Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Uzinduzi wa Biblia ya Kihehe

Biblia kwa Lugha ya Kihehe Yazinduliwa Rasmi Iringa – Miaka 30 ya Kazi Yafikia Tamati

Na Mwandishi Wetu, Iringa

29 Juni 2025

3

Dr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.

Mgeni rasmi. 

Mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi, ambaye alikipongeza Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) kwa kazi kubwa na ya kipekee ya kutafsiri Neno la Mungu katika lugha mbalimbali za makabila nchini. ‘‘Biblia hii ni zawadi kubwa kwa jamii ya Wahehe na kizazi kijacho. Nitalitunza Neno hili takatifu, na kila siku nitaanza siku yangu nikiwa nimesoma Biblia hii kwa lugha ya mama yangu,” alisema Mhe. Lukuvi.

6

Mhe. William Vangimembe Lukuvi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), akihutubia.

Biblia iliyotafsiriwa kwa lugha ya Kihehe imezinduliwa rasmi leo katika ibada maalum iliyofanyika katika Kanisa la Kristo Mfalme, Anglikana Iringa Mjini, mkoani Iringa, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, makanisa na jamii ya Wahehe kwa ujumla.

3.1

Askofu Joseph Mwenyekiti wa CCT Mkoa Iringa na Askofu Anglican Dayosisi ya Ruaha akifanya uzinduzi wa Biblia ya Kihehe.

6.9
5
3.2

Dkt. Alfred Elias Kimonge akizungumza kabla ya kukabidhi Biblia ya Kihehe ili izinduliwe.

6.8

Safari ya Miaka 30


Kwa mujibu wa Dkt. Alfred Elias Kimonge, Katibu Mkuu wa CBT, mchakato wa kutafsiri Biblia hiyo ulianza mwaka 1994 baada ya maombi kutoka kwa Makanisa ya Iringa. Mradi huo ulisimamiwa na Chama cha Biblia Tanzania kwa kushirikiana na makanisa mbalimbali, wataalamu wa lugha, wahakiki, watafsiri, na wadau wa ndani na nje ya nchi.

Dkt. Kimonge alibainisha kuwa tafsiri ya Agano Jipya ilikamilika mwaka 2004 na kuzinduliwa rasmi mwaka 2008. Tafsiri ya Agano la Kale ilianza mwaka 2009, na sasa Biblia kamili imekamilika na kuzinduliwa rasmi leo tarehe 29 Juni, 2025. ‘‘Biblia inayozinduliwa leo inapatikana katika matoleo mawili: toleo la Kiprotestanti lenye vitabu 66, na toleo lenye vitabu 72 lijulikanalo kama Deuterokanoni, linalofaa zaidi kwa matumizi ya Makanisa ya Kikatoliki (TEC),” aliongeza kusema.

‘‘Tunamshukuru Mungu kwa kuona siku hii. Hii ni ushuhuda wa kuwa Neno la Mungu linaweza kufika katika kila lugha, kwa kila mtu,” alihitimisha Dkt. Kimonge.

Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Iringa

Mhe Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo akitoa salaam za furaha Kwa kupata Biblia hiyo uku akisifu juhudi za watafsiri, wahariri, na wadau wa kiimani kwa kazi hii kubwa.

9.4
9.2

Mhe Justin Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo.

Risala na Maombi Maalum

Katika risala iliyosomwa kwa niaba ya Kamati ya Uzinduzi, viongozi wa makanisa na jamii walitoa wito kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kusaidia katika masuala yafuatayo:

  1. Kutambua Biblia ya Kihehe kama waraka rasmi wa lugha ya Kihehe
  2. Kuandaliwa kwa Kamusi ya Biblia ya Kihehe
  3. Kutolewa kwa Biblia ya Kihehe kwa njia ya sauti (Audio Bible)
  4. Kuwepo kwa Biblia ya Kihehe katika mfumo wa mtandaoni
  5. Kuhifadhi Biblia hiyo katika Maktaba na Makumbusho ya Taifa
5.1
2
8

Ushiriki wa Viongozi na Jamii

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na maaskofu kutoka madhehebu mbalimbali, wawakilishi wa serikali, wabunge, viongozi wa mila na mamia ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Iringa.

