SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

Program hii inatekelezwa na Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na dawati la vijana (Africa Youth Service -United Bible Society).

Madhumuni ya programu ni kuwasaidia, kuandaa, na kuwajengea vijana wadogo miaka 9-24 uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kwa ajili yao na kwa ajili ya maendeleo ya jamii, tukilenga kwenye masuala ya usawa na unyanyasaji wa kijinsia, ushiriki wa watu wenye ulemavu, elimu ya afya ya uzazi na ngono, mitandao ya kijamii, itikadi kali, na utunzaji wa mazingira.

Shughuli kubwa ya programu hii ni kutoa mafunzo kwa vijana wadogo, kupitia warsha shirikishi kwenye jamii yao kwa kushirikiana na makanisa pamoja na wadau wengine.

Walengwa wa mpanguu ni makanisa, shule, vikundi vya vijana, vituo vya watoto yatima,mashirika ya serikali,pamoja na wazazi/walezi.

IMG 3985 scaled

Wadau wa Mradi

IMG 4979 scaled

Majadiliano

IMG 5102 scaled

Pia program hii inalenga.

Kuwapa taarifa sahihi vijana wadogo kuhusu mabadiliko ya kubalehe na afya ya uzazi, ujinsia,

usawa wa kijinsia, watu wenye ulemavu, urafiki na kujithamini, mazingira na mabadiliko ya hali ya hewa

  1. Kuhimiza vijana kufanya maamuzi yenye afya na kuepuka ushawishi mbaya kutoka kwa marafiki, vyombo vya habari vya habari & mitandao na makundi yenye itikadi kali
  2. Kuwaandaa wadau wa program hii kuweza kutimiza wajibu wao wa kusaidia na kuchangia maendeleo chanya na shirikishi kwa vijana.

    Kulingana na nyenzo na shughuli zilizopangwa, malengo yafuatayo yatatumika:

    1. Kuwaandaa wazazi/walezi kuhimiza na kuwezesha maendeleo chanya na shirikishi kwa vijana.
    2. Kutoa mafunzo ya stadi za maisha kwa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu
    3. Kutoa maarifa ya kimsingi kuhusu VVU
    4. Kujenga ufahamu na kutetea haki za watoto, ikiwa ni pamoja na hatari ya unyanyasaji wa kingono
    5. Kuwapa wazazi na walezi ujuzi wa kufuatilia na kuwalinda watoto.
    IMG 4979 scaled
    MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

    MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

    LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA PROJECT.

    TAARIFA FUPI YA MPANGO & MAHAFALI YA SITA YA MPANGO HUU

    Mahafali ya sita ya mpango huu yalifanyika tarehe 17.2.2024 katika Ukumbi wa Nazarethi, Gairo mjini ambapo wanakisomo 421 walitunukiwa vyeti vya kuhitimu Kisomo cha watu wazima na Mkuu wa (w) ya Gairo. Mh. Jabiri Shekimweri.  Sherehe hizi zilihudhuriwa na wageni wengine akiwemo Katibu Mkuu wa Chama cha Biblia cha Tanzania, Dkt. Alfred E. Kimonge, Bodi ya wakurugenzi wa Chama cha Biblia cha Tanzania, wafanyakazi na viongozi wa makanisa na jamii kutoka wilaya ya Gairo na Kilosa.

    Mpango huu umeendelea kutekelezwa na Chama cha Biblia cha Tanzania katika (w) ya Gairo na Kilosa. Lengo kuu ni kuwasaidia wanawake na wasichana hawakuweza kwenda shule  na hawajui Kusoma na Kuandika.

    26 scaled

    Mmoja wa wanakisomo akipokea cheti cha kuitimu elfu hiyo.

