Kifahamu Chama Cha Biblia cha Tanzania (CBT).

Kifahamu Chama Cha Biblia cha Tanzania (CBT).

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

Mzee Daudi reading

KUWEZESHA UPATIKANAJI WA MAANDIKO MATAKATIFU KATIKA LUGHA INAYOELEWEKA VIZURI NA KWA BEI WANAYOIMUDU

1.Chama cha Biblia cha Tanzania ni nini?IMG 20181026 163614

Chama cha Biblia cha Tanzania ni Shirika la Kikristo lisilo la Kidhehebu lililoandikishwa mwaka 1965  chini ya Sheria ya Udhamini wa Vyama.

Chama cha Biblia cha Tanzania ni Mshiriki wa Muungano wa Vyama vya Biblia ulimwenguni ( United Bible Societies –UBS ) ambao kazi yake kubwa ni uenezaji wa Neno la Mungu kwa wingi na uhakika kama ifuatavyo:

–       Kueneza Neno la Mungu katika Lugha na Mawasiliano yanayokidhi mahitaji ya watu wengi Ulimwenguni.

–       Kueneza Neno la Mungu katika Tafsiri sahihi bila kupoteza uhalisi wa Maandiko Matakatifu.

–       Kuyauza Maandiko kwa bei wanayoimudi ili waweze kulifahamu Neno la Mungu.

  1. Kaziya Chama cha Biblia  ilianza lini Tanzania?

 20160917 160152( i ) Wamisionari wa kwanza kabisa nchini Tanganyika ndio walioanzisha kazi ya Chama kwenye karne ya 19.

 ( ii ) Kazi ya  kueneza  Biblia  iliendelea kukua na mwaka 1982 Chama kilifikia ngazi ya kuwa Mshiriki wa Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni na mwaka 1988 Chama kilipata uanachama kamili wa Muunganohuu.

3.Je kazi za Chama cha Biblia cha Tanzania ni zipi?

Chama cha Biblia cha Tanzania ni chombo cha Kanisa kinachotumika katika kutekeleza utume wa Kanisa  wa kuihubiri Injili kwa kila mtu.  Chama cha Biblia kinafanya yafuatayo:

a ) Kutafsiri Biblia katika Lugha mbalimbali za kienyeji.

Watafsiri wa Kikagulu b ) Kuchapisha katika Mitindo mbalimbali:

      – Biblia nzima.

      – Maagano na

      – Sehemu zake kwa wasomaji wapya.

 c )Kueneza Biblia,Maagano na sehemu zake kwa watu wote kwa kushirikiana na :

      – Makanisa na Mashirika yake.

      – Maduka ya Vitabu.

      – Watu binafsi pamoja na wakereketwa wa kujitolea.

 d )Kushirikiana na Vyama vingine katika kuhakikisha Biblia inasomwa kwa lugha zote za hapa Tanzania ili kila mtu auonje uzuri wa Yesu Kristo na kupata maisha mapya.

  1. Je, hadi sasa Chama cha Biblia cha Tanzania kimetafsiri Biblia katika Lugha zipi za kienyeji ?

medium 1 Chama hadi sasa kimemudu kutafsiri Biblia nzima katika Lugha  za:  Kiiraqw, Kihaya, Kinyakyusa, Kisukuma, Kijaluo, Kimasai na Kigogo. Pia kimeweza kutafsiri Agano Jipya katika Lugha za Kibena, Kimashami, Kivunjo, Kimochi, Kichasu( Kipare ), Kijita, Kidatooga, Igikuria, Kishambala, Kizaramo, Kinyiramba na Kirimi ( Kinyaturu )     Miradi ya Tafsiri inayoendelea ni ya Lugha za Kihehe, Kikaguru, Kiha na Kisukuma cha kisasa. Mbali na kuchapisha  Biblia, pia Chama kinachapisha matoleo yafuatayo:

–       Sehemu za Biblia.

–       Sehemu za Biblia kwa wasomaji wapya wanaojifunza Biblia kwa Kiingereza, Kiswahili na Lugha za Kienyeji.

