Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Biblia kwa Lugha ya Kihehe Yazinduliwa Rasmi Iringa – Miaka 30 ya Kazi Yafikia Tamati

Na Mwandishi Wetu, Iringa

29 Juni 2025

3

Dr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.

Mgeni rasmi. 

Mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi, ambaye alikipongeza Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) kwa kazi kubwa na ya kipekee ya kutafsiri Neno la Mungu katika lugha mbalimbali za makabila nchini. ‘‘Biblia hii ni zawadi kubwa kwa jamii ya Wahehe na kizazi kijacho. Nitalitunza Neno hili takatifu, na kila siku nitaanza siku yangu nikiwa nimesoma Biblia hii kwa lugha ya mama yangu,” alisema Mhe. Lukuvi.

6

Mhe. William Vangimembe Lukuvi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), akihutubia.

Biblia iliyotafsiriwa kwa lugha ya Kihehe imezinduliwa rasmi leo katika ibada maalum iliyofanyika katika Kanisa la Kristo Mfalme, Anglikana Iringa Mjini, mkoani Iringa, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, makanisa na jamii ya Wahehe kwa ujumla.

3.1

Askofu Joseph Mwenyekiti wa CCT Mkoa Iringa na Askofu Anglican Dayosisi ya Ruaha akifanya uzinduzi wa Biblia ya Kihehe.

6.9
5
3.2

Dkt. Alfred Elias Kimonge akizungumza kabla ya kukabidhi Biblia ya Kihehe ili izinduliwe.

6.8

Safari ya Miaka 30


Kwa mujibu wa Dkt. Alfred Elias Kimonge, Katibu Mkuu wa CBT, mchakato wa kutafsiri Biblia hiyo ulianza mwaka 1994 baada ya maombi kutoka kwa Makanisa ya Iringa. Mradi huo ulisimamiwa na Chama cha Biblia Tanzania kwa kushirikiana na makanisa mbalimbali, wataalamu wa lugha, wahakiki, watafsiri, na wadau wa ndani na nje ya nchi.

Dkt. Kimonge alibainisha kuwa tafsiri ya Agano Jipya ilikamilika mwaka 2004 na kuzinduliwa rasmi mwaka 2008. Tafsiri ya Agano la Kale ilianza mwaka 2009, na sasa Biblia kamili imekamilika na kuzinduliwa rasmi leo tarehe 29 Juni, 2025. ‘‘Biblia inayozinduliwa leo inapatikana katika matoleo mawili: toleo la Kiprotestanti lenye vitabu 66, na toleo lenye vitabu 72 lijulikanalo kama Deuterokanoni, linalofaa zaidi kwa matumizi ya Makanisa ya Kikatoliki (TEC),” aliongeza kusema.

‘‘Tunamshukuru Mungu kwa kuona siku hii. Hii ni ushuhuda wa kuwa Neno la Mungu linaweza kufika katika kila lugha, kwa kila mtu,” alihitimisha Dkt. Kimonge.

Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Iringa

Mhe Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo akitoa salaam za furaha Kwa kupata Biblia hiyo uku akisifu juhudi za watafsiri, wahariri, na wadau wa kiimani kwa kazi hii kubwa.

9.4
9.2

Mhe Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo.

Risala na Maombi Maalum

Katika risala iliyosomwa kwa niaba ya Kamati ya Uzinduzi, viongozi wa makanisa na jamii walitoa wito kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusaidia katika masuala yafuatayo:

  1. Kutambua Biblia ya Kihehe kama waraka rasmi wa lugha ya Kihehe
  2. Kuandaliwa kwa Kamusi ya Biblia ya Kihehe
  3. Kutolewa kwa Biblia ya Kihehe kwa njia ya sauti (Audio Bible)
  4. Kuwepo kwa Biblia ya Kihehe katika mfumo wa mtandaoni
  5. Kuhifadhi Biblia hiyo katika Maktaba na Makumbusho ya Taifa
5.1
2
8

Ushiriki wa Viongozi na Jamii

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na maaskofu kutoka madhehebu mbalimbali, wawakilishi wa serikali, wabunge, viongozi wa mila na mamia ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Iringa.

