CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO

CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA CHASHEREHEKEA MAHAFALI YA WANAKISOMO GAIRO – MOROGORO

Gairo, Morogoro | 05 Januari 2026

Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) kimefanya mahafali ya nane ya wanakisomo wa mradi wa Literacy for Women in Africa katika Wilaya ya Gairo, Mkoa wa Morogoro, tarehe 05 Januari 2026. Sherehe hiyo ilihusisha wahitimu wa elimu ya watu wazima waliopata mafunzo ya kusoma na kuandika kupitia mradi huo unaolenga kuwawezesha wanawake na wasichana ambao hawakupata fursa ya elimu rasmi.

IMG 5131 scaled

Sherehe hiyo ilifunguliwa rasmi kwa risala iliyosomwa mbele ya mgeni rasmi, Profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, ambaye aliwakilishwa na Diwani wa eneo hilo, pamoja na viongozi wa dini, viongozi wa vijiji vilivyofikiwa na mradi, na Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania aliyewakilishwa na Meneja wa Shughuli, Mchungaji John Mnong’one.

IMG 5061 scaled
IMG 5085 scaled

“Awali sikuweza kusoma wala kuandika. Kupitia mpango huu nimejifunza, na sasa naweza kusoma na kuandika kwa kujiamini. Hata nilipokwenda kupiga kura, nilijichagulia mwenyewe tofauti na zamani nilipolazimika kuchaguliwa na wengine.”

IMG 5035 scaled
IMG 5124 scaled
IMG 5153 scaled
IMG 5168 scaled

Akizungumza kupitia risala hiyo, CBT ilieleza kuwa mradi wa Literacy for Women in Africa ulianza kutekelezwa mwaka 2018 kwa kushirikiana na makanisa na wadau mbalimbali, wakiwemo Serikali za Wilaya za Gairo na Kilosa. Lengo kuu la mradi ni kuwasaidia wanawake na wasichana waliokosa elimu ya msingi kupata ujuzi wa kusoma na kuandika ili kuboresha maisha yao binafsi, kifamilia na kijamii.

Katika kipindi cha utekelezaji wa mradi huo, CBT imewafikia wanakisomo 3,200 wakiwemo wanawake wengi na wanaume wachache. Kutokana na uhitaji mkubwa uliojitokeza kwa wanaume wasiojua kusoma na kuandika, mradi ulipanua wigo wake na kuanza kuandikisha wanaume waliokuwa tayari kujiunga na madarasa ya elimu ya watu wazima (CHIBWEDA).

IMG 5049 scaled

Kwa mwaka 2025 pekee, mradi uliweza kufanya uhamasishaji na kuandikisha wanakisomo 595 (wanaume 145 na wanawake 450), kuanzisha madarasa mapya katika vijiji vya Mkalama, Masenge, Kinyolisi, Kisitwi, Nyangala na Luhwaji, pamoja na kutoa mafunzo kwa waalimu 30 wa elimu ya watu wazima yaliyofanyika Dodoma kwa muda wa wiki mbili. Aidha, vitabu vya kujifunzia (Primer books) vilichapishwa na kugawiwa kwa wanakisomo wote waliosajiliwa, na vitabu 300 vya hadithi (story books) vilitolewa kwa wahitimu kwa matumizi baada ya kuhitimu.

Katika mahafali hayo, jumla ya wahitimu 366 walikabidhiwa vyeti, ikiwa ni ishara ya mafanikio ya mradi katika kuongeza idadi ya watu wanaojua kusoma na kuandika kwenye jamii.

IMG 5054 scaled

Mradi huo umeleta matokeo chanya makubwa, yakiwemo kuongezeka kwa ujasiri wa wanawake kushiriki katika uongozi wa jamii, ushiriki wao katika shughuli za maendeleo, siasa na Kanisa, pamoja na kuimarika kwa uelewa wa jamii katika masuala ya afya, kilimo, ufugaji, mazingira na haki za kiraia. Wanufaika pia wameeleza kuwa mradi umewasaidia kusoma na kuelewa Neno la Mungu, kujiamini zaidi na kuimarisha mahusiano ndani ya familia na jamii kwa ujumla.

Rose Mrema

Literacy for Women coordinator, The Bible Society of Tanzania

Hata hivyo, CBT ilibainisha changamoto kadhaa, ikiwemo wanakisomo 185 kuacha masomo kati ya waliojiandikisha, uhitaji mkubwa wa mradi katika mikoa mingine nchini, upungufu wa fedha za kuendesha shughuli za mradi, pamoja na changamoto za miundombinu ya usafiri katika baadhi ya maeneo.

IMG 5155 scaled
IMG 5163 scaled
16
IMG 4950 scaled
IMG 5172 scaled
IMG 5031 scaled
IMG 5041 scaled
IMG 5009 scaled
Uzinduzi wa Mpango wa kuwafikia wanafunzi kupitia Biblia Inayoongea

Uzinduzi wa Mpango wa kuwafikia wanafunzi kupitia Biblia Inayoongea

Scripture Union Lunch scaled

Umoja wa Kujisomea Biblia Tanzania (Scripture Union Tanzania), kwa kushirikiana na Chama cha Biblia cha Tanzania na Talking Bible International, wamezindua rasmi mpango wa kuwafikia watoto mashuleni kwa kupitia Biblia Inayoongea. Uzinduzi huu ulifanyika tarehe 07 Septemba 2024 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Edmund Rice Sinon, jijini Arusha, chini ya uongozi wa Askofu Abel Mollel wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Kati.