Miongoni mwa viongozi wa dini waliokuwepo ni pamoja na:

  • Askofu Dkt. Blaston Gaville (KKKT – Iringa)
  • Askofu Dkt. Joseph Mgomi (Anglikana – Ruaha)
  • Mhashamu Romanus Mihali (RC – Iringa)
  • Askofu Prof. Mdegella, Askofu Mtetemela, na Askofu Ngalalekumtwa
6.7
14
15
6.4
Mangala
4.1

Kumbukizi za Watafsiri

Shukrani na heshima zilitolewa kwa watafsiri na wahakiki waliotoa mchango mkubwa, lakini hawakuweza kushuhudia uzinduzi huu, akiwemo:

  • Marehemu Mch. Lambert Mtatifikolo
  • Marehemu Mwl. Evaristo Mahimbi
  • Marehemu Mch. Israeli Kiponda

Hitimisho na Maono ya Baadaye

Biblia hii inatarajiwa kusaidia jamii ya Kihehe kusoma, kuelewa, na kuishi Neno la Mungu kwa undani zaidi katika lugha yao ya moyo. Viongozi walisisitiza kuwa kazi ya Mungu kupitia tafsiri ya Biblia inapaswa kuungwa mkono zaidi, ili kufanikisha tafsiri katika lugha nyingine za makabila ya Tanzania.

6.8
17

Comments

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU – WILAYA YA GAIRO, MKOA WA MOROGORO.

Tarehe: 8 Juni 2025
Mahali:Gairo, Morogoro

Uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu Unasisitiza Uthamini wa Lugha za Asili

Viongozi wakipokea Biblia ili Izinduliwe

Dr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.

Ibada na kubariki wa Biblia. 

Ibada ya uzinduzi na kubariki Biblia iliongozwa na Askofu Godfrey Sehaba wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Morogoro. Pia, viongozi wengine wa kidini waliohudhuria ni pamoja na Mch. Stanley Makasi Tabulu (Msaidizi wa Askofu KKKT), Askofu Frederick Chingwaba (Kanisa Huria Anglikana Tanzania)  na Msaidizi wa Askofu wa Jimbo Katoliki Morogoro.

Chama cha Biblia cha Tanzania (BST) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kiimani na kijamii,  tarehe 8 Juni 2025, ilifanikiwa kufanya uzinduzi wa Biblia kwa lugha ya Kikagulu, katika Wilaya ya Gairo, Mkoa wa Morogoro.

Hafla hii ya kihistoria iliongozwa na Mheshimiwa Lay Canon Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye alisisitiza umuhimu wa kuhifadhi na kuendeleza lugha za asili za Kitanzania. 

Kuonesha Biblia zilizozinduliwa

Askofu Godfrey Sehaba akifanya uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu

Wafurahiya Biblia yao
Mh. Paramagamba Kabudi

Mhe. Prof. Kabudi akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi  Biblia mpya ya Kikagulu.

Maneno ya Mgeni rasmi

Mheshimiwa Kabudi alibainisha kuwa lugha za asili ni hazina ya taifa na kwamba uandishi na utafsiri wa maandiko matakatifu kwa lugha za asili ni jambo la msingi kwa uenezi wa injili na utunzaji wa utamaduni wa Taifa. 

Katibu Mkuu wa Wilaya ya Gairo

Daudi Abdallah Sehaba (DAS wa Gairo) alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mheshimiwa Jabiri Omari Makame, akisifu juhudi za watafsiri, wahariri, na wadau wa kiimani kwa kazi hii kubwa. 

Daudi Abdallah DAS

Daudi Abdallah Sehaba (DAS wa Gairo)

Ngoma ya Kienyeji ya Vijana

Mojawapo ya kikundi cha ngoma za asili kikitoa burudani kwenye uzinduzi

Burudani na Furaha ya Wananchi .

Sherehe hiyo ilionyesha utamaduni wa Kikagulu kupitia ngoma na kwaya mbalimbali zilizofurahisha wageni na wananchi wa Gairo. Uzinduzi huo ulikuwa ni sherehe ya kipekee, ikiashiria mafanikio ya miaka ya juhudi za utafsiri na uchapishaji wa Biblia hii.

