Mkutano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024
5

Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia Tanzania, Askofu Dkt. Mark Malekana amesema katika ulimwengu huu ambao jamii inal­alamika kuhusu kuporomoka kwa maadili kutokana na mambo ya aja­bu yanayotokea, nguvu inayoweza kusadia jamii inayoathirika ni Neno la Mungu pekee.

Amesema hayo alipofungua Mku­tano Mkuu wa 39 wa Chama cha Biblia cha Tanzania wa Mwaka 2024 uliofanyika juzi Iju­maa Mei 30, 2025 katika ukumbi wa kanisa la KKKT jijini Dodoma.

Dkt. Malekana alisema Biblia ni maandiko matakatifu yatakayoweza kuibadilisha jamii kutoka kwenye kuwa ‘jamii ovu’ na kuwa jamii ‘in­ayompendeza Mungu’, hivyo am­etoa wito kwa Biblia kupelekwa kwa wahitaji.

“Wito wangu mkubwa, ambao pia ni wito wa mkutano huu siku ya leo ni wito wa kupeleka Biblia kwa vija­na, kupeleka Biblia kwa watoto, ku­peleka Biblia magerezani, kupeleka Biblia kwa kila mtu kwa maana Bib­lia ndio italiponya taifa letu,” alisema Dkt. Malekana na kuongeza:

“Tunashukuru katika kuendesha mambo yake kwa muda mrefu lakini tunashukuru kuona kwamba maku­sanyo ya Watanzania wenye kutoka madhehebu mbalimbali na watu binafsi yameongezeka, sisi Watan­zania tunaweza kutegemeza chama chetu cha Biblia kwa michango yenu kama wanachama, kwa michango yetu kama kanisa sambamba na michango kutoka kwa waumini mbalimbali wa madhehebu yote, Mungu akusaidie.”

7

“Unaposaidia Chama cha Biblia cha Tanzania, unaokoa kanisa na unaokoa Taifa la Tanzania, Mun­gu akubariki unaposaidia Chama cha Biblia cha Tanzania. Hivyo, mimi kama Mwenyekiti nawashukuru sana wajumbe waliohudhuria, na­washukuru kwa mwitikio wenu.”

3

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred Kimonge akisoma Mukhtasari wa Mkutano Mkuu wa chama kwa Mwaka 2023, alisema chama kimeendelea kushirikiana na shirika la ‘Talking Bible Internation­al’ kwa kuendelea kuwa kituo cha kupokea, kuandaa na kusambaza Biblia inayoongea kwa wahitaji ka­tika nchi za Mashariki,Kati, Kaska­zini na Magharibi mwa Afrika.

Alisema mwaka 2023 jumla ya nakala 1,404 za Biblia zinazoon­gea zilisambazwa katika nchi za Kenya,Uganda, Zambia, Eritrea na Niger.

MG 5069 scaled

Dkt. Kimonge alisema nchini Tanzania jumla ya nakala 1,800 zilisambazwa ambapo kupitia mradi huo wa makundi ya watu wasioona na wasiojua kusoma, ya­meweza kufikiwa kwa kushirikiana na makanisa, taasisi za dini na watu binafsi wa kujitolea (volunteers).

Aidha, Dkt. Kimonge alisema mradi wa Kamusi ya Biblia kutoka Kiebrania/Kiyunani _Kiswahili (Scholarly Dictionary) ambao una­husu kuundaa Kamusi ya Kiebra­nia/Kiyunani kwenda Kiswahili (Hebrew/Greek-Shwahili ) ilikami­lika Septemba 2023.

Alisema mradi wa Elimu kwa Wanawake (Literacy for Women in Africa), Chama cha Biblia Tanzania kimeendelea kuutekeleza katika Halmashauri ya Wilaya ya Gairo na Kilosa. Lengo la mradi huo ni ku­wasadia wanawake na wasichana ambao hawajui kusoma na kuan­dika kutokana na mazingira tofauti mbalimbali.

MG 4908 scaled

Dkt. Kimonge aliyataja mazingira hayo kuwa pamoja na tamaduni ambazo jamii iliamini mtoto wa kike hatakiwi kupele­kwa shule, hasa vijijini.

Alisema tamaduni hizo zilisababisha jamii kutoona umuhimu wa elimu na kujishu­ghulisha na shughuli nyingine kama kilimo na ufugaji.

24

Naye Mhazina wa Chama cha Biblia Tanzania, Fadha Chesco Msaga akisoma taarifa ya ya fedha kwa mwaka ulioishia Desemba 31, 2024 alisema: “Tunashukuru Mun­gu kwa mwamko ulionyeshwa na makanisa kwa kipindi cha mwaka 2024 katika kuchangia Biblia kwa watoto, vijana na wafungwa”.

13
33
23
21
35
34
20
39
32
25
9
8
MG 4465 scaled
MG 4780 scaled
MG 4658 scaled
MG 4876 scaled
MG 4883 scaled
MG 4884 scaled
MG 4793 scaled

Related Articles

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU

UZINDUZI WA BIBLIA YA KIKAGULU – WILAYA YA GAIRO, MKOA WA MOROGORO.Tarehe: 8 Juni 2025Mahali:Gairo, Morogoro Uzinduzi wa Biblia ya Kikagulu Unasisitiza Uthamini wa Lugha za AsiliDr. Alfred Elias Kimonge akikabidhi Biblia kwa ajili ya kuzinduliwa.Ibada na kubariki wa...

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa

Maafali ya Saba ya Mradi wa Literacy for Women in Africa.Mahali: ukumbi wa Nazareti, wilayani Gairo, mkoani Morogoro.Hafla hii ilihudhuriwa na viongozi wa dini na serikali wakiwemo wawakilishi kutoka ofisi ya Mkuu wa (W) ya Gairo pamoja na ofisi ya Mkurugenzi mtendaji...