Wanakisomo wa Elimu ya watu wazima katika msemo wa Kikaguru

Wanakisomo wa Elimu ya watu wazima katika msemo wa Kikaguru

Na. Ndugu Frank Makalla (Msimamizi Mkuu wa Mradi-CBT).

Chama Cha Biblia Cha Tanzania kilianzisha kisomo cha elimu ya watu wazima kwa kushirikiana na Chama Cha Biblia Cha Finland na SIL (Summer Institute of linguistic) mnamo mwaka 2017 na mwaka huo ulikuwa ni mwaka wa kuandaa vitabu kwa ajili ya wanakisomo wa elimu ya watu wazima katika msemo wa Kikagulu na kanisa katika eneo hilo lilishiriki kikamilifu kwa kutoa watafsiri na waandishi. Ndipo mradi ukaanza 2018 ukiwa na walimu 20 (ishirini). Walimu hao walianza na wanafunzi mia ishirini ambavyo wanafunzi 97 walihitimu na kupewa vyeti mwezi machi 2019.

Na baada ya hapo Madarasa ya kujifunza kusoma na kuandika yalianza mwezi wa nane 2019 katika vijiji 20 (ishirini) vingine na kila kijiji kina darasa moja na kila darasa lina walimu wawili 2 (wawili) na jumla ya wanafunzi ni 423 kwa vijiji vyote.

Madarasa hayo ishirini yanaendelea vizuri katika kiwango cha 97% (asilimia tisini na saba) wanaweza kusoma na kuandika. Tunatarajia watahitimu mwisho wa mwezi huu wa February 2020 na mahafali yatakuwa mwezi wa tatu  kuanzia tarehe 14/03/2020 (kumi na nne), 21/03/2020 (ishirini na moja) na 28/03/2020  (ishirini na nane) kwa maana yamegawanywa kwenye vituo vitatu ambavyo ni Gairo, Nguyami na Magubike.

IMG 20200124 WA0011

Darasa la Chibweda kijiji cha Kibedya

Mwalimu Devotha Madihi wa darasa la Chibweda kijiji cha Kibedya akifundisha darasani. Darasa hili lina mama mmoja mwenye watoto mapacha wanaonekana hapo chini na amekuwa akihudhulia vizuri sana darasani.

IMG 20200124 WA0012

Darasa la Chibweda Kijiji cha Berega

Wanakisomo wa darasa la Kikagulu katika Kijiji cha Berega wanajifunza kusoma na kuandika kwa kutumia lugha ya Kikaguru wakifundishwa na waalimu wao Rose Chitemo mwenye kilemba na Sofia Muhumba.

IMG 20200124 WA0016

Darasa la Chibweda Kijiji cha Berega

Mwanafunzi Merina Malali wa Darasa la Chibweda Berega akiwa anaandika kufuatia maelekezo ya waalimu.

IMG 20200124 WA0023

Darasa la Chibweda Kijiji cha Kiegea

Darasa la Kiegea wanafatilia mafundisho ya mwalimu ubaoni.

IMG 20200124 WA0025

Darasa la Chibweda Kijiji cha Tabuhoteri

Darasa la kijiji cha Tabuhoteli lina wakina mama wenye umri mkubwa na wana bidii sana katika kujifunza kusoma na kuandika.

IMG 20200124 WA0027

Darasa la Chibweda Kijiji cha Ibindo

Wanakisomo katika kijiji cha Ibindo wakipata maelekezo kutoka kwa walimu wao kuhusu kusoma na kuandika.

IMG 20200124 WA0016

Kujifunza kuandika

Mwanafunzi Merina Malali wa Darasa la Chibweda (mwenye kilemba cha pink) katika kijiji cha Berega akiwa anaandika kufuatia maelekezo ya waalimu.

Wanakisomo awa, wapo katika marudio wakisubiri kupewa mitihani yao ya mwisho ili hatimaye kukabidhiwa vyeti kwa wale watakaofaulu na kuhitimu masomo yao vizuri.