    23 scaled
    13 scaled
    12 scaled
    beauty esthetician 43

    SHUGHULI ZA UTEKELEZAJI

    Katika kipindi cha mwaka 2023, Chama cha Biblia kupitia mpango huu kiliweza kutekeleza shughuli zifuatavyo;

    • Kufanya uhamasishaji na kuandikisha wanakisomo 450 (Me 379 & Ke 71) kabla ya madarasa kuanza.
    • Mpango huu umelenga zaidi wanawake na wasichana, ila wapo pia wanaume ambao wamejiunga na madarasa na wamekuwa wanufaika wazuri. Takwimu zinaonyesha kuna idadi kubwa ya wanaume wasiojua kusoma na kuandika na mpango huu unawakaribisha.
    • Kufanya mafunzo kwa waalimu 30 wanaofundisha kwenye madarasa ya watu wazima. Mafunzo haya yalifanyika Dodoma kwa wiki mbili yakiongozwa na wakufunzi kutoka SIL Nairobi, Kenya.
    • Kuchapisha na kuwagawa vitabu 450 vya kujisome kwa wanakisomo wote waliojiandikisha.
    • Kuhamasisha na kuanzisha vikundi (improving literacy groups) vya kujisome vitabu vya hadithi. Vikundi hivi ni kwa ajili ya wahitimu ili kuweza kuendeleza ujuzi na kupata uzoefu zaidi katika kujua kusoma na kuandika. Hapa wananapata nafasi ya kujisomea vitabu vya aina mbalimbali, majarida, magazeti, Biblia pamoja na makala nyingine nyingi.

    Wawezeshe Kusoma

    MAFANIKIO.

    • Kuongezeka kwa wanajamii wanaojua kusoma /kuandika kila mwaka kwenye eneo la mpango.
    • Wanawake kupata na kugombea nafasi mbali mbali za uongozi kwenye jamii yao kutokana na uwezo wao.
    • Kumekuwa na jamii inayojiamini zaidi na yenye uelewa juu ya masuala mbali mbali.mfano Afya, kilimo, mazingira kuanzia kwenye ngazi ya familia.
    • Kumewasaidia kusoma Neno la Mungu pamoja na hii imeongeza ukuaji wa kiroho.
    beauty esthetician 38
    14 scaled
    28 scaled
    9 scaled
    22 scaled
    6 scaled
    4 scaled
    21 scaled
    17 scaled

    Blog

    Product Updates & Sales

    SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

    SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.

    SAUTI YA VIJANA WASAMARIA.Program hii inatekelezwa na Chama cha Biblia cha Tanzania kwa kushirikiana na dawati la vijana (Africa Youth Service -United Bible Society). Madhumuni ya programu ni kuwasaidia, kuandaa, na kuwajengea vijana wadogo miaka 9-24 uwezo wa kufanya...

    read more
    MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

    MAHAFALI YA SITA YA LWA KIKAGURU

    LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA PROJECT.TAARIFA FUPI YA MPANGO & MAHAFALI YA SITA YA MPANGO HUUMahafali ya sita ya mpango huu yalifanyika tarehe 17.2.2024 katika Ukumbi wa Nazarethi, Gairo mjini ambapo wanakisomo 421 walitunukiwa vyeti vya kuhitimu Kisomo cha watu...

    read more
    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya KaskaziniHabari Kamili.Chama cha Biblia cha Tanzania kimeendelea na huduma yake ya kugawa Biblia kwa baadhi ya magereza hapa nchini. Chama kimeendelea kutoa huduma hiyo kutokanana  sadaka na michango ya  wanachama wake, wadau mbali mbali...

    read more
    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Biblia kwa Wafungwa Kanda ya Kaskazini

    Habari Kamili.

    Chama cha Biblia cha Tanzania kimeendelea na huduma yake ya kugawa Biblia kwa baadhi ya magereza hapa nchini.

    Chama kimeendelea kutoa huduma hiyo kutokanana  sadaka na michango ya  wanachama wake, wadau mbali mbali na watu binafsi wenye mapenzi na neema ya kufanya kazi ya Mungu walioko ndani na nje ya nchi.

    Picha zinaonesha baadhi ya magereza yaliyoko katika kanda ya Kaskazini waliofikiwa na kugawiwa Biblia kutoka katika Chama cha Biblia chanTanzania.