Miongoni mwa viongozi wa dini waliokuwepo ni pamoja na:

  • Askofu Dkt. Blaston Gaville (KKKT – Iringa)
  • Askofu Dkt. Joseph Mgomi (Anglikana – Ruaha)
  • Mhashamu Romanus Mihali (RC – Iringa)
  • Askofu Prof. Mdegella, Askofu Mtetemela, na Askofu Ngalalekumtwa
6.7
14
15
6.4
Mangala
4.1

Kumbukizi za Watafsiri

Shukrani na heshima zilitolewa kwa watafsiri na wahakiki waliotoa mchango mkubwa, lakini hawakuweza kushuhudia uzinduzi huu, akiwemo:

  • Marehemu Mch. Lambert Mtatifikolo
  • Marehemu Mwl. Evaristo Mahimbi
  • Marehemu Mch. Israeli Kiponda

Hitimisho na Maono ya Baadaye

Biblia hii inatarajiwa kusaidia jamii ya Kihehe kusoma, kuelewa, na kuishi Neno la Mungu kwa undani zaidi katika lugha yao ya moyo. Viongozi walisisitiza kuwa kazi ya Mungu kupitia tafsiri ya Biblia inapaswa kuungwa mkono zaidi, ili kufanikisha tafsiri katika lugha nyingine za makabila ya Tanzania.

6.8
17

Comments

Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi

Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi

Mkuu wa KKKT ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, Dkt. Fredrick Shoo, amewataka Wakristo kuitunza na kuindeleza lugha zao za asili kwani ndio msingi na urithi walio nao.

Askofu Dkt. Shoo aliyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kimochi (Kichagga cha Old Moshi), iliyofanyika katika Usharika wa Bethel Msaranga, iliyoambatana na kuweka wakfu eneo la ujenzi wa Kanisa la Mtaa huo.

Askofu Dkt. Shoo alisema watu wengi wamekuwa wakipuuzia lugha zao na kusema ni vyema kujifunza na kuziendeleza lugha zao za asili. Katika Uzinduzi huo wa Biblia, Katibu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred Kimonge alisema mbali na Uzinduzi wa Biblia hiyo bado wanakabiliwa na changamoto ikiwemo wenye lugha zao kutotilia maanani na kutozipa kipaumbele.

“wengine wameshajiwekea kuwa kuwasiliana kwa lugha za asili ni udhaifu, wapendwa si kweli kwamba lugha za asili ni udhaifu. Lugha ya asili ndio inajenga moyo wa mtu na ndio lugha mama kwa wote wanaoishi,” alisema.

Addresses

16 Hatibu / 9th Road, Madukani Area.
P.O BOX 175, Dodoma -Tanzania.

Phone

+255 (0) 765 530 892

Email

info@biblesociety-tanzania.org

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma

Hatimaye Biblia ya Kisukuma yazinduliwa kwa kishindo mkoani Mwanza.

Na Felix Jones

Uzinduzi wa Biblia ya Kisukuma umefanyika katika Kanisa Kuu AIC Makongoro Mwanza na kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Umoja wa Makanisa mkoa wa Mwanza.

Akizungumza katika hafla hiyo Mch. Ipyana Mwangota kwa niaba ya mtafsiri mkuu wa Umoja wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (UBS), kuwa mchakato wa kutafsiri Biblia kwa lugha ya Kisukuma ulianza miaka thelathini iliyopita. “Tulifanikiwa kutafsiri sehemu ya Biblia kwa lugha kisukuma na kuzinduliwa mwaka 1895 na Mchakato ukaendelea tukapata Agano Jipya mwaka 1925 na baadae kufanyiwa marekebisho na atimaye kuzinduliwa mwaka 2001 na leo tunayofuraha kuzindua au kuweka wakfu Biblia kamili kwa lugha hii ya kisukuma mwaka huu 2021.”

Mch. Ipyana Mwangota

Meneja Tafsri akizungumza kwa niaba ya Mtafsiri Mkuu wa Umoja wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni (UBS) wakati wa hafla hiyo.

Pamoja na changamoto tulizokabiliwa nazo katika kutafsiri, kuichapisha mpaka leo inazinduliwa, tunakila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kusikia maombi yetu na haja yetu ya moyoni.

Kwa sasa jamii hii ina nafasi ya kumsikiliza Mungu akisema nao kwa lugha yao wenyewe na hivyo historia imejiandika kwa sababu watoto na wajukuu wataitumia Biblia hii kwa miaka mingi na kuienzi lugha yao. Pia ni jambo zuri katika kuihifadhi lugha ya Kisukuma kwa sababu wengi tunafahamu fasihi andishi inahifadhiwa kwa muda mrefu zaidi.

Mara baada ya hotuba hiyo fupi, Mch. Mwangota ndipo alipopata fursa ya kumkabithi Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Kimonge Biblia hiyo ya Kisukuma ili naye aikabidhi kwa Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande ili iweke wakfu tiyari kwa kutumika katika Kanisa la Mungu.