CHANGAMOTO:

Kwa kuwa hawa ni watu wazima zipo changamoto mbali mbali zinazoathiri mahudhurio darasani kama vile:- kazi za shamba, misiba kijijini na nje ya kijiji, kuumwa, kuuguliwa, mito kujaa na kuwatenganisha kwa muda, kutomaliza silabasi yao kwa wakati kwa kuwa wapo wenye kujifunza kwa polepole kulingana na umri wao na kusababisha waalimu kuwa fuatilia na kuwaelekeza kwa muda zaidi.  n.k.

Changamoto katika kuwafikia

Wakati mwingine kuna changamoto ya kuwafikia wanakisomo kwa sababu ya ubovu wa miundombinu hasa barabara kama picha inavyoonesha hapa chini.

IMG 20200124 WA0022

Kunasua gari

Wakati mwingine kipindi cha mvua changamoto kubwa ni barabara, mfano picha hiyo hapo Gari lilikwama kwenye matope kutokana ubovu wa barabara wakati tunakwenda kuona darasa la Mtumbatu na tulisaidiwa na wanakijiji kulinasua gari kwenye matope (Ndugu Frank Makalla akieleza).

MADARASA YA ELIMU YA WATU WAZIMA KWA LUGHA YA KIKAGULU {CHIBWEDA} AWAMU YA PILI GAIRO MKOANI MOROGORO.

MADARASA YA ELIMU YA WATU WAZIMA KWA LUGHA YA KIKAGULU {CHIBWEDA} AWAMU YA PILI GAIRO MKOANI MOROGORO.

MADARASA YA ELIMU YA WATU WAZIMA KWA LUGHA YA KIKAGULU {CHIBWEDA} AWAMU YA PILI GAIRO MKOANI MOROGORO.

IMG 20191021 WA0015

Mafundisho

Moja ya juhudi zinazofanywa na waalimu katika madarasa ya Lwakikagulu.

IMG 20191021 WA0020

Maelekezo

Mmoja wa waalimu wa Lwakikagulu akimuelekeza mwanafunzi kusoma na kuandika Lwakikagulu.

IMG 20191021 WA0017 3

Kujaribu

Mmoja wa wanafunzi Wazee wa lugha ya Kikagulu akijifunza kuandika.

IMG 20191021 WA0013

Mazoezi

Wanafunzi wa darasa la Lwakikagulu wakifanya mazoezi ya kuandika na mwalimu wao anawaangalia kwa umakini mkubwa.

IMG 20191021 WA0012

Kusikiliza

Mwalimu wa lugha ya Kikagulu akimsikiliza mmoja wa wanafunzi wake akisoma kitabu cha lugha ya Kikagulu.

Chama cha Biblia cha Tanzania, kimeanzisha utekelezaji wa mradi wa kujifunza kusoma na kuandika kwa watu wazima kwa lugha ya kikagulu.

Chama cha Biblia cha Tanzania, kimeanzisha utekelezaji wa mradi wa kujifunza kusoma na kuandika kwa watu wazima kwa lugha ya kikagulu.

1 Berega 1

ONGERA: Wakakugulu kwa kuhitimu Mafunzo ya kusoma na kuandika.

Chama cha Biblia cha Tanzania, kimeanzisha utekelezaji wa mradi wa kujifunza kusoma na kuandika kwa watu wazima kwa lugha ya kikagulu na kiswahili waliokosa fursa hiyo kutokana na sababu mbalimbali, katika vijiji 30 vya wilaya ya Gairo mkoni Morogoro ikiwa ni sehemu ya kuunga juhudi za serikali kupambana na adui ujinga.

Akizungumza kwenye mahafali ya kwanza yaliyojumuisha  wahitimu 97 wa elimu ya watu wazima yaliyofanyika katika kijiji cha Berega wilyanai hapa

4 Berega

Mratibu wa Mradi, Mwl. Frank Makala (Kulia) akitoa taarifa fupi ya mradi mbele ya katibu mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania.