    Tunamshukuru Mungu kwa neema hii. Tunaamini kupitia Biblia hizi watu watafikiwa na Neno la Mungu ambalo litabadilisha maisha yao, watazidi kumjua Mungu na kumtumikia. Tunaomba Mungu awabariki na aendelee kuwatumia ili kuwafikia walengwa wengi zaidi na kazi ya Mungu izidi kusonga mbele kwa ushindi mkuu.

    Wapare

    Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza (W) Same Kilimanjaro

    Hata Katesh wafungwa wanalitaja jjina la Yesu

    Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Kateshi

    Kazi njema Magereza ya kaskazini imeanzia Babati Yesu asifiwe

    Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza la Manyara Babati

    Wafungwa wa Arusha Mjini

    Ugawaji wa Maandiko Matakatifu (Biblia)kwa wafungwa wa Gereza Arusha mjini

    Wafungwa wa Mbulu wanamtukuza Mungu pia
    BST IMAGE

    Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

    MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

    MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

    MPANGO WA KISOMO CHA WATU WAZIMA – LITERACY FOR WOMEN IN AFRICA.

    Habari Kamili.

    Chama cha Biblia cha Tanzania kinaendelea kutekeleza mpango wa Kisomo cha elimu ya watu wazima katika wilaya ya Kilosa na Gairo kwenye vijiji 15 vilivyochaguliwa wakati wa kuanzishwa kwa mpango huu. Mpango wa Kisomo cha elimu ya watu wazima umeweza kuwafikia wanaume na wanawake 1500. Wanakisomo waliofikiwa na mpango huu wanajua kusoma na kuandika, maisha yao yamebadilika na wanaishi maisha ya kawaida kama walivyo watu wengine waliosoma. Pia ushirikishwaji wao katika masuala ya kijamii umeongezeka, wengine wamepata nafasi za uongozi kwenye jamii na Kanisa limeweza kuwa na washirika wanaoweza kusoma na kulielewa Neno la Mungu pia kufanya majukumu yao ya utumishi kwa weledi zaidi kulinganisha na ilivyokuwa kabla ya kujua kusoma na kuandika.

    Waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo scaled

    Waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo

    Ili kufanikisha mpango huu Chama cha Biblia kwa kushirikiana na SIL Nairobi walifanya mafunzo ya kuwajengea uwezo waalimu 30 wa Chikagulu. Mafunzo  hayo yalifanyika Dodoma kwa wiki mbili ambapo  waalimu waliweza kufundishwa  mada tofauti tofauti kulingana na mfumo wa mpango ulivyo, baadhi ya mada walizofundishwa ni mifumo ya literacy, sifa za mwalimu bora, sifa za mwanakisomo, majukumu ya mwalimu kabla  na akiwa ndani ya darasa.

    Kwa kipindi cha mwaka huu 2023, Chama cha Biblia cha Tanzania kimeweza kuandikisha wanakisomo 450. Wanakisomo waliojiandikisha  hawawezi kusoma, hawajawai kwenda shule na hawajawahi kukutana na jarida/ gazeti, kitabu chochote na hawajui kuandika. Madarasa yataanza mwezi June,2023 kwa kipindi cha miezi saba.

    Waalimu wa waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo scaled

    Waalimu wa waalimu wa Chikagulu wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo

    Askofu huyo aliwakumbusha washiriki wa mkutano huokumwomba Mungu zaidi kwa kuwa wanahubiri injili katika kizazi kinachobadilika lakini wao wanahubiri neno la Mungu lisilobadilika, jambo linaloibua changamoto mbalimbali ikiwemo lugha.
    Alitoa mfano kuwa wakati wao kama chama wanajitahidi kuhubiri injili kwa lugha ya
    Kiswahili inayosikika kwa watu wengi, lakini Kiswahili chenyewe kinabadilikabadilika.

    BST IMAGE

    Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

    MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

    MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

    MKUTANO MKUU WA 37 WA CHAMA CHA BIBLIA CHA TANZANIA

    Habari Kamili.