–       Vipeperushi maalum vya vifungu vya Biblia kwa matukio mbalimbali k.m kuzaliwa kwa Yesu,kifo cha Yesu,wagonjwa waliolazwa,na matukio mbalimbali k.m Uhuru, Rushwa nk.

–       Kanda naswa za Neno la Mungu.

–       Neno la Mungu katika Braille kwa wasomaji wasioona.

–       Neno la Mungu kwa maandishi makubwa kwa wenye udhaifu wa macho.

    Kwa kawaida tafsiri inafanywa  kutoka katika Lugha za asili za Kiyunani na Kiebrania,na hivyo kazi ya Tafsiri ni ngumu, inahitaji uangalifu wa hali ya juu na

    inachukua miaka kati ya  8 hadi 10  kutoa toleo moja, kama kuna watafsiri walioajiriwa kwenye mradi kwa wakati wote na kuna wachambuzi 10-15.

  1. Je Chama cha Biblia kinapata  wapi fedha za kukiendesha?

    Chama cha Biblia cha Tanzania kinaendeshwa kwa michango ya

–       Makanisa.

–       Taasisi mbalimbali za Makanisa.

–       Watu binafsi ambao ni wanachama.

–       Marafiki wa Chama.

–       Muungano wa Vyama vya Biblia Ulimwenguni ambao unatoa misaada ya Maandiko Matakatifu kutoka nje ambayo Chama kinayauza na kutumia sehemu ya mapato kuendesha huduma.

  1. Je Chama cha Biblia cha Tanzania kina mahitaji gani?

    Ili kutekeleza kazi zake za Kutafsiri, Kuchapisha na Kueneza Maandiko Matakatifu Chama cha Biblia chaTanzania kinahitaji kiasi kisichopungua  Dola Milioni moja za Marekani kwa mwaka.  Kama Kanisa na Wakristo binafsi watakuwa wanachangia kila mwaka  kwa uaminifu Chama kinaweza kuendesha kazi zake vizuri.

  1. Je, unawezaje kusaidia kazi za Chama cha Biblia ?

  DSC 6345 1  Kuna njia nyingi za kukisaidia Chama cha Biblia katika kazi zake na kinamualika kila Mkristo kushiriki yafuatayo:-

  ( i )Kujiunga na kuwa Mwanachama na kuchangia

      – Uanachama wa Maisha Mme na Mke shilingi 15,000= na ahadi isiyopungua shilingi 15,000=kwa mwaka.

      – Uanachama wa Maisha mtu mmoja shilingi 10,000= na ahadi isiyopungua shilingi 10,000= kwa mwaka.

      – Uanachama wa kawaida (bidii ) shilingi 5,000=kwa mwaka.

      – Uanachama wa kawaida kwa Wanafunzi wa Sekondari na Vyuo shilingi 2,000= au zaidi kwa mwaka.

      – Uanachama wa kawaida wa kushirikishwa kwa watoto na wanafunzi wa shule za Msingi shilingi 1,000= au zaidi kwa mwaka.

      – Uanachama wa Mashirika shilingi 50,000= na mchango usiopungua shilingi 50,000= kwa mwaka.

      – Mwanachama wa Biblia Moja kwa Mwezi ( Bible a Month Club) 5,000=, 10,000=, 15,000=, 20,000= au zaidi kwa mwezi.

 (ii )Tafsiri.

      Unaweza kusaidia Chama kwa :

–  Kuchangia Miradi ya Tafsiri kwa kutoa fedha taslimu.

–  Kuchangia Miradi ya Tafsiri kwa kuwapata Watafsiri wenye uwezo na Wachambuzi wenye mzigo na kazi hii.

– Kuchangia Miradi ya Tafsiri kwa kupitia Miswada ya Tafsiri.

(iii ) Uhamasishaji.

      -Kutoa sadaka au michango kila mara kwa Chama.

      – Kuhamasisha Makanisani juu ya Wiki ya Biblia ambayo ni kila wiki ya kwanza ya  Mwezi Novemba kila mwaka.