Mratibu wa mradi huo Frank Makala, alisema kuwa lengo ni kuwasaidia kujua kusoma na kuandika wote waliokosa fursa hiyo hapo awali.

Alisema kuwa wahitimu hao 97, ni sehemu ya 120 ambao ndiyo wajiiandkisha kujiunga na elimu ya watu wazima ya kusoma na kuanadika mwezi Septemba mwaka jana ambao wachache kati yao walishindwa kufika mwisho kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo hali ya kiuchumi.

“Hawa wahitimu wanaomaliza leo ni kutoka katika vijiji 10, ambavyo ndivyo tulianza navyo katika mradi kama awamu ya kwanza na leo 97 wameza kuhitimu na wote wanajua kusoma na kuandika wengine wachache wamekosa kufika siku ya leo kutokana na hali za kiuchumi kwani wengine walilazimika kwenda kwenye shughuli zao za kilimo ili kujitafuatia riziki”alisema Makala.

Makala aliongeza kuwa mradi huo wa kusoma na kuandika unatoa mafunzo kwa kutumia lugha na kiswahili na  kikagulu ili kuweza kuwawezesha wanafunzi kuelewa kwa wepesi.

“Tunatumia lugha mama ya kikagulu na kiswahili katika kufundisha na hii imetusaidia sana kuweza kuwafundisha wanafunzi hawa ambao ni watu waziama na wengi wao walikuja hawajui lolote kwenye upande wa kusoma, lakini kwa kipindi cha miezi sita kila mmoja anajua kusona na kuandika kwa lugha yake ya kuzaliwa ambayo ni kikagulu lakini pia wakati huohuo na kiswahili”alisema.

Alifafnua kuwa madarasa mengine katika awamu ya pili yanatarajia kuanza mwezi Aprili mwaka huu ambapo vijiji vingine 10 vitahusishwa na baadaye mwezi mei vijiji vingine 10 na watarajia hadi ifikapo Novemba 2019 kuwa na jumla ya vijiji 30, ambavyo vimefikiwa na mradi huo.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Askofu wa kanisa Agrikan Tanzania Dayosisi ya Morogoro, Canon Isack Mgego akizungumza katika mahafali hayo alisema wao kama kanisa wanajisikia faraja kuwa sehemu ya kuwawezesha watanzania katika kupambana na adui ujinga.

5 Berega 1

Mgeni Rasmi Canon Isaac Mgego akihutubia wakati wa sherehe hiyo

“Adui ujinga ni moja kati ya maadui ambao taifa letu linapambana nao na sisi kama kanisa tunayofuraha leo kuwezesha watu kujua kusoma na kuandika ili waweze kuondokana na umaskini ambao umekuwa ukiwakabili”alisema Mgego

.Naye mmoja wa wahitimu wa mafunzo hayo Saraha Robert, alisema kuwa anashikuru mradi huo kutoka Chama cha Biblia Tanzania kutokana na kumwezesha kujua kusoma na kuanadika na atoa rai kwa wengine kujitokeza katika kushiriki katika madarasa yanayofuata.

“Mimi nilikuwa sijui kabisa kusoma lakini kufunshishwa kusoma na kuandika kwa kutumia lugha yangu mama kuniwezesha kujua kwa haraka zaidi, na sasa nitaweza kusoma magazate,vipimo vya afya lakini pia matumizi ya dawa ninayoandikiwa hospitalini” alisema.

Matukio katika Picha

GS

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia akicheza na wanakisomo wakati wa mapokezi.