Lengo kuu la mpango huu ni kuyafikia mashule yote nchini Tanzania, kwa lengo la kurejesha maadili mema katika jamii na taifa kupitia mafundisho ya Neno la Mungu. Kwa sasa, mradi huu utaanza kutekelezwa katika mikoa ya Arusha na Manyara kabla ya kuenea nchi nzima.

Katika hafla ya uzinduzi, viongozi na wageni mashuhuri walihudhuria, wakiwemo:

– Askofu Paul Akyoo, Askofu Mstaafu wa KKKT Dayosisi ya Meru na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Umoja wa Kujisomea Biblia Tanzania.

– Dkt. Alfred Elias Kimonge, Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania.

– Dada Rhoda, Mwakilishi kutoka Chama cha Biblia cha Marekani.

– Dada Stella Mtui, Katibu wa Umoja wa Kujisomea Biblia Tanzania.

– Dkt. Nancy Kahuthia, Mwakilishi wa Umoja wa Kujisomea Biblia duniani.

– Kaka Paul Lindberg, Mkurugenzi wa Talking Bible International kwa eneo la Afrika.

– Kaka Teddy Tewodres, Mwakilishi kutoka taasisi ya Talking Bible International eneo la Afrika Mashariki.

Uzinduzi huu unatoa matumaini ya kuleta mabadiliko chanya kwa kizazi kipya kupitia mafundisho ya Biblia na kuimarisha misingi ya maadili katika jamii ya Watanzania.

JCO9752 scaled
JCO9776 scaled
JCO9632 scaled
JCO9722 scaled
JCO9716 scaled
JCO9827 scaled
JCO9810 scaled

Kuhusu Umoja wa Kujisomea Biblia Tanzania

Umoja wa Kujisomea Biblia Tanzania ni shirika lisilo la kiserikali linalolenga kueneza mafundisho ya Neno la Mungu kwa watoto na vijana mashuleni. Kupitia mpango wa Biblia Inayoongea, tunalenga kurejesha maadili mema katika jamii na taifa kwa ujumla.
Mpango wa Biblia Inayoongea unalenga kufikia mashule yote nchini Tanzania, kwa kuanzia na mikoa ya Arusha na Manyara. Lengo kuu ni kuimarisha misingi ya maadili kwa kizazi kipya kupitia mafundisho ya Biblia.

Uzinduzi wa Mpango wa Biblia Inayoongea

07 Septemba 2024

JCO9583 scaled

Uzinduzi wa mpango wa Biblia Inayoongea ulifanyika tarehe 07 Septemba 2024 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Edmund Rice Sinon, jijini Arusha. Hafla hii ilihudhuriwa na viongozi na wageni mashuhuri wakiwemo Askofu Abel Mollel wa KKKT, Dkt. Alfred Elias Kimonge, Dada Rhoda, Dada Stella Mtui, Dkt. Nancy Kahuthia, Kaka Paul Lindberg, na Kaka Teddy Tewodres.

Viongozi na Wageni Mashuhuri

Hafla ya uzinduzi wa mpango wa Biblia Inayoongea ilihudhuriwa na viongozi na wageni mashuhuri kutoka taasisi mbalimbali, wakionesha umoja na mshikamano katika kuleta mabadiliko chanya kwa jamii ya Watanzania.

Askofu Paul Akyoo
Askofu Paul Akyoo

Askofu Mstaafu wa KKKT Dayosisi ya Meru na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini

Dkt. Alfred Elias Kimonge
Dkt. Alfred Elias Kimonge

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania

Dada Rhoda

Mwakilishi kutoka Chama cha Biblia cha Marekani

Dada Stella Mtui
Dada Stella Mtui

Katibu wa Umoja wa Kujisomea Biblia Tanzania

JCO9804 scaled

Vipengele Muhimu vya Mpango

Biblia Inayoongea

Mpango huu unalenga kuwafikia watoto mashuleni kwa kutumia Biblia inayosikika, ili kuwasaidia kuelewa na kuishi mafundisho ya Neno la Mungu.

Kuimarisha Maadili

Kupitia mafundisho ya Biblia, mpango huu unalenga kurejesha maadili mema katika jamii na taifa kwa ujumla.

Kufikia Mashule Yote

Mpango huu utaanza kutekelezwa katika mikoa ya Arusha na Manyara, na baadaye kuenea nchi nzima, kuhakikisha kila mtoto anapata fursa ya kusikia Neno la Mungu.

Maoni na Ushuhuda

“Mpango wa Biblia Inayoongea ni muhimu sana kwa kizazi kipya. Unaleta matumaini ya mabadiliko chanya katika jamii yetu.” – Askofu Abel Mollel
“Ninaamini kwamba kupitia mpango huu, watoto wengi wataweza kuelewa na kuishi mafundisho ya Biblia, na hivyo kuimarisha maadili yao.” – Dkt. Nancy Kahuthia
“Uzinduzi wa mpango huu ni hatua kubwa katika kuleta mabadiliko chanya kwa jamii yetu. Tunatarajia kuona matokeo mazuri.” – Kaka Paul Lindberg

Changia Mpango wa Biblia Inayoongea