      – Kuanzisha Vikundi vya Biblia Moja kwa Mwezi ( Bible a Month Club-BAMC ) kwenye Makanisa na maeneo ya kazi.

      – Kusaidia kueneza Biblia kwa njia ya kuuza kwa kujitolea.

      – Kutoa njia mbadala au mawazo ya jinsi ya kutunisha Mfuko wa Chama ukishrikiana na Chama au kwa niaba ya Chama.

(iv ) Maombi.

     Ungana nasi katika kukiombea Chama.

( v ) Kujitolea.

     Unaweza kukisaidia Chama kwa kutoa muda wako na ujuzi wako wakati wowote kukisaidia Chama katika azma ya Kutafsiri, Kuchapisha, Kueneza na  katika kuhamasisha watu kutoa  kumfidia msomsji apate Biblia kwa bei nafuu.

  1. Kwanini Chama cha Biblia cha Tanzania kinatoa Maandiko Matakatifu bure kwa baadhi ya watu au vikundi ?

  18 2 Chama kinatoa Maandiko Matakatifu bure kwa baadhi ya watu wasio na uwezo wa kifedha kumudu kujinunulia,na vile vile ili kukidhi uhitaji wa Maandiko kwa

   Watanzania  walio wengi kinalazimika kuyauza kwa bei nafuu wanayoimudu ambayo iko chini ya ilyopangwa kuuzia.

  1. Wito wa Chama kwa Wakristo

    Chama kinatoa wito kwa Wakristo wote mmoja mmoja na Makanisa yote kujiunga na kuwa mwanachama wa Chama cha Biblia na kuchangia Chama

    fedha ,mawazo  nguvukazi na maombi ili kukiwezesha  kuendesha kazi zake za Kutafsiri,Kuchapisha na Kueneza Maandiko Matakatifu kwa watu wote

   Tanzania.

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA NA PROGRAMU YA BIBLIA MAGEREZANI

ZIARA KATIKA MAGEREZA YA MSALATO NA KONGWA DODOMA

Moja kati ya wajibu muhimu kwa Chama cha Biblia cha Tanzania ni kuhakikisha kuwa watu wote wanapata fursa ya kupata maandiko matakatifu. Kutokana na jukukumu hilo tarehe 27/11/2018 watumishi wa Idara ya Mahusiano na baadhi ya Wale wa Mawasiliano, walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Msalato Dodoma na kugawa Biblia, Sabuni na dawa ya meno kwa Wafungwa wa gereza hilo la Msalato. Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji akishirikiana na Msaidizi wake na Maafande wengine walitupokea vizuri sana na kutupa ushirikiano wa hali ya juu.

15

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Msalato Afande Huruma Mwakaji

18 2

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, viongozi wa kanisa la KKKT Dodoma na viongozi wa gereza la Msalato

Jukumu la kugawa Biblia halikuishia Gereza la Msalato tu kwani Tarehe 28/11/2018 Meneja Mahusiano na kikosi kazi chake walipata nafasi ya kutembelea Gereza la Kongwa Dodoma. Katika Gereza hili tulipokelewa vizuri sana na kupewa maelezo ya jinsi Wafungwa wanavyohitaji msaada wa Maandiko na vifaa vingne kwani wanatakiwa kjujitegemea.Chama cha Biblia tulifaulu kugawa Maandiko Matakatifu,sabuni, dawa ya Meno na Taulo za akina Mama.Mkuu wa Gereza Afande Nyonyi alishuru sana Chama cha Biblia cha Tanzania kwa msaada huo kwa Wafungwa.

8

Meneja Mahusiano wa Chama Cha Biblia Rev. Samweli Mshana akikabidhi Biblia na mahitaji mbalimbali ya wafungwa kwa Mkuu wa Gezea la Kongwa Afande Nyonyi

1

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Chama cha Biblia, mkuu wa jimbo wa kanisa la KKKT Kongwa (wa kwanza kulia) na viongozi wa gereza la Kongwa

 

Chama Cha Biblia Cha Tanzania Kimewafikia Watu Wenye Ulemavu.