Mwakilishi wa TC akimkabithi KM Biblia

Mwakilishi wa Translation Consultant (TC) Canon Ipyana Mwangota akimkabidhi Biblia ya Kisukuma Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge wakati wa Uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza

Kwa upande wa Katibu Mkuu Dkt. Alfred Kimonge aliomba Biblia hii itumike katika Ibada ili kazi hii iliyofanyika kwa miaka mingi na kwa gharama kubwa isiwe ya bure. Na zaidi aliongeza kuwa kwa niaba ya Chama cha Biblia cha Tanzania ni matumaini yetu kuwa injili ya Wokovu katika Yesu Kristo itawafikia wasukuma katika lugha yao ya moyoni na kusema sasa tumemtambua Mungu anasema na sisi kwa lugha yetu.

Hivyo Wasukuma nao watamsikia Bwana Yesu  kwa ukaribu wa moyoni ili wapate fursa ya kushiriki katika halaiki ya mwisho, kama Biblia isemavyo:-

“Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha (Wasukuma)…” (Ufu. 7: 9 – 12).

“Hivyo Ninayoheshima ya kukuomba Baba Askofu Mkuu kuwa uipokee Biblia hii na kuiweka wakfu” alisema Katibu Mkuu wakati wa kukabithi Biblia hiyo ili iwekwe wakfu.

KM akisoma Risala Mbele Ask. kabla kukabithi Biblia

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge akisoma hotuba mbele ya Askofu Mkuu Renatus Nkwande kabla ya kumkabidhi wakati wa Uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza.

Naye Dkt. Alfred Kimonge alipo maliza kusoma hotuba yake ndipo alipopata fursa ya kumkabithi Askofu Mkuu Renatus Nkwande Biblia hiyo ya Kisukuma ili aiweke wakfu tiyari kwa kutumika katika Kanisa la Mungu.

KM akimkabidhi Biblia ya Kisukuma Askofu

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania Dkt. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia ya Kisukuma kwa Askofu Mkuu Renatus Nkwande wakati wa uzinduzi wa Biblia hiyo ya Kisukuma katika Kanisa la AIC Makongoro Mwanza.

Askofu Mkuu Renatus Nkwande aliipokea kwa furaha kisha akaendelea na taratibu za kuiweka wakfu Biblia hiyo ya Kisukuma.

Ask Mkuu Renatus Nkwande akihutubu

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akisoma sala ya kuzindua hiyo Biblia ya Kisukuma wakati wa sherehe hizo za uzinduzi wa hiyo Biblia ya Kisukuma.

Ask Mkuu Renatus Nkwande akisaini

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akisaini Biblia ya Kisukuma kuwashilia kupokelewa na Kanisa.

Na hapa ni baadhi ya viongozi na waumini walio weza kuhudhulia katika hafla ya Uzinduzi huo.

Baada ya uzinduzi huo wa Biblia hiyo Baba Askofu na Balozi wa Chama cha Biblia cha Tanzania aliyewakilisha Bodi ya wakurugenzi ya Chama cha Biblia cha Tanzania alipata fursa ya kuhutubia wasukuma waliofika katika uzinduzi huo na pia kutoa salamu kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Chama cha Biblia cha Tanzania na kueleza dhima ya Chama katika mkutadha wa kuakikisha kila Mtu hapa nchini anakuwa na Biblia yake na kwa lugha anayeielewa asa kuwa na Biblia ya moyoni.

Askofu Muhagachi

Baba Askofu Amos Muhagachi ambaye ni Mwenyekiti msaidizi wa Bodi ya wakurugenzi na Balozi wa Chama cha Biblia akihutubia Kanisa kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi.

Kwa upande wa Mgeni rasmi Baba Askofu Mkuu Renatus Nkwande alikipongeza Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kazi nzuri sana ya kuakikisha kila mtu ana Biblia yake na lugha yake na kwa bei mtu anayoweza kuimudu huku akisisitiza Kanisa la Mungu katika kabila la Kisukuma kuhakikisha wanaweka ratiba ya kuwezesha Biblia ya Kisukuma inatumika ili watu weweze kumsikia Mungu akisema nao kwa lugha yao ya Moyoni.

Ask Mkuu Renatus Nkwande anahubiri

Askofu Mkuu Renatus Nkwande akihutubia Kanisa la Mungu katika Kabila la Wasukuma wakati wa uzinduzi wa Biblia hiyo ya kisukuma.