Ngoma ya Kienyeji
Kwaya Ikiimba

Shukrani na Tuzo

Mwishoni, Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia Tanzania, Dk. Alfred Elias Kimonge, alitoa shukrani kwa watafsiri na wadau wote waliofanikisha mradi huu wakiwemo Askofu Frederick Chingwaba– Mtafsiri, Askofu Michael Peter Nhonya – Mratibu na Mtafsiri wa Mradi wa Kikagulu na Wahariri wa Biblia ya Kikagulu pamoa na kuwapatia zawadi.

Katibu Mkuu akitoa zawadi kwa Askofu Chingwaba1
Katibu Mkuu akitoa zawadi kwa Askofu Nhonya
Watafsri Waakiki

Matukio katika Picha

Comments

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024
Comments
5

Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia Tanzania, Askofu Dkt. Mark Malekana amesema katika ulimwengu huu ambao jamii inal­alamika kuhusu kuporomoka kwa maadili kutokana na mambo ya aja­bu yanayotokea, nguvu inayoweza kusadia jamii inayoathirika ni Neno la Mungu pekee.

Amesema hayo alipofungua Mku­tano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024 uliofanyika juzi Iju­maa Mei 30, 2025 katika ukumbi wa kanisa la KKKT jijini Dodoma.

Dkt. Malekana alisema Biblia ni maandiko matakatifu yatakayoweza kuibadilisha jamii kutoka kwenye kuwa ‘jamii ovu’ na kuwa jamii ‘in­ayompendeza Mungu’, hivyo am­etoa wito kwa Biblia kupelekwa kwa wahitaji.

“Wito wangu mkubwa, ambao pia ni wito wa mkutano huu siku ya leo ni wito wa kupeleka Biblia kwa vija­na, kupeleka Biblia kwa watoto, ku­peleka Biblia magerezani, kupeleka Biblia kwa kila mtu kwa maana Bib­lia ndio italiponya taifa letu,” alisema Dkt. Malekana na kuongeza:

“Tunashukuru katika kuendesha mambo yake kwa muda mrefu lakini tunashukuru kuona kwamba maku­sanyo ya Watanzania wenye kutoka madhehebu mbalimbali na watu binafsi yameongezeka, sisi Watan­zania tunaweza kutegemeza chama chetu cha Biblia kwa michango yenu kama wanachama, kwa michango yetu kama kanisa sambamba na michango kutoka kwa waumini mbalimbali wa madhehebu yote, Mungu akusaidie.”

7

“Unaposaidia Chama cha Biblia cha Tanzania, unaokoa kanisa na unaokoa Taifa la Tanzania, Mun­gu akubariki unaposaidia Chama cha Biblia cha Tanzania. Hivyo, mimi kama Mwenyekiti nawashukuru sana wajumbe waliohudhuria, na­washukuru kwa mwitikio wenu.”

3

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred Kimonge akisoma Mukhtasari wa Mkutano Mkuu wa chama kwa Mwaka 2023, alisema chama kimeendelea kushirikiana na shirika la ‘Talking Bible Internation­al’ kwa kuendelea kuwa kituo cha kupokea, kuandaa na kusambaza Biblia inayoongea kwa wahitaji ka­tika nchi za Mashariki,Kati, Kaska­zini na Magharibi mwa Afrika.

Alisema mwaka 2023 jumla ya nakala 1,404 za Biblia zinazoon­gea zilisambazwa katika nchi za Kenya,Uganda, Zambia, Eritrea na Niger.

MG 5069 scaled

Dkt. Kimonge alisema nchini Tanzania jumla ya nakala 1,800 zilisambazwa ambapo kupitia mradi huo wa makundi ya watu wasioona na wasiojua kusoma, ya­meweza kufikiwa kwa kushirikiana na makanisa, taasisi za dini na watu binafsi wa kujitolea (volunteers).

Aidha, Dkt. Kimonge alisema mradi wa Kamusi ya Biblia kutoka Kiebrania/Kiyunani _Kiswahili (Scholarly Dictionary) ambao una­husu kuundaa Kamusi ya Kiebra­nia/Kiyunani kwenda Kiswahili (Hebrew/Greek-Shwahili ) ilikami­lika Septemba 2023.