Chama Cha Biblia Cha Tanzania Kimewafikia Watu Wenye Ulemavu.

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA KIMEWAFIKIA WATU WENYE ULEMAVU.

DSC02466

Miongoni mwa malengo ya Chama Chama Biblia cha Tanzania ni pamoja na kuhakikisha kila Mtanzania anafikiwa na neno la Mungu. Kupitia programu ama miradi mbalimbali inayofanywa na Chama Cha Biblia, hufanikiwa kuyafikia makundi mbalimbali ya watu katika jamii na miongoni mwa makundi hayo ni pamoja na walemavu ambapo ndani ya kundi la walemavu lipo kundi la vipofu yaani wasiokuwa na uwezo wa kuona. Ili kufikia azma yake ya kuhakikisha kila mtu anafikiwa na neno la Mungu watu wenye ulemavu wa macho ni kati ya kundi ambalo linatakiwa kufikiwa na huduma za Chama Cha Biblia.

Katika kulitilimiliza lengo hilo, Chama Cha Biblia cha Tanzania kupitia programu ya Biblia kwa vipofu (Braille Bible) kimefanikiwa kuwafikia watu 34 wenye ulemavu wa macho kutoka katika Kata 3 za Wilaya ya Kongwa ili kuandaa mpango wa pamoja kwa lengo la kuwapatia Braille Bible na Audio Bible ili waweze kukua kiroho.

Lakini pia walihamasishwa kuanzisha vikundi vya ‘Imani huja kwa kusikia’ kama sehemu ya wao kukutana na kujadili neno la Mungu kwa pamoja.

DSC02285Elisha Letema

Kimsingi walifurahi sana kutembelewa kwani Elisha Letema alisema “watu wenye ulemavu ni watu wanaotengwa sana na jamii kutokana na jinsi walivyo” lakini kwa kutembelewa na Chama Cha Biblia nao walijiona ni sehemu ya jamii na kusikia kupendwa mno na Mungu ambapo aliongezea kwamba mradi huu wa kuwapatia Biblia utawanufaisha sana kwani yeye anaamini hata wanadamu wakimtenga, Mungu haweza mtenga,, kwa hiyo kwa kupata Biblia itawasaidia kumjua zaidi Mungu na kumtegemea,, kumtumainia yeye daima.

DSC02331Judith Pembamoto

Lakini pia Judith Pembamoto aliongezea kwa kusema kuwa yeye hakuwa na ufahamu mkubwa sana juu ya elimu ya Mungu kwa sababu ya kukosa nyenzo ama vitabu vya dini ambapo akasema programu hii ya Braille Bible itamsaidia kumjua Mungu aliyeumba Mbingu na Dunia (Nchi)

Kitendo cha kuwatembelea na kuwafikia kiliwafanya wafurahi sana na kukishukuru Chama Cha Biblia cha Tanzania kwa kuwatembelea na kuwakumbuka kiasi cha kufungua mioyo yao na kuwa na utayari wa kushirikiana nao kwenye huduma zitolewazo na CHAMA CHA BIBLIA.

Braille Bible portions and Audio Bible for people with visual disabilities in Dodoma region.

Braille Bible portions and Audio Bible for people with visual disabilities in Dodoma region.

Project Summary

People with visual impairment  are stigmatized and discriminated by the community in Tanzania;and therefore their needs  are given little attention.Dodoma is the leading region with higher number of visually impaired persons in Tanzania because of trachoma infection.It is estimated 32%of entire population of people with disabilities were found to be persons with visual disability.In this project the Bible Society of Tanzania wants to address one of these challenges, which is to provide them with user friendly Scripture materials for them to read and listen.;so as the Word of God may transform their life.In implementing this project the Bible Society of Tanzania intends to distribute  Braille Bible portions and  Audio Bibles to 21,000 people with visual disabilities from January to December,2019.

Reason for Ranking

This program will help many visualy disabled people particularly in rural areas to know Christ.  It is also in line with the Philadelphia Promise that emphasizes reaching all audiences including those with disabilities with the Word of God.