     Mwenyekiti wa Bodi ya Chama
    cha Biblia Tanzania, Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana amesema chama hicho kitajitahidi kuendelea kuchapisha na kusambaza neno la Mungu ili liweze kumfikia kwa kila mtu na injili izidi kuhubiriwa.

    Alisema hayo katika Mkutano
    Mkuu wa Mwaka 2022 wa chama
    hicho uliofanyika katika ukumbi
    wa mikutano wa Kanisa la Kiinjili
    la Kilutheri Tanzania (KKKT) jijini Dodoma, Ijumaa wiki hii.

    Malekana, ambaye ni Askofu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato alisema kuwa mafanikio ya kidunia yanataka juhudi na akili zako za mtu, lakini bila Mungu juhudi na akili hizo haziwezi kumfikisha popote.

    Akinukuu maandiko kutoka katika kitabu cha Kutoka 33:15, mwenyekiti huyo wa bodi aliwakumbusha washiriki wa mkutano huo na jamii kwa ujumla, kuishi kwa kumwomba Mungu.

    “Katika maisha yako omba Mungu awe pamoja nawe, iwe ni biashara unafanya au utumishi popote pale. Yesu alisema pasipo mimi hamuwezi kufanya neno lolote, na sisi kama Chama cha Biblia tunamwomba Mungu awe pamoja nasi katika majukumu ya chama katika kutafsiri Biblia, kuchapisha, sambamba na kutawanya maandiko matakatifu”.

    “Kizazi hiki kinatakiwa watu warudi kwenye Neno la Mungu na kumtazama Kristo, na kwa upande wetu Chama cha Biblia tunajitaidi kuchapisha na kusambaza Neno la Mungu kwa kila mtu, wakiwemo watoto, wafungwa..na vijana ni kipaumbele cha Chama cha Biblia cha Tanzania

    MG 0054 scaled

    Picha kutoka kushoto ni Dkt. Alfred E. Kimonge katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, wa pili kutoka kushoto ni Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania, wa tatu kutoka kushoto ni Askofu Christian Ndossa wa Kanisa la Kilutheli la Kiinjili Tanzania Dayosisi ya Dodoma na Mwisho Askofu Amos Muhagachi, Makamu Mwenyekiti wa Bodi.

    MG 0063 scaled

    Askofu Christian Ndossa wa Kanisa la Kilutheli la Kiinjili Tanzania Dayosisi ya Dodoma akihudumu wakati wa mkutano huo.

    MG 0101 scaled

    Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania akionesha riport ya taarifa ya fedha

    MG 0102 scaled

    Dkt. Alfred E. Kimonge katibu Mkuu Chama cha Biblia cha Tanzania, akiwasilisha taarifa ya utendaji na fedha kwa mwaka wa 2022.

    MG 0070 scaled
    MG 0184 scaled
    MG 0105 scaled
    MG 0136 scaled
    MG 0138 scaled
    MG 0126 scaled
    MG 0125 scaled
    MG 0180 scaled
    MG 0229 scaled
    MG 0195 scaled
    MG 0201 scaled

    Katika maisha yako omba Mungu awe pamoja nawe, iwe ni biashara unafanya au utumishi popote pale. Yesu alisema pasipo mimi hamuwezi kufanya neno lolote, na sisi kama Chama cha Biblia cha Tanzania tunamwomba Mungu awe pamoja nasi katika majukumu ya chama
    katika kutafsiri Biblia, kuchapisha, sambamba na kutawanya maandiko matakatifu”.

    Askofu Christian Ndossa

    Askofu, KKKT

    Naye Askofu wa KKKT Dayosisi ya Dodoma, Christian Ndossa alisema neno la Mungu ndio msingi na taa za miguu ya chama hicho.

    Askofu Ndossa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo alisema kuwa, chama hicho kinaweza kuwa na vitabu vingi pamoja na mipango mbalimbali, lakini bila neno la Mungu kitakosa kitu cha kukisaidia.