2 Berega

Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Canon Boniface Mkami, Mwl. Ngobei, Mzee wa Kanisa, Mratibu wa Mradi Mwl. Frank Makalla kutoka Chama cha Biblia cha Tanzani. Wakisalimia

diwani 1

Utambulisho: Diwani wa Kata ya Berega Gairo Morogoro

Shangwe

Wahitimu wakishangilia kwa Furaha

 

8 Berega 1

Wanakisomo wakisoma Risala Mbele ya Mgeni rasmi

3 Berega

Katibu Mkuu wa CBT, akitoa maelezo mafupi kuhusu mradi wa Elimu ya watu wazima kwa wakina mama wa Kikaguru.

6 Berega

Mmoja wa wahitimu akipokea cheti wakati wa sherehe hiyo.

Chama cha Biblia cha Tanzania, kimeanzisha utekelezaji wa mradi wa kujifunza kusoma na kuandika kwa watu wazima kwa lugha ya kikagulu.

Adult villagers in Gairo given another chance to learn how to read, write.

Under Literacy Women in Africa Program (LWA) Adult Villagers in Berega Gairo Morogoro Tanzania given another chance to learn how to read and write.

1 Berega

CONGRATULATION: Photo that include the graduates, the guest of honor and the General Secretary of the Bible Society of Tanzania and other guests that were invited.

ADULT villagers in Gairo District in Morogoro Region who missed the formal primary education have another chance to learn how to read and write, thanks to the Bible Society of Tanzania. The society in collaboration with the Bible Society of Finland has initiated a programme to enable the villagers, especially women, to learn to read and write in their own language in Kaguru.

9 Berega

Graduate students playing and dancing with great joyful during their graduation.

Reading out a statement on behalf of fellow students, Buitisi Lirni thanked the Bible Society for the efforts that have made them achieve the goal.

8 Berega 1

Bi. Buitisi Lirni, Reading out a statement on behalf of fellow students.

She said now they can easily read the bible and other literature in Kaguru language and Kiswahili. “We missed this opportunity at early stages in life due to various but we can now read and write through the support of the Bible Society of Tanzania” she said.

She said through the programme they can now read the bible and other publications, noting that the programme has helped expand their horizon.

Speaking at the meeting the General Secretary of the Bible Society of Tanzania, Mr. Alfred Kimonge the programme undertaken through cooperation with Bible Society of Finland was to help women, especially those in the villages to read and write.

3 Berega 1

The General Secretary of the Bible Society of Tanzania, Mr. Alfred Kimonge (Standing) speaking during the Graduation.

He said women have shown great strength in fostering cooperation in any society and helped bring the desired changes, thus it was prudent to empower them to read the bible and other literatures.

Mr. Kimonge also observed that the church has a role to play in transforming the society, adding the program is in line with the government’s efforts to provide basic education to all Tanzanians. The General Secretary stated that Tanzania is among the five countries (Tanzania, Kenya, Malawi, Ethiopia and Namibia) globally that benefit from the program aimed at providing basic Learning skills using the respective people’s mother tongue.

“I am impressed by what I have seen here, now that you are able to write and read out your own statement, this is a clear indication the program has opened opportunity for to read more” he said.

He said bible translation in Kaguru language will be out soon, thus they will be able to read the word of God by themselves in their own language.

Also, Mr. Frank Makalla he said, these teachers are expected to start training new students on April 8, 2019 in those particular villages.

But also there will be training for other new twenty teachers, from ten other villages. From there they will start to register a new illiterate people (Women) and those students will begin their training on June 2019 at Berega Village.

4 Berega

Mr. Frank Makalla (Right) who is program coordinator speaking during the Graduation ceremony.

Guest of honor at the event, Canon Isaac Mgego noted that it was great honor to have people learn in their native language, that they understand most

5 Berega

Canon Isaac Mgego speaking during the graduation.

He said through the program, Kaguru tribe that was at the verge of extinction will now have its rightful honor once again. ”Please public more books in Kaguru language to help maintain our heritage as well as helping young generation to learn the language” he said.

However, he cautioned that using mother tongue should be used to help foster development instead of causing discrimination and division among them.

6 Berega

One of the graduates receiving certificate from the guest of honor.

× How can I help you?