“They were all excited, because each one of them heard the believers speaking in his or her own language.” Acts 2:6b

 

Project Goal

Goal.

  •  People with visual Disabilities (PVDs) about 21,000 in Dodoma rural area to be reached by the word of God and their life get transformed.

Objectives.

  • To produce and distribute 10,000 Braille Bible portions to people with Visual Disabilities.
  • To provide 11,000 Audio Bible to those who are not literate in Braille.

 

Project goal’s relationship to overall bible society strategy

The Bible Society of Tanzania strategic objective is to make Scriptures available to all Tanzanian to help them to transform their lives. In the Bible Society of Tanzania strategic objective people with visual disabilities are among the targeted audiences; therefore, implementation of this project as Scripture distribution is to achieve one of the strategic focuses of the Bible Society of Tanzania . This program will be implemented as one of the Good Samaritan projects  among Bible Society of Tanzania programs on Biblical perspective. In implementing the Good Samaritan program; experience from the field showed that people with visual disability had no access the Word of God because they had not been provided with the relevant and appropriate Bible material (Braille) – be it Braille or Audio Scriptures.

View this Bible Society’s Strategy ››

This project has not yet submitted an update

Strategic Fit

Connecting your project to your Bible Society’s overall mission strategy

How does your project relate to the Philadelphia Promise?

This project target visually disabled persons who are also one of the targeted audiences as is in the Philadelphia Promise commitment one; “helping all people have and engage with the Bible”.

About the beneficiaries

How did you arrive at your beneficiary impact number?

The total number of the visually impaired persons in project area is 41,985. For easy implementation of the project, the Bible Society of Tanzania chose 50% of total  number of the visually impaired persons in this specified period of the project.

Beneficiary focus

41,985 which is 32% of the entire population of people with disabilities were found to be persons with visual disability.Many visually impaired persons live in rural areas. They cannot afford to access Braille Bible portions. Therefore there is a need to find the solution on how to help them to get Braille Bibles portions.

How have the needs and perspective of the beneficiaries helped shape the design of the project?

Visually impaired Persons have been  a marginalized community; many blind persons have experienced quite a number of obstacles to full inclusion in their religious/spiritual communities. From research PVDs say;  “We have had less access to the collection plate; hymnals, textbooks, Sunday bulletins, newsletters, and other printed materials; transportation; social activities; teaching and leading opportunities. But most of all, we lack being accepted as equals to other members of the community” (https://nfb.org/Images/nfb/Pub…)

National Context

According to the Population and Housing Census 2012; 8% of the population were people with disabilities ( PWD’s). Dodoma region had 2.08 million people out of which 130,400 were people with disabilities. 41,985 which is 32% of the entire population of people with disabilities were found to be persons with visual disability (Kondoa  5,588, Mpwapwa 5,275, Kongwa 4,869, Chamwino 8196, Dodoma Municipal 7039, Bahi 5681 and Chemba District 5067).

Need

The Bible Society of Tanzania learned that there are indeed many People with Visual Disabilities in Dodoma region. People with disabilities needs attention to their challenges.In this project the Bible Society of Tanzania wants to address one of these challenges, which is to provide them with user friendly Scripture materials for them to read and listen. Society’s intervention of the challenges that people with disabilities face is low because they are marginalized. The government and some of the Non-governmental organizations are taking different initiatives to address these challenges.The Bible Society of Tanzania is one of the few organizations taking these such initiatives.

How this project will help the beneficiaries

They will have access to Scriptures.

They will be nurtured by the Word of God.

Non-Christian People with Visual Disabilities will have the opportunity to encounter with the Word of God.

The word of God will transform their lives.

Scripture & Prayer

Key Verse

Leviticus 19:14 Do not curse the deaf or put a stumbling block infront of the blind,but fear your God. I am the Lord

Prayer points

Pray for  funding  of this project.

Pray for proper implementation of this project.