    “Tunaweza kuwa na mipango mbalimbali, tukawa na vitabu vingi, tukasoma maandiko ya wataalamu lakini tukakosa kitu
    cha kutusaidia kama tutakosa neno la Mungu ambalo ndio taa ya miguu yetu na mwanga katika maisha yetu sisi tulio wanachama wa Chama cha Biblia Tanzania,”
    alisema.

    Askofu huyo aliwakumbusha washiriki wa mkutano huokumwomba Mungu zaidi kwa kuwa wanahubiri injili katika kizazi kinachobadilika lakini wao wanahubiri neno la Mungu lisilobadilika, jambo linaloibua changamoto mbalimbali ikiwemo lugha.
    Alitoa mfano kuwa wakati wao kama chama wanajitahidi kuhubiri injili kwa lugha ya
    Kiswahili inayosikika kwa watu wengi, lakini Kiswahili chenyewe kinabadilikabadilika.

    Kwa upande wake Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Alfred Kimonge alisema wanayo
    kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa rehema na baraka zake kwa mwaka wa 2022.

    “Hakika umekuwa mwaka wa baraka kwetu, umekuwa mwaka wa kuinuliwa na kuendelea kufanya kazi ya Mungu kwa ujasiri na bidii baada kipindi cha mpito ambacho dunia ilikubwa na ugonjwa wa hatari wa mlipuko wa Covid-19. Hakika Mungu ni mwaminifu sana kwetu,” alisema.

    BST IMAGE

    Sign up for the Bible Society of Tanzania mailing list

    Uenezaji wa Maandiko kwa 2022

    Uenezaji wa Maandiko kwa 2022

    Taasisi yetu kwa mwaka uliopita uliambatana na Baraka zake. Muungano wetu wa vyama vya Biblia ulimwenguni ulituweka katika mpango wa kuwafikia watu milioni moja ulimwenguni walio katika mazingira magumu au walengwa ambao hawana uwezo wa kununua Biblia. Tanzania tulipewa nakala 50,000 za Biblia. Biblia hizo tulizigawa katika mashule na magereza.

    Mch. John Mnongone akimkabidhi SSP Nelson Kanyungu askari anayehudumia Ibada katika gereza la Kigoma
    20220928 134320 scaled

    Mch. John Mnong’one akimkabidhi SSP Nelson Kanyungu askari anayehudumia Ibada katika gereza la Kigoma. Picha ya Pili akikabidhi viongozi wa Makanisa yaliyomo katika Kambi ya wakimbizi Nyarugusu Kasulu

    20220713 140251 1 scaled
    Watoto wa Shule ya Msingi Suguta Kongwa1
    Watoto wa Shule ya Msingi Suguta Kongwa2

    Watoto wa shule ya Mshingi Suguta Kongwa wakifurahia kupata Biblia.

    Uenezaji wetu Mwaka huu ulikuwa kama ifuatavyo.

    Biblia 500, 0000

    Agano Jipya 59,000

    Sehemu za Bibia portion 1,800

     

    FCBH

    Akina mama hawa wa Kabila la Kibarbaig walisikiliza mpango wa FCBH walihitimu kupewa Biblia bure. Walikataa kupokea Biblia ya bure wakalipia Biblia zao kwa furaha.

    Tulipowambia kuwa wana stahili,

    walisema heri kutoa kuliko kupokaea

    BIBLIA INAYOONGEA.

    Tunamshukuru Mungu kwa taasisi yetu kuingia  mkataba na  Shirika la Talking Bible International kuwa Chama cha Biblia cha Tanzania tumekuwa kituo cha kuandaa na kugawa Biblia TB inayoongea kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Mpaka sasa tumeandaa na kugawa nakala 450 za TB kwa nchi za Kenya, Uganda na Zambia.

    Watumishi wakiandaa TB

    Hapa watumishi wa Chama cha Biblia wakiandaa TB katika lugha ya Kibemba na Kitonga tayari kwa kuzipeleka Zambia

    Mwaka huu CBT kiliendesha semina kwa wasioona 18 na kuwafundisha kusikiliza Agano Jipya .

    TB

    Give Today

    Children

    Prison

    Membership

    Youth

    Blind

    Other

    Get In Touch

    × How can I help you?