27/11/2018 watumishi wa Idara ya Mahusiano na baadhi ya Wale wa Mawasiliano, walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Msalato Dodoma na kugawa Biblia, Sabuni na dawa ya meno kwa Wafungwa wa gereza hilo la Msalato. Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji akishirikiana na Msaidizi wake na Maafande wengine walitupokea vizuri sana na kutupa ushirikiano wa hali ya juu.
Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji
Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, viongozi wa kanisa la KKKT Dodoma na viongozi wa gereza la Msalato
Jukumu la kugawa Biblia halikuishia Gereza la Msalato tu kwani Tarehe 28/11/2018 Meneja Mahusiano na kikosi kazi chake walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Kongwa Dodoma. Katika Gereza hili tulipokelewa vizuri sana na kupewa maelezo ya jinsi Wafungwa wanavyohitaji msaada wa Maandiko na vifaa vingne kwani wanatakiwa kjujitegemea.Chama cha Biblia tulifaulu kugawa Maandiko Matakatifu,sabuni, dawa ya Meno na Taulo za akina Mama.Mkuu wa Gereza Afande Nyonyi alishuru sana Chama cha Biblia cha Tanzania kwa msaada huo kwa Wafungwa.
Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Kongwa Afande Nyonyi
Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, mkuu wa jimbo wa kanisa la KKKT Kongwa (wa kwanza kulia) na viongozi wa gereza la Kongwa
by The Bible Society of Tanzania | Jul 21, 2021 | News, Uzinduzi
Hatimaye Biblia ya Kisukuma yazinduliwa kwa kishindo mkoani Mwanza.
Na Felix Jones
Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma umefanyika katika Kanisa Kuu AIC Makongoro Mwanza na kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Umoja wa Makanisa mkoa wa Mwanza.
Akizungumza katika hafla hiyo Mch. Ipyana Mwangota kwa niaba ya mtafsiri mkuu wa Umoja wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (UBS), kuwa mchakato wa kutafsiri Biblia kwa lugha ya Kisukuma ulianza miaka thelathini iliyopita. “Tulifanikiwa kutafsiri sehemu ya Biblia kwa lugha kisukuma na kuzinduliwa mwaka 1895 na Mchakato ukaendelea tukapata Agano Jipya mwaka 1925 na baadae kufanyiwa marekebisho na atimaye kuzinduliwa mwaka 2001 na leo tunayofuraha kuzindua au kuweka wakfu Biblia kamili kwa lugha hii ya kisukuma mwaka huu 2021.”

Meneja Tafsri akizungumza kwa niaba ya Mtafsiri Mkuu wa Umoja wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (UBS) wakati wa hafla hiyo.
Pamoja na changamoto tulizokabiliwa nazo katika kutafsiri, kuichapisha mpaka leo inazinduliwa, tunakila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kusikia maombi yetu na haja yetu ya moyoni.
Kwa sasa jamii hii ina nafasi ya kumsikiliza Mungu akisema nao kwa lugha yao wenyewe na hivyo historia imejiandika kwa sababu watoto na wajukuu wataitumia Biblia hii kwa miaka mingi na kuienzi lugha yao. Pia ni jambo zuri katika kuihifadhi lugha ya Kisukuma kwa sababu wengi tunafahamu fasihi andishi inahifadhiwa kwa muda mrefu zaidi.
Mara baada ya hotuba hiyo fupi, Mch. Mwangota ndipo alipopata fursa ya kumkabithi Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Kimonge Biblia hiyo ya Kisukuma ili naye aikabidhi kwa Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande ili iweke wakfu tiyari kwa kutumika katika Kanisa la Mungu.

Mwakilishi wa Translation Consultant (TC) Canon Ipyana Mwangota akimkabidhi Biblia ya Kisukuma Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge wakati wa Uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza
Kwa upande wa Katibu Mkuu Dkt. Alfred Kimonge aliomba Biblia hii itumike katika Ibada ili kazi hii iliyofanyika kwa miaka mingi na kwa gharama kubwa isiwe ya bure. Na zaidi aliongeza kuwa kwa niaba ya Chama cha Biblia cha Tanzania ni matumaini yetu kuwa injili ya Wokovu katika Yesu Kristo itawafikia wasukuma katika lugha yao ya moyoni na kusema sasa tumemtambua Mungu anasema na sisi kwa lugha yetu.
Hivyo Wasukuma nao watamsikia Bwana Yesu kwa ukaribu wa moyoni ili wapate fursa ya kushiriki katika halaiki ya mwisho, kama Biblia isemavyo:-
“Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha (Wasukuma)…” (Ufu. 7: 9 – 12).
“Hivyo Ninayoheshima ya kukuomba Baba Askofu Mkuu kuwa uipokee Biblia hii na kuiweka wakfu” alisema Katibu Mkuu wakati wa kukabithi Biblia hiyo ili iwekwe wakfu.