Project Activities

Project activities

  • To identify  people  who are Visually impaired  in collaboration with partners :- Local government, Churches and organisations of Persons with visual disability. (January- March 2019).
  • To order and produce braille and Visual materials (January-May 2019)
  • To sensitize Disabled Persons Organizations and partners for collaboration during implementation of the project (February-May 2019)
  • To distribute Audio Bibles to the PVDs (June-October 2019)
  • To distribute Braille Bibles to the PVDs (June-October 2019)
  • To encourage the formulation of Bible reading groups among Persons with Visual Disability and  equip church leaders with skills of teaching Bibles to person with visual disability.
  • To conduct follow up and  collect testimonies, photos and other information for report writing. (November 2019)
  • To evaluate the program and create progress reports in collaboration with partners (November 2019)
  • To prepare end of year report and reporting. (December 2019)

Project partners

  • The Church and Disabled Persons Organization will identify the beneficiaries and help in distribution of the Scripture materials.
  • Donors will provide funding for printing Braille and buying digital audio devices.
  • The Bible Society of Tanzania will provide the Scriptures and follow-up.
Empowering Orphans and Vulnerable Children in Mbarali District.

Empowering Orphans and Vulnerable Children in Mbarali District.

Mbeya is one of the biggest cities in Tanzania after Dar es Salaam, Mwanza, and Arusha. It is the region through which the Great North road passes (i.e Cairo to Cape Town). Also it is one of the main roads in Tanzania, which begins from Dar es Salaam to Tunduma (The city of Mbeya region). It is one of the busy road with many truck cargoes which go through the region to Malawi, Zambia, and the Democratic Republic of Congo. Mbeya region is among three leading regions with high HIV infection rates at national level by 9% after Njombe 14.8% and Iringa 9.1%. The risk of HIV and AIDS is though high. (TACAIDS 2011-2012).

Mbarali District which is targeted program area has high HIV infection rate in the region, due to influx of visitors, fast local growing population, and cultural practices such as Polygamy, widow inheritance, multiple conjugal partners, cleansing widows, promiscuity among married men and married women and premarital sexual relationship. HIV/AIDS pandemic has claimed many lives and left many orphaned children in Mbarali District and some of them are HIV positive.

 imagesOrphanimagesOrphan
Joel

Joel is an orphan who has lost both parents. We visited his home and this is what he had to say to us: “My name is Joel and I am 14 years old. I used to live in Kawetere in Mbeya region with my parents and everything was fine. My parents had a farm and they used to grow all kinds of food and we could go to school. Unfortunately my father died in 2010 then my mother followed in 2013. Then our life changed. There was no one to take care of us. We were there alone in the house that our parents left. Our aunt felt disappointment for us and she brought us here to live with her family. Her husband left his home two years past, no one knows where he his. The only problem now is that our aunt is frequently sick and she cannot support us even though she is trying. She used to sell firewood but now due to her health she can not do it. So now I am responsible for earning money for us. I go to the hills to collect firewood but it is not easy for me. I frequently have chest pains but I guess it is because I carry very heavy logs. Unfortunately I have no way out. My younger brother has a job shepherding goats and he earns 2000 Tsh./month ($1). I have another sibling who is living with my grandmother but we are better off here than she is. Neither my brother nor I go to school.

Through a holistic value based approach,( spiritual, emotional, and psychological), orphans and vulnerable children will have been directly empowered to live a healthy life by 2020.

There was no one to take care of us. We were there alone in the house that our parents left. Our aunt felt disappointment for us and she brought us here to live with her family. Her husband left his home two years past, no one knows where he his. The only problem now is that our aunt is frequently sick and she cannot support us even though she is trying. She used to sell firewood but now due to her health she can not do it. So now I am responsible for earning money for us. I go to the hills to collect firewood but it is not easy for me. I frequently have chest pains but I guess it is because I carry very heavy logs. Unfortunately I have no way out. My younger brother has a job shepherding goats and he earns 2000 Tsh./month ($1). I have another sibling who is living with my grandmother but we are better off here than she is. Neither my brother nor I go to school.