Alisema mradi wa Elimu kwa Wanawake (Literacy for Women in Africa), Chama cha Biblia Tanzania kimeendelea kuutekeleza katika Halmashauri ya Wilaya ya Gairo na Kilosa. Lengo la mradi huo ni ku­wasadia wanawake na wasichana ambao hawajui kusoma na kuan­dika kutokana na mazingira tofauti mbalimbali.

MG 4908 scaled

Dkt. Kimonge aliyataja mazingira hayo kuwa pamoja na tamaduni ambazo jamii iliamini mtoto wa kike hatakiwi kupele­kwa shule, hasa vijijini.

Alisema tamaduni hizo zilisababisha jamii kutoona umuhimu wa elimu na kujishu­ghulisha na shughuli nyingine kama kilimo na ufugaji.

24

Naye Mhazina wa Chama cha Biblia Tanzania, Fadha Chesco Msaga akisoma taarifa ya ya fedha kwa mwaka ulioishia Desemba 31, 2024 alisema: “Tunashukuru Mun­gu kwa mwamko ulionyeshwa na makanisa kwa kipindi cha mwaka 2024 katika kuchangia Biblia kwa watoto, vijana na wafungwa”.

13
33
23
21
35
34
20
39
32
25
9
8
MG 4465 scaled
MG 4780 scaled
MG 4658 scaled
MG 4876 scaled
MG 4883 scaled
MG 4884 scaled
MG 4793 scaled

Related Articles

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU – WILAYA YA GAIRO, MKOA WA MOROGORO.Tarehe: 8 Juni 2025Mahali:Gairo, Morogoro Uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu Unasisitiza Uthamini wa Lugha za AsiliDr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.Ibada na kubariki wa...

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024

Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024

Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia Tanzania, Askofu Dkt. Mark Malekana amesema katika ulimwengu huu ambao jamii inal­alamika kuhusu kuporomoka kwa maadili kutokana na mambo ya aja­bu yanayotokea, nguvu inayoweza kusadia jamii inayoathirika ni Neno la Mungu pekee....

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa.

Mahali: ukumbi wa Nazareti, wilayani Gairo, mkoani Morogoro.

Picture5

Hafla hii ilihudhuriwa na viongozi wa dini na serikali wakiwemo wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa (W) ya Gairo pamoja na ofisi ya Mkurugenzi mtendaji pia Afisa mipango na Afisa maendeleo ya jamii ambapo waliwapongeza sana wahitimu kwa juhudi zao kubwa na kusisitiza umuhimu wa elimu katika maendeleo ya jamii.

Chama cha Biblia, kupitia mradi wake wa Literacy for Women in Africa, kimefanikisha hatua muhimu katika kuimarisha elimu ya wanawake nchini. Mahafali ya saba ya mradi huu yaliyofanyika tarehe 23 Januari 2025 katika ukumbi wa Nazareti, wilayani Gairo, mkoani Morogoro, yaliwahitimu wanawake 353 katika ngazi ya A ya kusoma na kuandika.

Picture6
Picture4

Mradi wa Literacy for Women in Africa umeleta mabadiliko makubwa katika maisha ya wanawake hawa. Wengi wao sasa wanaweza kusoma Biblia, kuendesha biashara ndogo ndogo, na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii zao.

“Shuhuda kutoka kwa mmoja wa wahitimu: “Kabla ya kuanza kusoma, nilikuwa tegemezi sana. Sasa naweza kusoma na kufuatilia habari, na hata kuandika barua ya maombi ya kazi na kushiriki na mambo mbalimbali ya kijamii kama kupiga kura na kuchagua viongozi na hata kugombea nafasi za kiuongozi kama uenyekiti wa mtaa. Maisha yangu yamebadilika kabisa!”

Picture Mzee
Meza kuu wakifurahia jambo wakati wa maafali

Mahafali haya yamekuwa ushahidi tosha wa kwamba elimu ni nguvu. Chama cha Biblia kinaendelea kujizatiti kuhakikisha kuwa wanawake wengi zaidi wanapata fursa ya kujifunza na kukuza uwezo wao. Tunawashukuru sana wadau wote kwa ushirikiano wenu katika kufanikisha mradi huu.

Wahitimu
Picture ya Pamoja
2
Picture3
7

Matukio katika Picha

Comments