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge akisoma hotuba mbele ya Askofu Mkuu Renatus Nkwande kabla ya kumkabidhi wakati wa Uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza.
Naye Dkt. Alfred Kimonge alipo maliza kusoma hotuba yake ndipo alipopata fursa ya kumkabithi Askofu Mkuu Renatus Nkwande Biblia hiyo ya Kisukuma ili aiweke wakfu tiyari kwa kutumika katika Kanisa la Mungu.

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia ya Kisukuma kwa Askofu Mkuu Renatus Nkwande wakati wa uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza.
Askofu Mkuu Renatus Nkwande aliipokea kwa furaha kisha akaendelea na taratibu za kuiweka wakfu Biblia hiyo ya Kisukuma.

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akisoma sala ya kuzindua hiyo Biblia ya Kisukuma wakati wa sherehe hizo za uzinduzi wa hiyo Biblia ya Kisukuma.

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akisaini Biblia ya Kisukuma kuwashilia kupokelewa na Kanisa.
Na hapa ni baadhi ya viongozi na waumini walio weza kuhudhulia katika hafla ya Uzinduzi huo.
Baada ya uzinduzi huo wa Biblia hiyo Baba Askofu na Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania aliyewakilisha Bodi ya wakurugenzi ya Chama cha Biblia cha Tanzania alipata fursa ya kuhutubia wasukuma waliofika katika uzinduzi huo na pia kutoa salamu kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Chama cha Biblia cha Tanzania na kueleza dhima ya Chama katika mkutadha wa kuakikisha kila Mtu hapa nchini anakuwa na Biblia yake na kwa lugha anayeielewa asa kuwa na Biblia ya moyoni.

Baba Askofu Amos Muhagachi ambaye ni Mwenyekiti msaidizi wa Bodi ya wakurugenzi na Balozi wa Chama cha Biblia akihutubia Kanisa kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi.
Kwa upande wa Mgeni rasmi Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande alikipongeza Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kazi nzuri sana ya kuakikisha kila mtu ana Biblia yake na lugha yake na kwa bei mtu anayoweza kuimudu huku akisisitiza Kanisa la Mungu katika kabila la Kisukuma kuhakikisha wanaweka ratiba ya kuwezesha Biblia ya Kisukuma inatumika ili watu weweze kumsikia Mungu akisema nao kwa lugha yao ya Moyoni.

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akihutubia Kanisa la Mungu katika Kabila la Wasukuma wakati wa uzinduzi wa Biblia hiyo ya kisukuma.
by The Bible Society of Tanzania | Jun 24, 2021 | UpComingEvent
Tunakualika Karibu Ushiriki nasi katika
Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma
Jumapili, Juni 27, 2021
Mahali: KANISA LA AIC MISSION MAKONGOLO – MWANZA
Saa 08:00 Mchana – 12:00 Jioni
Tukio la bure kabisa
Imetafsiriwa na Chama cha Biblia cha Tanzania
Jinunulie Biblia yako katika lugha yako ya mama
Pia kinawakaribisha wanachama wote wa Chama cha Biblia walioko mkoa wa Mwanza kwenye uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma.
Uzinduzi huo utafanyika katika kanisa la AIC Makongoro, Jumapili tar.27.6.2021 kuanzia saa 8 mchana hadi 12 jioni.
Muda huu utawapa nafasi waumini kutoka madhehebu mbali mbali kuweza kushiriki tukio hili, baada ya kumaliza ibada za Jumapili ndani ya makanisa yao.
Wanachama wote mnakaribishwa kushiriki tukio hili muhimu na la kihistoria kwa Chama cha Biblia, Kanisa na jamii nzima ya Kisukuma.
Upatapo taarifa hii mkaribishe na mwenzako, Wakristo kutoka madhehebu yote mnakaribishwa.
Tuunge mkono kwa kushiriki kikamilifu katika uzinduzi wa Biblia hii.
Tukutane AIC Makongoro kwenye uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma Jumapili.
Karibuni 🙏🙏🙏
BIBLIA hiyo itakuwa inauzwa kwa bei ya punguzo.
Jiandae upate nakala yako pia.
Mungu ataongea na wewe kwa lugha yako ya Kisukuma.