Heri ya Siku ya Wanawake Duniani (IWD)
Watoto katika kituo cha SAAFAD Membe.
Kituo hiki kiko Kijiji cha Membe, Kata ya Membe na Wilaya ya Chamwino katika Mkoa wa Dodoma.
Katika kusherekea sikukuu ya wanawake Duniani, wanawake wa Chama cha Biblia cha Tanzania, wadau na Chama cha Biblia cha Tanzania wamejumuika leo tarehe 08/03/2022 kuazimisha siku hiyo kwa kuwatembelea watoto wanaolelewa kwenye kituo cha SAAFAD Membe.
Katika siku hiyo wanawake wa Chama cha Biblia wamepata fursa ya kukutana na watoto zaidi ya 100 wanaolelewa kwenye kituo hiko ambao ni yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu. Ilikuwa ni ya furaha kwa wanawake, watoto wenyewe pamoja na wageni wengine walioshiriki kwenye sherehe hiyo.
Wanawake hao walipata mda wa kuzungumza na watoto hao kuhusu mada mbali mbali zikiwemo athari za mimba utotoni, umuhimu wa kujitunza na jinsi kuepukana na vishawishi wanavyokutana navyo katika makuzi yao na kuliishi Neno la Mungu wanalofundishwa na walezi wao kituoni hapo.
Watoto walipata muda wa kushirikisha story za maisha yao. Huyo binti anashuhudia namna mama yake alivyomkataa na wadogo zake mara tu baba alipofariki na mama kuolewa na mwanaume mwingine. Wote wanalelewa kwenye kituo cha SAAFAD.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni
“Kizazi cha Haki na Usawa kwa Maendeleo Endelevu.”
Baadhi ya watoto walifanya matembezi wakiongozwa na Mch.Samweli Mshana wa Chama cha Biblia Tanzania.
MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA.
MPANGO WA KUWAPATIA MAANDIKO MATAKATIFU (BIBLIA) WATOTO, VIJANA NA WAFUNGWA MAGEREZANI NCHINI TANZANIA. 1. UTANGULIZI. Chama cha Biblia cha Tanzania (CBT) ni shirika la Kikristo lililoandikishwa mwaka 1970 na kupewa nambari S0 5722. Ni mwanachama wa Muungano waVyama...
MPANGO WA ELIMU YA WATU WAZIMA.
Mpango wa elimu ya watu wazima. Chama cha Biblia kimeeendelea na mpango huu wa elimu ya watu wazima katika (w) ya Kilosa na Gairo-Morogoro kwa lengo la kuwasaidia wanawake na wasichana ambao hawakubahatika kwenda shule kwa sababu tofauti tofauti waweze kusoma na...
MPANGO WA WATOTO WALIOKO KWENYE MAZINGIRA MAGUMU.
Mpango wa watoto walioko kwenye mazingira magumu. Chama cha Biblia kupitia mpango huu kimeendelea kuwafikia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kwa kuwapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo katika masuala ya; Elimu ya afya ya uzazi, UKIMWI, Jinsi ya kumtambua...
MPANGO WA BIBLIA YA NUKTA NUNDU.
Mpango wa Biblia ya nukta nundu. Chama cha Biblia cha Tanzania kinaendelea na mpango huu wa kuwafikia wasiiona katika wilaya ya Kongwa-Dodoma. Chama cha Biblia kwa kushirikiana na kanisa la Anglican Kongwa kimeweza kuanzisha maktaba kwa ajili ya Biblia ya Nukta nundu...
Get Involved
We have Bibles in different Tanzanians languages that you can read online. You can also download Bible reading plans to guide you through the Bible.
Donate Today or Get Involved